Diss gone sour:¨Hata Msupa S is way better than you. Uza mbogo tu!¨ fans strike back at Noti Flow in her self-praise diss post

Kenyan female rapper, Noti Flow disses fellow female rappers articulating that the only competition she has in AFRICA, is Rosa Ree Alone!!!

She takes to Instagram while on holiday to forewarn female rappers who think they can beat her at her game.

https://www.instagram.com/p/Bv3viCGANzH/

She is currently out on adventure with lover, Colonel Mustafa.

Badass Tanzanian female rapper, Rosa Ree is known for her ´Banjuka´ and Up In the Air´ jams.

Backlash

However, seems she wasn´t well conversant with her b*tchy attitude and fans came out to counter her disses:

Girl you have a long way to go!!! Many people haven´t heard of your a***!

nasra.khan

@notiflow Lmao ????????????????????continue consoling urself there some real bitches making music kula lip undamages pole pole hakuna mwenye haja na wewe..????

sheilah_fridah

Ukijiita queen of rap @petramuzic tutamuita nini king of rap????????????….you are lost.

Be humble dunia ndogo????

mariamu_missvee

Too much pride

mutie64

Lakini huyu dame hujifeel sana na hana mistari then she does the baddest mistake by comparing herself to the best FemCee in Africa …very stupid

@notiflow

you ain´t sh*t.. stop comparing yourself to Rosa Ree na bado huwezani na Xtatic, Femi One, Kiki, Wangechi and all other female rappers in the mainstream [Kenya].

Hauna Flow, Hauna barz, uko tu na mdomo mingi.

Kami hii kitu umeandika ni nyingi but no point in it.. you´re a whack FemCee my dear.. Hata Msupa S is way better that you.. so acha kubonga sh**t.. keep them for yourself please

jamesweezy_real_rapper

Huna lolote wewe hata unaimbaga nn ??

Ety Africa…ww uza mboga

kelvin_ngisa

“Wanawake Lazima Tuwape Heshima Wanaume”- Rosa Ree

Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayetamba kwa miondoko yake ya kuchana Rosary Robert maarufu kama Rosa Ree amefunguka na kusema kuwa ni vizuri kama Wanawake watawapa heshima wanaume.

Rosa Ree ameibuka na kusema kwamba ni vizuri Sana  kama Wanawake Wataanza kuwapa heshima wanaume heshima wanayostahili hasa kwa sababu ya mambo mengi ambayo wanayowafanyia.

Katika mahojiano aliyofanya na kituo kimoja cha habari, Rosa Ree amefunguka haya kuhusu heshima kwa wanaume:

Kiukweli inabidi tuwape heshima wanaume, wanajitahidi sana kutufanya tuwe na furaha sio kila siku kuwaimbia wanawake tu kwenye mapenzi, wanaume wanafanya mengi sana kwa ajili yetu ndio maana nimeandika wimbo huu kwa ajili yao”.

Rosa Ree ametoa Wimbo Wake Mpya wa ‘Asante Baba’ ambao ndani yake una ujumbe wa kushukuru wanaume.

Rosa Ree Atangaza Kuachana na Uongozi Wake

Mwanadada Rosa ree ameamua kutangaza na kusema ukweli kuwa kwa muda sasa amekuwa hafanyi kazi na uongozi wake aliokuwa akifanya nao kazi , uongozi ambao makao yake yalikuwa nchiki Afrika ya Kusini.

Rosa ree anasema kuwa yeye na uongozi wake wa Dimo wamekuwa hawafanyai kazi pamoja kwa sasa kutokana na sababu ambazo haziwezi kuzuilika kwa muda na ndio maana tangu mwaka 2018 October msanii huyo amekua akifanya kazi na watu wke wa awali.

Hata hivyo mwanadada huyo anasema kuwa inaishukuru kampuni hiyo kwa kufanya nayo kazi kwa kipindi walichokuwa pamoja ingawa pia kufanya kazi pekeyake kumemfanya kuwa imara zaidi.

Rosa anasema kuwa tangu ameachana na kampuni hiyo  mpaka sasa ameweza kutoa nyimbo mbili ya banjuka pamoja na asante baba ambazo pia zimekuwa zikifanya vizuri kwa sasa.

Rosa ree alitangaza kuwa katika mkataba na Dimo kwa miaka 3 ikiwa mkataba huo ungeanza kufanya kazi March 2018.

Rosa Ree Adai Bado Mdogo Mambo Ya Mapenzi Hataki

Msanii wa Bongo fleva anayefanya hip hop pia Rose Robert maarufu kama Rosa Ree ameibuka na kudai kuwa sababu inayomfanya asiharakishe kuingia kwenye mapenzi ni uamuzi.

Rosa Ree ameibuka na kudai kuwa anapokuwa hayupo kwenye mapenzi haimaanishi kuwa hakuna watu wanaomfuta kwa lengo la kumshawishi Lakini yeye mwenyewe ameamua kutulia kwenye sekta hiyo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi cha Refresh cha Wasafi Tv, Rosa Ree amesema kuwa anaamini kuwa umri wake bado mdogo hivyo hana papara na mapenzi.

