“Mali gani hiyo?” Harmonize reacts to ex wife suing him over properties she bought him

They say Kenyan and Nigerian men are croocks. They can trick you into falling in love, make you open up about passwords, savings and what you don’t see coming is the breakup.

I can promise you that this is the kind of character development most women have in common and whether a guuuud or bhaaad gurl…character development is a must when it comes to these two African men.

Sarah takes Harmonize to court

Well with this, I’m starting to wonder whether Harmonize has any Kenyan roots cause damn…ameruka ex wife kipetero kiyesu after she allegedly took him to court demanding he gives her half of everything he owns.

This is allegedly because back when they were married and had dated for 4 years – she invested in some properties, cars and business in Tz but the only mistake she made is put them under her beau’s name. Sema mapenzi.

I divorced her

Anyway now that the love they once shared already faded away….we’re left witnessing what looks like a nasty divorce about to go down.

Speaking on the case, Harmonize a few hours ago shared a screenshot between him and current fiance, Kajala where they are seen discussing the divorce.

At one point Harmonize is seen talking about properties…which he says Sarah Michelloti left him with nothing – adding that by the time she left Harmonize didn’t even have a place to sleep. Wait….ati?

 

And from the post above, he also hints that she may want him back as her husband, but problem is – his heart belongs to another.

Nataka niandike, Taraka 3. Sio Mke wangu. Umalaya sio chaguo langu.

Alaaah!

Bitterness galore: Harmonize’s ex mzungu wife threatens to spill singer’s secrets on social media

Harmonize dumped his mzungu wife,Sarah Michelloti over unknown issues; but after the lass exposed him for being impotent- then I guess this where she totally lost him.

So far Harmonize has moved on with actress Kajala who is the current girlfriend; and word on the streets is that Harmonize is happier than he was before. The only problem is – he moved on with one of his exes good friends hence ruining an all time relationship between Kajala and Wolper.

Harmonize with Sarah Michelotti

Sarah Michelloti to ruin Harmonize

Well, judging from how fast Harmonize moved on – it only proves that he had been seeing Kajala on the low; hence making his ex wife more bitter.

Harmonize’s girlfriend with daughter, Paula Kajala

However it looks like Sarah now wants to pay back by revealing deep and dark secrets about Harmonize. This is because Sarah Michelloti was the closest ally Kondeboy had at the time when he was leaving WCB; and due to the hard times he was facing – he got to open up to his dear wife.

Harmonize and fiancée Sarah during his ´Marry Me´ song video shoot

Unfortunately some of this information will not only ruin Harmonize’s reputation; but will shed light to how he met, seduced and used the Michelloti family. Well, I smell trouble but since Harmonize is the one who brought this to himself – then let’s see how he will handle the alleged Italian mob family – Michelloti.

Anyway Sarah wrote;

Hello beautiful people! Please be sure to keep an eye on my page as on this few days I will be doing an interview revealing all the truth about the end of my relationship with Harmonize. Stay tuned for more information! Thank you all for your love and support through this time. Your mind comments and messages keep a smile on my face. ????????

Explained! Harmonize discloses reason behind Italian girlfriend´s tattoo on his arm

Bongo artist, Harmonize discloses that girlfriend, Sarah´s unconditional love and support drove him to tattoo her name on his arm.

The bongo flava star´s recent stunt has been his girlfriend´s name tattooed on his arm, leaving many speculating that she played a major role in purchasing high end cars for his parents.

Unfortunately, Harmonize speaks a different language after revealing heartwarming reasons behind the tattoo.

https://www.instagram.com/p/By2K5T4Hs4C/

Speaking to Tanzanian media, Konde Boy discloses:

Sarah kwasabu, mimi tangu, sijawai kuwa katika mahusiano, ikafika miaka mitatu.

Me and Sarah now we are 3 years old.

According to Harmonize, this is the first relationship he has had going for 3 years plus and he feels honored.

However, Sarah is no ordinary woman for him because he naturally feels the vibe coming from an open, honest and supportive woman.

Lakini ni mwanamke ambae she love me, and she support me.

Ananiappreciate.

Navosema kusupport, ni mwanamke ambae ananifanya nikiamka asubui, just feeling comfortable.

Sijawai kuona ata akimeseji mtu anatuma.

Yaani, kama anazungumza na watu, I don´t know.

But sijai kuona, sijai ata kuhisi kwamba labda kuna vitu anafanya different.

Harmonize closes off by expressing his love for his better half who has been there for him despite pressures that come from fans and the world of secular music.

So, namheshimu, nampenda pia.

Lakini pia amekua na mimi sambamba.

Si kazi yetu ni ngumu sana, wasichana wanakua ni wengi, sometimes namkosea na vitu kama hivo.

https://www.instagram.com/p/ByzoBRzgZ9Q/

Harmonize sends the Internet into a frenzy after tattoing Italian girlfriend´s name on his arm

Bongo flava singer, Harmonize is serving goals after gifting parents heavy machines and now tattoos his mzungu girlfriend´s name on his arm.

It is no lie that the young star is thriving in the lucrative media industry, releasing hit after another seemingly beating Diamond Platinumz at his own game.

