Dogo Janja afunguka kuhusu mavazi yake

Rapper wa bongo Dogo Janja ni mmoja wa wasanii ambao wanatambulika kuvaa kama mastaa wa uingereza. Yeye mwenyewe huwa na style yake mwenyewe na hapo awali aliwahi kudai kuwa hakuwa msanii ambaye anaweza kufikia kiwango cha kuvalia.

Hivi karibuni alifunguka kuongea kuhusu mavazi yake katika mahojiano na Dj Show ya Radio One. Kulingana na Dogo Janja watu wengi wamekuwa wakidhani mtu anapaswa kuwa na hela mingi ili apendeze kitu ambacho si cha ukweli… Dogo alisema;

“Watu wamekuwa wakilinganisha muonekano wangu na fedha, ninachoamini kuvaa sio fedha nyingi sana ila kuvaa ni passion ya mtu, so kila mtu anavaa ndio maana nikasema ukivaje unapendeza kitu ambacho kipo watu wanavaa huwezi kutembea utupu hata siku moja,”

Nuh ataja sababu itakoyomfanya amchukue mtoto wake baada ya kuwachana na mke wake

Nuh ameweka wazi kuwa ameachana na mke wake lakini msanii huyu hakutaja sababu za kuachana.

Hata hivyo amemruhusua alikuwa mke wake kumlea mtoto wao wa kike aitwaye, Anyaghile. Lakini akizungumza na 5Selekt ya EATV hivi karibuni Nuh alisema kuwa aliyekuwa mke wake ashaolewa tena lakini ameapa kuwa hakuna kitakacho mfunga yeye kumchukua mwanawei wapo atafanyiwa vitu ambavyo si sawa.

“Mtoto still yupo na ningetamani sana kukaa naye tangu akiwa mdogo lakini nashindwa kufanya hivyo kwa sababu ya umri lakini nikiona mwanangu wanamfanyia vitu ambavyo si sawa nitaenda kumchukua na kukaa naye mimi mwenyewe,”

Aliongeza;

“Kwa hiyo nampa muda nione, nikienda nikakuta mwanangu amenenepa, ana furaha, yupo poa ataishi naye mpaka umri utakapofika lakini nikienda nikakuta mwanangu amepungua nambeba na kuondoka naye.”

Lucy Komba awapasha mashabiki wa Zari wanaomtusi Hamisa Mobetto

Muigizaji wa bongo Lucy Komba amefunguka kwa mara ya kwanza kuwakomesha watanzania ambao wanamtukana Hamisa Mobetto kisa kuwa mtoto aliyezaa ni Diamond Platnumz.

Hii ni baada ya wengi kudai kuwa kunauwezekano wa mtoto huyu wa pili wa Mobetto kuwa wa Diamond Platnumz ambaye anasemekana aliwahi kutoka kimapenzi na Hamisa Mobetto.

Lucy Komba

Hata hivyo Lucy Komba aliwatoa wengi povu kwa kuandika;

“Samahani lakini kimenichoma. MABOGAS YA TZ YANAMPONDA MTZ MWENZIO YANAMSIFIA BOGAS MWENZIO sijui yanafikiri yatapewa ule urithi. Mbona waganda hawambabaikii acheni umasikini wa kujirahisisha. Au mnafikiri mtapitishiwa kila mmoja karanga moja moja ya bure,”

Aliongeza,

“Hongera mwanamke mwenzangu, wanajifanya roho ngumu tu kukuponda wakati roho zinawauma unatoa vitu hasa mwanamke unazaa huku unatabasamu. Wale wanaoniponda eti ningekuwa mzalendo nisingeolewa na mzungu, Yes nimeolewa na mzungu sababu sina ubaguzi wa rangi wala ukabila na tangu nimeolewa sijawahi kutukana kaka zangu wakisfrika kwa hiyo lazima mjue kutofautisha A na B. Pili anayewapa taarifa nimeachwa nahisi kama kachelewa kuwataharifu halafu mwambieni awape taarifa kamili maana huwa anaingia insta na kuzizungusha bado hajawapata taarifa za kunichamba huku mmesimaisha visimi. Ukweli unauma mmepewa ukweli wa huyo stranger wenu aliyenenepesha miguu kiuno kimeshindikana kukipunguza mnalia chambeni tu mniongezee followers maana nilikuwa sijaamka bado kujua kumbe umaarufu wa bongo unatokana na vichambo. GOODMORNING.,”

Esha Buheti alifungua mtoto wa kike

Esha Buheti ndio mama mpya bongo baada ya kujifungua mtoto wa kike leo. Muigizaji huyo wa filamu za bongo amebarikiwa na mtoto siku kadhaa baada ya Linah, Faiza Ally na Hamisa Mobetto kujifungua salama.

Kulingana na habari zinazoenea, Esha alijifungua Latina hospitali ya Sali International iliyopo ushuani Masaki.

Kama wenzake Esha alithibitisha taarifa hizo kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kupost picha ya mtoto wake chake na kuandika;

“Alhamdullilah ni mtoto wa kike, asante Mungu kwa zawadi hii, asanteni wote kwa dua zenu mimi na mtoto tupo salama.”