Mapenzi yapo, napenda familia yangu, nampenda Mwenyenzi Mungu, napenda pesa, mimi mdogo sana, am very young, yaani sio kwamba hawapo ambao hawatamani kuwa na Rosa Ree lakini hatuendani”.

Ingawa Rosa Ree ameshatajwa kuwahi kuwa kwneye mahusiano na wasanii Kama Young Dee na Bill Nas Lakini aliwahi kukataa na kusema kuwa wale ni washkaji zake tu.

Mapenzi yapo, Napenda pesa :-Rosa Ree

Mwanadada mwenye sifa za kipekee huku watu wakimsma sana kuhusu swala lake na kutokuwa na mahusiano amefunguka na kuelezea kwa nini kwa sasa hataki sana kujikita katika mahusinao kama mashabiki zake wanavyomuhoji huku wakitaka kuweka mahusinao yake hadharani.

Rosa ree anasema kuwa kitendo cha yeye kutokuwa katika mahusinao haimaanishi kuwa hakuna wanaomfuta kwa ajili ya kuwa nae katika mahusiano lakini kwake anaona mud wake bado kwa sababu anaamini kuwa yeye bado mdogo sana.

mapenzi yapo, napenda familia yangu, nampenda mwenyezi mungu na pia napenda sana pesamimi mdogo sana , am very young , yaani sio kwamba hawapo wanaotamani kuwa na rosa ree hapana lakini tu  hatuendani.

Mara nyingi mwanadada huyo amekuwa akisisitiza kuwa watu wasiomuenoa kama yuko tofauti kwa sababu ya swala la mapenzi tu kwa sababu hata yeye ana moyo wa kupenda na pia anaogopa kuumizwa.

Rosa Ree Ataja Sababu Za Kuonekana Kuwa Mgumu

Msanii wa muziki wa hip hop nchini anayefanya vizuri na ngoma yake ya ‘One way’ Rosemary Robert maarufu kama Rosa Ree amefungukia madai ya wadau wengi kuwa yeye ni mgumu.

Rosa Ree amesema kuwa watu wengi wanamuona mgumu kutokana na mavazi yake na jinsi alivyo lakini siyo kihivyo bali hapendi kujibebisha kama wafanyavyo wanawake wengine.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Rosa alisema kuna watu wengi wanamuona ana mambo ya kiume kwa sababu hajawahi kuonyesha mpenzi wake hadharani na hiyo ni sababu ya uhusiano wake wa kimapenzi kuwa binafsi zaidi.

Unajua wengi hawanielewi wanasema nina tabia za kiume lakini ukweli sipendi kujibebisha au kujilegeza na pia uhusiano wangu wa kimapenzi ni binafsi zaidi sipendi kuweka hadharani kabisa” .

 

Rosa Ree Akiri Kuacha Pombe Baada ya Kuona Haina Nafasi Katika Maisha Yake.

Mwanadada Rosa Ree anaetikisa kwa sasa katika anga za muziki wa hip-hop nchini amefunguka na kusema kuwa japokuwa hapo awali alikuwa akinywa sana pombe lakini alikuja kugundua kuwa hatakiwi kutawaliwa nayo hivyo aliamua kuachana  nayo.

Akiongea na EATV, rosa reee anasema “unajua pombe ukiipa nafasi kubwa ya kutawala maisha yako hautaweza kuiacha hata mara moja, ila wewe ukiitawala pombe unaweza kuiacha na ndio maana hata mimi niliweza “

Mbali na kuwa msanii wa hip-hop rosa ree amekuwa na muonekano wa tofauti sana na wasanii wengine wa kike hata anavyosema kuwa atumii kilevi inaweza kuwa ngumu baadahi ya watu kuamini kutokana na muonekano.

Rosa atoa ufafanuzi picha yake Dc Jokate Mwegelo

Mwanadada Rosa Ree amefunguka  na kuelezea kwa undani juu ya picha inayosambaa katika mitandao ya kijamii ikimuonyesha yeye akiwa amepiga picha na mheshimiwa Dc Jokate Mwegelo miaka ya hapo nyuma.

Picha hiyo ambayo watu wengi walidhania kuwa kutakuwa kuna wimbo mpya katia ya wadada hao wawil, Rosa Ree amekanusha na kusema kuwa waiwli hao waliwahi kufukiria kufanya project moja ya nywele ambayo ilikuwa chini ya Jokate na kampuni yae ya Kidoti.

Rosa Ree anasema kuwa “actual sio ngoma , ilikuwa ni project ya nywele tulikuwa tunataka kufanya na nina kumbuka kipindi hicho nilikuwa the industry,tulikuwa tunaweka brand ya nywele na tulitaka kuweka brand ya rosa ree na kidoti kwa pamoja.”

