Muna Love Arudi Tena Vitani Na Baba Patrick

Rose Alphonce maarufu kama ‘Muna Love’ amerudi tena kwenye headlines ikiwa ameingia tena kwenye mvutano na aliyekuwa mume Wake Peter Komu ‘Baba Patrick’ huku Safari hii wakipelekana

Gazeti la Ijumaa linaripoti kuwa Muna Love alikwenda mahakamani ili kudai talaka yake na kugawana vitu ambavyo walichuma pamoja walipokuwa wote.

Unajua ninamshangaa sana Muna, amekwenda mahakamani, anasema ile nyumba ni ya kwake, lakini wauzaji wa kile kiwanja wapo na kama haitoshi hadi mafundi waliojenga wapo kwa hiyo tuiachie mahakama ifanye kazi yake. Talaka sawa, kama yeye ameamua, siyo mbaya kwa kuwa hawapo pamoja kwa kipindi kirefu. Kwa hiyo kama anadai talaka ni sawa tu, kwa kuwa tunasikia anahitaji kuwa huru na pengine anataka kuolewa na mwanaume mwingine”.

Baada ya tetesi hizo Gazeti la Ijumaa Lilimsaka Peter ambaye alifunguka haya kuhusu tetesi hizo:

Ni kweli nilikwenda mahakamani Magomeni (Dar) na Muna. Anataka mgawano wa mali na talaka. Ninachojua talaka zina process (taratibu) zake, lakini kesi ni tarehe 20 ya mwezi ujao (Februari) hivyo Muna anatakiwa afike na mashahidi“.

Muna na Peter waliingia kwenye mgogoro tangu walipofiwa na mtoto wao, Patrick ambapo kuliibuka mkanganyiko na sintofahamu ya kujua baba halisi wa mtoto kufuatia uwepo wa baba mwingine, Casto Dickson.

Muna Afungua Patrick Foundation ya Mwanae.

Mwanadada Muna love amefanikiwa kufungua Foundation yake itakayo itwa Patrick Foundation ambayo itakuwa na kazi ya kusaidia watoto wenye matatizo mbalimbali katika jamii huku lengo kubwa ikiwa ni kwa ajili ya kuwasaidia  na pia kumkumbuka mtoto wake.

Muna amekuwa akiguswa sana na kutokuwepo kwa mtoto wake huyo ambae  alifariki mwaka huu, hivyo Muna aliamua kufanya hivyo kama kuguswa na watoto wanaoteseka mitaani .

Dhumuni la muna inadhihirika sana pale aliapoanza kutembea mikoa mbalimbali kwa ajili ya kusaidia watoto hao  waliopo mitaani na wale walio wagonjwa ambao wamekuwa wakikosa misaada ya kiafya na pia kielimu.

 

 

 

Muna Awachana Wanaotaka Kujua Undani wa Maisha Yake.

Msanii wa Filamu chini, amefunguka juu ya watu wanaotaka kujua kila kitu katika maisha yake moja ya maswali hayo ni kuwa anafanya kazi gani na hela anatoa wapi? Muna kupitia ukurasa wake wa Instagram, amechapisha kuwa inatakiwa wajiulize amewezaje kupita katika moto mkali wa maumivu na kwa muda mchache yuko imara.

“Kama mwanamke unaejiamini lazima ujitambue wewe ni nani?Na unataka nini?Haijalishi umeumizwa kiasi gani na umekosa tumaini kwa ukubwa gani. Kuwa na furaha ni jukumu lako wewe mwenyewe,” amesema Muna.

“Hili swali kila siku mnaniuliza sijui hufanyi kazi ila unaela ?sijui mliziona wapi? unafanya biashara gani? , kila kitu mnataka kujua naomba Jambo moja ambalo mnatakiwa hasa kujua ,mjiulize nimewezaje kupita kwenye moto mkali na wamaumivu kwa Muda mchache na niko imara ?, mnazani ni mimi peke yangu ningeweza au nigejikwamua hapana , kuna mkuu kuliko wanadamu ndiyo anaenipa Jeuri na kufanya vile nyinyi mnavyoniona mpaka kuna wakati na mwambia Baba mi nakosa cha kuwajibu hawa zaidi ya kuwambia kwa Yesu kutamu.na apo Baba Ameni busti tu bado ajaachilia vya kuwashangaza ndo mtaelewa…. Njooni kwa Yesu mfurahi milele.”

Wolper Amwaga Povu Zito Kisa Muna

Muigizaji wa Bongo movie na mwanamitindo maarufu Jacqueline Wolper amejikuta akiporomosha mvua ya matusi pale alipoulizwa kuhusu sakata la Muna.

Muna ametawala vichwa vya habari kwa wiki kadhaa kufuatia skendo yake ya kumtelekeza mtoto wake wa kwanza anayeitwa Brian na majibizano a familia yake Kwenye vyombo vya habari.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Jacqueline Wolper amewajia juu watu wanaoingilia ugomvi wa familia za watu wanaowaona Kwenye mitandao ya kijamii.

Watu wa Instagram ni washenzi na hawajielewi, tena ni wapuuzi na wapumbavu. Kazi kufuatilia maisha ya watu tu, kwa nini wasimuache Muna mambo yake na familia yake, kila mtu abebe msalaba wake”.

 

Sakata La Muna Kutelekeza Mtoto Lachukua Sura Mpya

Siku mbili zilizopita stori iliyotawala Kwenye mitandao ya kijamii ni Tetesi za Mwanamuziki wa nyimbo za Injili Rose Alphonce maarufu kama Muna Love.

Global Publishers waliripoti kuwa ndugu wa karibu wa Muna ndio wamemnyooshea kidole kwa kitendo chake cha kumtelekeza mtoto wake Nyumbani kwao Moshi.

Baada ya taarifa hizo kuzagaa Mtandaoni Muna alikana kabisa na kusisitiza wanaosambaza taarifa hizo wana nia moja tu ya kumchafua ili aonekane mbaya.

Siku ya leo Muna Kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika kuwa Mtu ambaye amesambaza taarifa hizo yuko mikononi mwa polisi na ambaye amemtuma ni mama yake mzazi na dada yake:

 

Muna Akumbwa na Skendo Ya Kutelekeza Mtoto

Msanii wa nyimbo za Injili Rose Alphonce Nungu maarufu kama Muna Love amejikuta katika skendo nzito ya kutelekeza mtoto wake wa kumzaa.

Global Publishers wanaripoti kuwa pamoja na Muna kunukuliwa akisema kwamba Patrick alikuwa mwanaye pekee, lakini nyuma yake kuna madai kuwa alizaa mtoto mmoja wa kiume (jina linahifadhiwa kimaadili) mwenye umri wa miaka 13.

Katika mahojiano aliyofanya na Ijumaa Wikienda, Ndugu yaka na Muna alimwaga ubuyu kuwa, kitendo cha Muna kutangaza kuhudumia watoto wa watu wengine huku akimuacha mtoto wa kumzaa akiwa analelewa na watu wengine, kinawakwaza ndugu walio wengi.

Tunashangaa sana Muna huwa hamtambulishi kabisa mtoto wake mkubwa na nasikia alisema aliwahi kuzaa mtoto akafa wakati mtoto yupo hai na anatakiwa apate upendo kutoka kwa mama yake.

Kinachouma ni kwamba Muna sijui ataishi maisha ya kuigiza mpaka lini ilihali anawasaidia watoto wenye matatizo, hatukatai ni wajibu yeye kusaidia, lakini amwangalie na mtoto wake ambaye alimtoa katika tumbo lake. “Mtoto huwa anawaambia wenzake shuleni kuwa mama yake mzazi ni Muna na wenzake wanamwambia mbona hawajawahi kumuona akija kumwangalia? Mtoto anaishia kulia tu.

Baada ya Tuhuma hizo gazeti hilo lilimsaka Muna ili kupata ukweli wa mambo ambapo amekana kabisa taarifa hizo:

Hakuna Mtu Aliyeumizwa na Msiba Wa Patrick Zaidi Yangu-Muna

Mwanamuziki wa nyimbo za Injili na mdau mkubwa wa Bongo fleva Rose Alphonce maarufu kama Muna Love amefunguka na kusema hakuna mtu aliyeumizwa na msiba wa mtoto Patrick Zaidi yake kama mama.

Muna amefunguka kutokana na maneno ambayo amekuwa akikumbana nayo Kwenye mitandao ya kijamii ambapo watu wamekuwa wakimponda kutokana na maamuzi yake ya kutumia Kifo Cha mwanaye kama ushuda kanisani.