Apart from his business´ promising graph, Konde Boy has his love life blooming if not already blossomed.

The Wasafi artist has been dating his Italian fiancee, Sarah Michelotti for 2 years now, before romantically proposing to her just April 2019.

Unfortunately, his side chic, Nana Shanteel just gave birth last week, to his baby girl but Harmonize´s relationship seems unshaken.

Harmonize sends the internet into a frenzy after tattooing Sarah´s name on his arm, in big script letters.

https://www.instagram.com/p/ByxJ107IGpd/

Question

However, what many don´t seem to understand is how he tattooed her name, without thinking of breakup possibilities.

Mkiachana inakua sarafina????????

 

????????????that way he wont cheat on you right ?????????????????think and think twice anyway none of my business !

Harmonize Akana Mahusiano Yake na Sarah Mzungu

Msanii wa muziki wa Bongo fleva kutokea kwenye Label kubwa Bongo WCB, Harmonize amejikuta akijikanyaga Baada ya kuulizwa kuhusu Mpenzi Wake na kuishia kukana mahusiano yake na Sarah Mzungu.

Harmonize yupo nchini Nigeria na siku ya jana,  Jumatatu Februari 25, 2019 alitembelea kwenye kituo cha radio cha The Beat 99.9 FM cha jijini Lagos kwa ajili ya Media Tour.

Kwenye mahojiano hayo, Harmonize aliulizwa maswali kadhaa na swali la kwanza lilikuwa ni “Tunamuona mwenzio Diamond yupo na Tanasha vipi wewe upo single?”.

DAHH MIMI? NIPO SINGLE NA NATAFUTA PIA…HAPANA NATANIA SIPENDI KUZUNGUMZIA SANA MAHUSIANO YANGU, UNAJUA MIMI MASHABIKI WANGU NI WANAWAKE NINAVYOJIBU WENGINE WATAJISIKIA VIBAYA”.

Kiukweli ni kwamba Harmonize yupo kwenye mahusiano ya muda mrefu na Mpenzi wake Sarah ambaye pia yupo kwenye moja ya nyimbo zake ambayo ipo kwenye EP yake.

Wolper Afunguka Kuwaingilia Harmonize na Sarah Tena

Mbunifu wa Mavazi na Muigizaji wa Bongo movie Jacqueline Wolper ameibuka na kujibu Tuhuma Za kuingilia tena mahusiano ya aliyekuwa Mpenzi Wake Harmonize na Mpenzi Wake Mpya Sarah.

Sakata hilo lilijitokeza siku chache zilizopita baada ya Wolper alionekana kuuimba katika akaunti yake ya instagram wa mapensi mabaya akimaanisha ‘mapenzi mabaya’ na yeye kubadilisha na kuimba kinyume.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Wolper alisema kuwa amejisikia tu kuimba kinyume kuwa mapensi mazuri.

Lakini watu wanazungumza vingine kwamba namchokoza lakini isivyo hivyo. Nimejisikia tu kuimba haijalishi yeye ndiye ameanza kuimba lakini mimi nikaona niimbe kinyume na yeye alivyoimba ni vile nimejisikia tu kufanya hivyo”.

Baada ya video ile kusambaa watu wengi walichukulia kuwa Wolper amefanya vile ili kumsanifu Sarah hasa kwa sababu wawili hao hawaivi kabisa.

 

Harmonize Afungukia Ujauzito Wa Sarah

Msabii wa muziki wa Bongo fleva Kutoka katika Label ya WCB, Harmonize amefunguka na kutoa majibu kuhusu utata wa ujauzito wa Mpenzi Wake Sarah.

Wiki chache zilizopita Sarah alitupia picha zilizomuonesha ni wa kujifungua muda wowote. Kabla ya kutupia picha hiyo kulikuwa na madai na minong’ono mingi kuwa mchumba huyo wa Harmonize alikuwa haonekani mara kwa mara kwenye mitandao ya kijamii kama ilivyokuwa huko nyuma kwa sababu eti alikuwa analea mimba hiyo hivyo hakutaka kujitokeza hadharani.

Lakini alipohudhuria Birthday party ya Msanii Wolper Wiki iliyopita na kuonekana akiwa hana ujauzito maneno Mengi yalizuka na kushangaza wengi walioamini mzungu huyo ni mjamzito.

Baada ya kuzidi kwa minong’ono Gazeti la Ijumaa, lilimfuata Mpenzi Wake Harmonize ili kupata ukweli wa mambo ambapo alifunguka:

Sidhani kama kila kitu ni vizuri kukiweka kwenye hadhara. Ni jambo kubwa hilo, lakini ni la kifamilia zaidi.

Kama anavyoonekana, hajajifungua na hana mimba kweli. Mara kadhaa Sarah amekuwa akidaiwa kuwa mjamzito, lakini hazina ukweli”.

Jacqueline Wolper Ashabikia Mapenzi Ya Harmonize na Sarah

Muigizaji wa Bongo movie na mbunifu wa mavazi Jacqueline Wolper ameshangaza wengi Baada ya kuonekana akiwa anashabikia Penzi la hasimu Wake Sarah na Harmonize.

