Mwarabu Fighter Afunguka Baada Ya Kupata Ajali

Bodyguard wa staa wa Bongo fleva na CEO wa WCB Diamond Platnumz, Mwarabu Fighter amefunguka kwa mara ya kwanza tangu apate ajali ya gari mapema wiki iliyopita.

Mlinzi wa Diamond Aliripotiwa kupata ajali hiyo mbaya wiki iliyopita ambayo kwa kiasi kikubwa ilimpa majeraha maeneo ya uso.

Baada ya kulazwa hospitalini kwa muda wa siku kadhaa Mwarabu Fighter ameonekana kupata ahueni na kusema kuwa kama si mipango ya Mungu basi angekuwa ameshafariki dunia kutokana na ajali hiyo.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Mwarabu Fighter aliandika ujumbe huu:

Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kuiona siku ya leo maana kama sio mapenzi yake inawezekana kabisa leo hii nisinge kuwepo kutokana anajali mbaya sana nilio nusurika…?”.

Harmonize Afungukia Ushindani Uliopo WCB

Msanii wa muziki wa Bongo fleva kutoka WCB Harmonize amefunguka na kuelezea ugumu uliopo katika kufanya kazi kama msanii wa label ya WCB kutokana na ushindani.

Harmonize amefunguka na kuweka wazi kuwa ushindani ndani ya Label hiyo kati ya wasanii ambao wapo ndani ya Label ndio ugumu ambao upo humo.

Kwenye mahojiano na Planet Fm, Harmonize amesema ugumu uliopo WCB ni kila msanii ana uwezo mkubwa, hivyo kila mmoja anahakikisha anafanya kazi nzuri.

Ugumu ni pale ambapo unafanya kazi na wasanii wote ambao ni talented, so way competion katika kurekodi ngoma kila mtu anataka kutoa ngoma yake kali kumshinda mwenzake, so ugumu unaanzia hapo“.

WCB ni Label kubwa kabisa Tanzania na inabeba wasanii wanaofanya vizuri sana, wasanii hao kama vile Diamond Platnumz, Rayvanny, Harmonize, Rich Mavoko, Mbosso na wengineo.

 

Mbosso- Ujana Ulinipelekea Kupata Watoto Katika Umri Mdogo

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva kutoka katika label ya WCB, Maromboso au maarufu kama Mbosso amekiri kuwa na watoto wawili katika umri mdogo ni matokeo ya balehe.

Mbosso ambaye kwa hivi sasa anaendelea kufanya vizuri na ngoma yake ya “Nadekezwa” ni Baba wa watoto wawili ambao watoto wote wana umri sawa lakini ni mama tofauti.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, Mbosso amekiri kuwa pamoja na kila mmoja kuwa na mama yake lakini hana uhusiano na kama zao kwa sasa kila mmoja ameshaolewa.

Sipendi kuwa muongo na sitakuwa na dhambi ya uongo, huwa inatokea katika ukuaji (balehe) hususani sisi watoto wa kiume, kuna vitu utajizuia navyo lakini hutashindwa tu.

Kwa hiyo sitaki kuwa muongo, ilitokea ikawa hivyo nimekuwa baba nina watoto wangu wawili, tunaishi vizuri“.

Mbosso alianza muziki katika umri mdogo baada ya kujiunga Kwenye kundi la muziki la Yamoto Band miaka kadhaa iliyopita.

Mbosso- Nyimbo Zangu Hazipigwi Redioni

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva kutoka label ya WCB Maromboso au maarufu kama Mbosso ameongelea Kitendo Cha nyimbo zake kutopigwa na baadhi ya media.

Mkurugenzi wa WCB Diamond Platnumz amekuwa kwenye mgogoro na baadhi ya vyombo vya habari hadi kupelekea nyimbo zake kufungiwa na vituo hivyo.

Wasanii wote ambao wako chini ya WCB wamekuwa wakibaniwa nyimbo zao kupigwa Kwenye Media hizo na Mbosso akiwa mmoja kati ya wasanii hao.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, Mbosso ameweka wazi kuwa ingawa  nyimbo zake hazipigwi na baadhi ya media lakini anashukuru zinadai kila vyema kwa mashabiki zake.