Siku ya leo Muna alifanya mkutano na waandishi wa habari kwa ajili ya kutangaza Tamasha lake la Kidini litakalofanyika siku ya Jumamosi na aliweka wazi kuwa atatoa ushuhuda wake kuhusu Kifo Cha mtoto wake Patrick.

Kwenye mahojiano na vyombo vya habari, Muna alijibu tuhuma za kumtumia mtoto wake ambapo alifunguka:

Kwanza hakuna mtu anayeweza kusema ameumizwa na Kifo Cha Patrick zaidi ya mama mzazi na mimi tangu niingie Kwenye wokovu naamini hakuna mtu atakayeweza kuishi milele kila nafasi itaonja mauti lakini mimi natumia mwanangu ili kubasdilisha watu Ikiwa mimi mwanangu amenibadilisha nilikuwa mtu wa ajabu nilikuwa natukana na kufanya mambo mengi ya ajabu lakini niangalie leo hii nilivyobadilika”.

Mtoto wa Muna, Patrick alifariki dunia miezi michache iliyopita baada ya kuugua kwa muda mrefu.

 

Muna Apewa Maono Ya Kusaidia Jamii na Marehemu Patrick

Msanii wa Bongo movie na mdau mkubwa muziki wa Bongo fleva Rose Alphonce maarufu kama Muna Love amefunguka na kutaja sababu ya yeye kujikita katika kusaidia jamii kwa sasa.

Muna amefunguka baada ya kuonekana akijikita sana katika kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu na magonjwa ni katika kumuenzi mtoto wake aliyeaga dunia mwezi uliopita.

Kwenye mahojiano na gazeti la Amani, Muna alisema kwa sasa watu wengi wamekuwa wakimuona akifanya shughuli mbalimbali za kusaidia wenye uhitaji, kazi ambayo ataifanya kwa kadiri ya uwezo wake wote kumuenzi marehemu mwanaye.

Nafanya hivi kwa sababu ni maono toka kwa Mungu, pia naona ndio njia pekee ya kumuenzi mtoto wangu kwa sababu yeye alikuwa na upendo na watoto wenziye, ilikuwa ukimpa kitu ale, hawezi kula lazima ampe na mwenziye na hata kama kipo kimoja basi yeye hatakula atampa mwenziye“.

Patrick mtoto wa Muna aliugua mwezi uliopita nchini Kenya alipoenda Kwenye matibabu baada ya kuugua kwa kipindi kirefu.

Sina Mpango wa Kuzaa Baada Ya Patrick Kufariki- Muna

Msanii na mdau mkubwa wa Bongo fleva Muna Love amefunguka na kuongelea maisha baada ya Kifo Cha mwanaye Patrick aliyefariki mwezi uliopita baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Zikiwa zimepita siku 40 tangu Mtoto wa Muna Patrick afariki Dunia, Muna anafunguka

Kwenye mahojiano na Global Publishers Muna amefunguka kuwa pamoja na kuwa 40 ya Patrick ilikuwa jana lakini yeye sio mtu wa kuweka 40 kwa sababu ni Mlokole:

Kwanza watu wafahamu mimi sina 40, nimeokoka na mwanangu kashaenda kwa baba yake nimemaliza, ila kwa sasa mimi bado nafunga tu mpaka nielekezwe nini cha kufanya lakini nashukuru nimeshaanza kuhudumia watoto wenzake ambao tayari wameanza kupata matibabu, nashukuru sana Mungu kwa hilo“.

Lakini pia Muna alifunguka na kuweka wazi kuwa hana mpango wa kuzaa mtoto mwingine:

Pengo kwangu hakuna nimeshasema Patrick, kamaliza kazi yake aliyotumwa na baba na mimi sasa hivi sina mpango wa kuzaa mtoto mwingine kabisa, nafanya kazi ya baba kwanza, ninachofanya sasa hivi ni kuwasaidia watoto wenzie matibabu basi”.

Muna amekana vikali Tetesi za kutaka Kuolewa na Joel Lwaga na kudai ni maneno maneno ya watu yeye hana mpango wa Kuolewa kwa sasa.

Muna Love warned by Tanzania Music Foundation for not completing divorce 

The Tanzania Music Foundation has warned gospel singer Muna Love who is currently in Kenya to preach.

According to the foundation, the singer needs to complete her divorce first from the father of her late son Casto Dickson. The singer was on the headlines a few weeks ago after her son’s death which saw his ex-lover and husband claim paternity of the boy.

According to Global Publishers, the foundation’s President Dr. Donald Kisanga explained that they have just heard stories about the two despite seeing them at every gospel event together.

“Tumekuwa tukisikia tu kwamba Joel na Muna wanaishi kinyumba lakini bado hatujapata ukweli wa hili jambo maana ni muda mrefu tunawaona wako kwenye kila huduma pamoja nasi tunawachukulia ni marafiki tu.” he said.

Take actions

He went on to add that they are currently investigating the case and if  it’s true, she will be barred from the foundation and from singing.

Muna love

“Sasa baada ya tetesi hizo kuzidi, kamati yetu ya maadili ipo kazini kwa sasa kufanya uchunguzi kama kweli wanaishi au walikuwa wanaishi pamoja au laa na endapo itathibitika kuwa ni kweli tutawafuta uanachama pia kuwafungia kuimba maana wanachafua waimbaji wote wa injili ambao wanaaminika ni watumishi wa Mungu.” he added.

“Tunamshauri huyo Joel kuwa makini kama huyo Muna kweli ni mke wa mtu na hajapewa talaka aachane naye hata kama ni mchumba wake kama inavyosemekana kwani akiendelea kung’ang’ania itamletea matatizo,” he said.

Muna Afunguka Kuhusu Ugawaji wa Nguo za Marehemu Patrick.

mwanadada muna love amefunguka na kuongelea swala linalosambaa katika mitandao ya kijamii kuhusu ugawajiwa nguo za mtoto wake aliyeafriki wiki chache zilizopita huku watu wakisema kuwa marehemu ameacha nguo nyingi sana kiasi kwamba wanashangaa muna atazipeleka wapi nguo hizo.

Huku watu wakijaribu kuraka kufuata mila na desturi za kawaida za kifamilia za kitanzania kuwamba kila baada ya 40 ya marehemu basi mali na kila alichoacha marehemu kinaweza kugawiwa kwa watu au kukabidhiwa mtu kwa ajili ya kukitunza , kukiendesha au kukimiliki basi hii ni tofaiuti kna kile anachokiamini muna kuhusu kila alichokiacha mtoto wake.

Muna ansema kuwa ajui chochote kuhusu 40 katika msiba kwa sababu ameshazika na amemaliza , anackofanya sasa ni kueneza neno la mung na kutoa ushuhuda, lakini pia hawezi kugawa nguo za mtoto wake hata kama zipo nying kwa sababu mtoto wake aliacha maona na inabidi yafuatwe hivyo haweiz kugawa nguo.

mimi ni mkristo , na mambo ya 40 siyajui, ninachojua mimi ukimaliza msiba tu unaendelea na mambo yako na kuhusu mavazi ya mwanangu sitayagawanya kwa sababu mwanangu aliacha maono na maono yake lazima yafuatwe.-Aliongea Muna akiwa nchini Kenya aliposema kuwa yupo katika kazi ya kulitukuza neno la Mungu.

“Muna ni Mwanamke Shupavu Sana”- Joyce Kiria

Mtangazaji wa kipindi cha ‘Wanawake Live’ na mpiganaji wa haki za wanawake Joyce Kiria amemkingia kifua Muna Love na kumtaja kama mwanamke shupavu.

Siku chache zilizopita Muna amekuwa akikosolewa sana baada ya kuonekana amerudi Kwenye maisha yake kama kawaida baada ya Kifo Cha mwanaye Ikiwa zimepita wiki chache tu.

Mashabiki wamemjia juu Muna kutokana na mavazi yake ambayo amekuwa akivaa na hata kuposti picha Kwenye mitandao ya kijamii na kuendelea na maisha yake kama kawaida.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Joyce Kiria amedai Muna yuko sahihi kwa hivi sasa anavyotoka na kuonekana kwenye mitandao kabla ya kumaliza 40 ya mtoto wake aliyefariki kwa sababu hana sababu ya kuendelea kulia na kujifungia ndani kama watu wanavyomtaka.

Mimi binafsi nampongeza sana kwa kile anachokifanya sasa hivi, inaonekana jinsi gani alivyo shupavu maana bila hivyo basi angekuwa anaishi kwa maumivu makali tena ya kumsababishia athari ndani ya moyo”.

Mashabiki walimjia juu Muna baada ya kuamua kuongea na waandishi wa habari siku chache baada ya Kifo Cha mwanaye na sasa ameonekana nchini Kenya na kuendelea na maisha yake kama kawaida wakati mtoto wake hjafikisha siku 40 tangu afariki.