Wiki iliyopita kuna tetesi zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Harmonize na Wolper wamerudiana Baada ya kuonekana wakiwa karibu katika tamasha zima la Wasafi Festival.

Lakini Harmonize na mpenzi Wake Sarah walionekana kuzima tetesi hizo Baada ya kuposti video iliyowaonyesha wawili hao wakiwa wanacheza pamoja na kukumbatiana kwenye nyumba yao.

Siku ya jana ilikuwa ni siku ye kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Wolper ambaye alifanya party yake kubwa na kualika wasanii wakubwa lakini cha kushangaza aliwaalika Harmonize na Sarah pia.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Wolper aliposti video ya Harmonize na Wolper na kuisindikiza na maneno haya:

https://www.instagram.com/p/BrDmRCCnUsh/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=ijbkt2241p33

Katika kuonyesha kuwa Harmonize na yeye Hana tatizo na Wolper alimposti katika ukurasa wake wa Instagram na kumtakia Birthday njema.

Harmonize na Sarah Wazima Tetesi Za Kuachana Kwa Staili Hii

Mwanamuziki wa muziki wa Bongo fleva Harmonize na Mpenzi Wake Sarah wamezima tetesi zilizokuwa zinasambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa wameachana.

Harmonize na Sarah wameachia kipande cha Video kinachowaonyesha wakiwa wanacheza wimbo mpya wa Harmonize aliomshirikisha Rayvanny ‘Para nawe’ na kukumbatiana kimahaba na kuonyesha kuwa wapo pamoja.

https://www.instagram.com/p/BrC0I0oHdIu/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=1w96soh00gm09

Kipande hicho cha video kimewekwa mtandaoni na Harmonize mwenyewe pamoja na mpenzi wake huyo ikiwa ni siku chache baada ya kuripotiwa kuwa wamemwagana kisha kurudi kwa mpenzi wake wa zamani, Jackline Wolper.

Tetesi za kuvunjika zilianza Baada ya Harmonize kuanza kuonekana pamoja na Harmonize katika tamasha la Wasafi Festival na hata kukumbatiana stejini huku Mpenzi Wake Sarah akiwa nje ya nchi na kupelekea tetesi za kuachana.

Harmonize na Wolper Mapenzi Moto Moto

Msanii wa Bongo fleva nchini kutoka WCB Harmonize na msanii wa Bongo movie Jacqueline Wolper wamezidi kutengeneza headline kwa tetesi za kurudisha Penzi Lao Kama zamani.

Wawili hao wameendelea kuzua gumzo baada ya Harmonize kutangaza kurudi kwa Wolper wake ambaye alimwagana naye miezi kadhaa iliyopita. Ishu nzima ilijiri usiku wa kuamkia juzi Jumamosi katika shoo ya Wasafi Festival iliyofanyika mjini Iringa na kusababisha mji huo kutikisika.

Gazeti la Ijumaa Wikienda linaripoti kuwa Wikiend iliyopita katika Uwanja wa Samora, Harmonize alimpandisha stejini Wolper kama ‘sapraizi’ na kumwangukia akimuomba warudiane, jambo ambalo Wolper alilikubali mbele ya maelfu ya mashabiki wao.

Naomba niseme wazi hapa hadharani kuwa nimerudi kwa Wolper wangu”.

Kufuatia kile kilichojiri mjini Mtwara ambapo Wolper alieleza nia yake ya kumrudisha Harmonize kwenye himaya yake ambapo wengi waliamini kuwa wawili hao wamerudiana maana wahenga walisema kiporo hakihitaji kupashwa na moto mwingi.

Pamoja na kuwepo kwa tetesi za wawili kurudiana Mpenzi wa siku nyingi wa Harmonize, Sarah ambaye kwa sasa yupo nyumbani kwao nchini Italy lakini amesema wazi kuwa yeye na mpenzi wake Harmonize bado wako wote na anategemea kurudi Tanzania muda wowote.

“Sarah Hajakasirika Nilivyokumbatiwa na Wolper”- Harmonize

Msanii wa muziki wa Bongo fleva kutokea katika label ya WCB Harmonize ameibuka na kudai kwamba Mpenzi Wake Sarah hajamind kitendo cha yeye kukumbatiana na Ex Wake Wolper.

Wikiend iliyopita mkoani Mtwara kwenye tamasha la Wasafi Festival Harmonize alirekodiwa akikumbatiana na Ex Wake Wolper wakati wa kusalimiana mara moja tetesi zilianza kusambaa kwamba wawili hao wamerudiana.

Tetesi hizo zilizimwa na Mpenzi wa Harmonize, Sarah ambaye Kupitia ukurasa wake wa Instagram alisema yeye na Harmonize hawajaachana na hawategemei kuachana na muda si mrefu angejiunga naye Mtwara kwa ajili ya shoo hiyo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa Wikienda, Harmonize alisisitiza yeye na Wolper ni washkaji tu na wapo kikazi ila Mpenzi Wake ni Sarah na hajamind alivyoona video za wawili hao kukumbatiana:

Wolper ni mtu wangu wa karibu na nilifurahi  kumuona akishiriki tena na Wasafi na kuhusu Sarah najua hawezi kumaindi kwani anaelewa kuwa tupo Mtwara kikazi zaidi”.

