Siendi kwenye show bila milioni 5:-Shilole

Mwanadad shiloleh amefunguka na kusema kuwa katika muziki wake hawezi kufanya show bila kuwa na makubaliano ya malipo ya kiasi cha shilingi milioni tano na yule anaemuhitaji la sivyo hawezi kwenda.

Shiloleh ameyasema hayo siku ya leo alipokuwa katika kipindi cha leo tena akiwa na mume wake wa ajili ya kutambulisha wimbo wake mpya.

Shiloleh anasema kuwa amekuja kutafuta pesa hivyo hawezi kufanya kazi bila kuwa na makubaliano ya pesa hiyo labda iwe ni tamasha wa ajili ya kuwasaidia na kusapoti wanawake wenzake.

Bila milioni tano mimi sifanyi show. siendi kwenye show kwa sababu ya maisha,mimi ni brand kubwa hivyo tukikubaliana naenda ila  ila siend kwenye shoo bila milioni tano.Na hii inajulikana kabisa labda wanawake wenzangu ndio ntawasaidia  ambao  ambao wanajituma kwa kuandaa matamasha.

 

Shiloleh Afunguka Swala la Kumzalia Uchebe.

Mwanadad Shiloleh amefunguka na kuelezea kuhusu swala lakutaa kumzaliwa mume wake Uchebe ambae kwa sasa wanatimiza zaidi ya mwaka tangu kufungwa kwa ndoa hiyo lakini hakuna dalili ya Shiloleh kuwa mjamzito.

Hata hivyo wawili hao pamoja na kwamba wameoa , lakini tayari kila mmoja tayari alikuwa na watoto wawili hivyo kufanya familia yao kuwa na watoto wanne  tayari.

Shiloleh anasema kuwa hata yeye amekuwa akitamani sana kumzalia mume wake huyo mtoto kama zawadi lakini anaamini kuwa muda utakapofika basi kila kitu kitakuwa sawa.

 

Shilole aelezea Mh. Rais alivyosaidia ujenzi wa Nyumba yake.

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva ambaye pia ni mjasiriamali wa chakula, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amefunguka kuwa Rais Magufuli amechangia kukamilisha ujenzi wa nyumba yake.

Shilole amesema kuwa moja kati ya pesa alizopata na kuziwekeza katika ujenzi wa nyumba hiyo, zilitokana na kampeni za urais mwaka 2015 wakati wakimnadi mgombea wa chama cha mapinduzi (CCM), ambaye ndiye rais wa sasa Dkt. John Magufuli.

“Nyumba yangu imejengwa na muziki pamoja na kampeni za kumnadi Rais Magufuli, maana tulikuwa tunalipwa na tulilipwa pesa nyingi ndipo niliamua kuwekeza kwenye nyumba yangu”, amesema Shilole.

Shilole ameongeza kuwa, “Mimi ni mnyamwezi nimetoka Tabora kuja mjini kutafuta sijaja kuangalia maghorofa ya Dar, nilivyopata ile hela tu nikasema naenda kununua kiwanja moja kwa moja lakini wapo walionunua magari”.

Shilole ni miongoni mwa wasanii wa kike waliofanikiwa kumiliki mjengo na kuuonesha kwenye ukurasa wake wa ‘Instagram’ mwaka uliopita, ambapo amesema kuwa mjengo huo aliujenga kidogo kidogo na unapatikana maeneo ya Majohe, Gongo la mboto jijini Dar es salaam.

Shiloleh Amkumbuka Sharo Millionea

Mwanadada Shiloleh amefunguka na kusema kuwa moja kati ya watu anaowakumbuka sana katika maisha yake  ni msanii sharo millionea ambae amefariki miaka mingi nyuma kuwa ndio alikuwa alimpenda na kumchukulia kama ndugu yake katika sanaa.

Shiloleh ambae aliongea na ilifika sehemu alishindwa kuendelea kuongea anasema kuwa , Sharo Millionea alikuwa hawezi kukaa mbali na yeye kiasi kwamba hata alipokuwa akitaka kwenda kulala alikuwa radhi alale sebleni .

Ikumbukwe kuwa shilole  na Sharo Milionea walikuwa marafiki sana kiasi kwamba ikifikia hatua baadhi ya mashabii walikuwa wakihoji sana mahusiano yao kutokana na ukaribu wao.

Shiloleh Atoa Angalizo kwa Wanaomuwinda Mume Wake.

Msanii wa muziki Bongo, Shilole amechimba mkwara kwa wale wote anaoamini kuwa wanamnyemelea mume wake, Uchebe.

Muimbaji huyo ameeleza kuwa toka mwanzo aliridhika na hali ya mume wake lakini sasa watu wanapoona anang’aa ndipo wanamnyemelea. Kupitia ukurasa wake Instagram ameandika;

“Nililizika na hali yako tangu mwanzo mpaka sasa unashaine Ila wadangaji msivyo na haya mnaanza
kumwambia Mume wangu Uchebe Umekuwa Handsome, Mkome Namtunza! zamani mlikuwa wapi??,” ameeleza Uchebe.

Shilole na Uchebe walifunga ndoa December 07, 2017 na mwaka jana Uchebe alioonekana kwenye video ya muimbaji huyo inayokwenda kwa jina la Mchakamchaka

Chid ni Msanii Mkubwa Anapaswa kupewa Hesima Yake :-Shiloleh

Mwanadada Shilole amefunguka na kusem kuwa sabau kubwa iliyomfanya yeye kumshirikisha Chid benz katika wimbo wake mpya ni kwa sababu Chid benz ni msanii kama walivyo wasanii wengine na wala sio vinginevyo.

Akiulizwa kuhusu baadhi ya wasanii kuwa wakimsema na kumuweka katika makudi mabaya shiloleh anasema kuwa watu wanatakiwa kungalia aliotoka Chid Benz na kitu alichowahi kufanya katika muziki wa bongo fleva na sio kumdhaurau kwa sasa kwa sababu ameshuka.

watu hawaelewi tu, chid benz ni msanii mkubwa sana na anapswa kuoewa heshima yake kwa sababu ameweka mchango  mkubwa sana katika kuisimamsiah bongo fleva,  kwanini watu wanasema kuwa sio msanii? Na mimi nilimchukua yeye kwa sababu chid ana uweoz wa kuandika ngoma kuliko hata wanavyofikria wao.

Shiloleh anakiri kuwa ngoma yake mpya ambayo amemshirikisha chid benz yeye hakuiandika bali iliandikwa na chid benz mwenyewe.

Nyumba Mpya ya Shiloleh Yampa Jeraha.

Mwanadad Shiloeh amefunguka na kusema kuwa nyumba yake mpya ambayo amehamia siku za hivi karibuni ilimtoa ngeu baada ya kudondoka katika nyumba hiyo usiku alipokuwa narudi katika kazi zake.

Akionekana kama mtu aliyepigwa kutokana na majeraha makubwa aliyokuwa nayo hasa sehemu za usoni na hata watu kuhisi pengine labda ampigwa na mume wake alipokuwa katika siku ya mwanadada Nandy , Shiloleh alikanusha taaarifa za kupigwa na kuesma kuwa ni baada ya kuhamia katika nyumba yake ndipo alipopata hayo majeraha.

Shiloeh anasema ‘unajua kuwa juzi juzi ndio nimehamia kule kwenye nyumba yangu majohe sasa nilikuwa nimerudi usiku na nilikuwa nimerudi nimechoka na hakuna umeme bado basi niliporudi nikawa nimejigongwa kwa sababu ya giza.Nyumba yenyewe nilikuwa bado sijaizoea na hii pati nimealikwa na nilimwaidii nandy kuwa nitakuja kwaio nisngeweza kuacha kuja.