 

Baada ya Msiba Mzito, Muna Aanza Kujirudisha Mitandaoni,

MUIGIZAJI Muna Love ambaye hivi karibuni alipata msiba kwa kuondokewa na mtoto wake, Patrick, amefunguka na kusema kila binadamu hupitia magumu lakini haimanishi kwamba Mungu anakuwa amekuacha badala yake anakufanya uwe imara na kumwonyesha shetani kwamba ‘wewe ni mtoto wake’.

Muna ametoa kauli hiyo kupitia akaunti yake ya Instagram na kumshukuru Mungu kwa yote aliyomtendea huku akisisitiza kwamba ataendelea kumtumikia muumba wake milele.

“Mungu anawapenda watu wote bila kujali wewe ni nani na unatabia gani mbele zake …na atatumia njia anazojua ili zikufikie na umtambue urudi kwake ukazaliwe upya… na hata pale anakupa jaribu sio kama hakupendi au anataka akuumize hapana, anakupa jaribu na pia anajua utaliweza na hatoweza kukuacha kamwe atakupa na njia za kupita.

“Mungu kwenye kila jaribu lile la aina yoyote jua yupo nyuma yako na anakukomaza ili kumuonyesha shetani kua wewe ni mtoto wake na anajivunia wewe sasa ,usiwaze kumuhukumu Mungu au kuumia kwanini umepitia hilo bali mshangilie na kumtukuza uone matunda atakayokupa ????????

“Asikudanganye mtu Mungu awezi kukuacha upitie gumu bila kukupa njia na roho mtakatifu akakuongoza asante Mungu wangu nitakutumikia milele,” amesema Muna.

 

Ray c Ampongeza Muna, Amwambia Ametua Mzigo.

Baada ya muna kuongea yaliyopo moyoni mwake kuhusu swala la marehemu mtoto wake Patrick   kusema wazi juu ya baba wa mtoto wake kuna watu waliongea mengi kila mtu akim-judge  Muna kwa lake huku wengine wakisema kuwa ameyafanya mapema sana mambo hayo alitakiwa kusubiri mpaka 40 ya mtoto huyo  ipite ndio aongee hayo.

Lakini wapo waliomtetea na kumuona kama alichokifanya labda kinaweza kumsaidia kukaa kwa amani lakini pia labda kingeweza kufunga midomo ya baadhi ya watu waliokuwa wakimhukumu bila kujua kwa nini yalitokea yaliyotokea.

Ray c ameguswa na maamuzi ya Muna na hivyo aliamua kuongea kuhusu swala hilo la kumpongeza kwa kumwambia kuwa aloichokifanya kimeweza kumuondolea mzigo wa maumivu yake aliyokuwa nayo kuhusu mtoto wake.

Una uhuru wa kuwa muwazi pale unapoona mambo fulani yamekuumiza au hayajakaa sawa,kuongea kuna kufanya nafsi yako inakaa sawa,safi muna ninaamini kuna kamzigi flani umekatua  kutoka kwenye moyo…good job.

Grieving Bongo singer Muna Love narrates how Mercy Masika helped her throughout her son’s sickness and in death

Muna Love recently lost her son Patrick Peter who was suffering from brain tumor. The late Patrick died at Nairobi West Hospital, he was in a coma for six days.

Speaking to journalists at her home in Mbezi, Tanzania, Muna Love praised Kenyan singer Mercy Masika for helping her throughout her son’s sickness and in death.

The Bongo singer reveals that it was Mercy Masika who linked her with the best doctor at Nairobi West Hospital;

“Tulipofika Kenya tulipokelewa na Mercy pamoja na mume wake. Kisha baada ya kukaa nao wakaniunganisha na Daktari mkubwa wa watoto nchini Kenya. Hivo tukaenda kumuona Daktari aliyeitwa Dr.Bore. Daktari akatupa maelezo ya kupata huduma katika hospitali za Nairobi. Kulingana na maelezo ya Daktari tukaona tutamudu huduma ya Nairobi West. Hivyo tukiwa kwenda hospitalini ili Patrick aanze matibabu,” Muna Love narrated.

The late Patrick Peter
The late Patrick Peter
Unwavering support

Muna Love says Mercy Masika also facilitated the transfer of her son’s body to the mortuary when he finally died. She says the ‘Mwema’ hit maker also made the necessary airport arrangements to transport the body from Kenya to Tanzania for burial.

“Baada ya kupata taarifa kuwa mtoto amefariki, Mercy pamoja ma mume wake walinisaidia kupata uhifadhi wa mwili wa mtoto. Kuna wengine pia kama vile akina DJ MO, Evelyne Wanjiru walichanga fedha ili niweze kusafirisha mwili mpaka Tanzania. Walinipeleka kwa Kampuni ya Lala Salama ambayo ilipewa jukumu la kuitoa maiti Nairobi West Hospital. Tulisaini mkataba wa kushughulikia mwili wa marehemu kisha tukakata tiketi za Ndege. Sikuweza kusafiri na mwili kwa sababu za clearance kule airport,” said Muna Love.

 

 

 

 

“Mimi na Wema Tutaenda Kumtembelea Muna Labda Tufukuzwe”- Steve Nyerere

Muigizaji wa Bongo movie Steve Nyerere ameweka wazi kuwa hana kinyongo na Muna hata baada ya povu alilomtolea Povu Kwa waandishi wa habari Lakini ameshapanga kwenda kumtembelea.

Sakata hili lilianza wiki chache Kwenye msiba wa mtoto wa Muna ambapo Steve alionekana kuingilia mambo ya kifamilia ya Muna na kutangaza Kwenye mitandao ya kijamii taarifa ambayo Muna amedai haikua ya kweli.

Lakini siku ya jana Steve ametangaza kumsamehe Muna na kudai anajua hiki ni kipindi kigumu kwa Muna kwani bado anamuomboleza mtoto wake hivyo haoni sababu ya kuweka kinyongo.

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Steve  amedai kuwa yote ambayo ameongea Muna siku ya jana kuhusu yeye sio ya kweli na tayari ameshamsaheme ambapo amepanga safari ya kwenda kumtembelea akiwa na Wema Sepetu.

https://www.instagram.com/p/BlaXDuthZLR/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=1lebqzhdtqbzi

Steve Nyerere Afungukia Sakata Lake na Muna Atangaza Kumsamehe

Muigizaji wa Filamu za kibongo na kiongozi wa Kamba hiyo Steve Nyerere ameibuka na kuongelea sakata lake yeye na Muna na kutangaza kuwa ameamua

Muna alipoongea na waandishi wa habari, alikanusha baadhi ya taarifa ambazo zilitolewa na Steve Nyerere zikidai kuwa muigizaji huyo amekubali kushirikiana na Mumewe Peter Komu katika kumzika mtoto Patrick ambaye Muna amekanusha kuwa sio wa Peter bali ni wa Casto Dickson.

Steve alifunguka siku ya jana Kwenye mkutano na waandishi wa habari ambapo ameamua kupangua hoja zote zilizotolewa na Muna ambazo zinamuhusu yeye.

Kwanza nimpe pole dada yangu Muna kwa kupita katika kipindi kigumu sana, kwa kuondokewa na mtoto. Tulikuwa tumejipanga kwenda kumuona, tukaambiwa kwa waliokoka huwa hawana 40, lakini kwa mzazi lazima kuwepo na 40. Mimi siyo mjinga wa kukurupuka tu kutangaza kuhusu msiba bila kuambiwa na wahusika wa msiba, sikukurupuka, mimi ni mtu mzima, nina familia na watoto, nilipewa maagizo hayo na Muna mwenyewe akiwa na ‘mumewe’ Joel Lwanga wakiwa Kenya, alinipigtia simu.

Nimemsikia akizungumza maneno mazito, eti nyumba anayoishi Peter haina hati, kama haina hati basi itakuwa ni ya serikali wakachukue nyumba yao. Anatukandamiza na kutoa voice, ametoa hisia zake kwa Watanzania, ametufundisha sisi vijana na wazee. Tukisema tufuatilie tutakuta mtoto uliyemsomesha hadi chuo kikuu ni wa mlinzi, mwanamke mwenye busara lazima awe na staha, ndoa siyo kitu cha mchezo jamani.

Nimemsamehe Muna kwa sababu hajui kama anachokizungumza anakifahamu. Hili liwe funzo kwa dada zetu, mimi nimemsamehe hata nikikutana naye asiogope kunisalimia, Shilole naye amemsamehe, usipoimamini biblia utamwamini sheria”.