Harmonize Akana Tetesi Za Kumchumbia Sarah

Staa wa muziki wa Bongo fleva kutoka katika label matata WCB Harmonize ambaye kwa sasa anafanya vyema kabisa na ngoma yake ya ‘Kwangwaru’ amefunguka na kukataa tetesi zinazodai kuwa amemvisha Pete mpenzi wake Sarah.

Tetesi za Harmonize kumvusha pete ya uchumba mpenzi wake Sarah zilianza kusambaa wiki chache zilizopita baada ya kuposti picha Kwenye mitandao ya kijamii zikiwaonyesha Harmonize akimvisha pete ya thamani Sarah.

Tukio hilo la kuvalishana pete lilionekana kwenye mitandao ya kijamii siku chache baada ya wawili hao kugombana na kurushiana maneno kwenye Instagram baada ya Tetesi za Harmonize kuchepuka.

Kwenye mahojiano aliyofanya alipokuwa nchini Kenya kwa ajili ya shoo yake Harmonize aliwaambia Pulse Live kuwa hajamvalisha pete ya uchumba Sarah kama Tetesi ila wapo mbioni kufanya hivyo:

Sijamvisha Pete mchumba wangu,… na Ndoa bado unajua siku zote ndoa ni mipango na ikifika wakati wa engagement nitawatangazia”.

Mwezi uliopita Harmonize alikumbwa na tetesi za kuchepuka na wasichana kadhaa ikiwemo msanii wa nyimbo za Injili kutoka Kenya na mtangazaji kutoka Nigeria lakini pia Ex wake Jacqueline Wolper.

Harmonize Amtaka Mpenzi Wake Azoee Kusikia Ana Michepuko

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva kutoka WCB anayeendelea kufanya vyema sana  Harmonize amemfungukia mazito mpenzi wake Sarah na kumsisitizia kuwa hana michepuko.

Harmonize ambaye amekuwa Kwenye headlines sana kwa tuhuma za kuchepuka amefunguka na kukataa tuhuma hizo lakini pia amesema Tetesi hizo ni lazima kwa mtu maarufu kama yeye na hata mpenzi wake Sarah lazima azizoee tu:

Harmonize alifunguka hayo nchini Kenya alipokuwa kwenye shoo yake ambapo kwenye mahojiano na Pulselive na kumtaka mzungu wake kuwa mvumilivu:

Sio Kitu Kibaya maanake wivu pia ni Mapenzi, lakini kitu ambacho Sarah inafaa ajue kuwa ukikubali kuwa na Msanii lazima kuna vitu lazima tu ukubaliane navyo tu. Na Life style ya msanii inakaa vipi kuna wengine ni mashabiki na siwezi goma kupiga picha nao maanake bila wao mimi sipo. Kwa hivyo natumai tu anafaa kuelekezwa alafu atajua jinsi ya kuhandle situation kama hizo”.

Sarah na Harmonize waliingia Kwenye mgogoro mkali mapema mwezi huu baada ya Tetesi za Harmonize kuwa Kwenye Mahusiano ya Kimapenzi na wanawake kadhaa.

Harmonize Amvisha Pete Ya Uchumba Mpenzi Wake Sarah

Staa wa muziki wa Bongo fleva kutoka label ya WCB anayefanya vizuri na ngoma yake ya ‘Kwangwaru’ Harmonize amemvalisha Pete ya uchumba mpenzi wake mwenye asili ya Italia Sarah Michelotti.

Harmonize na Sarah walikuwa kwenye mgogoro wiki chache zilizopita baada Sarah kumtuhumu mpenzi wake huyo kwa kuchepuka baada ya kuona picha zake na mtangazaji kutoka Nigeria Nancy Isime na kudai ni wapenzi.

Lakini Sarah na Harmonize walionekana kumaliza tofauti zao siku chache zilizopita baada ya kuonekana pamoja Kwenye shoo  ya Kusi Night wakiwa wanakumbatiana stejini.

Hatimaye wawili hao wameweka wazi kuwa wamechumbiana baada ya Kuposti video iliyomuonyesha Harmonize akimvalisha Sarah Pete na Sarah Kuposti Kwenye ukurasa wake wa Instagram na Kuandika “Thank You Baby ♥️“.

 

Harmonize Afunguka Baada Ya Kumwagana na Sarah

Staa wa muziki kutoka WCB Harmonize amefunguka kwa mara ya kwanza tangu sakata litokee wikiendi iliyopita na kusababisha yeye na mpenzi wake Sarah kutofautiana.

Harmonize na Sarah walikamata headlines mwishoni mwa wiki hii baada ya wawili hao kurushiana maneno Kwenye mitandao ya kijamii na hata matusi yaliyopelekea kumwagana baadae.