Hata hivyo majeraha hayo hayakumfanya shiloleh kuwa mnyonge katika pati hiyo ambayo nandy alikuwa pia anafanya uzinduzi wa album yake ya kwanza.

Shiloleh Apiga Marufuku Mumewe Kutumika Katika Video.

Mwanadada Shilole amefunguka na kusema kuwa hataki kusikia mtu yoyote anataka kumtumia mume wake katika video yoyote kwa sababu wamekuwa wakimsumbua kila maa hasa baada ya mwanaume huyo kuonekana katika mja ya video ya shiloleh mwenyewe.

Akiongea na waandishi wa habari wikiendi hii alipokuwa katika uzinduzi wa albumu ya msanii Nandy , Shiloleh anasema kuwa inawezekana kwli wengine wanataka kufanya nae kazi kwa nia nzuri lakini yeye hataki  kumuona mume wake katika video za watu wengine.

no nilishamwambia kabisa dont do that, unajua kuwa kuna muda wamekuwa wakimtafuta tu lakini mimi nilishakataa kabisa kufanya nao kazi, ingawa wanaweza kutaka kumchukua kwa nia nzuri lakini sitaki kabisa, na ninatangaza kabisa kuwa sitaki msanii yoyote kumtumia mume wangu

Shiloleh na uchebe wamefunga ndoa mwanzoni mwa mwaka huu na mpaka sasa wanaingai katika idadi ya wasanii wachache walioweza kukaa muda bila kuwa na mikwaruzano ya hadharani

Ngoma ya Champion Nimepewa na Chid Benz ;-Shiloleh

Mwanadada Shiloleh amefunguka na kusema kuwa wimbo wake mpya wa champion ulikuwa ni kama zawadi kutoka kwa Chid benz kwa sababu alimpigia simu na kumwambia kuwa amemtayarishia wimbo na alipomtumia  aliupenda na kuingiza vocal zake ambazo sehemu nyingine anaimba akiwa anachana.

Shiloeh anasem hayo alipokuwa akitambulisha wimbo huo wa champion alipokuwa clouds media , na kusema kuwa katika wimbo huo amekuwa togfauti kwa sababu anachana.

ngoma yangu ya champion humo ndani nimechana na ngoma hii nimeandikiwa na kaka yangu Chid benzi, nakumbuka alinipigia simu usiki na kuniambia kuwa kuna zawadi anataka kunipa na kweli alinitumia na mimi nikaingia coko na  hata alivyokuja alishangaa.

Shiloleh aliwahi kufunguka na kuwaomba mashabiki kuacha kumsema na kumchukulia vibaya Chid benz kwa sababu kwa sas ameazna kubadilika na hayupo kama vile alivyokuwa zamani zaidi sana anachohitaji ni maombi ili aendelee kuwa sawa.

Shishi Awashangaa Wanawake Wanaotukana Katika Mitandao ya Kijamii.

Mwanadada shiloleh amefunguka na kusema kuwa amekuwa akwashangaa sana wasichana wanaokaa kutwa kutykana na watu katika mitndao ya kjiamii kama hawana kazi za kufanya wakati kuna mambo mengi ya kushughulika nayo.

Shiloleh anasema kuwa aina hiyo ya wanawake wanakera na pia wanatia aibu sana wanawake wenzao , hivyo waache mara moja na kufanya vitu vingine vya maana.

Akiongea  katika mahojiano, shiloleh anasema “nashangaa kuona watoto wa kike wako busy kutukana  katika mitandao ya kijamii, wakumbuke kuwa hata bibi pia alikuwaga msichana kwaio waache hayo mambo na waanze kufocus katika mambo ya muhimu katika maisha”

Kwa kuongea hapo, shiloleh pia anasema kuwa watu waache kumsema vibaya msanii Chid Benz kwa sababu kwa sasa hayuko kama alivyokuwa zamani na kwamba amebadilika sana.

Mi Siwezi Kugombania Jina, Ninagombania Hela.;-Shiloleh.

Mwanadada Shilole amefunguka na kusema kuwa kwa upande wake anaona hakuna maana sana ya kukaa na kugombania jina ambalo unaweza kutafuta la kwako na kulitengeneza na likawa kubwa .

Shiloleh anasema kuwa kwa wema sepetu kuitwa Tanzania sweethaert ni jina lake alilopewa na watu hivyo ni lazima watu wengine wakae wakiliheshimu jina hilo lakini pia hakuna haja ya kugombana kwa sababu ya hilo.

Shiloleh anasema kuwa kwa upande mwingie anawao watu hao ni wajinga kwa kugombania jina  badala ya kugombania ela kwa sababu kwa upande wake yeye anawaza ela na sio jina.

hayo ni maneno tu yanayokuwa yanaongelewa kama mimi ninavyosemaga shishi trumph lakini trump mwenyewe yuko huko, mwenye jina atabaki kuwa mwenye jina tu kwa

sababu tayari watu walishampa, kwanza mimi nitaona ujinga kama wanabaki kugombania majina.mimi nagombania ela i dont need to kugombania jina, why cant you choose another name.

Wema na hamisa wamekuwa wakirumbana katika mitandao kwa sababu ya jina la Tanzania Sweetheart.

Shiloleh Amtupia Bango Diamond Kuhusu Tetesi za Kulogwa na Wanawake.

Ikiwa katika mitandao ya kijamii kumekuwa na habari za kuwa mwanamuziki Diamond Platinumz amekuwa akilogwa na mama wa mtoto wake mdogo anaejulikana kama Hamisa Mobeto, habari ambayo ime-trend sana ktaika mitandao wikiend hii na wiki hii yote kwa ujumla mwanadada shiloleh nae ameamua kupigilia msumari wa moto kutoka katika habari hiyo.

Katika ukurasa wake  wa instagram, Shiloleh aliandika  baada ya kuweka picha ya Diamond Platinumz huku akimtania kuwa muonekano wake mpya unavutia kufuatia kusuka kwake nywele huku akisema kuwa na ndio maana wanawake wamekuwa wakimloga.”kakangu diamond umedamshi na ndio maana wanawake wanakuloga”

Hata hivyo tangu kumesambaa kwa maneno hayo katika mitandao ya kijamii mwanadada Hamisa Mobeto hajataka kuongea kitu kuhusu hilo zaidi ya kuonyesha shughuli zake zikiendelea kufanikiwa.

Shiloleh Amsifia Uchebe Kwenye Mambo ya Chumbani.

Mwanadada abaesifika kwa kupika chakula kitamu katika mgahawa wake wa shishi food , Shiloleh amefunguka na kusema kuwa amekuwa akiwaponda sana wanaume wa Dar kutokana na tabia zao za kupenda kula chipsi mayai na kuwaita kuwa hao sio wanaume halisi.

Shiloleh anasema kuwa pamoja na hayo anaona kuwa wanaume hao wanaopenda chipsi hawawezi kumpata kwa sababu mume wake sio legelege kama wanaume wa aina hiyo kwa sababu mume wake  sio mla chipsi kama mwanaume mwingine.

Akimsifia mume wake Shiloleh anasema kuwa hawezi kumfananisha mwanaume wake na mwanaume mwingine yoyote kwa sababu ya shughuli kubwa aliyonayo chumbani haifanani na mwanaume yoyote.

Shiloleh na Uchebe wameoa mapema mwaka huu na ndoa yao imekuwa ni ndoa tulivu isiyokuwa na migogoro na kuwa shiloleh anasema kuwa mume wake ni mume halisi aliyekuwa akimuhitaji siku zote.