Rosa Ree Asema Sababu ya Kufeli kwa Show Yao .

Wiki kadhaa zilizopita iliripotiwa  kuwa kulikuwa na show iliyofanyika nje ya nchi iliyomhusisha Rosa Ree na Aslay ambapo walilalamikiwa kwa sababu hakukuwa na mashabiki katika ukumbi waliofanyia show.

Inasemekana kuwa uwaja huo ulikuwa mtupu kabisa na haikuwa kawaidia kwa watu kutokutoka katika show za wasanii wa kitanzania kwa sababu nyimbo za huku zinapendwa sana na watu wa je .

Hata hivyo baada ya kuulizwa na XXL , rosa ree alijibu sababu kubwa ya kufeli kwa shoo hiyo ni kutokana na maanadalizi machache ya promoto na ukizingatia kuwa hawakuwahi kufanya kazi hawali na promota huyo.

akiongea na XXL,  anasema “show haikuwa poa na watu hawakuwa wengi kwa sababu promota hakujiandaa vizuri, yeye hakufanyaia matangazo nakumbuka baada ya kupata visa ndio alianza kutangaza show.watu waliojua kama kuna show walikuwa wachache, lakini mimi ni mfanya baishara najua kuna kupata na kukosa , ni promota wa kwanza kufanya nae kazi lakini aliwahikufanya kazi na Mh Temba nadahani aliamini kuwa show itakuwa poa  kwa sababu wasanii wote tulikuwa wakali.

Rosa Ree watolea Povu Wanaomsema Kuhusu Style Yake ya Kubinua Midomo.

Mwanadada anaefanya vizuri katika ku-rap Rosa ree amefunguka na kusema kuwa anakerwa sana na watu wanaokaa na kumsema vibaya kuhusu tabia yake ya kubinua midomo ilhali hakuna cha maana wanachomuongezea katika maisha yake na katika kile anachokifanya.

Rosa ree amesema kuwa hiyo ni style yake ya pekee yake katika nyimbo zake na inawezekana ndio inayowatofautisha na watu wengine.

hawanilipii bili pamoja na kubinua kwangu midomo na kutoa ulimi, sasa hivi nina super market , nimefanya kolabo na wasanii wengine  wa kimataifa, nafany vitu vikubwa mimi mwenyewe maneno ya watu hayajiandiki usoni wala hazilipi bili ila zingekuwa la ningejali.

Kujiamini na Kusimamia Ninachokiamini Kimenipa Mafanikio-Rosa Ree

MSanii wa Muziki wa Bongo fleva anayetamba kwa miondoko yake ya kipekee ya kurap amefunguka na kutoa siri yake iliyompa mafanikio mpaka leo yupo alipo kama Mwanamuziki.

Rosa Ree ambaye amewahi kufanya vizuri sana na wimbo wake ‘Way Up’ amefunguka na kuweka wazi siri ya mafanikio yake kwanza ni kujiamini halafu na kuamini anachokifanya.

Kwenye mahojiano na  Global Publishers, Rosa Ree alifunguka kuwa muda mwingi huko nyuma watu walikuwa wanamwambia kwamba anajifanya mnyamwezi kwa soko la Bongo hawezi kufika popote, lakini hakuwasikiliza kwa sababu alikuwa anawaza kwenda kimataifa.

Nisingejiamini na kusimamia kile nilichokiamini kiukweli nisingefika mahali nilipo leo, siku zote nilikuwa ninatazama soko la kimataifa, kwa hiyo hata maneno ya kunikatisha tamaa sikupenda kabisa kuyapa nafasi”.

Rosa Ree alizidi kupata mafanikio hivi karibuni baada ya kusaini dili la mamilioni na Recording Label  kutoka Afrika ya kusini ambayo ilimpatia nyumba mbili za kifahari.

Rosa Ree Afunguka Hakuna Mwanaume wa Kumhonga

Mwanadada anaefanya vizuri katika kiwanda cha muziki kwa upande wa rap ,Rosa ree amefunguka na kusema kuwa katika maisha haliyoishi mpaka kufikia sasa hivi aona kama kuna mwanaume anaeweza kumhonga hela nyingi za yee kuridhika nazo .

Mwanadada huyo ambae amekuwa akionekana na muonekano wa kiume kila siku na imekuwa ikisemekana kuwa hana mwanaume katika maisha yake ya kimahusiano anasema kuwa haoni kama mwanaume anaweza kumpa ela yoyote inayoweza kumridhisha.

Pia rosa ree anasema kuwa huwa hawaelewi sana wanaume wanapokuja na kumhonga kwa sababu anakuwa haelewi kama  ndio wanaonga au wanajaribu ” mimi sihongeki , kwaio hata mtu akinionga huwa nashindwa kuelewa ni kwamba annihonga au ananijaribu.”