Ukizungumzia moja ya wasanii ambao hawakupata bahati ya kupata nafasi kubwa kwenye radio station, mimi pia naweza kusema nipo.

Sikupata bahati kabisa nyimbo kupigwa kwenye radio station lakini wananchi wamenipokea, wamesema Mbosso tunakusapoti, wamenisapoti nashuru leo nimefika nilipofika”.

Baada ya media zaidi ya nne kugoma kupiga nyimbo za Diamond na wasanii wote wa WCB, Diamond alifikia uwaumuzi wa kufungua Stesheni yao ya Wasafi Tv.

Bodyguard wa Diamond Apata Ajali na Kupasuka Kichwani.

Body guard wa msanii mkubwa bongo mwarabu fighter amepata ajali katika maeneo ya Mbezi Afrikana alfajiri ya leo na kuumia  maeneo ya kichwa na kuwahishwa haraka  hospitali ya Lugalo ii kupatiwa huduma ya kwanza ambapo baada ya hapo mgonjwa huyo aliwahishwa na  gari la wagonjwa na kupelekwa hospitali ya Muhimbili.

Hata hivyo Mwarabu anasema kwa sasa anaendelea vizuri na anawashukuru watu wote waliojitokeza kumsaidia katika kpind alichokuwa amepata ajali hiyo,akiongea na waandishi wa habari akiwa hospitalini hapo Mwarabu Fighter anasema

namshukuru mungu sana mpaka hapa sasa hivi maana madaktari wamenipigania sana m ilikuwa alfajiri mida ya saa kumi na moja nilipoata ajali lakininalitokea msamaria mwema akanikimbiza  lugalo na kukutana na daktari alienipigania sana na mpka kuwekwa katika ambulance na kufikishwa hapa na kama mnavyoona hapa kumekuwa na huduma nzuri sana tangu nimefika”

 

Mbosso Awalaumu Mashabiki Kwa Video Yake Chafu

Mwanamuziki wa Bongo fleva kutoka label ya WCB Maromboso au maarufu kama Mbosso ameelekeza lawama kwa mashabiki baada ya video yake kusambaa Kwenye mitandao ya kijamii.

Siku chache zilizopita video ilisambaa mtandaoni iliyomuonyesha Mbosso akiiwa stejini akitumbuiza kwenye shoo ya Kusi night huku akimbambia msichana mmoja katika staili za kimahaba.

Video hiyo ilisababisha mashabiki kumjia juu Mbosso huku wakiwarushia lawama WCB na kudai wamembadilisha Msanii huyo na kumfundisha tabia mbaya.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5 Mbosso amefunguka hay kuhusu video ile:

Unajua watu wengi wanaamini mimi nimebadilika lakini hakuna kuna baadhi ya vitu vinachangia hasa kwenye shoo inakulazimu ufanye vitu fulani ili watu wafurahi kwaiyo unajikuta unafanya vitu fulani ili shoo ipendeze na watu wafurahi na mashabiki wawe na shangwe na wewe ndio inabidi uwape burudani mashabiki  zako”.

Lakini pia Mbosso amesisitiza kuwa yeye binafsi hakupenda kufanya vile ila kutokana na msukumo wa mashabiki waliokuwa wanampa ukumbini pale akajikuta akifanya vile.

WCB Wagoma Nyimbo Zao Kupigwa na Habari Zao Kuripotiwa na Baadhi Ya Media

Label au kundi linalofanya vizuri hivi sasa nchini WCB linaloongozwa na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz limetoa tamko rasmi la kuwataka baadhi ya media wasipige nyimbo zao.

Meneja wa label hiyo Babu Tale ametoa tamko hilo jana wakati akichonga na waandishi wa habari Kwenye uzinduzi wa Wasafi Tv Kwenye king’amuzi cha Startimes.

Babu Tale amevitaka vyombo vilivyokataa kupiga nyimbo zao Mwanzoni viendelee hivyo hivyo na hata visijaribu kuripoti taarifa zao.