Shiloleh Awatolea Povu Walimshambulia Baada ya Kumuomba Sapoti Rais.

mwanadada Shilole hivi karibuni alituma salamu zake kwa rais wa Tanzania na kumuomba aje kujaribu kula chakula chake katika mgahawa wake wa shishi food , Shiloleh alisema kuwa moja ya ndoto zake ni kumuona rais akila chakula chake na anatumaini kuwa Rais atamsikiliza ombi lake na kumjibu kwa kujongea mgahawani hapo.

Hata hivyo wapo waliomua kama anaigiza au anatafuta kiki hivyo kuanza kumshambulia kwa uamuzi wake huo, basi shiloleh nae hakuona uvivu kuwajibu kwa kuwatolea povu katika ukurasa wake wa instagram na kusema

Niombe radhi kwa walionilelewa vibaya maana mimi huwa si-fake masha kabisa, naishi maisha yangu.sina utajiri huo kama mnaosema na hata nyumba niliojenga nilijenga kwa kujiwekea kidogo kiodgo kama mam ntilie na msanii, na ndio maana hata nilipofanikiwa niliona bora kushare na nyie ili kuwaonyesha ni jinsi gani mnaweza kunisapoti na kufika hapa nilipofika.

Nilichoomba juzi kwa baba magufuli ni sapoti na kuendelezwa kwa wanangu katika vipaji wanavyosomea,mimi napambana sana ili wanangu wapate kusoma lakini natamani sana kuwapa zaidi ya kile ninachowapatia, kwaio nikaona kwanini nisiweke kilio changu kwa mheshimiwa rais wakati yeye ni mtu anajali sana elimu ya watoto wa kike.

Mwanadada shiloleh ambae kila siku amekuwa akipambana kufikia malego yake hakuona aibu kuweka wazi kwa mba anatamani sana kupata sapoti ya elimu ya watoto wake kwa mheshimiwa rais kwa sababu anatamani watoto wake wafike mbali na pale anapooona yeye kwa sasa wanaweza kufika.

Shiloleh Atuma Meseji kwa Rais Magufuli.

Msanii wa muziki shiloleh ametuma salamu zake  kwa Mh rais Magufui na kumtaka aende nyumbani kwake ambapo anafanya shughuli zake za upishi kwa ajili ya kufanya shughuli zake za uuzaji wa chakula.

Shilole anasema kuwa kwa jinsi alivyo na matumaini na Mh rais anaamini kuwa akipata salamu hizo basi anajua kuwa atakuja kwa sababu ana matumainai hayo.

shiloleh ni moja ya wasanii ambao wamekuwa na uhamasishaji sana kuhusu maswala ya jamii na watu wengi wamekuwa wakitamani mafankio yake ukizingatia kuwa mwanadada huy ni moja ya wasanii walipitia maisha magumu kabla ya kufanikiwa.

Namuomba mh rais magufuli aje kwangu aje kula chakula changu pale shishi food ilo ndo ombi langu kubwa kwa mh rais , na ninaona kabisa kuwa matumaini yapo.

Tukinyimwa Tiketi Tutaaandamana, Nampenda Sana Zari.-Shiloleh

Mwanadada Shiloleh amefunguka na kusema kama endapo watanyimwa ticket ya kwenda kusherekea sherehe ya mtoto wa diamond huko Afrika yaKusini basi wataandamana kwa sababu walishapewa ahaadi ya kwenda nchini humo.

Akiongea na waandishi wa habari, shiloleh anasema kuwa kwake hana wasiwasi kwa sababu Diamond tayari alishamwambia amtumie paspoti yake ya kusafiria hivyo wala hana wasiwasi na safari lakini ikitokea kuwa hajapata tiketi basi ataandamana.

Hata hivyo , Shiloleh anasema kuwa kwake haoni sababu ya kumchukia Zari kwa sababu kama atamchukia basi atakuwa na wivu wala sio kitu kingine.lakini pia anasema kuwa watu wanaojifanya kumpenda sasa hivi walikuwa wapi pindi Diamond akitafuta mtoto.

tiketi ya nini wakati tayari tulishawekwa kwenye tiketi ya pamoja, na safari haijawa-cancelld, wewe nani kakwambia, tutaandamana.

wakati Nasibu alipokuwa anangaika kupata mtoto hakuna aliyejitokeza kumpa mtoto, dada wa watu katoka huko kaja kampa watoto wawili.mimi nitasema namchukia huyo dada kwa kipi, huo ni wivu wa maendeleo tu, yule dada ana akili sana na mimibado nitaendelea kuwa team zari kwa sababu nampenda , ana akili sana.

Shiloleh Kutoa Ngoma na Chriss Brown.

Mwanamuziki Zuwena Mohamed amefunguka na kusema kuwa anatarajia kuusambaza na kupamnua wigo wa muziki wake anaofanya sasa hivi na kwa kulithibitisha hilo amesema kuwa ameanza kuchart na baadhi ya wasanii kutoka nje na mmoja wapo ni msaniiwa kimataifa Chriss Brown.

Akiongea na Lady Hahaa wa kipindi cha african wired kutoka Clouds Media, Shiloleh anasema kuwa alimtumia meseji Chriss Brown wiki hii na alipomuuliza kama anamjua msanii huyo wa kimataifa alikiri kujua na kwamba wanajianda kufanya nae kolabo.

Shiloleh anasema kuwa hata alipomtumia smsm DM , chriss brown alimpongeza kwa jitihada zake katika muziki na katika kujifunza lugha ya kingereza na pia wamekubaliana kutoa nyimbo ya pamoja.

 i was calling the message on DM on instagram, i went hii bro its me shishi baby and he say oooh youu, and i  say yeah its me.-aliongea shiloleh hukua akiojitahidi kuongea na kingereza chake cha kusuasua na kusema kuwa alipomuuliza chriss kuhusu kumjua alijibu kuwa anamjua na anaijua Tanzania.

Mimi na Shiloleh Atuongei kwa Sababu ya Mwanaume._Khadija Ziota.

Mwanadada kutoka mwanza anaejulikana kama Khadija Ziota aanaesadikiwa kuwa ni mwanamke anaemlea Harmorapa kwa sasa amefunguka na kusema kuwa yeye na Shiloleh ni ndugu lakini wamekuwa hawaongei wala kupatana kwa sababu ya mwanaume ndio aliewagimbanisha.

Mimi na shiloleh atuongei kabisa, hatupatani hata kidogo kwa sababu ya mwanaume.mimi na shiloleh ni mtoto wa baba mkubwa na mdogo.lakini kwa sababu ya mwanaume katusababisha kwa sasa hatuongei kabisaa,na hata tukikutana hatuna hata salamu kabisa na hata kupigiana simu hakuna na imeshakuwa muda mrefu sana sasa hivi.

Alipoulizwa kuhusu mwanaume huyo , mwanadada khadija alimtaja mwanaume huyo kuwa na Nuh mziwanda, ambae hapo awali aliwahi kuwa mpenzi wa shilolhe kabla hajaachana nae na kuolewa na uchebe.

Mwanadada huyo ambae kwa na mna moja ama nyingine amekuwa akiongea maneno mengi mitandaoni kuhusu wasanii mbalimbali huku akionekana kuwachafua, inasemekana kuwa anatafuta kiki ili kujulikana mjini.

Shiloleh Apata Deal la Kujifunza Kingereza .

Mwanadada shiloleh amepata dili la kusomeshwa na British Council baada ya kuonekana hawezi kuongea kingereza ingawa dhumuni lake kubwa limekuwa ni kutaka kuongea kingereza kila anapofanya interviews.

shiloleh ambae mara nyingi amekuwa akiongea kingereza pamoja na kukosea lakini amekuwa akiongea hivyo hivyo amesaini dili hilo la kujifunza kingerza mpaka pale takapojua kukiongea kabisa kwa udhamini wa taasisi hiyo.