“Natamani Kuzaa” Elizabeth Michael ‘Lulu’ afunguka kuhusu kuwa mama

Elizabeth Michael ‘Lulu’ ni mmoja wa wanawake maarufu Tanzania kwa sababu ya sinema za Kibongo. Hata hivyo wenzake wamekuwa wakizaa na kulingana na mahojiano yake na 4-Tamu pia yeye anatamani mtoto.

Hii ni mara ya kwanza kwa Lulu kusema haya. Katika mahojiano yake Lulu alisema kuwa imefika wakati na yeye anatamani sasa kuzaa.

Aliendelea kusema kuwa umri wake unamruhusu na akipata mwanaume wa kumzalia basi atajaribu kupata mtoto. Akizungumza na 4-Tamu alisema;

Lulu Micheal

“Natamani tu na mimi nipate mtoto sema ndiyo hivyo bado natengeneza mipango ya mimi kuwa mama tena mama bora,”

‘Baba’ ya mtoto wa Hamisa Mobetto ajitokeza

Dennis Louis ambaye ni mshindi wa milioni 50 za Tanzania Movie Talent amejitokeza kudai kuwa mtoto wa Hamisa Mobetto ni wake kupitia mtandao wake wa Instagram.

Muigizaji huyo alianzak kwa kusema kuwa Diamond Platnumz sio baba ya mtoto yule bali yeye ndio baba wa halali. Dennis Louis aliweka post hiyo huku akiwaacha wengi kama wameshangaa. Aliandika;

“Mengi yamesemwa nimevumilia vya kutosha mwenye mzigo nadhani mshanijua!! Kabla hamjaandika mambo zenu muwe na evidence za kutosha!!. Basi wenye wivu watasema Photoshop shubaaamit!!! #babajunior #comingsoon”

Hata hivyo hakuwachia hapo kwani aliweka post nyingine yenye picha yake na Hamisa Mobetto ameandika,

“son you have a bright future behind you…#eyoo! It’s a boy”

Mashabiki nao ambao wamekuwa wakifuatilia akaunti za Hamisa na Tanzanian baby walimshambulia huku wakisema kuwa wanajua kuwa msanii huyo anatafuta Kiki.

Kufikia Sasa Hamisa bado hajaweka wazi mtoto wake huyo wala baba ya mtoto wake.

 

Harmonize azungumzia kuhusu mjengo wake

Muimbaji kutoka label ya WCB, Harmonize amefunguka kuhusu mjengo wake ambao ni wa ghorofa akizungumza kwenye mahojiano hivi karibuni.

Kulingana na Harmonize mjengo wake unawezekano wa kukamilika mwishoni wa mwaka huu. Hata hivyo, Harmonize alikataa kufunguka kuhusu gharama aliyotumia kutengeneza ghorofa hiyo.

Harmonize alisema;

“Kwa hiyo flow ya kwanza tayari bado ya pili, kidogo kidogo tunajikongoja tukipata 200 tunaweka. Sio kitu kizuri kusema (gharama) nadhani lakini imetumia hela nyingi”

Harmonize aliendelea kwa kudai….

“Siwezi nikakadiria lakini imekula hela nyingi, show zenyewe hizi kwa mwaka sita/saba na usawa wenyewe ulivyo mgumu lakini nashukuru sio show pekee zinazonipatia hela kuna mishe nyingine, kwa hiyo siwezi kujua ni kiasi gani imekula lakini imekula hela nyingi,”

Ben Pol aweka wazi kwa nini hataki kuongelelea maisha yake ya kibinafsi kwa sasa

Muimbaji wa bongo, Ben Pol amefunguka kudai kuwa kwa sasa hataki watu wamuulize kuhusu maisha yake ya kibinafsi wala mahusiano yake, Ebitoke na mtoto.

Hii ni kwa sababu ya kazi anayoifanya kwa sasa. Akizungumza kwenye mahojiano, Ben Pol alisema;

“Kwa series ya kazi zangu zinazokuja ningependa sana vitu binafsi nisiviongelee zaidi au hadi pale nitakapokuwa tayari kuzungumzia Ben Pol anafanya nini sasa hivi nianze kuzungumzia,”

Akaendelea kwa kusema;

“kwa hiyo sipo comfortable sana kusema vitu binafsi mahusiano, sijui mtoto nataka kupunguza kuvizungumzia hivyo vitu kwa sasa hivi kusema kweli,”

 

Daktari maarufu Bongo adai kuwa Wolper ni ‘Wife material’

Japo Wolper bado hajapata mtu ambaye anaweza kumuoa mrembo huyu wa muvi za bongo sasa hivi anatoka na mwanaume ambaye anasemekana ni mdogo kumshinda.

Hii iliwafanya watu wengi kumchana lakini Daktari mmoja kutoka Bongo, Dk Fadhili Emily ameonekana kuwa na maoni tofauti. Akizungumza katika mahojiano alisema kuwa mrembo huyu akona uwezo wa kuwa mke mzuri kwam tu yeyote.