Irene Paul Amkingia Kifua Muna

Msanii wa filamu za Kibongo, Irene Paul ameibuka na kumkingia kifua mwanadada Muna Love na kudai watu lazima waheshimu hisia za watu na kuweka mawazo yao pembeni.

Suala hili  limekuja baada ya sakata lililozuka jana baada ya Muna kufanya maongezi na waandishi wa habari na kuweka wazi kuwa Peter sio Baba wa marehemu Patrick na kumtaja Casto kama Baba Lakini pia aliweka wazi kuwa nyumba anayoishi Peter ni ya kwake na hati zote.

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Irene Paul amemtetea Muna na kuwaomba watu wamuache aongee anachotaka kuongea kwani bado yupo kwenye maonbolezo ya mtoto wake.

Mimi nina mawazo kama walivyo watu wengine lakini ningependa tuheshimu hisia za Muna kama mzazi ambaye ni muhusika Mkuu wa mtoto aliyefariki na Kwenye maisha kila mtu ana jinsi ya ku-deal na stress kuna wengine wanapenda kuongelea matatizo yao na wengine wanapenda kunyamaza kwaiyo lazima tuheshimu mawazo ya watu”.

Kikao hiko cha Muna na waandishi wa habari hakikuaa vizuri na baadhi ya watu waliohisi ni mapema sana kuzungumza kwani mwanaye amekufa wiki mbili tu zilizopita na mmoja kati ya watu hao ni msanii Shilole:

“Shilole Angetaka Kiki Angeenda Beach na Uchebe Wake na Kuvua Nguo Zote”-Nay Wa Mitego

Msanii wa MuzikiSana wa Bongo fleva Nay wa Mitego amemjia juu Msanii mwenzake Shilole baada ya kuingilia kati sakata la Muna na kumrushia maneno katika Interview mbali mbali.

Nay ameibuka na kumkingia kifua Muna na kumtolea povu Shilole na kudai anatafuta kiki Kupitia ishu ya Muna na hana lolote kingine linalomsumbua.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Nay wa Mitego alimuandikia ujumbe huu Shilole:

Shiloleeee Zainabuuu nadhani ulimiss tu Media dada yangu nadhani umefanikiwa kwa kiasi chake. Ulichokosea ni ishu uliyoingilia yaani gear  yako. Sioni alichokosea huyo unayemuita mdogo wako Muna ameongea mengi ambayo watu walitaka kujua nini kilichokuwa kinamsumbua Patrick.

Sasa ungetaka kiki mngeenda Beach na Uchebe wako mnavuana nguo zote alafu mbapiga picha halafu mnaposti bila hata caption halafu mtaona kiki yake ingekuwa noma.Lakini hili la Muna umejichoresha tu umeonekana ulikuwa unatafuta…..Mtazamo wangu tu”.

Sakata kati ya Muna na Shilole lilianza baada ya Muna kufanya Interview na kuweka wazi kuwa Casto ndiye Baba halali wa marehemu mtoto wake Patrick na mambo mengine ambayo yalionekana kutompendeza Shilole.

Ushauri wa Muna kwa Wanawake Wenzie

Mwanadada Muna love ameamua kutoa ushauri wa bure kwa wanwake wenzie wanaobeba mimba  za baba wengine na kuwapa wanaume wengine wazilee mimba hizo eti kisa wanaume waliowapa mimba wamekataa mimba zao.

Akiongea katika Press Conference aliyoifanya leo nyumbani kwake, Muna alisema kuwa wakati wa mazishi aliongea na casto na walikubaliana kuwa wayamalize matatizo yao na kukubali maiti kufikia nyumbani kwa peter kwa sababu tu walikuwa hawataki kugombana  na ndugu na walitaka msiba huo upite lakini sio kwamba mtoto Patrick ni mtoto wa Peter.

Muna anasema  Casto alimwambia “mama pati mimi na wewe tunaujua ukweli ila huwezi kuwabadilisha watu,nimekosea kwa nafis yangu naomba unisamehe kwa sasa hivi tujifanye wajinga tu ili mtoto haifadhiwe kwa sababu kosa tulilokosea ni kuandika jina la mtoto na jina la baba mwingine.

Baada ya kuongea hivi muna nawashauri wanawake wengine na kusema “mimi leo nakiri kwa wanawake wenzangu kuwa hata kama mwanaume mkiwa na mapenzi kiasi gani na una mimba ya mwanaume mwingine usikubali kumpa akalea tu.

Hata hivyo uamuzi wa muna kuongea na waandishi umepokelewa tofauti sana na watu mbalimbali huku wengi wwakisema imekuwa mapema sana kwake kuongea na waandishi kutokana na msiba mkubwa uliompata.

 

 

 

Shiloleh Amtolea Mapovu Muna “Utapata Tabu Sana”

Baada ya kuongea na waandishi wa habari, mwanadada Muna alisema mengi huku akisema kuwa anao uthibitisho wa kutosha kuwa mtoto wake patrick ni mtoto wa Casto na wala sio vinginevyo, huku akisema kuwa  hakuwahi kuwa na mahusiano na peter hata siku moja bali alikuwa akimchukulia kama baba yake na mtu wake wa karibu.

Kila mtu ameyapokea maneno ya Muna kwa hali tofauti lakini shiloleh ni moja ya watu walionhea mara tu  baada ya mahojiano hayo kuisha na kumshangaa sana muna kuwa amepata wapi nguvu ya kusimama na kuwaita waandishi wa habari mpaka kuja nyumbani kwake na kuongea kile alichokiongea .

Shiloleh anasema kuwa hata kama alichokiongea kina ukweli lakini hakupaswa kuonyesha au ku-prove chochote kwa mtu yoyote kwa sababu hata 40 ya mtoto wake ilikuwa bado haijafika.

Muna unaenda kuita press conference,ufanyiwe interviw for what, unafurahia nini, unawaia unawaambia nini na juzi tu umetoka kuzika mtoto wako.unataka kuthibitisha kuwa huyo mtoto ni wa casto hatutaki kujua, we dont need it…mimi ni dada yako kama ungekuwa na shda ungenifata tu kama unavyonifataga kwenye mengine…muna utapata tabu sanaa.

Shiloleh ameonyeshwa kusikitishwa sana na kitendo cha muna kumkana mume wake ambae amefunga nae mpaka ndoa kwa ujinga wake mwenyewe.

Muna Love Amkana Peter Kweupe, Asema Hakuwahi Kuwa na Mahusiano Nae.

Mwanadada Muna Love ameibua mazito baada ya kukana kumjua peter kama mume wake wa ndoa na kusem akuwa peter anamchukulia kama baba yake , kama rafiki yake na kama ndugu na wala sio tofauti na hapo.

Alipokuwa akiongea na waandishi wa habari, Muna alisema kuwa   hata ile nyumba ya Mwananyamala ambapo anakaa peter  na ndipo ilipofikia maiti ya mtoto wake Patrick  ni ya kwake na kwamba haikuwa na hati bali leseni ya makazi tu wala sio vinginevyo.

nyumba ya mwananamala ni ya kwangu na kila kitu kinachohusu mwananamala ni cha kwangu na hata document ninazo ile numba haina hati ila ina leseni ya makazi,mimi peter nilipokuwa nakaa nae alikuwa kama rafiki na kama mtu wangu wa karibu tu , tuliamua kufanya msiba wa baba pale kwa sababu mimi nilikuwa katika mahusiano na mtu mwingine.

 

 

 

 

Muna Amtaja Baba wa Patrick kuwa ni Casto

Mwanadada muna love amewaita waandisi wa habari mapema leo nyumbani kwake kwa ajili ya kuongea nao kuhusu maswala yaliyokuwa yamezuka katika mitandao ya kijamii baada ya kutokea kwa msiba wa mtoto wake.

Muna anasisistiza kuwa pamoja na kwamba alikubali mtoto wake kufikia nyumbani kwa Peter lakini iyo aiwezi kubadilisa ukweli kuwa patrick ni mtoto wa casto na wala sio mtoto wa peter kama ilivyokuwa  ikieleweka hapo awali.

Muna anasema kuwa kwa sasa yeye ameokoka na hawezi kusema uongo kuhusu ukweli wa marehemu mtoto wake.

 nimeokoka na nina muamini Mungu, na bado nitaendelea kusimama kwenye ukweli kuwa Patrick baba  yake ni Casto

Mke Mwenzie na Muna Afungukia Mahusiano Yake na Peter

Wiki chache zilizopita picha za mume wa Muna Love, Peter Zacharia na mwanamke mwingine anayeitwa Rehem zilisambaa Kwenye mitandao ya kijamii.