Rosa Ree Azidi Kung’ara Nchini Afrika Ya Kusini

Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri na miondoko yake ya kipekee ya kuchana Rosary Robert Kimario maarufu kama Rosa Ree ameendelea kung’aa Zaidi Sauzi.

Rosa Ree ambaye mwezi uliopita alisaini mkataba mnono na kampuni ambayo inasimamia kazi zake ya  Afrika ya Kusini imeendelea kumsimamia kazi zake vyema na hata kumtangaza zaidi nchini humo.

Rosa amesemekana kuwa gumzo nchini humo kutokana na Media Tour anayefanya nchini humo ambapo mbali na kuzungumza Kizungu lakini kwa kiasi kikubwa amekuwa akizungumza Kiswahili, ili kuonyesha kwamba ni Mtanzania, lakini pia amefunguka kwamba kwa sasa kazi zake kwa kiasi kikubwa atakuwa anafanyia nchini humo kwa sababu menejimenti yake inatoka huko.

Kiukweli Sauz kwa sasa kumekuwa kama nyumbani, ninafanya ziara nyingi kila kukicha na menejimenti yangu imenitengenezea mazingira mazuri ya kufanya kazi. “Baada ya kumaliza tour kuna kitu kikubwa pia kinakuja, mashabiki wangu wakae mkao wa kula”.

 

Rosa Ree Azidi Kung’aa na Uongozi Mpya, Akabidhiwa Gari

Mwanadada rosa ree ambae hivi karibuni nyota yake inaonekana kung’aa sana kwa sasa amekabidhiwa gari jipya na uongozi wake mpya ambao umesaini mkataba mpya kwa sasa chini ya DIMO PRODUCTION .

Katika ukurasa wake wa instagram, Rosa ree aliweka picha akiwa katika gari jipya na kuandika maneno yaliyoonyesha kuwa gari hiyo amekabidhiwa na uongozi wake huo.

Rosa ree wiki chache zilizopita alisema amekabidhiwa nyumba yenye thamani ya zaidi ya milioni 400 na sasa amekabithiwa gari aina ya benzi atakalokuwa akitumia akiwa nchini Afrika ya Kusini.Kwa sasa Rosa ree yupo nchini afrika ya kusini kwa ajili ya kuutangaza muziki wake.

Alichokisema Nahrel Kuhusu Rosa Ree na lebel ya Afrika ya kusini

Mtayarishaji wa muziki kutoka katika kundi la Navy Kenzo nahrel amezungumzia msanii aliyewahi kumsaini katika lebel yake na kisa kuondoka na kuanza kufanya kazi zake mwenyewe Rosa Ree ambae kwa sasa anafanya vizuri sana ktika game kama rapper wa kike.

Nahrel amethibitisha kuwa msnaii huyo kwa sasa amepata dili nono la kusainiwa na moja ya lebel kubwa nchi afrika ya kusini inayojulikana  kama DIMO PRODUCTION ya nchini humo.

mimi nadhani tulichokifanya tumekifanya kwa uwezo wetu,tuliweza kutengeneza kitu ambacho kilionekana.we are proud kutengeneza wasanii kama yeye ambao leo hii wanaweza kuonekana kusainiwa na lebel nyingine ni dili kubwa sana na hata sisi tulivyoamua kuwasaini ilikuwa ni kwa ajili ya kuwasapoti.kwaio Rosa Ree anapopata dili lingine na mimi napata moyo wa kuendelea kusapoti wengine.ninaamini kuwa itamfikisha sehemu nyingine ambayo pengine mimi nisingeweza.

Rosa Ree alianza kufanya kazi na kundi hilo akiwa kama msani aliyesainiwa hapo na kutengenezwa katika kundi hilo mpaka pale iliposemekana kuwa kulitokea mtafarauku uliowafanya kushindwa kufanya kazi pamoja , lakini sasa hivi mambo yanaenda vizuri na kupata menejementi nyingine.

Mimi Napenda Sana Wanaume;-Rosa Ree

Mwanadada Rosa Ree amefunguka na kuwashangaa Baadhi ya mashabiki wanaokaa na kumuhukumu kuhusu swala la mahusiano kwa sababu amekuwa kimya na wala hataki kumuonyesha mtu anaetoka ane kimapenzi.

Rosa Ree anasema kuwa wapo baadh wanaomwita kuwa ni msagaji lakini amekuwa akishangaa swala hilo kwa sababu kwa upande wake aamini swala la Mapezi ya jinsia moja hivyo  wake si kitu cha kawaida.

Hata hivyo Rosa Ree anasema kuwa anaamini kuwa mwanamke ameumbwa kwa ajili ya mwanaume hivyo usagaji kwake sio dili.

hivi karibuni walisema natoka na MT . mara natoka na Billnass kisa tu tulisafiri tukaenda kutoa ngoma nje ya nchi, am just working guys, mimi sijui kuhusu hiyo idea ya wasichana kuwa wasagaji lakini ilishazoeleka kuwa ili msichana aweze kufanya mzuki wa hip-hop lazima awe mgumu kama mwanaume,wakikuona umevaa kama mwanamke wwanaanza kukuliza kwanii umevaa hivyo.

i dont believe in mapenzi ya jinsia moja,i love men men, nawapenda sana wanaume na ninaamini kuwa wanaume wameumbiwa sisi.