“Nimeona kwenye mitandao, wanamuandama kuwa hajatulia na kwamba ana msururu mkubwa wa wanaume ambao ametembea nao, kimsingi huyu mrembo hajapata tu mtu sahihi lakini anafaa kuwa mke wa kulea familia kabisa,”

Hata hivyo daktari huyu pia anasemekana kuwa hapo awali alitoka kimapenzi na Wolper lakini wakamwagana kwa sababu ambazo sio wengi wanajua.

 

Zari Hassan na Diamond Platnumz washerehekea siku ya kuzaliwa ya mtoto wao, Princess Tiffah

Diamond na mpenzi wake Zari The Bosslady walisherehekea siku ya kuzaliwa ya Princess Lattifah Jumapili hii iliyopita kwa kumuandikia ujumbe ambao umewaacha wengi wakifurahia kupitia mitandaoni yao ya Instagram.

Hii ni baaad ya Zari alipojifungua mtoto wa kwanza wa miaka miwili iliyopita. Kupitia mtandao wa instagram, wazazi hao walionyesha furaha zao kupitia ujumbe wao.

Zari aliandika,

“It’s princess world…happy birthday my one and only princess_tiffah.”

Na akaongeza kusema;

“My Princess….. May God see you through with nothing but the best. May you be blessed from this day forward. Most of all, May you be a Godly child. Without God we are nothing. Happy birthday @princess_tiffah,”

Diamond Platnumz naye akaandika;

“Happy 2 years mama, Words Can’t express how much i love you my Tee….

Tiffah ni miongoni mwa watoto maarufu Africa yote.

 

Jini Kabula aeleza familia yake ilivyomtemga baada ya kuugua ugonjwa wa akili

Miriam Jolwa anayetambulika Kama Jini Kabula ni muigizaji aliyepata umaruufu kupitia tamthiliya ya Jumba la Dhahabu. Hata hivyo kwa hivi sasa anaonekana hali ya akili haiko sawa.

Baada ya Wolper kujitokeza na kuwaomba wasanii wenzake kumsaidia Jini, Global TV online iliweza kukutana na yeye Bamaga- Mwenge jijini Dar es Salaam ambapo walizungumza na yeye na kulingana na walichotangaza, ni kweli Jini anapitia wakati mgumu.

Mrembo huyu alifunguka kudai kuwa wetu ana tatizo kwenye akili yake na akaendelea kukiri kuwa ndugu zake walimpeleka Muhimbili ambako alilazwa kwenye wodi ya wagonjwa akili kwa zaidi ya mwezi mmoja na kumtenga.

Kwa Sasa hana sehemu ya kuishi na ndugu, jamaa na marafiki zake, wamemtenga kutokana na matatizo aliyonayo na kumbidi kutangatanga mitaani.

Tazama mahojiano yao hapa;

Faiza Ally aachia picha za mtoto wake, Lil Junior

Muigizaji wa Bongo muvi ambaye pia ni mwanabiashara , Faiza Ally, alijifungua mtoto wa kiume na amempa jina la Lil Junior.

Faiza Ally

Mrembo huyo pia hivi Leo amewachia picha kadhaa kumuonesha mtoto wake ambaye anaaminika kuwa muindi au mzungu. Kupitia mtandao wake wa Instagram aliandika kusema;

“Asanteni sana ndugu zangu Watanzania nimeishiwa na maneno kwa mapenzi yenu. Najiona kila kona kwenye kurasa mbalimbali za marafiki, umbea, habari yaani najihisi kupendwa. Na nimezidi kutambua kuwa uwepo wangu upo, naomba niwaambie nawapenda sana, natambua uwepo wenu wote, natamani ningejibu kila comment , nipite kila kurasa, nijibu msg zote DM na WhatsApp ndiyo usipime yote hayo ni mapenzi, najisikia baraka kwa kweli, furaha yangu inazidi mara dufu ALHAMDULILLAH. Nawatakia kila la kheri na baraka tele kwenu, wanaotafuta watoto Mwenyezi Mungu awajaalie kila la kheri mpate, na waliopata INSHAALLAH, Mwenyezi Mungu awatunzie wawe watoto wenye baraka kwenu AMEN YARAB. Nawapenda Watanzania, naipenda Tanzania, Mungu tubariki sisi na vizazi vyetu AMEN.”

Tazama picha hiyo hapa;

Wolper awasihi raia na wasanii wa Bongo movie kumsaidia Jini Kabula anaye Ugua

Jackline Wolper ambaye ni malkia wa bongo movie amejitokeza kuwaomba wasanii wenzake na raia pia kumsaidia Mariam Jolwa anayejulikana kama Jini Kabula aneyeugua ugonjwa wa akili.