Tunaendelea kuwaomba waendelee kushinikiza wafanyakazi wao wasipige nyimbo zetu.

Hatutaki kuona wanapiga nyimbo zetu wala kutoa habari zetu kwa sababu wao walitukataa mwanzo, tunawakataa kwa sababu wao walitukataa“.

Diamond amekuwa katika mgogoro mzito na Media mbali mbali ambazo zimekuwa hazipigi kabisa nyimbo zake ambazo ni Clouds Media na hata East Africa Radio na Tv.

 

Zari Sio Chanzo Cha Diamond Kukonda, Babu Tale Ataja Sababu Hizi

Staa wa muziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz ambaye pia ni CEO wa WCB amekuwa kwenye headlines sana na moja kati ya vitu vinavyo trend ni mwili wake kuisha.

Baada ya Diamond kuonekana anapungua mwili kwa kasi habari zilisambaa Mtandaoni kuwa kisa ni Zari ambapo ilidaiwa baada ya kumwagwa na Zari Diamond alipata mawazo sana na hata kudaiwa eti sahivi hapati matunzo aliyokuwa anapata wakati yupo na Zari.

Lakini Meneja wa Diamond, Babu Tale amefunguka na kuweka wazi kuwa sababu za Diamond kupungua mwili kwa muda mfupi kuwa ni kukosa muda wa kulala kutokana na jukumu zito la ujio wa Wasafi TV.

Kuna baadhi ya watu wanasema msanii wangu anapungua mimi na nenepa navimba, Kama hamjui Media sio kitu kidogo, wakati tunaanza tulijua ni kazi ndogo, kwa miezi sita non stop msanii wangu analala masaa mawili tu, kwa sababu ya kuandaa hiki mnachokiona machoni mwenu.. Wiki mbili za mwanzo tukawa tunakasirika kwa nini anafanya kazi ngumu, ilipofika mwezi tukawa tunaona  ana-loose weight (kupungua uzito) na bado kazi zinaendelea tukawa tunashangaa ana nia gani huyu”.

Lakini pia mwana Familia wa Diamond mwenyewe,ambaye ni dada yake Esma aliwahi kunukuliwa akisema kaka yake kapungua kwa kumiss penzi la Zari.

Uzinduzi wa Wasafi Tv Kwenye Startimes (+picha)

Msanii wa Bongo fleva na CEO wa WCB Diamond Platnumz ametangaza rasmi kuingia ubia na king’amuzi cha Startimes ambacho kitarusha matangazo ya Wasafi Tv.

Siku ya jana Diamond Kupitia ukurasa wake wa Instagram alitangaza kuwa atakuwa na mkutano na waandishi wa habari katika hoteli ya Slipway siku ya leo saa tano asubuhi.

Diamond amezindua rasmi Wasafi Tv ndani ya Startimes Tanzania Bara na visiwani ambayo itakuwa inaruka Live Kupitia chaneli namba 444 katika king’amuzi hiko.

Wasafi Tv tayari inapatikana katika king’ Cha Azam na sasa unaweza kuipata kupitia king’amuzi cha Startimes.

Hizi ni baadhi ya picha za matukio yaliyojiri ukumbini hapo:

 

 

Huddah Afungukia Mahusiano Yake na WCB

Socialite maarufu kutoka Kenya mrembo Huddah Monroe maarufu kama Huddah The Bosschick amefungukia uhusiano wake na Label maarufu nchini WCB.

Huddah alitua nchini Tanzania mwishoni mwa wiki hii na mara moja alionekana akiwa katika ofisi za WCB na CEO wake staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi The Playlist ya Times FM, Huddah amesema kuwa ukiachilia mbali sababu za kibiashara, amekuwa akivutiwa na uchapakazi wa timu nzima ya WCB.

The vibe is, WCB napenda sana ni watu wanajima, watu wana njaa ya maisha , so for me WCB have the some kind of vibe the i have. Wanapenda maisha mazuri, so they very work hard hawalalai saa 24 wapo kwenye kazi, so that I like that”.