Picha hizo zilizowaonyesha Peter na Rehem wakiwa kwenye mahaba mazito kitandani zilisambaa na kusababisha maneno maneno ambapo Peter alikuja kuweka wazi kuwa aliyesambaza picha hizo ni Muna.

Rehema ameibuka na kuweka wazi kuwa zile picha hazina tatizo kwa sababu yeye na Peter wote ni watu wazima alafu Muna ndio alimuacha Peter.

Kwenye mahojiano na Global Publishers  Rehema amesema kwamba anamjua aliyezisambaza picha hizo ila kiufupi Muna atambue yule baba ni mtu mzima na yeye aliondoka kwa hiyo asingeweza kuvumilia kuishi bila ya kuwa na uhusiano.

Jamani Peter ni mtu mzima siyo mtoto, Muna atambue kuwa aliondoka kwake hivyo asingeweza kuishi mwenyewe“.

 

Peter Amtuhumu Muna Kwa Kusambaza Picha Zake Chafu Mtandaoni

Mzazi mwenza wa Muna anayejulikana kama Peter Zachariah amemjia juu mzazi mwenzake na kudai yeye ndiye mtu  aliyehusika kwa usambazaji wa picha zake Chafu Kwenye mitandao ya kijamii.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Peter alidai kuwa anajua wazi anayezisambaza picha hizo mitandaoni ni Muna kwa nia ya kumchafua kwa sababu Aprili, mwaka huu alirudi nyumbani kwake Mwananyamala-Kisiwani na kujifanya kuwa anapanga vitu vyake ndani ya nyumba hiyo kumbe nia ni kunasa picha hizo.

Unajua chochote kinachoendelea hivi sasa najua wazi ni mpango wa Muna, anajitahidi kuufanya ili mimi nionekane wa ajabu baada ya kuona watu walivyonichukulia tofauti kwenye kipindi chote cha msiba wa mtoto wetu hivyo anataka kunichafua lakini mimi kwa hilo sitetereki“.

Peter amekiri alikuwa Kwenye Mahusiano na mwanamke huyo baada ya kuachana na Muna na kumtaja kwa jina la Rehema na kudai kuwa Muna anamfahamu mwanamke huyo.

Kinachonishangaza mimi Muna anataka kujifanya huyo mwanamke ni mpya kwake lakini sio kabisa, anajua kila kitu na jinsi alivyokuwa akitangatanga kwa wanaume tofautitofauti, mimi ningeishi vipi kama mwanaume? Nafikiri anajua fika kwa kufanya hivyo atanichafua mimi kumbe anajichafua yeye”.

Mgogoro wa Muna na mumewe ulijulikana hadharani hivi karibuni mara baada ya mtoto wao kipenzi Patrick kufariki nchini Kenya alipokuwa amekwenda kutibiwa.

Mara baada ya Patrick kufariki, mjadala mzito uliibuka mitandaoni ambapo kuna baadhi walisema baba yake ni Mtangazaji wa Clouds TV, Casto Dickson aliyewahi kuwa mpenzi wa Muna lakini wengine wakasema ni wa Peter.

Muna alipotafutwa atoe neno kuhusu tuhuma hizo hakupatikana haraka. Siku chache zilizopita Muna alitangaza atafanya mkutano na waandishi wa habari na kujibu tuhuma zote.

Steve Nyerere Atangaza Kujivua Uongozi Wa Misiba

Muigizaji wa Bongo movie Steve Nyerere amefunguka na kutangaza kujivua Rasmi nafasi ya kiongozi wa misiba mbali mbali inayowahusu wasanii wa Bongo movie.

Steve amesema ameamua kujitoa katika nafasi hiyo kutokana na fedheha ambayo amekuwa akiipata kutoka kwa watu kutokana na nafasi hiyo.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Steve Nyerere amedai kuwa amekua akijitoa kwenye misiba ya wasanii wenzake lakini licha ya wema wake huo amekuwa akivuna skendo za ajabuajabu (kama ulaji fedha za rambirambi) na matusi jambo ambalo linamhuzunisha na kuiathiri familia yake.

Unajua mimi nina wa­toto, sasa wanapoona ya­nayoandikwa mitandaoni ya kunitukana na kunifedhehesha kwa vitu vya uongo wa­tanichukuliaje, niseme tu huu msiba wa mtoto Patrick Peter ambaye ni mtoto wa msanii mwenzangu Muna ndiyo wa mwisho, sitajihusisha tena na uongozi; kwenye misiba nita­shiriki kama mtu wa kawaida”.

Steve Nyerere amekuwa akirushiwa tuhuma mbali mbali na watu ambao wamekuwa wakimtuhumu kwa Kula rambi rambi ambapo juzi juzi ndugu wa Agnes Masogange walilalamika kuwa hawa kupokea rambi rambi tangu ichangishwe na Steve.

Muna Kuvunja Ukimya Kufuatia Kifo Cha Patrick

Muigizaji wa Bongo movie na mdau wa Muziki wa Bongo fleva Rose Alphonce maarufu kama Muna Love amesema yupo tayari kufunguka kufuatia Kifo Cha Mtoto wake.

Kwenye mahojiano na Bongo 5, amesema kwamba atazungumzia kuhusu ugonjwa wa mtoto wake, alivyoanza matibabu mpaka kifo chake pamoja na mambo mengine ambayo yalikuwa yanatokea.

Nisikilizwe nachotaka kuongea toka mwanangu ameumwa mpaka kufariki sikuongea kitu, Ni watu tu walikuwa wanaongea na kunihukumu, wiki ijayo nitazungumza na waandishi kuweka sawa yote”.

Wiki iliyopita Mtoto wa Muna aliyeitwa Patrick alifatiki dunia lakini gumzo kubwa lilizuka Kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari baada ya kutojulikana nani hasa Baba wa mtoto.

Wanaume wawili walijitokeza kama Baba wa watoto ambao ni Peter aliyejitambulisha kama mume wa ndoa wa Muna na Casto ambaye alikuwa anajulikana kama ndio baba wa mtoto.

Mgogoro huo ulisabisha mvutano kati ya familia ya Muna naya Peter kuhusu msiba ufanyike wapi lakini baadaye wawili hao walikubaliana msiba ufanyike kwa Peter na ndipo ratiba ya mazishi ilivyoanza mpaka malaika huyo wa Mungu kuzikwa katika makabduri ya Kinondani jijini Dar es salaam.

Mainda Aitupia Lawama Mitandao Ya Kijamii Kwa Sakata La Msiba Wa Patrick

Msanii Mkongwe wa filamu za kibongo (Bongo movie) Ruth Suka maarufu kama Mainda, ametupa lawama zake zote kwa mitandao ya kijamii baada ya sakata la mazishi ya mtoto Patrick.

Mainda amefunguka na kudai isingekuwa uwepo wa timu timu Kwenye mitandao ya kijamii basi anaamini mtoto Patrick angezikwa vizuri bila ya mashabiki kuingilia Familia ya watu.

Kwenye mahojiano yake na Global Publishers. Mainda alisema anaamini watu wa mitandaoni wamechangia kwa kiasi kikubwa kuweka taarifa za upotoshaji kati ya Muna na mumewe Peter ambazo zimesababisha wawili hao washindwe kuelewana haraka.

Jamani hivi ni vitu gani? Ndiyo maana mimi sipo kwenye mitandao nina sababu kubwa sana. Kuna upotoshaji wa hali ya juu na kama isingekuwa mambo ya matimu haya kusingetokea mvutano mkubwa uliokuwepo na kusababisha mambo mazito kwenye msiba wa mtoto asiyekuwa na hatia kabisa“.

Mvutano mkubwa ulitokea hasa kwa sababu ya mgawanyiko wa kifamilia lakini baadae walifikia uamuzi sahihi na siku ya Jumamosi mtoto Patrick alipumzishwa kwa amani.

Wema Atangaza Rasmi Kumaliza Bifu Na Muna

Muigizaji wa Bongo movie Wema Sepetu ametangaza Kumaliza rasmi bifu lake na aliyekuwa rafiki yake wa siku nyingi Muna Love ili waishi kwa Amani na Upendo.

Wema amefunguka hayo siku ya  Jumamosi, Julai 7, 2018 katika viwanja vya Leaders vilivyopo Kinondoni jijini Dar wakati wa kuaga mwili wa mtoto Muna, Patrick aliyefariki dunia Nairobi nchini Kenya, Julai 3 na kuzikwa siku ya Jumamosi katika Makaburi ya Kinondoni.

Pole zangu ziende kwa wazazi wa Patrick ambao ni Muna na Patrick, Muna ni rafiki yangu wa muda mrefu, nisingemjua Muna basi nisingemjua Patrick. Nilimpenda sana Patrick, japo sijabahatika kupata mtoto lakini nafahamu maumivu mnayopitia kwa kupoteza mtoto wenu“.