Kupitia mtandao wake Wa a Instagram Wolper aliandika kusema;

Natamani niongee mambo mengi sana juu yako lakini natamani ata kukusaidia urudishe akili yako swali ni kwamba nimechelewa??nakama nimewahi je nitafanikiwa kweli. sasa tuzungumze jambo jamani maana siju hizi tarfa tunazipata insta naona nalangu niliongelee insta wanatasnia wenzangu tunamsaidiaje mwenzetu nini kimekuta kipi je nayoyasikia ndio hayo????nakama ndio mbona kuna wataalam wakusena nae naakakaaa sawa. Basi watanzania wenzangu naombeni tuchangie maoni yenu hapa nakama nim2 uwezi toa ushauri hapa basi tuma msg kwakupitia cm hii 0765776776 basi tuweze kumrudisha kabula jamani. naandika msg hii huku nalia namoyo mdogo sana usiweza kuvumilia naumivu nakumbuka nimishawahi kumwambia kabula we nimwanamke mzuri sana bongo movie lkn natamani kujua tatizo nini kacheka tuu akachukua nguo akaondoka sikupata muda wakuzungunza nae ….sasa npo safarini hope kesho au kesho kutwa nikijaliwa tukutane kwaoamoja .. Bongo movie tumfwate alipo jamani tujue tunamsaidiaje nimeona vdio anaongea sjui niamechanganyikiwa masikn me ata nashindwa kuandika jamani ….

Nuh Mziwanda akiri kubadili dini

Mkali wa Bongo Fleva Nuh Mziwanda amesema kuwa Sasa yeye ameirudia dini yake ya kwanza, Mkristo, baada kuachana na aliyekuwa mke wake.

Nuh alisema haya baada ya kuzungumza na XXL ya Clouds FM, huku aliendelea kusema ni kweli alikuwa kanisani Jumapili hii iliyopita na kukiri kuwa habari zinazoenea mitandaoni ni za kweli. Msanii huyu alisema;

“Nimerudi kwa Mungu wangu ili mambo yangu yaende vizuri maana tunafanya muziki wa dunia anatusamehe ila kurudi kwake pia ni jambo la kawaida sana.”

Aliendelea kwa kujibu tariffs zilizotolewa na aliyekuwa mke wake kuwa ameacha kumjali mtoto wake. Nuh alisema;

“Mara ya mwisho nilikuwa na Anyagile kwenye photoshoot ya ngoma yangu mpya jana kwa Mx Carter, inayotoka hivi karibuni sasa yeye anavyosema sijamuona mtoto muda mrefu sijui anamaanisha nini. Anaongea vibaya kwenye media sio vizuri, mimi na fan base yeye mwanamke anatakiwa ajue anaongea nini, ila muache aongee akikua ataacha, vile vile mimi sina tatizo naye kama kaolewa, yeye si ndio kaamau mimi bado kijana na kila mtu anafanya anachotaka mimi nimemrudia mungu huwezi jua atanipatia mke mwingine mwema”.

Faiza Alley ajifungua mtoto wa pili (video)

Mrembo wa Tanzania na pia malkia wa Filamu Faiza Alley amejufingua mtoto wa pili kulingana na ujumbe alioweka mtandaoni wake wa Instagram.

Faiza Ally
Faiza Ally

Faiza ambaye anatambulika na wengi kutokana na mavazi yake ya kushangaza alitangaza habari hizi kwa kuweka video fupi ya mtoto huyo akiwa hospitalini, na kuandika

“ALHAMDULILLAH @lijunior_ well come to the world baby.”

Faiza amejiunga na wanawake maarufu bongo waliobahatika kupata watoto mwaka huu. Tazama video hiyo hapa;

https://instagram.com/p/BXUSHSigswW/

Hamisa Mobetto aachia picha mpya kuonesha ujauzito wake

Mrembo wa Tanzania Hamisa Mobetto leo ameachia picha mpya huku akionekana kuonesha ujauzito wake kupitia mtandaoni wake wa Instagram.

Hamisa Mobetto aliambatanisha picha zake kwa kuweka wazi kuwa amemfungulia mtoto anayemtarajia akaunti mpya ya Instagram ambayo ameiweka jina la ‘Tanzanian baby’ na kufikia saa hii imepata followers/mashabiki 4702.

Hata hivyo Hamisa ameweka picha mbili ambazo amevalia nguo nyekundu huku akionekana amekumbatia mimba yake. Tazama picha hizo hapa;

Abdu Kiba adai hajamuona wa kushindana na Ali Kiba

Msanii wa bongo Abdu Kiba amefunguka kudai kuwa kaka yake, Ali Kiba, ni msanii ambaye bado hajapata mtu ambaye anaweza kumfikia ikifikia wakati wa kutunga na kuachia nyimbo.

Akizungumza na kipindi cha XXL cha Clouds Fm hivi karibuni Abdu Kiba alisema kuwa yeye na Ndungu yake hawapendi kuhusishwa na team za kimuziki au kuonekana wanajipanga kushindana na watu fulani.

Aliendelea kwa kusema kuwa yeye na Kaka yake bado wanafanya kazi ambazo bado hawajapata watu wa kushindana nao.

“Sisi tunachukulia ni changamoto kwa sababu sisi hatushindani, tunafanya kazi na hatujaona bado wa kushindana nao, hakuna mtu wa kushindana na sisi, yaani sijamuona wa kushindana naye na hakuna wa kushindana na sisi na sisi hatushindani,”

 

Shetta hatimaye awajibu mashabiki wake

Msanii wa bongo Shetta aliachia ngoma yake mpya ‘Wale Wale’ hivi karibuni na kulingana na YouTube inaonekana kuwa Shetta aliangusha wimbo ambao umewaacha mashabiki huku kama wamefurahi.