Shiloleh amekuwa moja ya wanawake majasiri na wenye uhamasishaji mkubwa sana katika jamii kila siku kutokana na mambo mengi anayoyafanya yanayowapendeza jamii yake.

Sikutaka Mwanaume wa Kunilamba Lips :-Shiloleh

Mwanadada shiloleh amefunguka na kusema kuwa ndoa yake inaendelea vizuri na hata hakuna anayemaini kuwa ndoa ile iliyosemwa sana ingeweza kutulia na kufikia hatu ailiyofikia sasa hivi kama wengi walivyokuwa wakidhani.

Shiloleh anasema kuwa alipoanza mapenzi alikuwa akikuta na wanaume tofauti tofauti ambao hawakuwa wamefikia kiwango alichokuwa akikitaka yeye cha kutokubembelezwa kama  walivyokuwa wakifanya lakini alipokuata na Uchebe aliona kuwa uyo ndio mwanaume aliyekuwa akimtaka.

Shiloleh anasema kuwa alikuwa akitafuta mwanaume ambae akikosea anweza kumpa za uso na akamrekebisha na sio kumbembeleza au kumuogopa tu bila kuwa na ukali ndani yake na ndio maana tangu amefunga ndoa watu wamekuwa wakishangaa sana mafanikio yake.

sikutaka mwanaume wa kunilamba lips, nilitaka mwanaume ambae nikizingua nakula za  uso na anayesimama kama mwanaume na watu waliongea mengi sana kwanini uchebe  na sio mwanaume  mwingine lakini kwa  sasa wanashangaa mafanikio yangu.

 

 

Mange Kimambi Amtolea Uvivu Shiloleh

Mwanadada anaesifika katika mitandao kwa ajili ya kukososa na kutoa siri za wasanii na watu wengi marufu nchini Mange Kimambi amemtolea uvivu msanii wa bongo fleva Shiloleh  baada ya msanii huo kumkosoa Muna love kwa kufanya press conference na kuelezea scenario ya kifo cha mtoto wake.

Katika press hiyo ambayo muna aliamua kuweka wazi juu ya mahusiano yake na Peter ambae ndie iliyesemekana kuwa ndie baba wa mtoto na kusema ukweli kuwa mtoto ni wa Casto, aliwagusa watu wengi akiwemo shihsi ambae alianza kumtukana muna kwa kumwambia kuwa alipaswa kusubiri mpaka 40 ya mtoto wake ipite.

Hata hivyo Mange kimambi nae alikuja kuibuka na kuanza kumtolea mapovu shishi na kumwambia kuwa wasanii wengi wa bongo wamekuwa na tabaia ya kuchagua watu wa kuwakosoa kwa kuwaona kama wanaweza kubishana nao au la na ndio maana imekuwa raisi kwa shiloleh kumsema Muna.

kwa mujibu wa Mange kimambi anashangazwa na shiloleh kwa sababu mambo kama hayo yaliwahi kutokea huko nyuma kwa baadi ya wasanii lakini hakuwasema kama alivyomsema Muna sasa hivi.lakini pia sio kwa kumuonyesha kumschukia Muna au Shiloleh  Mange kimambi anasema inawezekana shilole akawa yuko sawa lakini kwanini hakuwahi kuwa-judge na waliowahi kufanya hivyo huko nyuma

Shiloleh Amtolea Mapovu Muna “Utapata Tabu Sana”

Baada ya kuongea na waandishi wa habari, mwanadada Muna alisema mengi huku akisema kuwa anao uthibitisho wa kutosha kuwa mtoto wake patrick ni mtoto wa Casto na wala sio vinginevyo, huku akisema kuwa  hakuwahi kuwa na mahusiano na peter hata siku moja bali alikuwa akimchukulia kama baba yake na mtu wake wa karibu.

Kila mtu ameyapokea maneno ya Muna kwa hali tofauti lakini shiloleh ni moja ya watu walionhea mara tu  baada ya mahojiano hayo kuisha na kumshangaa sana muna kuwa amepata wapi nguvu ya kusimama na kuwaita waandishi wa habari mpaka kuja nyumbani kwake na kuongea kile alichokiongea .

Shiloleh anasema kuwa hata kama alichokiongea kina ukweli lakini hakupaswa kuonyesha au ku-prove chochote kwa mtu yoyote kwa sababu hata 40 ya mtoto wake ilikuwa bado haijafika.

Muna unaenda kuita press conference,ufanyiwe interviw for what, unafurahia nini, unawaia unawaambia nini na juzi tu umetoka kuzika mtoto wako.unataka kuthibitisha kuwa huyo mtoto ni wa casto hatutaki kujua, we dont need it…mimi ni dada yako kama ungekuwa na shda ungenifata tu kama unavyonifataga kwenye mengine…muna utapata tabu sanaa.

Shiloleh ameonyeshwa kusikitishwa sana na kitendo cha muna kumkana mume wake ambae amefunga nae mpaka ndoa kwa ujinga wake mwenyewe.

Shiloleh Kufuata Nyayo za Mzee Yusuph

Mwanadada Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole amefunguka na kusema kuwa kadri siku zinavyokwenda anaona kama inawezekana yeyekufuta nyayo za moja ya msanii mkubwa wa taarab aliyepita ya kuachana na muziki na kufanya mambo mengine ya kijamii.

Akiongea katika futari iliyoandaliwa na msanii mwenzie Iren uwoya pamoja na mumewe dogo janja anasema kuwa kwa jinsi mwezi huu mtuklufu ulivyomfunza mengi anaona kabisa kuwa hana muda mrefu anaweza kupiga chini muziki na kufanya vitu vingine.

si unaona ninavyopendeza na vazi hili la kiislamu,basi kwa taarifa yako sina muda mrefu na mimi nitaacha muziki kama alivyofanya Mzee Yusuf

Kikubwa na kizuri ni kwamba nina vyanzo vingine vya kimapato,unajua kuwa nina ule mgahawa  na biashara zingine , hizo zinaweza kabisa kunifanya niendelee kuishi pale nitakapochukua huo uamuzi.

 

Mzazi Mwenzie na Shilole Afariki Dunia,

Mwana dada mpambananji , Zuwena Mohamed amefikwa na msiba wa kuondokewa na mzazi mwenzie walie bahatika kupata nae mtoto mmoja wa kike wa kwanza,mwanaume huyo aliekuwa akiitwa Elias makala amefariki leo huko Igunga Mkoani Tabora ambapo alikuwa haugui kitu chochote.

Shiloleh amethibitisha kifo icho cha mzazi mwenzie baada ya kusema kuwa marehemu hakuwa  anaumwa chochote ila alikuwa akitoka katika sherehe na kurudi nyumba na ndipo mauti yalipomkuta.

Shiloleh anasema kuwa marehemu alikuwa mzima na mara ya mwisho kuwasiliana nae ilikuwa miezi miwili iliyopita , Lakini kwa taarifa alizozipata kutoka kwa ndugu zinasema hakuwa na ugonjwa wowote uliomsumbua kabla.

Marehemu na msanii Shiloleh walifanikiw akupata mtoto wa kike ambae ndie mtoto wa kwanza wa shilole ambae sasa hivi ana miaka 14.

Shiloleh Akataa Watoto Wake Kufuata Nyayo Zake

Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Shilole amesema mavazi anayovaa kwenye shoo au sehemu mbalimbali za starehe hayupo tayari kuwaona watoto wake wakiiga.
Mrembo huyo amedai kuwa watoto wake wanatakiwa kujua kuwa mama yao yupo kazini na si aina ya mavazi anayopenda kuyavaa

.
Amesema kuwa “Watoto wangu nawalea katika maadili siwezi kuwalea maisha ya kistaa kama ambayo mimi nayafanya, mavazi ninayovaa sehemu mbalimbali ni kutokana na kazi yangu na wanalijua hilo.