Rosa Ree Afunguka Kuhusu Kujiunga WCB

Msanii wa Bongo fleva Rosary Robert ‘Rosa Ree’ aliyejizolea umaarufu kutokana na  miondoko yake ya kuchana amefunguka juu ya mipango ya kusaini na Label maarufu nchini WCB.

Rosa Ree ambaye amekuwa akiulizwa mara kwa mara kama ana mpango wa kujiunga na label hiyo ameweka wazi kuwa hajwahi kufikiria kujiunga WCB.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, Rosa Ree ambaye awali kabisa alikuwa katika label ya The Industry amesema  kuwa hawajawahi kuzungumza hilo ila ni watu ambao wamekuwa bega kwa bega na yeye katika muziki wake.

Hapana ilikuwa hamna, ndiyo timu mzima ya WCB wamekuwa wakinisapoti katika muziki wangu. Nafurahia hilo ila hatukuwahi kufikia hatua hiyo”.

Rosa Ree aliondoka The Industry, record label inayomilikiwa na Nahreel na Aikah wa Navy Kenzo mwaka jana oktoba na amekaa bila management kwa miezi kadhaa mpaka aliposainiwa mapema mwezi huu.

Rosa Ree Atoboa Siri Ya Kuzidi Kufanikiwa

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya vyema kabisa kwa staili yake ya kuchana mwanadada Rosary Robert ‘Rosa Ree’ ametaja siri ya mafanikio yake.

Rosa Ree ni moja ya msanii ambaye amepata umaarufu kutokana na staili yake ya kipekee kabisa ya kuchana inayomtofautisha na wasanii wote wa Bongo fleva.

Kwenye mahojiano yake na gazeti la Risasi Vibes, Rosa Ree alisema kuwa, siri hiyo ni namna ya uimbaji wake kwani haujakaa Kibongo sana na anajiweka ‘kimtoni’ zaidi ndiyo maana anafanikiwa.

Ukiwasikiliza wanamuziki wa kike wa Bongo, wengi wanavyorap ni ‘local’ ndiyo maana hata hawatusui kama mimi, kikubwa aina yangu ya uimbaji inanifanya kupata mashabiki wengi zaidi nje ya Bango”.

Rosa Ree anayeendelea kufanya vizuri na ngoma yake ya ‘Way up’ amezidi kupata mafanikio zaidi kwani wiki chache zilizopita alitangaza kupata uongozi mpya kutoka South Africa ambao umemzawadia mijengo miwili huku mmoja wa Bongo ukiwa na thamani ya milioni 400.

 

Rosa Ree Anunuliwa Mjengo Wa Milioni 400 na Uongozi Mpya (+picha)

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya miondoko ya kurap Rosa Ree ameanika mijengo yake miwili aliyonunuliwa na uongozi wake mpya.

Siku ya jana Rosa Ree aliita waandishi wa habari Kwenye mjengo wake mpya wenye thamani ya shilingi milioni 400 ili kutambulisha uongozi wake mpya uliopo nchini Afrika ya Kusini unaoitwa Dimo Production South Africa.

Rosa Ree ametangaza kusaini mkataba wa miaka mitatu na record label ambayo imeweka wazi kuwa imeamua kumnunulia nyumba mbili moja nchini Tanzania na nyingine nchini South Africa.

Hizi ni baadhi ya picha za mjengo huo uliopo nchini South Africa:

.

.

.

.

Nahreel Afungukia Ishu Ya Rosa Ree Kuondoka The Industry

Mwanamuziki wa Bongo fleva kutoka katika kundi la Navy Kenzo, Nahreel amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu msanii Rosa Ree kuondoka Kwenye label yake ya The Industry.

Msanii wa kike anayefanya vizuri kwa hivi sasa Rosa Ree alianza kujulikana baada ya kusainiwa chini ya label ya The Industry inayomilikiwa na Nahreel ambaye pia ni producer.

Rosa Ree alitangaza kuondoka kwenye label hiyo mapema mwaka jana baada ya kuwepo humo kwa muda mrefu huku akidai sababu pekee iliyomuondoa ni kuisha kwa mkataba wake na kusisitiza hana ubaya nao.

Lakini baadae Rosa Ree aliweka wazi kuwa kuna baadhi ya mambo ambayo yalifanyika ndani ya label hiyo ambayo hayakumfurahisha ikiwemo kukataa kumpa akaunti yake ya Youtube hali iliyoashiria kulikuwa na kabifu fulani.

NAhreel anefunguka kwa mara ya kwanza na kumuongelea Rosa Ree tangu alipoondoka The Industry ambapo kwenye kipindi cha Refresh cha Wasafi Tv ameweka wazi hakukuwa na bifu baina yao bali mwenyewe aliomba kuondoka.