Hata hivyo, Shetta ameonekana kuwajibu mashabiki wanaodai asikae kipindi kirefu bila kutoa ngoma.

Shetta

 

Hii ni baada ya kukawia zaidi ya miezi 10 bila  kutoa wimbo. Akizungumza na E-Newz ya EATV Shetta alisema;

“Mimi naamini katika kitu ambacho nakifanya, nimeshauriwa nifanye back to back lakini hata hiyo itaongezeka ngoma moja au mbili, sidhani kama natakiwa nifanye vitu ambavyo watu wanasema au wanafikiri ni sawa, mimi natakiwa niamini katika kitu ambacho nafanya,”

Aliendelea kwa kusema;

“Lakini kutokana mashabiki wanataka pia nafuata kile wanachopenda nitajaibu kubadilika ila katika moyo wangu siamini katika kutoka nyimbo nyingi. Bajeti pia huwa inabana kutokana kitu ninachotaka kukifanya pia ni kikubwa,”

Hii ndio sababu Barnaba hataki kufanishwa na mtu yeyote

Msanii wa Bongo Fleva, Barnaba amesema kuwa hakuna msanii yeyote Bongo anayeweza kufananishwa naye kwa sababu yeye anauelewa muziki ambao anaoufanya.

Akizungumza na Mikito Nusunusu , Barnaba alisema kuwa kipaji chake amekitoa kwa mungu na anamshukuru Mungu kwa kumjalia kipaji cha kipekee kwenye muziki na kwamba ataendelea kukitendea haki. Alisema;

“Mimi ni mwanamuziki na si msanii, lazima kwanza utofautishe mambo hayo mawili, ndiyo maana ninaweza kutunga na kuimba na hata kutumia vyombo vyote vya muziki, hiyo ndiyo maana halisi ya mwanamuziki. Naomba sana nisifananishwe na mtu kwenye eneo hilo. Nilizaliwa kuburudisha watu na ninafanya muziki kama sehemu ya maisha yangu, siangalii fedha na masilahi, muziki uko kwenye damu,”

Shilole atangaza harusi baada ya kutolewa posa

Kuna fununu kuwa msanii wa Bongo Fleva, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ au ‘Shishi Baby’ ametolewa posa na mchumba wake ambaye bado hajamjulisha kwa mashabiki wake.

Kulingana na chanzo kilicho ongea na Ijumaa Wikienda inasemekana kuwa shishi hataki watu wakimjua mwanaume wake kwa ajili anataka kuiweka ndoa yake iwe Siri, chanzo hicho kilisema;

“Si unawajua tena mastaa wetu? Hawachelewi kufanya yao ndiyo maana Shishi hataki kumwanika mwanaume wake kwa madai kwamba anaogopa wajanja wasije wakapita naye kama ilivyo kwa yule aliyekwapuliwa na Nisha (mwigizaji Salma Jabu).”

Aliendelea kwa kusema;

“Baada ya mbilingembilinge nyingi za mjini, hatimaye Shishi sasa anaolewa na hapa tunapoongea ndiyo kwanza watu wamerudi Dar kutoka Igunga (Tabora) nyumbani kwa akina Shishi kupeleka posa. Kwanza ishu ilikuwa ni kumtambulisha mwanaume kwao ndipo wakaona wamalize kabisa na suala la posa hivyo kifuatacho ni kufunga ndoa ambayo nasikia itakuwa ndani ya mwaka huu,”

Hata hivyo Ijumaa Wikienda ilipompigia Shishi kujua kama ni ukweli alifunguka kusema;

“Wewe ujue tu ni kweli nimechumbiwa lakini kuhusu kumwanika mtarajiwa wangu, kwa kweli sipo tayari. Maana kwa upande wa wanaume wanaonyatia wanawake wa watu wanaitwa Team Fisi, sasa sijui kwa upande wa wanawake. Au tuseme Team Fisi kwa upande wa wanawake.”

Aliendelea,

“Lakini kimsingi mchumba wangu ni mtu wa kawaida sana na siyo staa,” alisema Shishi na kutoa mwanya kwa mahojiano zaidi kuhusu ishu hiyo.

Kuhusu harusi yake Shishi alisema,

“Mashabiki wangu wajue tu itakuwa soon na itakuwa ya aina yake kwani itafanyika uwanjani na mashabiki wataingia kwa kadi. Mchango utakuwa mdogo ili watu wengi zaidi wahudhurie.”

“Nisipobahatika kupata mtoto nitafunga uzazi” Wema Sepetu asema

Tanzanian sweetheart Wema Sepetu hi karibuni alifunguka kuhusu suala la kupata mtoto katika mahojiano aliyofanya na gazeti la Ijumaa Wikienda hivi karibuni.

Mrembo huyu ambaye ni mmoja wa waigizaji ambao wamefanya vizuri kwenye industry ya Tanzania amedai kuwa kwa sasa akona mpenzi ambaye wametulia pamoja na pia wanajaribu kupata mtoto pamoja.

Wema Sepetu

Aliendelea kwa kudai kuwa baada ya kupoteza mapacha wake imemchukua muda kuwasahau lakini kila kitu hufanyika kwa nguvu za mwenyezi mungu.