Pia amesema kuwa watoto wake hawana dalili za kuja kuwa mastaa, hivyo lazima wakae mbali na aina hiyo ya mavazi kwa kuwa wanalelewa mazingira ya dini,”.

Utani wa Idris kwa Shiloleh

Mchekeshaji Idris Sultan amemtania Shiloleh huku akimsifia kama mwanamke jasiri anaejiamini na kujituma kuliko wanawake wengine waliozoea kuletea kila siku.Hii inakuwa sio mara ya kwanza wa baadhi ya wasanii kugundua umuhimu wa Shiloleh katika jamii.

Pamoja na kwamba Idris aliandika maneno haya kwa njia ya utani lakini imeleta hamasa sana kwa vijana wengine na kuweka gumzo katika mitandao ya kjamii,

Ana nyumba, ana biashara kama tatu, ana watoto watatu na ameolewa  ni marufu na pia ni baby face .mimi nina kiingereza tu hapa , tuendelee kuendekeza ujinga tutajua nani anamcheka mwenzie.

Shiloleh Kuja na Kitabu cha Stori ya Mapenzi

Akiwa kama moja wa wasanii wapambanaji sana, mwanadada shiloleh ametangaza kuja na kitabu chake akishirikiana na mwandishi mmoja kitakachokuwa kikizungumzia histori yake ya mapenzi.

Shiloleh amekuwa ni moja wa wanawake na wasanii wachach wenye uharaka wa kuthubutu kila inapotokea

hey guys kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikianda kitabu changu na mwandishi chipukizi  ni romantic novel ambayo  inavutia kwa wapenzi wa vitabu  vya love story kama fans wangu naomba mkae mkao wa kula  kupakuwa kitabu hiki, kitazinduliwa baada ya mwezi mtukufu  kuisha.are you guys excited as i am?get ready  for heart broken.

 

 

Mimi Sina Competition na Shiloleh:-Esha Buheti

Mwanadada wa bongo movie esha buheti amefunguka na kuongelea uhusiano wake na shiloleh kama watu ambavyo wamekuwa wakiwashindanisha katika swala zima la mapisha na kusemekana wawili hao kwa sasa hawaelewani kwa sababu hiyo,

Akiongea na mwandishi wa habari, esga anasema kuwa kwa upande wake hana ushindani na mtu yoyote zaidi ya kwamba anachojua kila mtu anafanya kazi zake mwenyewe na kila mtu ana wateja wake lakini pia anshangaa kwanini watu wengi wamekuwa wakimshindanisha na yeye wakati kuna wasanii wengi tu ambao ni wapishi.

Competion gani, mimi si-compet na mtu yoyote na hakuna biashara mamabyo ni ya mtu  au kuwa hii imepangwa kufanywa na mtu fulani tu hapana,na hayo ni maneno ya watu nimekuwa nikiyachukia sana kwa sababu mimi sina competition na shiloleh , kwanini mbona watu wengi wanapika tu kuna open kitchen anapika , uwoya anapika lakini wao wamekazana na shiloleh tu kuna nini au vigezo gani vya kunilinganisha nae.

Siwezi kulinganishwa na shilole kwa sababu yeye nilishamkuta akifanya alafu hata menu zetu ni tofauti sana.

Baada ya Kupewa Tuzo,Shiloleh Atoa Shukuran kwa Aunty Ezekiel

Siku ya May 13 ilikuwa pia siku aalumu na muhimu kwa Shiloleh hasa baada ya kupokea tuzo kubwa ya kutambulika kwa machnago wake katika tasnia ya muziki na pia kama mwanamke mpambananji katika tasnia ya muziki na filamu pia lakini akiwa kama wanamke anaepambana kuhudumia jamii.

Aunty Ezekiel alimpa shiloleh tuzo ya kutambua mchango wake mkubwa wa kuhamasisha jamii kwa kile aanacho kifanya katika jamii na pia kuhamamsisha watu wengi waliokata tamaa.

Katika uzinduzi wa filamu yake ya mama, Aunty Ezekiel alitoa tuzo hiyo kwa shiloleh na kupokealwa na snura na kisha kumfikishia mwenye nayo.baada ya kupokea tuzo hiyo Shiloleh kupitia ukurasa wake wa Instagram aliandika

Naamini kuna wengi wanaostahili tuzo hiilakini siwezi kuwa na maneno mengi ya kutosha kushukuru  kwa heshima kubwa ulionipatia mama cookie, nashukuru sana  kwa zawadi nzuri.tuzo ya mama bora mpambanaji  bora kwa bongo fleva na movies katika uzinduzi wako wa filamu ya mama.lakini pia nakupongeza sana kwa kazi nzuri na product ya spray ulioizindua, wewe ni mwanamke shupavu.

Mama yangu aliniacha nikiwa mdogo sana kwaio nikaelewa mazingira magumu ya kuishi bila mama,na ndio maana siku zote nitapambana sana kwa ajili ya wanangu, ukiwagusa wanangu  umenigusa mimi.Hawa ndio watu pekee ninaoweza kusema nitakufa kwa ajili yao.

Shiloleh amekuwa akitambulika kama msanii na mwanamke mwenye moyo wa uthubutu na kujiamini sana ktikakufanya vitu na amekuwa moja ya wanawake wenye kuleta hamasa sana ukiangalia jinsi alivyoanza na mpaka sasa hivi alipofikia , watu wengi wanapata moyo kupitia yeye,.

 

Shiloleh Ajipanga Kurudi Shule Tena.

Mwanadada na msanii maarufu zuwena mohamed ambae siu chache zilizopita alikuwa amepata nafasi ya kwenda kutembelea chuo cha NCT ambapo alipata nafasi pia ya kuona kozi mbalimbali zinazopatikana chuon hapo na kuongea na baadhi ya wanafunzi alifunguka na kuhaidi kuwa atajipanga na yeye kurudi chuoni hapo kwa ajili ya kuongeza elimu kuhuusu mapishi.

Shiloleh ambae ukiachana na kazi ya muziki anayoifanya lakini pa ni mpishi mzuri wa chakula na amekuwa akiwalisha watu wengi jijini, amesema kuwa kuna haja ya yeye kurudi chuo na kusomea kozi hiyo ili kuongeza ujuzi zaidi.

kutoka katika chuo cha NCT waliandika haya baada ya shishi kuondoka chuoni hapo” siri imefichuliwa na shishi mwenyewe  mmiliki wa mgahawa wa shishi food kuwa kumbe mambo yanalipa sana , ila yeye hakusita kufika chuoni hapa NCT kuiongezea thamani ya chakula chke kwa kupata dondoo  juu ya ukarimu na ufahamu kuhusu  ujasiriamali lakini pia  utaalamu katika maswala ya food production.

alisema kuwa atakuja yeye na team yake kupata kozi fupi , ulikuwa ni wakati mzuri kukutana na anayeitumikia sekta ya ukarimu wake  na wale wanaojiandaa  nafasi bado ni nyingi , hataki  ujinga wa kupishana na fursa.aante sana shishi kwa kupata nafasi ya kutembelea hapa.

Shiloleh anawekwa katika list ya wasanii wanaojituma na kufanya kazi buoa kukata tamaa hasa  kutokana na kuamua kufanya muziki na mapishi kwa wakati mmoja.

Sio kwa Sababu Msanii Basi Ukae Ndani Kama Mtoto:-Shiloleh

Msanii wa kike nchini , shiloleh anaweza kuwa ni moja ya wanawake jasiri na wenye moya wa pekee,hii haimaanishi kuwa wengine hawapaswi kupewa pongezi hizi, lakini pale mtu anapofanya jambo zuri kwa jamii ni bora kumsifia na kumpa pongezi zake ili wengine waige na pia kuendlea kumtia moyo mhusika.