Huddah ambaye ni Mfanyabiashara anayemiliki make up line yake inayoitwa Huddah Cosmetics ambayo imekuwa ikifanya vizuri.

Huddah Monroe alikuja nchini Tanzania kwa ajiili ya ku-host show ya Harmonize iliyofanyika siku ya leo June 16, 2018.

Nandy Alikuwa Msanii wa WCB Kabla ya Kutoka:Lizer

Mtayatrisha ji wa nyimbo nyingi kutokaWCB Lizer amefunguka na kusema kuwa katika maisha yake elimu yake aliyoishia ni darasa la saba na alifaulu vizuri lakini alikataa shule na kusababisha kufukuzwa nyumbani ndipo alipoamua kukimbilia Burundi alipotokea nyumbani kwao kigoma na ndipo alipoenda kujifunzia muziki.

Lizer anasema kuwa alijifunza kuimba na baadae kuwa producer ndipo moja ya wasanii nchini Burundi alipomtambulisha kwa Diamond lakini Diamond alimuomba kufanya nae kazi na alikataa lakini kutokana na hali ya amani kutokuwa shwari nchini Burundi aliona bora arudi Tanzania ambapo baaada ya muda aliona maisha yanabadilika na kumtafuta Diamond na kukuta nafasi yake bado ipo na ndipo alipoanza kufanya kazi na Diamond.

Hata hivyo alipoendelea kuongea lizer alitoboa siri na kusema kuwa nandy pia alikuwa msani kutoka WCB lakini alipoona amekaa muda mrefu bila kutoa ndipo alipoamua kuanza kufanya kazi zake .

Hata hivyo Lizer anasema kuwa tangu ameanza kufanya kazi na wcb, ndoto zake imewea kutimia kwa 70% na kwamba kuhusu kufanana kwa nyimbo zake katika beats , hiyo ni identity yake ambayo anaitengeneza.

Rosa Ree Afunguka Kuhusu Kujiunga WCB

Msanii wa Bongo fleva Rosary Robert ‘Rosa Ree’ aliyejizolea umaarufu kutokana na  miondoko yake ya kuchana amefunguka juu ya mipango ya kusaini na Label maarufu nchini WCB.

Rosa Ree ambaye amekuwa akiulizwa mara kwa mara kama ana mpango wa kujiunga na label hiyo ameweka wazi kuwa hajwahi kufikiria kujiunga WCB.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, Rosa Ree ambaye awali kabisa alikuwa katika label ya The Industry amesema  kuwa hawajawahi kuzungumza hilo ila ni watu ambao wamekuwa bega kwa bega na yeye katika muziki wake.

Hapana ilikuwa hamna, ndiyo timu mzima ya WCB wamekuwa wakinisapoti katika muziki wangu. Nafurahia hilo ila hatukuwahi kufikia hatua hiyo”.

Rosa Ree aliondoka The Industry, record label inayomilikiwa na Nahreel na Aikah wa Navy Kenzo mwaka jana oktoba na amekaa bila management kwa miezi kadhaa mpaka aliposainiwa mapema mwezi huu.

Queen Darleen Athibitisha Kurudi kwa Zari Mjengoni, Amtupia Hamisa Dongo

Mwana dada pekee kutoka katika lebel ya wcb leo amethibitisha kurudi kwa  zari katika mjengo wa WCB  baada ya kuondoka na kugombana kaka yao muda mrefu lakini kumetokea usuluhihso na kurudi.

mwanadada huyo aliweka picha ya kaka na wifi yake huyo huku akiandika kwa kuwapa taarifa watu  amabo kwa namna moja ama nyingine inawza kusemekana kuwa ni hamisa amabe alikuwa katika penzi zito na daimond hivi karibuni.

 

Zamaradi Athibitisha Show ya WCB Itapamba Moto.