Muna pole sana, najua ulivyompenda Patrick, na mapenzi yako kwake ndiyo yametufanya hata sisi tuwe hapa leo, mimi huwa napenda sana watoto, najua hakuna mzazi anayependa kumzika mwanaye, ninaamini Mwenyezi Mungu atakupa nguvu wewe na baba Patrick.

Ninaomba tuyaache ya mitandaoni, najua mtoto wenu atafurahi huko aliko akiona mnaupendo na hakuna mgawanyiko kama huu ambao tumekuwa tukiuona. Muna unajua nakupenda na nitaendelea kukupenda, yaliyopita si ndwele tugange yajayo”.

Miaka miwili iliyopita Wema na Muna waliongia Kwenye bifu zito Kwenye mitandao ya kijamii na hata kuvunja urafiki wao.

Mazishi Ya Mtoto Wa Muna, Patrick Peter (+picha)

Mtoto wa msanii wa Bongo movie na mdau wa Bongo fleva Rose Alphonce maarufu kama Muna Love aliyeitwa Patrick Peter ameagwa rasmi siku ya Jumamosi katika viwanja vya leaders.

Patrick alifariki wiki iliyopita Nchini Kenya, Nairobi na kuzikwa siku ya Jumamosi katika makaburi ya Kinondoni.

Hizi ni baadhi ya picha za mazishi ya Patrick Peter katika makuburi ya Kinondoni:

.
.
.

Ndugu wa Peter Wamshukuru Muna Kukubali Suluhisho la Mazishi.

Baada ya mgogoro wa muda mrefu na baadae kufikia muafaka wa sehemu ya kuzika na wapi mait ya mtoto itafikia, ndugu wa baba mzazi wa mtoto patrick wamefunguka na kumshuru sana muna kwa uamuzi wake aliofkia wa kukubali kila kitu kiende sawa ili kumpumzisha mtoto  huyo.

Muna ambae hapo awali alisema kuwa patrick sio mtoto wa Peter bali ni mtoto wa Casto alikataa maiti ya mtoto huyo kufikia kwa Peter mwananyamal na kutaka ifikie nyumbani kwake mbezi lakini baada ya kufanbya maongezi ya muda mrefu huku steve nyerer akishughulika na hilo muna alikubali kila kitu,

akiongea na waandishi, Bazo Peter, mdogo wake na Peter amefunguka na kumshukuru Muna kwa uamuzi huo na kumtia moyo pia “tunamshukuru sana Muna love kwa kuwa na utu na hali ya uelewa  bada ya kuonea nae kupitiamarafiki zake wa karibu na ndipo alipotuelewa na sasa tuna amani kabisa.

patrick atafikishwa Dar Es Salaam siku ya ijumaa na kupelekwa mochwari ya mwananyamala ambapo siku ya jumamosi wataaga mwili huo Leaders club na baada ya hapo wataenda kuzika katika makaburi ya Kinondoni.

Steve Nyerere Amwagia Povu Zito Muna

Muigizaji wa Bongo movie na kiongozi wa moja wa wasanii wa filamu nchini Steve Nyerere amewajia Muna na Familia yake juu ya sintofahamu zinazoendelea hivi sasa juu ya msiba wa mtoto wa Muna , Marehemu Patrick.

Steve Nyerere amemvaa mama wa mtoto huyo (Muna) na kumwambia aache kuwayumbisha watu badala yake aungane na mume wake wa ndoa (Petere Zacharia) ili kusitiri mtoto wao kwa heshima kuliko kuwafaidisha watu kwa mameneno na mifarakano yao mitandaoni.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Steve Nyerere amemwaga povu hili:

Muna Muna Muna Muna Muna, naomba unisikilize popote ulipo, huu muda si wakufukua makaburi.
Wewe muna kwangu ni mama bora, ulimpenda mwanao ulisimama na mwanao mpaka kipindi cha mwisho. MUNGU akupe nguvu Muna.

Muna embu kaa tena chini jifikilie, ulitumia nguvu akili na maarifa yako yote na WATANZANIA wakatokea kukusapoti kwa namna moja ama nyingine. Kila mtu ameguswa na msiba wa mwanao ndani ya nchi na nje ya nchi, basi nakuomba Muna tumia busara sana weka utoto pembeni, Mweke shetani pembeni shilikiano na MUME wako wa NDOA kumpumzisha mtoto wenu.

“Matatizo yenu wekeni kando kipindi hiki kigumu Muna msiwape watu faida Muna, Naimani umeokoka basi kwenye hili kuwa na HOFU na MUNGU, sizani Muna kama aya tunayo yasoma mara mtoto wa huyu mara wa huyu, mara niliolewa nikiwa na mimba kama yanakujenga.

Bali nazani yanabomoa heshima yako.Dada nakuomba Fumba macho hili lipite nazani ata Patrick uko alipo analia kuona mfarakano huuuu. Msimtese mtoto uko alipo, tumieni busara sana .Baada ya maziko ayo mambo yenu mtaendelea nayo kwa sasa ushauri wangu ungana na family muweze kumpa heshima mtoto wenu inayo mmstahili.

Washauri wa Muna nawaomba unganeni na family ya Peter kumpa heshima mtoto wenu inayo mmstahili sisi wangine tupo pande zote ila atupendezwi na haya tunayo yaona nilizani ni muda muafaka wote kukusanyika mwananyamala kwa Peter kuhakikisha tunampumzisha kijana wetu asante“.

 

Ugonjwa Uliomuua Mtoto Patrick Wabainika

Siku ya Jumanne usiku mtoto wa Muna aliyekuwa anaitwa Patrick aliyekuwa na miaka 8 aliaga dunia hospitalini alipokuwa anatibiwa Nairobi nchini Kenya.

Global Publishers wanaripoti kuwa katika harakati za kutaka kujua nini hasa kilimuua mtoto huyo walianza kuongea na Muna ambaye yupo nchini Kenya kwa hivi sasa ambapo alifunguka:

Kinachomsumbua mwanangu ni uvimbe kwenye ubongo na hajaamka kwa siku sita huku akiwa amelazwa katika chumba cha uangalizi maalum ‘ICU’ hivyo tunasubiri aamke ndipo madaktari waangalie kama watamfanyia operesheni au la“.

Muna alifunguka hayo kabla ya taarifa za Kifo chake.

Lakini pia Daktari ambaye amewahi kumtibu mtoto na yeye alifunguka kuhusu ugonjwa wa mtoto:

Dk Chale alisema uvimbe kwenye ubongo kitaalamu huitwa ‘Brain Tumour’ ambao unaweza kuwa wa kawaida au kansa na husababishwa na njia kuu mbili; moja ni ubongo wenyewe na pili kutokana na viungo vingine.

Katika njia ya kwanza ni kwamba inawezekana ugonjwa huu ukarithi kutoka kwa familia kama baba au mama amewahi kuwa na matatizo hayo basi lazima na wengine warithi. Sababu nyinginezo ambazo zinachangia ni maambukizi ya virusi wa ugonjwa huo kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, sababu za kimazingira ambayo mtu anaishi, kemikali za viwandani, vipodozi, chakula, dawa na nyingine nyingi.

Katika njia ya pili ya viungo vingine hutokana na kama mtu ana kansa ya mapafu, kizazi, matiti, figo, tezi dume hizi huweza kusa babisha uvimbe kwenye ubongo. Dk Chale aliendelea kufafanua kuwa uvimbe kwenye ubongo kwa upande wa watoto mara nyingi huwa ni kansa na siyo wa kawaida ndiyo maana huua haraka sana na hawawezi kupona maana uvimbe huwa chini ya ubongo na siyo kwa juu kama inavyokuwa kwa watu wazima.

Mwenyezi Mungu aendelee kufika za roho ya marehemu mahala pema peponi Amina.

Muna Amtaja Casto Kama Baba Wa Mtoto Ahaidi Kumuumbua Peter

Muigizaji wa Bongo movie na mdau mkubwa wa muziki wa Bongo fleva Muna Love amefunguka na kuweka wazi kuwa Baba wa mtoto wake Marehemu Patrick ni Casto Dickson.

Kauli hiyo imekuja baada ya utata kutanda kuhusu nani ni Baba wa mtoto baada ya mwanaume mwingine anayeitwa Peter kujitambulisha na kudai kuwa yeye ndio Baba wa mtoto.