Katika msiba wa Agness Masogange, msanii Shilole aliwahi kufika kwenye msiba huko mbeya pamoja na kwamba alikuwepo pia Leaders Club kwa ajili ya kuaga mwili wa marehemu . alkini hata alipofika jijini mbeya shilole alionekana kuwa busy sana hasa upande wa jikoni,

Shilole mwenyewe anakwambia kuwa yeye ni mtoto wa kiek hivyo isngekuwa rahisi kukaa ndani tu wakati kuna kazi nyingi nje zilikwa zikitakiwa kufanyika hasa katika swala la kupika.Shilole aliweka umaarufu na usanii pembeni na kuamua kuingia jikoni kusaidia wanawake wengine.

hii ni kazi ya wanawake , ukiwa msanii sio kwamba lazima ukae ndani tu , wewe sio mtoto kwamba unatakiwa kukaa ndani tu lazima ujishughulishe na wanawake wenzio, kwaio mimi nilivyofika tu nikauliza jiko liko wapi,kabla ya kuzika inabidi watu wale na kuna wengine waliopoa hapa pia ni watu wanahitaji msaada.uUkiwa mwanamke ni lazima ukae na wanawake wenzio ufanye kazi.

Shiloleh Afikishwa Mahakamani Kwa Kosa la Utapeli.

Msanii wa mzuki wa kizazi kipya nchini, zuwena mohamed maarufu kama shiloleh amefikishwa mahakamani leo kwa kosa la kuchukua  pesa ya shoo  kiasi cha shilingi milioni 3 ikiwa ni  pesa aliyokuwa amelipwa kwa ajili ya kufanya shoo lakini siku ya tukio msanii Shiloleh alishindwa kuonekana katika shoo hiyo na kushindwa kutoa taarifa kwa waandaji wa shoo hiyo  kwa muda muafaka,hivyo kusababisha hasara.

Shiloleh amefikishwa katika mahakama ya Mwanzo manispaa ya Kinondoni leo na kupewa hukumu ya shilingi mil 14, ikiwa ni pamoja na fidia ya kumsababishia hasara Mama  Mary Musa  aliyemlipa kwa ajili ya kufanya shoo siku ya pasaka mwaka 2017  Mbagala Kijichi ambapo baada ya kulipwa alishindwa kufika ukumbini hapo kwa muda hivyo mashabiki na wapenzi wa burudani kushindwa kuvumila na kupandwa nahasira iliyosababisha kuvuja na kuharibu mali.

Kwa mujibu wa GPL, shiloleh alipofanya kosa hilo alitakiwa kurudisha pesa hizo lakini alikuwa akipuuza agizo hilo la mahakama kwa muda wote ndipo mama huyo alipoamua kufatilia zaidi na hukumu kutolewa leo kuwa ndani ya wiki moja Shiloleh anapaswa kulipa fidia hivyo na kama hatashindwa basi mali zake zitashikiliwa na mahakama.

Shiloleh amefika mahakama hapo akiwa na mume wake uchebe lakini baadae alianza kuangu akilio baaada ya hukumu kutolewa.

 

Shiloleh Afunguka Anachopenda Kwa Uchebe

Msanii wa musiki wa bongo fleva shiloleh amefunguka na kutaja mambo anayoyapenda kwa uchebe na jinsi gani amekuwa moja ya wanaume wanaomsapoti na kumjali sana kimaisha pamoja n kwamba watu wamekuwa wakisema kuwa hawatadumu kutokana na ukweli kwamba mara nyingi  amekuwa hadumu na wanaume katika mahusiano.

Shiloleh anasema kuwa anashukuru mungu kwa sababu pamoja na skendo nyingi alizowahi kuzipitia kabla ya kumpata uchebe lakini ameweza kukubalika ukweni (kwa wazazi wa uchebe).

ninashukuru mungu sana wakwe zangu ni wacha mungu na wananielewa sana na mimi ninawaelewa sana,hawapendi kusikiliza maneno ya watu wanatambua muda wa kazi ni upi na  na muda wa nyumbani ni upi hivyo tunaishi kizungu.

Hata hivyo shiloleh anaendelea kwa kusema kuwa kipindi cha nyuma alikuwa hajatulia kwa sababu alikuwa anatafuta mwanaume wa kutulia nae ila kwa sasa anatulia kwa sababu anaamini kwa uchebe ndio amefika.

unajua kipindi cha nyuma watu niliokuwa nao wote walikuwa wanataka niendelee kujichetua,sikuwa na mtu sahihi wa kuniongoza lakini nilipompata uchebe tu alianza kuwa ananikosoa, na kunirudisha katika msati ulionyooka, na ndio maana sasa hivi nimebadilika sipo kama zamani.

nilikuwa nahitaji mtu ambae atakuwa ananikosoa pale ninapokosea kila mara,lakini pia mtu ambae atakuwa ananijali mud wote na hivyo vitu nilikuwa nakosa mara ya kwanza.

Shiloleh aliendelea kumsifia mwanaume wake kwa kusemakuwa watu wanaweza wasielewe kila kitu anachoongea lakini anapenda sana kumuona Uchebe akicheka.

macho ya uchebe mie hoi,napenda sana tabasamu lake hasa pale anapocheka meno yake yote huwa hayaonekani.kwa mtu wa kawaida hawezi kuelewa lakini napenda  macho yake akitabasamu.

Shiloleh Ajutia Vivazi vya Mitandaoni

Kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia , biashara nazo zimekuwa na watu wamekuwa wakiweza kuagiza bidhaa katika mitandao kwa kupitia simu na bidhaa zinakuwa zinafika pale zinapohitajika.

Msanii wa bongo fleva , Shiloleh wikiendi hii alizua gumzo katika mitandao baada ya nguo alikuwa amevaa katika special party ya WCB kumuacha maziwa wazi na kuoneka kama haijampendeza kwa tukio kama hilo.na hata katika mitandao ya kijamii watu wengi walianza kumsimanaga kwa kitendo chake cha kuvaa gauni kama hilo.

Lakini kama kawaida ya Shiloleh sio mtu wa kuficha mambo, baada ya kuona watu wamemzungumzia sana hakusita kutoa dukuduku lake kuhusu nguo hiyo ambayo iliwaacha watu midomo wazi kwa kumsema.

Shilloleh alisema kuwa nguo hiyo alikuwa ameiona katika mtandao na kuiagiza kwa lengo la kuivaa akiamini kuwa atapendeza na kutokea kama alivyoiona kwenye picha kama ilivyo kawaida ya watu wengi wakiamini kuwa nguo hizo zitawatoa kama walivyoziona katika mtandao.

Katika ukurasa wake wa instagram shiloleh aliweka picha hiyo na kuandika “yaani kama nitaagiza mimi nguo mtandaoni tenaaaa………..wallah lbda mimi sio dada Mwajuma.”

                                                  

Alichokiandika shiloleh baada ya kupokea maoni mengi juu ya muonekano wake .

                                                     

Muonekano wa Shishi baada ya kuvaa nguo aliyoiagiza mtandaoni.

Billnass Ampa Uchebe Dhana za Kupambana na Nuh Mziwanda

Msanii Billnas amemzawadia uchebe zawadi ya vifaa vya kufanyia mazoezi huku akimwambia kuwa amefanya makusudi kumleta vifaa hivyo ili aweze kufanya mazoezi na kuwa fit ili aweze kupambana na watu wanaomfatilia mkewe Shiloleh hasa msanii mwenzao Nuh Mziwanda.