Hata hivyo aliweka wazi kuwa asipopata mtoto kabla ya kufikia miaka 32 basi atafunga kizazi. Lakini akona uhakika kuwa atapata mtoto kwani amepata ufumbuzi wa kitaalam na kujua tatizo lake ni lipi. Alisema;

Ndiyo na tena safari hii nisipobahatika kupata mtoto hadi ninafikisha umri wa miaka 32 (kwa sasa ana 29), nitafunga kizazi.

 

Aunty Ezekiel avunjika moyo baada ya ‘mama’ yake kufariki

Wikendi hii iliyopita mrembo wa filamu za bongo Aunty Ezekiel alimpoteza nyanya yake ambaye alimlea toka utotoni na kulingana na habari zinazoenea, bibi yake alikuwa kama mama na baba kwake baada ya wazazi wake kufariki.

Picha zinazoenea mitandaoni Aunty Ezekiel anaonekana kuwa na majonzi mengi lakini marafiki zake walikusanyika kumfriji huku wengi wakiandika ujumbe kupitia nguvu kumtia nguvu.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Aunty Ezekiel aliandika kusema;

Kweli la mungu halina muhamuzi mungu akuweke mahari pema peponi bibi

“Usiogope maneno ya watu” Diamond Platnumz amwambia Harmonize

Wikendi hii iliyopita, Diamond Platnumz, Harmonize na warembo wao walifika katika klabu maarufu ya Nairobi, B Club kuwatumbuiza mashabiki wao wa Kenya katika show iliyowavutia wengi.

Wakali hao wawili wanaaminika kuwa marafiki wa karibu waliwapa wengi kitu cha kuongea hasa baada ya kuonekana na warembo wao, Zari na mpenzi mpya wa Harmonize anayetambulika kama Sarah.

Hata hivyo Diamond Platnumz aliwashangaza wengi baada ya kumuandikia Harmonize ujumbe kupitia Instagram huku akimsihi asiogope maneno ya watu kwani wamepata fedha na mali ya kutosha kupitia muziki wao.

Tazama picha hiyo hapa;

https://instagram.com/p/BXMcjb7FSgD/

Ruby afunguka baada ya kudaiwa kuwa ujauzito wake ni wa Alikiba

Mwanamziki wa bongo Ruby anadaiwa kuwa na mimba ya Alikiba, hata hivyo hakuna aliye na uhakika wala dhibitisho tosha kuhusu uvumi huu.

Akizungumza na Bongo 5 hivi karibuni Ruby alikiri kuwa amesikia maneno Hata, lakini kulingana na yeye huu ni uvumi usio na ukweli wowote.

Ruby aonyesha mimba yake

Ruby aliendelea kuongeza kwa Sasa amezoea kusikia watu wakidai kuwa yeye ni mpenzi wa Kiba, lakini hana la kusema kwa sababu uhusiano wake na Kiba ni wa urafiki tu.

Tazama mahojiano yake na Bongo 5 hapa;

Harmonize amshirikisha Mr Nice kwenye video yake mpya!

Mkali wa label ya WCB Harmonize ameachia video mpya ‘Sina’ ambayo inaonekana kuwapendeza wengi baada ya kumshirikisha Mr Nice Kama video vixen wake.

Mashabiki wamemshukuru Harmonize na label ya Wasafi kwa kumuamuni Mr Nice na nafasi hiyo ya kuieleza hadithi ambayo Harmonize anayoielezea kwenye wimbo huo.

Itazame video hiyo ambayo imeongozwa na director Khalfani.

Wema Sepetu afunguka kueleza kinachomkera kuhusu Tanzania ya sasa

Mrembo wa filamu Wema Sepetu ameonekana kukasirishwa na alichofanyiwa mtu mmoja aliyekutana na yeye mahakamani hivi karibuni.

Wema Sepetu aliweka tweet kadhaa kupitia mtandao wa Twitter huku akionekana kama amekasirika kwa kilichomtokea mtu huyo wakati wa kusikiliza wa kesi ya Mh.Tundu Lissu.

Aliandika tweet hizo akisema;

 

Z-Anto amtaja mnigeria atakaye shirikiana na yeye hivi karibuni

Z-Anto ambaye ni mmoja wa wasanii ambao walianza muziki zamani ameonyesha uwezo wa kurudisha nyimbo kama za hapo mbeleni baada ya kuachilia nyimbo kadhaa.

Hata hivyo bado hajapata nafasi ya kushirikiana na wasanii wengi lakini kuna uvumi kuwa staa huyu wa Bongo Fleva, huenda akafanya kolabo na pacha wa Kundi la P-Square, Peter Okoye.

Akizungumza na Over Ze Weekend, Z-Anto alianza kuupongeza uongozi wake wa South For Life (SFL) kwa kumsaidia kuachia nyimbo mzuri zinazovuma kwa sasa. Aliendelea kuwashukuru kwa kkumuunganisha na wasanii wakubwa akiwemo Peter Okoye. Z-Anto alisema,

“Ni furaha ya juu niliyonayo. Yote kwa sasa nawaachia South For Life kwani nipo chini yao, endapo mipango itakaa poa basi mtanisikia nikipaa kimataifa,”

Mashabiki wake Wa Afrika mashariki kwa hivi sasa wanaingojea kuiona project yake.