Harmonize anafunguka kuhusu sakata hilo na kuweka wazi kilichokuwa kinatokea pale ni wivu wa kimapenzi ambao Sarah anao juu yake hasa pale alipomuona akiwa na wadau wa muziki wa kike.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Wasafi Tv, Harmonize anafunguka kuhusu sakata hilo lililotokea kati yake na Mpenzi wake Sarah:

Unapoamua kuwa na mtu unatakiwa ujue huyo mtu ni wa aina gani, anafanya kazi gani, ukishajua hivyo unakuwa ni rahisi zaidi ku-deal naye.

Nakutana na watangazaji, wasanii inatakiwa ni badilishane nao mawazo, sasa ukiwa unaendekeza kila saa masuala ya kimahusiano inakuwa unanirudisha nyuma kwa namna moja au nyingine”.

Harmonize ameweka wazi kuwa sakata  hilo lilianza baada ya Sarah kujaribu kumpigia kwa muda mrefu na yeye kutokana na kuwa bize na kazi alishindwa kupokea simu na hivyo kusababisha kukosa maelewano.

Penzi la Harmonize na Sarah Linapumulia Mashine

Penzi la staa wa Bongo fleva kutoka WCB Harmonize na mpenzi wake mzungu Sarah limedaiwa kuwa linapumulia mashine baada ya kugombana wikiendi iliyoisha.

Kupitia mitandao ya kijamii Harmonize na Sarah walidhihirisha kuwa katika mafarakano baada ya Sarah kumwaga povu Kwenye ukurasa wa Instagram wa Harmonize.

Huku sababu juu ya kugombana Ikiwa ni wivu wa kimapenzi, Sarah alionekana kuona wivu baada ya Harmonize kuposti picha akiwa na mwanadada ambaye ni mtangazaji nchini Nigeria anayejulikana kama Nancy Isime, ambako Harmonize ameenda kikazi.

Basi Sarah akiwa nyumbani wivu ukamshika alipoona picha hiyo alianza kumshushia matusi ya nguoni Harmonize huku akimjulisha yule mdada  kuwa yeye ndiye mwanamke halali wa Harmonize.

Baada ya povu hilo kuendelea basi Sarah akahamia kwa mwanadada aliyekuwa na Harmonize akampa na yeye vya kwake kuonyesha kukabwa na wivu uliopitiliza.

Baada ya sakata hilo Harmonize alitangaza yeye na Sarah wameachana baada ya kuposti kwenye ukurasa wake wa Snapchat kuwa yupo single:

 

 

Harmonize Amlipua Wolper na Kumuanikia Listi Nzima Ya Wapenzi Wake

Msanii wa Bongo fleva kutoka WCB Harmonize ameingia Tena Kwenye bita ya maneno na Ex girlfriend wake staa wa Bongo movie Jacqueline Wolper.

Siku ya jana kuna video ilisambaa Kwenye mitandao ya kijamii iliyomuonyesha Wolper akimrushia Dongo Sarah ambaye ni mpenzi wa Harmonize kwa kumuita Mlezi wa wana baada ya taarifa kusambaa kuwa kamtosa Harmonize na kumchukua Mwarabu Fighter.

Baada ya kuona video hiyo, Harmonize alitokwa na povu zito kwani kwa Kupitia ukurasa wake wa Instagram alimtetea mpenzi wake Sarah na kusema yeye sio Mlezi wa wana ila Wolper ni Mlezi wa Wana na kuambatanisha na listi kamili ya wanaume wote aliokuwa nao Kwenye Mahusiano.

Hii sio mara ya kwanza kwa Harmonize na Wolper kuwa na sintofahamu na hata Wolper na mpenzi wa Harmonize Sarah.

Wolper Amtupia Dongo Zito Sarah Wa Harmonize na Kudai ni Mlezi Wa Vijana

Muigizaji wa Bongo movie Jacqueline Wolper amemtupia Dongo zito Sarah baada ya habari zake za kumtosa Harmonize na kumchukua Bodyguard wa Diamond, Mwarabu Fighter.

Siku mbili zilizopita stori iliyotrend kupita zote ni ya mpenzi wa Harmonize Sarah kumtosa mpenzi wake na kumchukua Mwarabu Fighter.

Inasemekana Sarah amefufa ameoza kwa Mwarabu kiasi ya kwamba anamuhudumia ipasavyo yaani kampangishia hadi nyumba yaani zile huduma zozote alizokuwa anapata Harmonize zimehamia kwa Mwarabu.

Kama utakumbuka Kuwa Sarah na Wolper ni maadui wakubwa na kisa kikiwa ni penzi la Harmonize na juzi tu wametoka kumgombania Harmonize.

Baada ya tetesi hizo za usaliti kusambaa mitandaoni Sam Misago Tv walimsaka Wolper na kumuuliza nini maoni yake juu ya ishu hii kumuhusu Sarah na Wolper ameishia kumtupia dongo zito Sarah:

Duh iyo ishu mbona ni exclusive kabisa sijaisikia lakini freshi tu mbona yule demu ni Mlezi wa wana labda kachoka kumlea mwana kaamua kumchukua mwana mwingine freshi tu”.