Rosa Ree watu wamemjua Kupitia The Industry na kama alivyosema yeye time ilivyofika alitaka kuondoka na sisi tukamuacha aende but hatuna tatizo Rosa”.

 

Rosa Ree Amekuja Na Mini Supermarket Yenye Thamani Ya Milioni 30

Mwanamuziki wa Bongo fleva Rose Kimario maarufu kama Rosa Ree ameingia Kwenye ulimwengu wa kibiashara baada ya kufungua mini supermarket yake mpya aliyoipa jina la Rosa Ree Mini Supermarket.

Risa Ree alitumia ukurasa wake wa Instagram kutangaza habari hiyo njema na kuandika maneno haya:

Rosa Ree amefanya Interview na Millard Ayo Tv na ameweka waiz kuwa imemgharimu zaidi ya milioni 30 kuwekeza Kwenye biashara ile

Ile ni Supermarket yangu na ninategemea kuifungua rasmi wiki ijayo hivi sasa tupo Kwenye maandalizi ya mwisho ni kitu ambacho nilipanga kufanya kwa muda mrefu sasa.

Kusema ukweli nimewekeza pesa nyingi lakini kwa haraka haraka nimewekeza zaidi ya milioni 30 na nina mpango wa kufungua supermarket kubwa zaidi ya ile”.

 

Rosa Ree Atoa Siri ya Mafanikio kwa Mwanamke.

Akiwa kama msanii wa kike amabe ilifika sehemu aliona kuwa anaweza kusimama peke yake katika muziki na hakuna wa kumuangusha, Rosa Ree amefunguka na kuelezea kwa makini kabisa ni jinsi gani mwanamke anapaswa kufanya ili kuweza kufanikiwa na ku-win ndoto zako.

Akiyaongea hayo  katika siku ya wanawake Duniani, yeye pia ni moja ya wanawake jasiri sana na walioweza kuamini kuwa aina ya muziki anaoufanya sio lazima kufanywa na mwanaume ndio uonekane kama umefanywa.

Rosa Ree anasema kuwa lazima mwanamke ajiamini sana ili kuweza kufanikiwa lakini pia inabdidi awe na bidii katika kutimiza ndoto yake.

Kwa wanawake wote wenye vuipaji, kikubwa ni kujiamini tu.unatakiwa kujiamini ili uweze kukamilisha ndoto.

pili kuwa na imani na kile kitu uanataka kukifanya,tatu ni kutia bidii , huwezi kuwa na ndoto alafu hautii bidid ili ifanikiwe  na kukamilisha malengo yako.

Mwanadada huyo amehaidi kutoa wimbo mpya siku ya tarehe 9 mwezi huu na kuwaomba mashabiki zake kuupokea vizuri.

Rosa Ree Awatolea Povu The Industry na Kusema Hawawezi Kumshusha

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayetamba kwa miondoko yake ya kurap na hata kupewa jina the rap Godess Rose Kimario ‘Rosa Ree’ amewatolea povu zito wale wote wanaotaka kumshusha hawataweza kushusha kipaji chake kikubwa.

Rosa Ree alipata umaarufu kwa mara ya kwanza baada ya kuwa chini ya uongozi wa The Industry ambao uko chini wa Nahreel na Aikah Navykenzo.

Tangu alipoondoka kwenye label hiyo na kuanza kufanya muziki kama Solo artist Miezi michache iliyopita siku zote amekuwa akisisitiza kuwa hana bifu wala ubaya na Navykenzo.

Lakini siku chache ziliopita Rosa Ree aliibuka na kuongelea mchezo mchafu aliofanyiwa na Uongozi wake wa zamani ambapo amedai wamefuta baadhi ya video za nyimbo zake YouTube ambazo zilikuwa kwenye kurasa yao lakini pia amesema nyingine wamezishusha wameziweka private jambo ambalo amedai limemrudisha nyuma.

Rosa Ree amefanya Interview na Enews ya East Africa Tv amekiri pamoja na kwamba kitendo hiko kimemrudisha nyuma lakini hakijamkatisha tamaa na hakiwezi kushusha kipaji chake:

Kusema ukweli walivyoshusha video zangu kuna thamani ambayo imeshuka kidogo na ninajikongoja kuweza kupita ile sehemu ambayo ilikuwa zinaweza kunifikisha lakini siamini kama video zikishushwa kwenye YouTube na kipaji changu kimeshushwa kwaiyo nina iyo imani kwamba bado kipaji changu kipo na bado uwezo wangu upo na nitaendelea kufanya vyema”.