Jumamosi wikiendi iliyopita Uchebe na Shiloleh walifanya weddingparty baada ya kufunga ndoa mwezi mmoja uliopita,party hiyo ilifanyika masaki jijini Dar es Salaam ilikuwa ya kufana sana na walikuwepo  wasanii wengi wakiwemo wasanii wa kundi kubwa nchini la Wasafi likiongozwa na meneja wao Diamond platinumz.

Wakati wa kuto zawadi kila mmoja alikuwa na chake mkononi lakini kwa upande wa bilnass aliona isiwe shida bali kumsaidia uchebe kuwa fit kwa kumpa  ahadi ya kumtafutia vifaa vya mazoezi huku akimwambia afanye mazoezi ili apambane na Nuh mziwanda.

najua mwanangu ashrafu anapenda nini,anapenda michezo ya ngumi kwaio na mimi kwa kulitambua hilo  na mimi nitamzawadia vifaa vya mazoezi kwa ajili ya fitness.ufanye mazoezi hata ya kupambana na kina nuh mziwanda , sisi watoto wa kiume inabidi kujilinda pale inapobidi.-Alisema Bilnass.

Ukiachna na vikwazo vingi walivyopitia shiloleh na uchebe mpaka kufikia hatua ya kukamilisha ndoa hiyo ikiwani pamoja na kukataliwana baaadhi ya ndugu na kusema sana katika mitandao, Nuh Mziwanda alikuwa ni mmoja wa watu waliokuwa wakiliandama sana penzi la wawili hao mpka kufikia hatu ya kutaka kuwagombanisha kwa kuvujisha picha za uchonganishi.

Nuh mziwanda alikuwa mwanaume wake na shiloleh kabla ya kukutana na uchebe, nuh alikuwa ni moja ya kikwazo sana kipindi cha maandalizi ya harusi ya wawili hao kupelekea hadi kufunga ndoa kimyakimya.

Siku hiyo ilikuwa ni moja ya siku ya bahati kwa msanii shiloleh na mme wake uchebe kutokana na zawadi nyinge walizpokea kutoka kwa wasanii wenzao  ikiwemo gari,ahadi za kusaidia katika kazi na ada za shuke kwa watoto wake.Wasanii wengi waliohudhuria waliwatakia maisha mazuri na yenye baraka katika katika ndoa yao .TUNASEMA HONGERA KWAO.

 

 

 

Viongozi Wa Dini Walimshauri Shiloleh Ndoa Ya Kimyakimya

Msanii wa muziki wa bingo fleva nchini zuwena mohamed maarufu kama shiloleh amefunguka na kusema kuwa kufunga ndoa ya kimya kimya alishauriwa na viongozi wa dini na ndio maana ndoa yake ilikuwa haijatangazwa ingawa watu walikuwa wakijua kuwa atafungua ndoa.Lakini pia shilole anasema kuwa upinzani alioupata kutoka kwa dada yake ambae hakutegemea kwa sababu alikuwa mtu wa karibu nae ulimfanya kufunga ndoa kwa haraka zaidi.

Shiloleh alisema kuwa viongozi wa dini walimshauri kuwa ndoa haitangazwi kwa sababu kuna watu wanaweza kuwafanya kubadilisha maamuzi yenu na mkashangaa ndoa ikabadilika na ikashindwa kufanyika kabisa.

Niliambiwa kuwa sio kila mtu anapenda kusikia jambo jema hilo, wengine wanaweza  kukufanyia husda ili jambo lako jema lisifanikiwe  kwaio nikaamua kuwasikiliza lakini sio kwamba sitafanya sherehe. –Alifunguk Shiloleh

Akiongelea swala la dada yake kumkataza kufunga ndoa na mwanaume wa ndoto zake shilole anasema kuwa

Unajua haya mambo ni ya kifamilia, lakini mimi ninawatoto wawili kwaio hawezi kunipangia  mwanaume wakuolewa nae. Alisema Shishi baby.

Hata hivyo shiloleh anasema kuwa pamoja na kwamba ndoa ilifanyika kimya kimya lakini anatehemea kufanya sherehe kubwa itakayo kata na shoka na wale watu wake wa karibu wote watahudhuria na kufahia sherehe hiyo ambayo amehaidi kutangaza hivi karibuni huku ikisemekana kuwa sherehe ya ndoa hiyo itafanyika December 25 mwaka huu.

shilole alifunga ndoa na Uchebe , mwanaume ambae inasemekana pia kuwa alimuacha mke wake kwa ajili ya shiloleh na kuamua kumpa talaka mwanamke aliyekuwa nae kwa kipindi hicho.Hata hivyo mapenzi yao yamedumu mpaka sasa wameamua kufunga ndoa.

 

 

Shamsa Ford Ampa Darasa La Ndoa Shiloleh

Mwanadada mrembo anaejihususha na bongo movies lakini pia ni mjasiriamali maarufu baada ya kuijingiza huko baada ya kuolewa na mpenzi wake Chid Mapenzi, amefunguka na kumsahuri mwanadada Zuwena maaarufu kama Shiloleh jina la kisanii juu ya maisha ya ndoa aliyoyaanza hivi karibuni.

Shiloleh amefunga ndoa na mpenzi wake wa muda mrefu kidogo anaejuliakana kwa jian la Uchebe wiki iliyopita ndoa ambayo ili-trend sana katika mitandao baada ya kuwashangaza watu wengi amabo walihisi kuwa ndoa hiyo haitaweza kufungwa kutokana na migogoro iliyojitokeza hivi karibuni baada ya kuvuja picha zikimuonyesha mwanadada huyo akiwa na mpenzi wake wa zamani ambae pia ni msanii mwenzie Nuh Mziwanda .

Shamsa Ford  akitumia uzoefu wa ndioa yake aliyofunga mapema mwaka huu amemshauri Shiloleh  kutulia katika ndoa yake  na kuachana na sifa za kuwa maarufu kutokana na usanii wake bali atulie ili kuweza kufaidi matunda ya ndoa yake.

Katika ukurasa wake wa instagram Shamsa ameamua kufunguka kuhusu swala ilo na kumpongeza kwa uamuzi aliouchukua

Hongera sana mama umefanya maamuzi sahihi ya kumpendeza Mwenyezi Mungu cha muhimi uwe mke bora wa kitanzania kwa mumeo na ustar uache pembeni ‘mumuweke Mungu mbele yenu,uvumulivu na kuheshimiana Inshallah mtazikana,karibu kwenye chama mama …sasa nyie mnaosubiri matajiri wawaoe wakati matajiri wana wake zao  mtasubiri sana mpaka uso  uote sugu,uzuri  na ustar uana mwisho wake  itafika muda hata inzi hakusogelei. HONGERA MAMA

Alichokiandika shamsa ford katika ukurasa wake wa instagram

Mwisho huu w mwaka umekuwa mwaka mzuri kwa baadhi ya wasanii ambao wameamua kuachana na ukapela na kujiingiza katika maswala ya familia.PONGEZI NYINGI KWA SHILOLEH NA MUME WAKE.

 

Shilole na Uchebe Kufunga Ndoa Hadharani,Hakuna Kadi Ya Mwaliko.

Kwa muda sasa kumekuwa na  gumzo  mitadaoni kuhusu ndoa ya mwanadada Shiloleh na mumewe mtarajiwa  anaejulikaa kwa jina moja  la Uchebe. Wiki kadhaa zilizopita Uchebe alithibitisha kufanyika kwa ndoa hiyo mwaka huu mwezi Disemba na kuwa honeymoon atampeleka mke wake huyo mtarajiwa Ulaya.