Bifu laWolper na Sarah lilianza baada ya Sarah kuanza kuchepuka na Harmonize wakati Wolper yupo Kwenye Mahusiano na Harmonize.

 

Sarah Wa Harmonize Adaiwa Kufa na Kuoza Kwa Penzi la Bodyguard Wa Diamond

Mpenzi wa msanii wa Bongo fleva kutoka Label ya WCB Harmonize, Sarah maarufu kama Sarah Mzungu amejikuta ndani ya skendo nzito baada ya kudaiwa kuhamisha penzi lake kutoka kwa Harmonize kwenda kwa Bodyguard wa Diamond.

Habari kutoka Kwenye mitandao ya kijamii zinadai kuwa hivi sasa Sarah amehamisha penzi kwa Bodyguard wa Diamond anayeitwa Mwarabu fighter na kudaiwa kumsahau mpenzi wake Sarah.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Mange Kimambi amepasua jipu hilo na kudai harmonize anamlilia Sarah asimtose kwani keshahamisha majeshi kabisa kwa Mwarabu fighter:

Basi mnaambiwa Sarah wa Harmonize yuko deep in love na Mwarabu yaani sahivi Harmonize ndio analia mzungu asimkimbie ila bibie mnaambiwa anampenda Mwarabu Fighter. Siku hizi mnaambiwa Mwarabu gym anafanya, Collesium bibie analipia, ana maisha mazuri mzungu anampa hela balaa Mnaambiwa mapenzi moto moto”.

Baada ya tetesi hizo kuingia kwenye mitandao ya kijamii mara moja Sarah alianza kuposti kukana tetesi hizo Lakini mara moja Mange alidai kuwa anayeposti vile sio Sarah bali ni harmonize ambaye ana password ya akaunti ya Sarah.

Harmonize aliposti picha ya Mwarabu Fighter na kuandika maneno haya kuashiria Stori hiyo haina ukweli:

 

 

Harmonize- Nipo Tayari Kumuoa Sarah

Mwanamuziki wa Bongo fleva kutoka WCB Harmonize amefunguka na kuweka wazi mipango yake ya kumuoa mpenzi wake Sarah.

Kwa muda mrefu kumekuwa na maneno mengi kuhusu Mahusiano ya Harmonize na Sarah huku wengi wakidai Harmonize hana mapenzi ya kweli kwa Sarah bali yuko naye kwa ajili ya pesa.

Huku dhana hiyo ikiwa imepandikizwa na Ex wa Harmonize, Jacqueline Wolper ambaye alisema Harmonize alianzisha Mahusiano na Sarah wakati wako pamoja kwa sababu alikuwa anamuwezesha kifedha.

Lakini Harmonize ameibuka na kuweka wazi kuwa anampenda Sarah na hivi sasa yuko tayari kumuoa mwanamke wake huku akipuuzia maneno yote ambayo yanasemwa na watu.

Kwenye mahojiano na The Playlist ya Times Fm, Harmonize aliweka wazi mipango yake ya ndoa baada ya kuulizwa na Lil Ommy kama ana mpango wa kumuoa Sarah:

Ndiyo nataka nimuoe Inshallah”.

Harmonize anafanya vizuri na nyimbo zake mbili ambazo ni Kwa ngwaru aliyomshirikisha Diamond Platnumz na wimbo wake mpya Dm Chick ambao amemshirikisha Sarkodie.

Wolper: Siwezi Kusapoti Tena Kazi Za Harmonize

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara Jacqueline Wolper amefunguka na kusema kuwa hawezi hataweza kukaa na kusapoti kazi za Harmonize sababu anamuonea huruma mpenzi wake Sarah.

Siku chache zilizopita Wolper alitengeneza headlines kwenye mitandao ya kijamii baada ya yeye na mpenzi wa Harmonize Sarah kurushiana vita ya maneno kwenye Instagram.

Ambapo Sarah alimtaka Wolper aache kumtumia Meseji za kumtaka Mpenzi wake Harmonize jambo ambalo lilinkera Wolper kwani aliweka wazi kuwa akaunti yake ya Instagram ilidukuliwa hivyo hakuwa yeye aliyekuwa anatuma Meseji.

Kwenye mahojiano aliyofanya leo na Sam Misago Wolper amesema kuwa ameamua kuacha kabisa kusapoti kazi za Harmonize:

Mimi sio mswahili na wala sina uswahili tulianza mapenzi kwa mimi kusapoti kazi zako lakini sasa naona ili nisikwaze mahusiano yako naona bora nisisapoti kazi za Harmonize kwa sababu yule mwanamke wake anahitaji kuhurumiwa”.

Lakini pia Wolper amesisitiza kuwa amefikia uamuzi wa kumblock Harmonize na Sarah kwenye Instagram ili aepushe maneno maneno.

Wolper: Sarah wa Harmonize Ana Matatizo Ya Kisaikolojia, Anahitaji Msaada

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara maarufu, Jacqueline Wolper amemtolea povu zito hasimu wake namba moja Sarah mzungu ambaye ni mpenzi wa Ex boifrendi Harmonize.