Pia Rosa Ree aliulizwa kuhusu uhusiano wake na Navy Kenzo kwa sasa endapo kuna bifu lolote ambalo linapelekea wao kumfanyia hivyo yeye na alisema:

Sina mawasiliano yoyote na Navykenzo kwa muda mrefu Lakini naamini ni kwa sababu ya majukumu mimi niko busy na muziki wangu hivyo sijaweza kuwasiliana nao lakini na wao wamepata mtoto ambalo ni jukumu kubwa naamini hivyo siwezi kujiuliza kwa nini hatuwasiliani”.

 

Rosa Ree:Siwezi kufanya Kazi na Mtu Nisie-endana Nae.

Msanii wa muziki  wa kike wa Hip-Hop nchini Rosa Ree amesema kuwa kwa sasa  hawezi kufanya kazi na msanii yoyte ambae hawaendani nae kimuziki kwa sababu anapenda kufanya azi inayoeleweka na itakayowakonga mashabiki zake.

Rosa Ree ameyasema hayo baada ya kutoa wimbo wake unaojulikana kama marathoni ambao amemshirikisha billnass hivi karibuni na kukubali kuwa yeye na billnass wameweza kufanya kazi hiyo naikafanya vizuri kwa sababu kuna kitu cha kimuziki kinachowaunganisha na kuendana sana.

Bill nass kabisa nimshikaji wangu sana na nimoja ya wasanii wenye vibes sana,ni myu wangu wa karibu na tuna vibes  sana,as  a person yeye ni mtu poa sana.napenda sana watru ambao wapo Og,alafu kitu kingine ni kwamba siwei kufanya kazi namtu ambae sina vibes nae kabisa, mtu ambae hana positives vibes.

Rosa Ree na Billnas wametoa wimbo wao mpya hivi karibu na kuwafanya kuwa karibu zaidi, lakini kama ilivyo kawaida watu wengi wameanza kutilia mashaka uhusiano wa wawili hao lakini wao wameshakanusha taarifa hizo.

Rosa Ree Akanusha Kutoka Kimapenzi na Young Dee

Msanii wa muziki anaefanya vizuri kwenye hip-hop Rosa Ree amefunguka na kukanusha tetesi zinazosambaa kuhusu yeye kuwa na mahusiano ya kimapenzi na msanii mwenzie Yound Dee kwa muda sasa.Rosa Ree amesema kuwa watu wamekuwa wakizusha mambo hasa wanapoona watu wamekuwa na ukaribu hata kama ni wa kibiashara na kikazi.

Rosa Ree amefunguka na kusema kuwa kwa muda sasa amekuwa singo bila kujiingiza katika mahusiano yoyote na ikitokea siku akiwa katika mahusinoa yaliyo serious basi  lazima atawatambulisha mwanaume  lakini sio kupitia katika kurasa za udaku kama inavyotokea saa hivi kwa young dee.

Niko singo siko kwenye mahusiano yoyote yale na mtu yoyote yule,na hata akija mtu na nikawa nae katika mahusiano ntamtambulisha tu kwenu kwa njia proper sio kwa kupitia udaku na sijawahi kutoka na Young Dee ni mwanangu tu nafanya nae kazi na tumekuwa watu wa karibu.

Wasanii wengi wamekuwa wakiambiwa au kuhisiwa kuwa wanatoka na wasanii wenzao lakini wanakuwa wanakanusha lakini ukweli wanaokuwa nao wenyewe na mbaya zaidi mambo yanapokuwa magumu ndio siri zinaanza kuvuja na kushindwa kuyatatua matatizo yao ingawa sio vizuri kuonyesha mahusiano yao katika mitandao.

 

Rosa Ree Afunguka ni Sababu Gani Zilimpelekea Kumtosa Fid-Q

Msanii wa kike anayetamba kwa staili ya peke yake ya kuimba na kurap Rosa Ree, amefunguka kuwa ni sababu gani iliyompelekea kumtosa mwanamuzi mkongwe  Fid-Q.

Rosa Ree anayetamba na wimbo wake mpya wa ‘Dow’ amekuwa katika vichwa vya habari hivi karibuni baada ya habari kutapakaa kuwa amehama label ya The Industry ingawa ameendelea kusisitiza kuwa hana shida nao lakini za chini ya kapeti zinadai mengine. Kumekuwa na tetesi nyingi kuwa mkali wa mashairi, Fid-q alipomtaka Rosa Ree wafanye kazi alikataa.

Kwenye mahojiano aliyoyafanya na Lilommy, Rosa Ree amefunguka yafuatayo kuhusiana na masuala hayo:

Naweza kusema wimbo wa Fid-Q ni moja Kati ya vitu ambavyo The Industry imeniangusha sana, nilitumiwa hiyo nyimbo na nikaandika mpaka verse lakini ikawa inatakiwa ipite kwanza kwa Nahreel sasa baada ya kufika huko sikujua nini kilitokea lakini sikurudishiwa tena kile kitu kilinishangaza kwa sababu Fid ni moja Kati ya wasanii wakubwa sana lakini sina tatizo naye ni kaka yangu tuko fresh”.