Marehemu Patrick na Peter

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Muna ameweka wazi kuwa hataki utata huo anachotaka ni kumzika mtoto wake na kumtaja Casto kama Baba na msiba utakuwa nyumbani kwake Mbezi:

Jaman jamani ?????? naomba nimzike mtoto wangu ???? vaeni viatu vyangu. Kuna siri kumbwa amjawahi kuijua nawaomba nimzike mtoto wangu alafu ndiyo mnitukane. Mimi ?????? naumia jamani, namuheshimu Peter siwezi kuweka kitu hapa maana nitamwaibisha….Siwezi kumsema Casto maana yeye anajua wapi alikosea, nawaombeni jamani, naomba nataka kumzika mwanangu. Miaka miwili nahangaika na Paty wangu ????????, nimalize kumzika niongee.

Nnyiwe wanawake mnaonihumuku, vaeni viatu vya siri nilizohifadhi… baba wa mtoto ni Casto, inatosha ????????, nitukaneni mimi nife ila Paty ni kiongozi alieniongoza nione maisha mapya na nimjue Mungu… Nitalia milele mimi.

Paty wangu????????leo wanakugombania mwaanangu, natamani urudi mara moja??????????… Mwanangu ntaleta ijumaa na ntamzika Jumamosi?????, msiba uko kwangu Mbezi Beach“.

 

 

Zari Afunguka Kuguswa na Kifo Cha Mtoto wa Muna

Zarinah Hassan ‘Zari The Bosslady’ amefunguka na kuweka wazi uchungu alioupata baada ya Muna kufika na mtoto wake usiku wa jana.

Mtoto wa Muna na Casto Dickson Patrick,  alifariki dunia siku ya jana Nairobi nchini Kenya baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Zari ambaye na yeye ni mama wa watoto watano amefunguka na kuonyesha kuimizwa na Kifo Cha mtoto huyo na kuandika maneno haya kwenye ukurasa wake wa Instagram:

 

 

 

TANZIA- Mtoto wa Muna na Casto Dickson Afariki Dunia

Mtoto wa msanii na Mfanyabiashara Rose Alphonce Nungu maarufu kama Muna Love na Mtangazaji wa Clouds Tv Casto Dickson aliyekuwa anaitwa Patrick amefariki dunia siku ya jana.

Patrick ambaye alikuwa anaumwa miguu kwa muda  Alizidiwa mwishoni mwa wiki iliyopita na kupelekwa nchini Kenya, Nairobi kwa ajili ya matibabu.

Baada ya kukaa hospitali kwa siku kadhaa usiku wa jana Zamaradi alitangaza kwa Kupitia ukurasa wake wa Instagram kuwa mtoto Patrick aliyekuwa ana miaka saba amefariki dunia.

Mwili wa marehemu unatarajiwa kufika nchini siku ya Alhamisi kwa ajili ya maziko.

Mwenyezi Mungu ailaze mahakama pema peponi Amina.

Wasanii Waungana Kumsaidia Mtoto wa Muna

Mtoto wa msanii na muandaaji wa matamasha Muna love anejulikana kama Patric ambae mara ya kwanza alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya miguu na kumfanya mama ake kupitia katika majaribu yaliyomfanya muna kokoka na kumrudia Mungu ameanza kuumwa tena na kuonekana kuwa bado anahitraji uangalizi mkubwa wa  madaktari.

Mtoto huyo amabe anaonekana kugusa mioyo ya watu wengi katika tasnia ya sanaa , alianza kuwekwa katika mitandao ya kijamii siku ya jana huku watu wengi wakiandika maneno  ya masikitiko na yenye kutia faraja familia ya muna na ndugu zake kwa ujumla.

Hata hivyo wasanii wengi wameonekena kuguswa na tatizo hilo na kuamua kufanya harambee katika kitandao ya kijamii kupitia kurasa zao kwa ajili ya kuwaomba wadau na mshabiki kuchangia ili mtoto huyo aweze kusaidika katika matibabu yake.

Wema Havai Nguo za Ndani- Muna Love

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara Muna Love amefungukia tuhuma ambazo zimekuwa zikimuandama kwa muda mrefu kuhusiana na urafiki wake na Wema Sepetu.

Kwa muda mrefu kumekuwa na tetesi mbali mbali kuhusu sababu za kuvunjika urafiki wa Wema Sepetu na Muna.

Kama utakumbuka miaka ya nyuma Wema alikuwa na urafiki hasa na Muna walikuwa wanaonekana pamoja kila sehemu Lakini urafiki huo ulivunjika ghafla na kila mmoja alishika njia yake na kuendelea na maisha yake.

Lakini baada ya kugombana ilisemekana kuwa Wema aligundua kuwa Muna ni mshirikina na alikuwa anamuendea kwa waganga na kibaya zaidi ilisemekana kuwa Muna alikuwa anaiba nguo za ndani Wema (chupi).

Tuhuma hizo za kuiba nguo za ndani za Wema zilisambaa sana lakini juzi Kwenye mahojiano aliyofanya na Shilawadu ya Clouds Tv, Muna alikana tuhuma hizo na kudai hawezi kuiba nguo za ndani za Wema maana mtu mwenyewe havai nguo hizo.

Ngoja niongee ukweli kwa sababu nimeokoka nguo za ndani hizo ambazo wanasema alikuwa havai inakuaje nachukua nguo za ndani ya mtu ambaye alikuwa havai”.

Kwenye mahojiano hayo Muna alikiri kuwa hana tatizo na Tunda na hakutaka kabisa kuongea sana kuhusu mzazi mwenzake Casto Dickson.

Muna Kufuta Tatoo Kwa Zaidi ya Milioni Tano.

Mwanadada mjasilimali na muigizaji Rose Alphonce amefunguka na kudai kuwa atatumia zaidi ya milioni tano kufuta tatoo zilizopo mwilini mwake , Muna ambae alisema kuwa kwa sasa ameokoka hivyo tatoo hizo zimekuwa zikimnyima amani sana anatamani kuzifuta tatoo hizo na anaona kabisa kuwa ni lazima azifute.

Muna anasema kuwa mpaka sasa hivi ana michoro kama mitano mwilini mwake huku tatoo iliyopo shingoni ndio kubwa kuliko zote lakini alishafanya mpango wa kuuliza sehemu ambayo angeweza kufuta tatoo hizo na kuambiwa kuwa inawezekana kufutwa kwa milioni tano.

Tayari nimeshaulizia kwa wataalamu huko thailand,ambao watanifuta bila kupata madhara yoyote na wameniambia kuwa hizo zingine ndogondogo  zitakuwa ni chini ya milion 2.1.

 

Baada ya Uokovu,Tatoo Zinamtesa Munalove .

Msanii wa maigizo nchi, Muna Love amekiri kuwa tatoo alizochora mwilini mwake kipindi hajaokoka zimeanza kumtesa kwa sababu hata mtoto wake wa kiume amekuwa akimpigia kelele kila siku kuhusu kuziondoa tatoo hizo.

Muna ambae mara ya kwanza alikuwa katika mambo ya kidunia na baadae alipata matatizo makubwa yeye na mwanae yaliyoyafanya kuokoka na kumrudia mungu, anasema kuwa  anatamani kuzifuta tatoo hizo na kuondoa kabisa.

Mtoto wa kiume wa Muna ambae pia ameokoka amekuwa akimsumbua mama yake huyo kuzifuta tatoo hizo  kwani zinaenda kinyume na maadili ya uokovu.

                                           

                                                 Muna akiwa na mtoto wake.

 

Muna Awajibu Wanaomsema Kuhusu Ulokole na Tatoo Zake

Msanii wa bongo movies ambae pia ni mjasiliamali Rose Alphonce maarufu kama Muna amefunguka na kuwashangaa baadhi ya watu ambao wamekuwa wakimsemak kuwa anajifanya ameokoka wkati aamejaa tatoo katika mwili wake tena zinaonekana.

Mwanadada huyo ameonyeshwa kuwashangazwa na watu wanaomsema hivyo na kuwajibu kuwa kwa upande wake tatoo hizo haoni kama zinamsumbua chochote na swala la yeye kuokoka kwa sababu aliyyafanya hayo akiwa dhambini na sasa ameokoka kwaio anachoamini Mungu hatohesabu hayo makosa yake ilhali aliyafanya kipindi ambacho alikuwa hajatubu.

Muna anasema kuwa katika imani wanaamini kuwa mtu anapoamua kuokoka mungu aangalii makosa ya nyuma bali imani yake ya kuamua kuokaka na kurekebisha yake yaliyopita na kuwa mpya kwaio tatoo haziingiliani na swala la kuokoka.

Sidhani kama Mungu anaangalia tatoo zangu,ninachojua hatoangalia dhambi zangu bali atanipokea  na kufuta kila kitu changu ambacho kimekifanya  nyuma.kwasabau kama tatoo nishachora nyingi na hakuna njia ya kuzikwepa kabisa na kwasababu  nimetubu naamini kuwa Mungu atanisaidia.