Nae bibi harusi mtarajiwa amefumnguka na kusema kuwa ni kweli ndoa yao itafungwa hivi karibuni lakini haitakuwa kama ndoa zingine za wasanii ambazo ufanyika kimya kimya.Shilole ameongezea na kusema kuwa  katika ndoa yake haitakuwa na kiingilio wala mchango wowote hivyo yoyote anaetaka kuja atakuwa na uhuru wa kuhudhuria na itafanyika mahali peupe bila siri yoyote kama wanavyofanya wengine.

Ndoa yangu sitafanya ya siri kama mabvyo wamekuwa wakifanya wengine,nitafaya sehemu ya wazi kabisaa na wala hata  haitakuwa a kiingilio hata kidogo.napenda ndoa yangu ionwe na watu wote na kila mtu aweze kuhudhuria  na aoene kila kitu kinachoendelea.

Shiloleh amesema kuwa mpaka sasa ndoa hiyo  ina uhakika wa kufanyika  na amethibitisha kuwa mwanaume wake tayari ameshatoa mahali kubwa nyumbani kwao na ameshatambulika hivyo mipango ya harusi ndio inafanyika kwa sasa.

Shilole na Uchebe wamekuwa katika mahusiano kwa muda mrefu wa zaidi ya miezi sita sasa ambapo Uchebe aliachana na mke wake wa kwanza wa ndoa kwa kumpa talaka kwa madai ya kuishi na Shiloleh.Hata hivyo wawili hao ambao mpaka sasa wanafanya mpango wa kufunga ndoa wamekuwa wakikumbana na mameno mengi katika mtandao kutokana na mashabiki wa mwanadada huyo kuwa wanamsema anatembea na mwanaume aliye chini ya umri wake.

Shilole ni moja ya wasanii wa kike ambao wamekuwa ni mfano wa kuigwa kupitia kazi  anazofanya.Ukiachana na kazi ya muziki anayofanya ambyao ndio ilimtambulisha kwa mashabiki wake, Shiloleh pia aliona fursa ya kufanya biashara ya mama ntilie na ameweza kujitoa kotekote kwa kuwahudumia wateja wake wa chakula na mashabiki zake katika muziki.Hata hivyo  Shilole ameweza kumudu majukumu yote kulingana na mahitaji ya watu wake.

Shiloleh Na Uchebe Kufunga Ndoa,Honeymoon Ulaya

Mume mtarajiwa wa msanii Shiloleh, mwanadada ambae amekuwa ni moja ya wanawake wapambanaji katika maisha  amefunguka na kuongelea mipango yao ya harusi inavyokwenda na jinsi harusi iyo itakavyo fanyika.Mwanaume huyo anaejulikana kwa jina moja la Uchebe amesema kuwa mpiango ya  harusi ipo karibuni lakini nia yake kubwa katika harusi hiyo ni kumpeleka mke wake huyo Ulaya kwa ajili ya honeymoon yao.

Akiongea na East Africa, Uchebe amesema kuwa ndoa yao hiyo inategemewa kufungwa mwezi wa kumi na mbili(12) mwaka huu  kwa sababu yeye na mkewe mtarajiwa wameshakubaliana kabisa na taratibu za ndoa zimeshaanza kufanyika  na wanataka kuhararisha mahusiano yao.

“Mwenyezi Mungu ameshafanya wepesi  sasa hivi tupo katika  kwenye maandalizi, na Mungu akipenda mwezi wa kumi na mbili itakuwa ndoa kamili kwani taratibu zote nishazifuata,mahari nishatoa sidaiwi kabisa na honey moon nampeleka Ulaya” amesema Uchebe ambae ndie mume mtarajiwa wa Shiloleh

Uchebe ambae sasa hivi ni mume mtarajiwa wa Shiloleh, alishawahi kuwa na ndoa kabla ya hii inayoenda kufungwa sasa, ambapo inasemekana kuwa ndoa hiyo ilivunjika baada ya mwanaume huyo kuingia katika  mahusiano  na Shiloleh.

Ingwa kwa hivi karibuni pia kulikuwa na tetesi za wawili hao kuwa wameachana baada ya Shiloleh kusema kuwa yeye na vi-ben ten sasa basi, taarifa za kuachana kwao wamezikanusha na kusema bado wanaendelea  na mahusiano yao na kwa sasa wapo katika mipango ya harusi.

Mwanadada Shilole ni moja ya wasanii wa kike wenye kupendwa na mashabiki wengi sana lakini pia ni moja ya wasanii wenye ushawishi  mkubwa sana  kwa mashabiki wake.Ukiachana na kazi ya muziki anayofanya Shiloleh pia ni mama ntilie anaepika chakula mwenyewe na kuwahudumia wateja wake mwenyewe.Amekuwa ni mwanadada anaeangaliwa sana na watu na kuwa mfano wa kuigwa kwa watu wengine.

Ingawa kumekuwa na maneno yanayomkabili kuhusu tabia yake ya kutemba na vijana wenye umri wa chini yake , lakini hajawahi kuathirika na maneno hayo zaidi ya yeye kupiga kazi ili kuwaridhisha masbabiki wake.

Shilole Kuachana Na Vi-ben Ten

Mwanadada mrembo kabisa, jasiri na mpambanaji, anefanya vizuri katika muziki wake, Zuwena Mohamed  almaarufu kama Shilole, amefunguka na kusema kuwa kwa sasa hivi mapenzi na vi-ben ten anasimama kwanza kwa sababu havimpi faida yoyote.Shilole amefunguka na kusema kuwa alichogundua na kwamba hakijikita katika mapenzi hayamzalishii chochote lakini akijikita katika kazi anaona matunda yake hivyo kwa sasa bora afanye kwanza kazi.

“Jamani kwa usawa huu mtu hasipobadilika  na kuangalia kitu cha maana ni shida sana, mimi binafsi  mambo ya mapenzi sijui na vi ben ten vikae kwanza  vinisubirie kwanza huko, nifanye kazi zangu ili nipate kwanza maendelea yangu, sio mapenzi wanafaidi watu wa instagram tu,kukuangalia kila siku maisha yako.” alisema Shilole

Shiloleh ni moja wa wasanii wanaoingia kwenye kundi la wanawake wanaojiingiza kwenye mapenzi na vijana wanao wazidi umri,kwa  kipindi kirefu mwanamuziki huyo amekuwa akikumbwa na scandal za kutembea na vijana wanaowazidi umri na kuwatesa kwa sababu tu anawapa ela, mfano alishawahi kuwa na mahusiano na msanii mwenzie Nuh Mziwanda na baadae walikuja kuachana ambapo Nuh aliongea mambo mengi ya mahusiano yao ikiwa na lile la kuwa kipindi cha mahusiano yao alikuwa  hana sauti kwa mwanamke huyo.

Shiloleh  ambae kwa sasa yupo na uhusiano wa kimapenzi na kijana  Uchebe   inasemekana kuwa alikuwa  mume wa mtu lakini alikuja kumuacha mkewe kwa talaka kwa sababau ya kuishi na  Shiloleh pia ni kijana mwenye umri mdogo kuliko mwanadada huyo.Wawili hao wamekuwa wakionekana kuwa pamoja kwa muda mrefu na kusema kuwa hawategemei kuachana.

Ukiachana na kazi ya muziki, Shilole aliona fursa ya biashara ya chakula kwa upande mwingine na kuamua kuisogelea, biashara ambayo inamfanuy akukutana na mashabiki wengi zaidi na kuwa karibu na wateja wake pia.Pamoja na maneno mengi yanayozunguka mitandao juu yake Shiloleh ni mwanamke jasiri na anaeyeonekana kupitia mengi kwenye maisha kabla ya hapo hivyo kwa sasa yeye amuamua kufanya kazi tu.

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.