Hawa kutoka ‘Nitarejea’ alioshirikishwa na Diamond adaiwa kupotelea kwenye vileo!

Nitarejea ni wimbo ambao bado unafanya vizuri Hata baada ya kuachiwa mwaka Wa 2013. Diamond Platnumz alimshirikisha muimbaji anayejulikana kama Hawa na kutokana na sauti yake nzuri, mrembo huyu alitarajiwa kwenda mbali lakini hivyo sivyo mambo yalienda.

Hawa anasemekana kuwa alipata mtoto wake Wa kwanza anayedaiwa kuwa mtoto wa Diamond Platnumz na baadaye akafunga ndoa na mwanaume mwingine ambaye amemsababisha kuingilia vileo kutokana na ‘stress.’

Sasa hivi mrembo huyo amekiri kuwa maisha yake ilipotelea kwenye unywaji wa pombe kali aina ya gongo, kiasi cha kumfanya apoteze mwelekeo maishani mwake.

Akizungumza na Global TV Hawa alisema kuwa alijipata kwenye maisha haya baada ya mumewe kuondoka na kumuacha bila mawasiliano yoyote kwa muda wa miaka miwili baada ya kukaa kwenye ndoa yao kwa muda mfupi.

Kutoka na kufikiria sana, Hawa alitafuta namna ya kutoa ‘stress’ na akaingia kwenye vileo ambavyo vimemdhoofisha kimwili. Amedai kuwa amekonda huku akiomba msaada kutoka kwa mashabiki na wadau kumsaidia kuepuka maisha haya ambayo yanampeleka vibaya.

 

Profesa Jay atajavitu ambavyo vilimpendeza katika harusi yake

Msanii na mbunge kutoka bongo Profesa Jay alifunga pingu za maisha na mpenzi wake Grace – huku akiwavutia wengi kutoka Tanzania.

Sherehe ya harusi yake ilihudhuriwa na wasanii kama Diamond Platnumz, AY na wengi waliotumbuiza wageni na wazazi wa Profesa Jay na Grace.

Hata hivyo hivi karibuni msanii huyu alifunguka kutaja mambo matatu yaliyomvutia Profesa Jay katika harusi yake. Akizungumza na FNL ya EATV Profesa alisema,

“Chakwanza ni support kubwa ya watu wangu wa mtaa, nikaona watu wote wapo pale especially wasanii wenzangu walikuwepo sana sana, wengine walishindwa kuja kwa sababu mbali mbali,”

Aliongeza kusema;

“Pili media ime-play part yake vizuri sana, lakini kikubwa mbacho namshukuru Mwenyenzi Mungu mbele za haki nimejitahidi hata kuungainsha siasa zetu za Tanzania. Viongozi wote waliopata kuongea  walisema huyu jamaa ametuunganisha, watu wa vyama vyote walikuwa pale, watu wa dini zote walikuwepo pale, ni kitu kikubwa namshukuru Mungu,”

Huyu ndiye mrembo anayetoka na Gnex_thebaddest Wa Clouds FM?

Kuna fununu kuwa mtangazaji wa CloudsFM Gnex_thebaddest anatoka kimapenzi na mrembo mmoja ambaye ni mwanahabari kutoka Kenya, Kamene Goro.

Hii ni baada ya Gnex_thebaddest kuachia picha kadhaa kupitia mtandao wake Wa Instagram huku akimsifia mchumba wake kwa maneno matatu.

Kamene Goro pia amekuwa akiweka picha za Gnex_thebaddest akiziambatanisha na ujumbe unaodhibitisha kuwa wawili hawa wanauwezekano wa kuwa wapenzi.

Mrembo huyu wa Kenya anafanya kazi na kituo kinachoitwa Ebru Tv na ni mtangazaji wa habari za adhuhuri na anatambulika sana kutokana na umbo lake linalowatia wengi wasiwasi. Tazama picha zake hapa:

 

Sababu ya kesi ya Masogange kutosikilizwa mwezi huu

Agnes Gerald anayetambulika kama Masogange bado anangoja kusikilizwa kwa kesi yake baada ya kutofika mahakamani Jana, Julai 13, 2017 kama ilivyohutajika.

Kulingana na wakili wa mrembo huyu, inasemekana kuwa hangeweza kufika kutoka na kuumwa kwa mwili. Wakili wake, Reuben Simwanza akizungumza na hakimu aliomba radhi kwa mteja wake.

Agnes Masogange
Agnes Masogange

Hata hivyo wakili wa Serikali, Constantine Kakula, hakufurahishwa na maneno haya huku akikumbusha mahakamani kuwa hapo mbeleni Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri, alikuwa amepeana amri ya kuwa kesi hiyo ianze kusikilizwa Jana.

Agnes Masogange

Wakili wa Masogange aliweza kuisihi mahakama kuihairisha kesi kesi hiyo hadi July 25, 2017. Masogange hata hivyo ameshtakiwa kwa makosa ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroine na Oxazepam na Heroine.