Muna ambae kwa sasa anaonekana kujiweka karibu zaidi na Mungu na kusema kuwa ameokoka , ameonekana kuwa katima maombi muda mwingi na hata posti zake zimekuw zikithibitisha hivyo.

 

Muna Ahaidi Kufunga Mpaka Hukumu Ya Lulu Itakapokwisha

Muna , akiwa ni kama ndugu kwa Lulu Michael alijitolea kwa hiari yake kuwa dada wa hiari wa Lulu tangu kipindi wanaigiza wote kipindi wapo kaole sanaa group,  Muna amekuwa karibu na familia ya Lulu kwa kipidi chote cha raha na shida na sana sana   katika kipindi hiki cha miwsho cha kesi ya Lulu mpaka anapata hukumu yake. Pamoja na kwamba Muna  alikiri kuwa alikuwa na mgonjwa hospitali lakini bado Muna aliweza kuhudhuria katika kesi hiyo  kila siku ili kumfariji mdogo wake huyo.

Akiongea na waandishi wa habari, Muna alielezea jinsi ambavyo ameipokea hukumu ya mdogo wake Lulu kwa masikitiko ukizingatia ndie ndugu na rafiki wa karibu aliekuwa nae kwa kipindi kirefu na tangu wajuane hawajawahi kugombana,lakini pia Muna bado anajipa moyo na kusema kuwa hukumu ya miaka miwili kwa Lulu ni moja ya jaribu tu ambalo Mungu ameamua kumpitisha Lulu huku akimundalia mema zaidi mbele ya safari yake.

Unajua mimi namuamini sana mungu na ninaamini ilo  ni moja ya jaribu tu  ambalo Mungu ameamua kumpa Lulu lakini ipo siku litapita tu na lulu atarudi katika maisha yake ya zamani.-Aliongea Muna kwa kujipa matumaini makubwa

Lulu na Muna katika picha za pamoja

Hata hivyo kwa masikitiko makubwa kabisa Muna anasema kuwa atakumbuka sana kipindi amvacho alikuwa na Lulu,na kufanya mambo mengi kwa pamoja kwa shida na raha lakini leo anafanya peke yake, mbali na hayo muna amehaidi kufunga kwa sala kwa siku zote ambazo Lulu atakuwa hukumni ili kumuombea.

Nitakumbuka nyakati zote nilizokuwa na yeye kipindi yupo uraiani,lakini kuanzia siku aliyopewa hukumu kazi yangu ni moja tu  kufunga na kuomba kwa ajili yake.-Alimalizia Muna

Wapo wengi walionekana kuguswa na hukumu ya Lulu lakini pia Muna akiwa kama mwanafamilia na rafiki wa karibu wa Lulu Michael anaamini kuwa ndugu yake huyo anahitaji maombi ya muda mrefu ili kukabiliana na changamoto mbalimbali zitakazomkabili kipindi atakapokuwa gerezani ukizingatia wengi waliotoka huku wamekuwa wakielezea ugumu wa maisha ya kutokuwa huru.

 

Muna Azungumzia Ugumu Anaoupata Kwa Kesi Ya Lulu

Mwanadada mrembo anaejihusisha na uigizaji na  mjasiriamali   Rose Alphonce maarufu kama Muna Love amefunguka na kuongelea ugumu na kipindi kigumu anachopitia kwa kipindi hiki tangu kesi ya mdogo wake wa hiari Elizabeth Lulu Michael  imeanza.Muna Love amesema kuwa kwa kipindi hiki amekuwa na kazi kubwa  ya kuuguza mtoto wake ambae amelazwa muhimbili  kwa muda wa zaidi ya miezi miwili sasa na pia amekuwa akitakiwa kuoekana mahakamani ili kumsaidia na kumfariji mdogo wake Lulu Michael katika kesi ya mauaji inayomkabiri iliyokuwa ikisikilizwa mahakamani.

Akizungumza na Star Mix ya Global  , Muna ambae tangu kesi ya msanii mwenzie na mdogo wake huyo ianze amekuwa akonekana mahakamani bila kukosa anasema kuwa kwa takribani miezi miwili sasa amekuwa akimuuguza mwanae pale muhimbili lakini pia ana ndugu yake ambae pia anahitaji uwepo wake , hivyo inabidi aweze kufanya kotekote ingawa inakuwa inampa ugumu kidogo.

“Yaani najiona kabisa kama huu mwaka ni wangu,maana pale Muhimbili wameshanizoea kabisaa.Nimekaa muda mrefu nikimuuguza mwanangu mguu lakini ukiachana na mgojwa huyo pia  naangaika na upande wa pili kwa mdogo wangu Lulu mpaka nachanganyikiwa” alisema Muna Love

Kesi ya Lulu ambayo ilianza kusikilizwa mahakamani tangu Oktoba 19 inayohusu mauaji ya msanii mwenzie mkongwe ambae pia alikuwa ni mpenzi wake Steven Kanumba , iliendelea kwa muda wa takribani wiki mbili ambapo mashauri ya mwisho na hukumu yanatarajiwa kutolewa Novemba 13.Muna amekuwa ni mmoja wa watu wa karibu katika kumfariji Lulu kwa kipindi hiki kigumu ambacho anapitia na amekuwa nae bega kwa bega kila siku wanapokwenda mahakamani.

Ukiachana na wote kuwa wasanii katika tasnia moja, Lulu Michael na Muna Love wamekuwa marafiki na watu wa kakribu kama ndugu kwa muda mrefu na kusaidiana kwa mambo mbalimbali .Watu hawa wamekuwa kama ndugu sasa.

Muna pia alishawai kuwa rafiki wa karibu wa Wema Sepetu lakini mambo hayakuwa mambo na waligombana na kurushiana maneno katika mtandao wa instagram na kusababisha mahusiano yao kuvunjika

 

Bifu La Young Dee Na Dogo Janja,Chanzo ni Muna

Kwa muda sasa kumekuwa na chokochoko kati ya wasanii wawili wa muziki wa Bongo Fleva yaani Young Dee na Dogo Janja ambapo katika kufatilia sababu inaonekana ni yale maneno ambayo Young Dee aliyaongea yaliyokuwa yanamuhusu Dogo Janja na Young Killer Msodoki kuwa yeye (Young Dee) ni mkubwa kimuziki hivyo hataki kabisa kusikia watu wakimfanisha na wasanii hao wawili ambao kwake anawaona bado wachanga hawajamfikia kiwango chake. Young Killer alinyamzaza na hajaonekana kuongea chochote kuhusu ili lakini Dogo Janja hakuweza kuvumilia na kuamua kujibu maneno ya Young Dee na kumwambia kuwa hata yeye hawezi kulinganishawa  msanii kama yeye ambae anavuta unga, kabisa hawezi kuongea na ‘mteja’.

Bifu limeendelea na kuwa kubwa mpaka baadhi ya wasanii waliamua kuingia nakuwashauri kuyamaliza mambo hayo, kati ya wasanii hao ni pamoja na Nikki wa Pili.Lakini jana msanii wa muziki wa singeli Sholo Mwamba nae aliamua kufunguka kuhusu bifu ilo huku akiamua kumwaga ubuyu hadharani kuhusu sababu ya wasanii hao kugombana ni mwanamke.

Akiongea na eNews ,Sholo Mwamba ambae alikuwa chini ya menejiment ya Muna Entertainment alifunguka na kusema kuwa kwa sasa yeye na Muna hawafanyi kazi pamoja na sababu sio kwamba yeye alichokwa na Muna bali yeye alimchoka Muna, alipoulizwa sababau ya yeye kumchoka meneja wake alijibu “Kitu ambacho mimi kiliniuzi na nilikichoka kwa Muda ni kitendo cha sisi wanaume kufanya kazi na kutafuta ela  afu tukienda pale  kwa muna tunakuta madogo wengune wamekaa kwenye makochi wamejiachia, sisi wahuni tunaenda kuimba visingeli vijijini tunaleta mpunga kwa bosi alafu bosi anatumia na wajinga”aliongea Sholo Mwamba

hapo wote vingasti tu, tunawakuta pale kwa bimkubwa wanajiachia achia tu, Dogo Janja, Young Dee, wanagombana wanagombania demu, ila sisi tunakuja kwa bosi tunawakuta hayo mambo ya kugombana ni miyeyusho tu” aliongezea Sholo Mwamba

Hata hivyo Sholo pia anaonekana ana wivu wa mapenzi kwa Muna Love na kufikia hatua ya kusema ” namshangaa bosi si angenipa hata mimi, akinipa sisemi, tunakula kimyakimya”

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.