Siku ya jana Wolper na Sarah waliongia kwenye vita ya maneno kwenye mitandao ya kijamii baada ya Sarah kwa mara nyingine kumtuhumu Wolper kwa kumtaka Harmonize.

Sarah alimpa onyo Wolper na kumtaka aache kuongea na Harmonize ambapo alitupia screenshots za meseji ambazo amekuwa akimtumia Harmonize huku imeonekana wazi kuwa hamjibu.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, Wolper amemjia juu Sarah huku akidai lazima atakuwa na ugonjwa wa kisaikolojia na kutaka watu wampe msaada:

Hivi ni vitu vya kuona huruma na kusamehe kwa sababu yule dada ana wasi wasi maskini anaamini kwamba nitachukua chombo chake wakati mimi muda huo sina lakini anajua mimi ni kiboko yake kwaiyo anaamini kuwa nitamchukua kitu ambacho siwezi mimi nikipita nimepita siwezi kumchukua tena na cha muhimu yule dada anahitaji mtu wa kumpima akili yule dada sio mzima ana matatizo ya kisaikolojia haiwezekaani kitu kidogo analipuka vile”.

Wolper amefunguka kuwa akaunti yake ilikuwa hacked na mtu ambaye ali hack alikuwa anatuma meseji kwa watu mbali mbali dm ikiwemo kwa Harmonize.

Wolper na Sarah Warudi Vitani Kwa Ajili Ya Penzi la Harmonize

Msanii wa Bongo movie na mfanyabiashara Jacqueline Wolper na Sarah mzungu ambaye ni mpenzi wa Staa wa Bongo fleva kutoka WCB Harmonize wamerudi kwenye ya vita ya mtandaoni.

Wolper na Sarah wamerushiana maneno Kwenye mtandao wa Instagram ambapo Sarah amemtuhumu Wolper kwa kumtumia meseji za Siri Harmonize huku akijua wazi kabisa ni mpenzi wake.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Sarah ameandika maneno haya kumtolea povu Wolper na kumchana kuwa anamtongoza Harmonize na kumtumia meseji huku anaona wazi kuwa hamjibu na amemtaka Wolper aishi maisha yake.

Baada ya kutolewa povu hilo, Wolper alimrudishia kombora hilo Sarah na kuandika maneno haya:

 

Hii  sio mara ya kwanza kwa Wolper na Sarah kugombana kisa penzi la Harmonize siku za nyuma Sarah ameshawahi kuanika kuwa Wolper bado anamtaka Harmonize jambo ambalo Wolper amekuwa akikataa siku zote.

Sarah Amwaga Mamilioni Kumfurahisha Mpenzi Wake Harmonize

Harmonize amezidi kudhihirisha kuwa mpenzi wake mzungu ana hela chafu kwani amemzawadia saa yenye gharama kubwa.

Kwa kipindi kirefu Kumekuwa na taarifa kuwa Sarah ambaye ni mzungu mwenye asili ya Uitaliano ana mkwanja mrefu ambao ndio unamuweka mjini Harmonize na kumpa jeuri ya kutanua na kuishi kistaa.

Sarah kwa kuonyesha jeuri ya pesa aliyonayo ameamua kumnunulia mpenzi wake Harmonize saa ambayo inatajwa kuwa na gharama sana ambapo Harmonize aliweka saa hiyo Kupitia ukurasa wake wa Instagram na kumshukuru mpenzi wake kwa Zawadi hiyo na kuwasihi watu watafute bei yake.

Saa hiyo aliyozawadiwa Harmonize na mpenzi wake Sarah inajulikana kama brand ya Patek Phillipe saa hiyo inaonekana kwenye mtandao kuwa na thamani ya kuanzia dola za kimarekani 78,999 hadi 119,999 sawa sawa na shilingi za Kitanzania 177,755,649- 270,009,749.

Wolper: Sina Wivu Nimemualika Harmonize na Mpenzi Wake Kwenye Party Yangu

Muigizaji wa Bongo movie na mwanamitindo maarufu Bongo, Jacqueline Wolper amefunguka na kudai kuwa hana hata chembe ya wivu wa kimapenzi kwa Harmonize na mpenzi wake Sarah na ndio maana amewaalika wote wawili kwenye party ya birthaday yake.

Wolper na Harmonize waliachana miezi michache iliyopita baada ya kuwa pamoja kwa muda. Baada ya kuachana kila mmoja alimtuhumu mwenzie kwa kuchepuka huku Wolper akiweka wazi kuwa waliachana kwa sababu Harmonize alikuwa na uhusian na Sarah kwa sababu ya fedha alizonazo mzungu huyo. Lakini hata baada ya kuachana na kila mmoja kupata mpenzi ambapo Harmonize alianzisha uhusiano na Sarah na Wolper alianza uhusiano na Brown lakini bado wawili hao wamekuwa na bifu la chini chini.

Siku ya jana ilikuwa sherehe ya siku ya kuzaliwa ya Wolper ‘birthday’ ambapo yeye mashabiki zake pamoja na ndugu zake walienda kushiriki kula chakula cha mchana na kituo  cha kulelea watoto yatima Temeke. Lakini aliweka wazi kuwa party kubwa ya birthday yake itafanyika leo tarehe saba.