County Boy aeleza mipango yake ya kuwa kutanisha Alikiba na Diamond Platnumz

Mwananziki Country Boy kutoka Tanzania amefunguka kudai kuwa ana mipango ya kuwakutanisha Diamond Platnumz na Alikiba – kitu ambacho tunajua ni ngumu kufanyika.

Msanii huyu akizungumza na Daladala Beat ya Magic Fm alidai kuwa kwa hivi sasa anataka kuwashirikisha wasanii hawa kwa wimbo wake mpya, huku akitarajia kuwa watasikizana. Country Boy alisema;

“Round hii nataka nilete different sound kwa sababu tayari am rapper nataka nitengeneze sound mpya. Nawataka hawa malegendary wawili, hapa Alikiba, hapa Diamond ila siwashirikishi katika track moja, kila mtu na ngoma yake,”

Aliendelea kwa kusema…

“Kila mtu na upande wake natengeneza sound mpya, nahisi nitaleta kitu kikubwa. Ninachoshukuru kwa Mungu mimi nipo flexible naweza kurap katika beat yoyote,”

Hata hivyo wacha tuone Kama Country Boy ataweza kufanya hivi.

Aunty Ezekiel aachia picha mpya kuonesha Princess Cookie alivyokuwa mkubwa!

Muigizaji wa filamu Aunty Ezekiel anafurahia kumuona Cookie akiendelea kuwa mkubwa kila kuchao.

Cookie

Mrembo huyu hivi karibuni aliachia picha mpya za mtoto wake kupitia mtandao wa Instagram huku mashabiki wakiduwaa kumuona alivyokuwa.

Sasa hivi cookie ako karibu kufikisha miaka minne na tunavyojua ni kuwa mtoto huyu amejiunga na shule ili kujifahamisha na wenzake.

Hata hivyo, Ezekiel anaonekana ameipa kazi yake ya uigizaji ili kumpa mtoto wake attention. Tazama picha zao mpya hapa chini;

Chini Bees amjibu Chid Benz baada ya kumchana

Baada ya Chid Benz kumwambia msanii mwenzake Chin Bees awembunifu na kutafuta jina lingine…. Chin Bees ameamua kumjibu mwenzake.

Wawili hawa ambao wanaonekana kuwa na beef kutokana na kufanana kwa majina yao, uenda wakakosana baada ya Chin Bees kusema kuwa hawezi kubadilisha jina ili kumkwepa Chid Benz.

 

Akizungumza kwenye mahojiano na E-News ya EATV, Chin Bees ambaye ni mmoja wa wasanii wanaotamba kupiti nyimbo zake za bongo Fleva aliweka wazi kuwa hana mipango ya kubadilisha jina kwa kuwa hata yafanani. Chin Bees alisema,

“Mimi siwezi kubadilisha jina kwa sababu ya Chid Benz kwa sababu halifananini, very different. Mimi nafanya muziki wangu, siwezi nikakaa nipiganie jina, hivyo bro kama anahitaji jina dah!, sidhani kama jina langu linaendana na lake  me am do my thing.”

Haya basi tutazame tuone watakachafanya sasa!

Nuh Mziwanda afanyiwa upasuaji wa shingo

Msanii wa Bongo Nuh Mziwanda ameandika ujumbe kuwashukuru madaktari wa hospitali ya Mwananyala kwa kumfanyia upasuaji wa shingo baada ya kupata maumivu makali shingoni.

Nuh Mziwanda anayejulikana kwa hit song yake ya Jike Shupa, aliweka picha huku akionekana na bandage shingoni na tabasamu usoni kwa upasuaji salama.

Ingawa bado hajafunguka kusema kilichotokea, Nuh aliandika ujumbe kusema,

“Thanks Jesus….thanks MY SUPER DR KIWALE BINGWA kabisa wa upasuaji ‘Na MWANANYAMARA HOSPITAL kwa surgery (Upasuaji)uliokua chini ya shingo yangu’ bila kusahau MAMA yangu na ndugu zangu waliokua pamoja na mimi.naomba Maombi yenu Mashabiki wangu nirudi katika hali yangu na Kazi ziendelee.Love you.”

Msanii mpya wa Wasafi Records Lava Lava azindua video ya wimbo wake-Bora Tuachane

Lava Lava ameachia wimbo mpya Bora Tuachane ambao unawazingua wengi Afrika Mashariki. Tangu Diamond Platnumz kumtambulisha kama msanii wa Wasafi…Lava Lava amepata mashabiki wengi kwa muda mfupi kuonyesha kuwa yuko tayari kuwatumbuiza wengi.

Hata hivyo Lava Lava ameachia video yake ya kwanza tangu kuingia Wasafi. Video hii imekuja siku mbili tangu kuachia audio.

Mashabiki nao pia wameonekana kumpa support msanii huyu ambaye kwa hivi sasa anawazingua wengi. Sauti yake pia ni ya kumtoa nyoka pangoni na inaonekana kuwa atawapa Harmonize, Rayvanny na Rich Mavoko competition ya kutosha. Tazama video hiyo hapa.

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.