Zamaradi mketem akiwa kama moja ya viongozi wa  Wasafi Tv amethibitisha kuwa kuna show itakayo kuwa inaonyeshwa katika televisheni iyo ambayo itakuwa habari ya mjini itakapo anza.katika ukurasa wake wa instagram zamaradi aliandika,

Kuna vingi vikubwa vinakuja kutoka Wasafi Tv, ila niwe mkweli moja kati ya vitu vikubwa MNO ambavyo hata mimi binafsi i cant wait ni this BIG REALITY SHOW.. kumeshafanyika kadhaa Bongo, ila hii nakuhakikishia HAIJAWAHI KUTOKEA TANZANIA, na sio kwasababu ya watu walio mbele tu, ila pia TIMU KUBWA ILIYOJIPANGA nyuma ya reality show hiyo, bila kusahau exclusivity ambazo hata Dunia ya Social Medias haijawahi kuzishuhudia zitakazowekwa kwenye creativity ya ya hali ya juu, na hata uwazi mkubwa wa characters waliopo and how real watakuwa, Its time to watch OUR STARS and be proud of production ya vipindi vyetu.
Hao ni BAADHI tu ila kuna wengi (wahusika) utawaona humo and I swear hautachange channel kwa vyovyote on that Day’
The real life of WCB 
And BTW, Lifestyle ya Nani unayotamani kuiona kwa karibu zaidi kutoka Wasafi!!!???? Ama Nyumba ya nani utakayotamani kuiona zaidi kuliko nyingine!!? 

Abdu Kiba- Ninaweza Kufanya Kolabo na WCB Lakini Inategemea na Wimbo

Msanii wa Bongo fleva Abdul Kiba ambaye pia ni mdogo wa staa wa Bongo fleva Ali Kiba amefunguka na kudai kuwa yupo tayari kufanya Kolabo na mahsimu wao wakubwa WCB.

Sio siri kuwa Diamond na Ali Kiba hawapikiki chungu kimoja pamoja na kwamba wameshasema hawana bifu lolote lakini ni wazi kuwa Kumekuwa na tensions fulani baina ya makundi hayo mawili.

Lakini Abdu Kiba ameibuka na kudai kuwa kama ikitokea kuwa kuna wimbo ambao utakuwa na uhitaji wa msaniii kutoka WCB ndio ukae sawa hataona shida kumtafuta ili wafanye kazi.

Abdu Kiba amefunguka hayo Kwenye mahojiano na EFM Radio Lakini amejitetea Kuwa Mpaka sasa hajapata wimbo unaohitaji sauti kutoka kwa msanii yeyote wa WCB:

Kufanya kolabo na msanii yeyote kutoka WCB inategemeana na muziki gani ambao nimeimba, naamini kila muziki una sura ambayo inaonyesha ni nani unaweza kuimba naye, ikitokea kuna muziki ambao naona kuna haja ya msanii kutoka WCB nitafanya naye na kama sina tutabaki hivi hivi WCB na Team Kiba”.

 

Queen Darleen asema Diamond Atasubiri Yeye Aolewe Ndio na Yeye Aoe

Mwanadada pekee kutoka kundi la wcb  Queen Darleen,amefunguka na kusema kuwa wakati wake wa kuolewa ukifika lazima na yeye ataaolewa tu kwa sababu hata yeye ni binadamu na pia ni mwanamke kwaio hawezi kuacha kuolewa.

Watu wengi wamekuwa wakitilia mashaka sana mahusiano ya kimapenzi ya Queen Darleen kutokana na ukweli kwamba mwanadada huyo hajawahi kuonekana sana akiwa na mwanaume yoyote  na pia ni kutokana na muonekano wake ambao mara nyingi  anaonekana ni wa kiume.

Mimi sina shida , ndoa ni majariwa na kama mungu atanijalia basi na mimi  nitaolewa  na mimi ni binadamu na nina hisia vile vile  kwaio nikipata mwanaume na mungu akinijalia basi nitaolewa tu.

Hata hivyo queen darleen anasema kuwa pamoja na kwamba yeye bado hajajua muda wa kuolewa lakini yeye ni mkubwa sana kwa diamond kwaio lazima diamond atasubiri sana kuoa mpaka yeye aolewe kwanza.