Kwenye mahojiano na Millard Ayo Tv, Wolper aliweka wazi kuwa kwa sasa hana tatizo lolote na Harmonize wala  mpenzi wake mzungu Sarah ndio maana amewaalika kwenye sherehe yake:

Nimemualika Harmonize na sio yeye tu hadi mwanamke wake Sarah ili kuonyesha kuwa sina wivu wowote tupo sawa kabisa alafu ningekuwa nasikia wivu kama watu wanavyosema basi nisingewaalika kabisa yaani kwenye maisha mapenzi yanaisha na unatakiwa uendelee na maisha yako sasa mimi nimesha-move on na maisha yangu na nashukuru kwa sasa tumekuwa ndugu na Sarah inabidi tu awe ndugu yangu ili nimsaidie hata kujua kiswahili na pia nimsaidie kama Harmonize akichepuka nimpe nyendo zote ili nimwambie kama anachepuka kwaiyo inafika wakati watu inabidi tu muwe marafiki”.

 

Harmonize Amefunguka Kuhusiana na Ujauzito wa Mpenzi Wake Mzungu

Mwanamuziki wa Bongo fleva kutoka Wasafi Classic Baby (WCB), Harmonize amezidi kusisitiza kuwa mpenzi wake mzungu  Sarah ni mjamzito.

Baada ya kutangaza kuwa yeye na mpenzi wake huyo wanatarajia kupata mtoto na kuweka picha mbali mbali mtandaoni zinazomwonyesha mtoto akiwa tumboni (ultrasound), watu wamekuwa wakihoji ile mimba imeenda wapi kwani tumbo lake limezidi kuonekana dogo badala ya kukua kama wanawake wajawazito wengine.

Kwenye mahojiano na Times Fm Lilommy alimuhoji Harmonize juu ya ujauzito huo na haya yalikuwa majibu yake:

Sarah bado ni mjamzito na ninavyoongea na wewe amesafiri maana anajisikia vibaya kutokana na mimba yake amesafiri ameenda Italy nyumbani ila kingine ninachoweza kusema ni kuwa sisi waswahili na wenzetu tunaweza kuwa ni tofauti kidogo na vitu nitofauti yaani ukitumia jicho la kawaida huwezi kujua yaani hapa ninavyo zungumza na wewe anaumwa anaumwa vibaya sana ujauzito unampelekesha”.

Harmonize ameongezea kuwa endapo mtoto wake atazaliwa wa kiume basi atapendelea kumwita ‘Ibrah’.

Baada ya kutangaza kuwa wanategemea kupata mtoto miezi kadhaa iliyopita watu walishangaa kuona Sarah haonyeshi mabadiliko yoyote katika mwili wake ndipo habari za chini chini zilianza kuwa Sarah sio mjamzito bali ni stories waliotengeneza ili kupata kiki na kumuumiza roho mpenzi wake Wa zamani Jacqueline Wolper, habari ambayo Harmonize ameikana mara moja.

Harmonize: Namchukulia Wolper Kama Shabiki Wangu Tu

Msanii wa Bongo fleva maarufu kama Harmonize ameibuka na kudai kuwa anamchukulia Wolper kama shabiki wake tu na hakuna kingine.

Mwanzoni mwa wiki hii Jacqueline Wolper, ambaye ni mpenzi wa zamani wa Harmonize na Sarah, ambaye ni mpenzi wa sasa wa Harmonize waliingia katika vita kali ya maneno mtandaoni baada ya Sarah kudai kuwa Wolper bado anamtaka Harmonize. Sarah alivujisha meseji za Wolper mtandaoni na kupelekea Wolper kuchefukwa hivyo kumwambia Sarah kuwa alimuazima Harmonize kwa muda tu anaweza kumchukua muda wowote.

Baada ya hapo Wolper alianza kujirekodi anaimba wimbo mpya wa Harmonize unaotamba hivi sasa ‘Shulala’ na hivyo kupelekea minong’ono ya watu kuwa Harmonize na Sarah wameachana na Wolper kamchukua tena Harmonize kwani alimwambia siku nikimtaka Harmonize namchukua tena.

Kwenye mahojiano aliyoyafanya na XXL ya Clouds Fm, Harmonize aliweka wazi kuwa anashukuru mchango mkubwa wa Wolper katika nyimbo yake mpya kwani amejirekodi video mbili akionekana akifurahia wimbo huo.

Nadhani mwanzo ilikuwa ni hasira tu, nashukuru kuona mchango wa Wolper kwani namchukulia kama shabiki wangu tu”.

Pia kwenye mahojiano hayo Harmonize aliweka wazi mipango yake ya kuupeleka mziki wake kimataifa zaidi kwani hivi karibuni anategemea kusafiri kwenda Ghana kwaajili ya kurekodi video ya wimbo aliomshirikisha msanii Sarkodie kutoka Ghana, huu ni muendelezo tu wa mafanikio ya Harmonize kwani wimbo wake huu mpya wa ‘shulala’ amemshirikisha msanii Mkubwa kutoka Nigeria, Korede Bello.

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.