Pia Rosa Ree alifunguka kuwa hana muda wa kuwaza mapenzi kwa sasa kwaniyuko bize na kuzisaka pesa kwanza na kuboresha maisha yake.

Rosa Ree Kufuata Nyayo Za Diamond,Ni Baada Ya Kupata Dili Nono

Msanii anaefanya vizuri kwa sasa katika anga za muziki wa bongo , Rosa Ree amekuwa msanii wa kwanza wa kike lakini wa pili kutoka Tanzania kupata deal kubwa kutoka katika kampuni ya Belaire baada ya Diamond kupata dili hili week chache zilizopita.Kampuni iyo ambayo ina mabalozi wengine wakubwa duniani  kama Rick Ross  inaendelea kuona kazi nzuri wanazofanya wasanii wa Tanzania na kuamua kufanyanao kazi,

Akiongea na mwandishi wa habari msanii Rosa Ree amethibitisha kupata dili ilo na anasema kuwa anahisi ni kwa sababu ya muziki na kazi zake kufanya vizuri ndio maana ameweza kuchaguliwa lakini hajui nini kuliwasukuma kampuni iyo kumuangalia na kumchagua msanii kama yeye ambae ndio kwanza anaibuka na kuanza kufanya vizuri tofauti na Diamond ambae amekuwa katika industry ya muziki kwa muda mrefu kidogo.

To be honest mimi sijui kwa sababu na mimi nimechaguliwa hivyhivyo tu na wao wenyewe hata sikujichagua, au kujipendekeza nikasema labda nina quality sana , kwaio hata ukiniuliza sijui ni quality gani Belaire wanaangalia kuchagua wasanii  na sijui ni zipi waliangalia wakaona Rosa Ree anafaa” alifunguka Rosa Ree

Hata hivyo Rosa Ree anasema kuwa muda mwingine vile unavyojichukulia ndivyo na watu wanaokuangalia watakuchukulia pia kana unakaa kutokujiamini itakuwa hivyo kwa watu pia”lakini najua kwamba ukiweza kujichukulia mwenyewe kwa uzito fulani  na watu wanaweza kukuchukulia kwa uzito huohuo na kwa thamani hiyo na ukijikuta unafika katika viwangi vikubwa” aliongezea mwanadada huyo

Rosa Ree ni msanii chipukizi ambae alianza kazi chini ya lebel ya The industry, hata hivyo kutokana na juhudi zake kwa sasa anafanya kazi vizuri akiwa kama moja wa ma-rapper bora wa kike Tanzania mwenye style ya pekee katika uimbaji,kama ilivyo kwa Diamond, Rosa Ree pia amepata dili la kuwa msanii anatoka Tanzania wa kike atakae kuwa balozi wa kinywaji chenye brand  kubwa duniani cha Belaire.

Rosa Ree Afunguka Kuhusu Kuondoka Kwenye Label Ya The Industry

Mwanamuziki wa bongo fleva anayefanya miondoko ya rap, Rosa Ree amefunguka na kukubali kuwa tetesi zilizoenea kuwa yeye ameachana na label ya The Industry ni kweli.

Label ya The Industry ambayo inasimamiwa na wanamuziki kutoka Navy Kenzo Nahreel na Aika iliyokuwa inasimamia kazi za mwanadada Rosa Ree ambaye amepata umaarufu kutokana na staili yake tofauti na wasanii wengine ya kuimba kwa kurap huku watu wengi wakimfananisha na rapa maarufu kutoka Marekani mwanadada Nicki Minaj.

Kwenye mahojiano na Millard Ayo Tv, Rosa ree alifunguka zaidi kuhusiana na uamuzi wake wa kuondoka katika label hiyo;

Ni kweli kwa sasa sipo tena kwenye label ya The Industry ila sio kwamba nimeondoka au kuendelea ila ni mkataba umeisha at the moment na tuko salama kabisa ni vitu vya mkataba ni masuala ya biashara haituingilii kwenye urafiki au ufamilia tunaoweza kuwa nao kwaiyo tunaishi kama zamani tupo freshi na bado ni marafiki kwaiyo hamna kitu chochote kibaya kilichotokea kati yetu. Pia napenda kuwashukuru kwa mchango wao ambao wameweza kuweka kwenye mziki wangu kwani sio rahisi watu wakuamini kwaiyo ni kitu ambacho they really deserve credit for na walifanya kwa moyo mmoja kwaiyo nawashukuru kwa hilo “.

Baada ya Rosa Ree kuondoka The Industry hivi karibuni watu wengi walizusha kuwa ameondolewa kwa sababu ya mambo ya kiheshima na pi ailisemekana kuwa Rosa Ree alikuwa na ugomvi na First lady wa The Industry Aikah kitu ambacho wote wamekataa huku akisisitiza kuwa hana ugomvi nao bado ni marafiki kama zamani lakini tu mkataba wake umeisha ila kwa sasa Rosa Ree kasema anajisimamia mwenyewe.

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.