Mama Kanumba speaks after Wema Sepetu confesses she aborted twice for Kanumba !

The late Kanumba passed on without leaving a child behind; only years later for Wema Sepetu to confess having aborted 2 of his pregnancies back when they were dating.

Mama Kanumba and Wema Sepetu

Wema Sepetu opened up about her abortions during one of her interviews on her Wema APP. The lady confessed to having aborted twice but the second abortion was done without the late Kanumba’s consent; since Wema felt that she was too young to have kids back then.

This was however the first time she confessed about the second abortion that has left her looking for a child everywhere. Speaking about  her abortions, Wema Sepetu opened up saying;

I feel like Kanumba cursed me. This is because he really wanted to see me, he would call every day two weeks before his death. We were to meet but we were super busy and could not. He called for like four times but we could not meet. We finally met at Bilcanas.

Wema went on;

He told me I owe him, he told me I will not get babies with anyone else because he was the father of my babies. He told me I owe him two babies. This is because I had terminated two of his pregnancies. Every time we used to meet he would remind me that I owe him. I saw him on Wednesday and I heard he was dead on Thursday.

Mama Kanumba speaks

Having lost her two sons, it is unclear as to whether Mama Kanumba has any grandchildren.

Speaking about Wema’s confession, mama Kanumba expressed disappointment especially since both her sons are dead and his eldest did not leave any children behind.

Mama Kanumba

The lady opened up saying;

  Jamani mpaka nywele zilinisisimka kabisa, natamani sana kuongea na Wema nikae naye maana uzuri ni kwamba amekiri mwenyewe kuwa alitoa mimba za mwanangu, yaani imeniumiza sana jamani.

She went on to conclude;

Natamani sana Wema aje nimuone, nina kitu nataka kumwambia na ninampenda kwa sababu ni binti wa tofauti sana kuliko alivyo Lulu, kwani kila anionapo popote anakuwa na furaha sana na mimi. Natamani Kanumba angekuwepo jamani

Mama Kanumba Amsifia Wema Sepetu

Mama wa msanii marehemu Steven kanumba amekuwa akitoa maoni mara kwa mara kuhusu tasnia ya sanaa nchini na jinsi ambavyo wasanii na marafiki waliokuwa karibu na mtoto wake wanavyomchukulia kwa sasa tangu alipofariki.

Mama huyo anasema kuwa wasanii wengi waliwahi kusaidiwa ili kunyanyuka na mtoto wake lakini wasanii hao kwa sasa hakuna hata mmoja anaemkumbuka kanumba na mbaya zaidi wanakuwa wakiona hata aibu kusema katika itandao kuwa waliwahi kusaidiwa na kanumba.

Hata hivyo mama huyo anasema kuwa katika wasanii wote amekuwa akimpenda sana Wema sepetu ambae amekuwa hoani aibu kusema kuwa alisaidiwa sana na Kanumba mpaka kuwa msanii.

Katika watu pekee ninaowapenda ni Wema Sepetu kwa sababu amekuwa akikumbuka sana fadhila za mwanangu marehemu Steven kanumba.

Alichosema Mama Kanumba Kuhusu Lulu.

Mama wa marehemu Steven Kanumba amefunguka na kusisitiza kuwa katika maisha yake hajawahi kumchukia msanii Lulu Michael kama ambavyo imekuwa ikisikika masikitonkwa watu na watu wengi kuamini hivyo kwa sababu ya kumuua mtoto wake.

Mama huyo anasema kuwa hajawahi kumchukia Lulu lakini amekuwa na uchungu kila siku kwa sababu kifo chake kimesababishwa na mtu mwingine.

Mama kanumba alipokuwa akiongea na EATV, anasema  “kanumba ni mwanangu na nilikuwa ninampenda sana na ukizngatia nilimlea kwa tabu sana lakini anatokea mtu anamuua, mimi simchukuii lulu mimi ninampenda sana, ninamtakia kila lenye kheri katika maisha yake.

Kama bado kuna kumbukumbu, mama kanumba na lulu walikuwa marafiki sana hasa baada ya kifo cha kanumba lakini baada ya hapo mahusiano yao yalianza kufa na hata kufikia hatua ya kuwa maadui wakubwa.

Mama huyo ukiachana na kulalamika  katika mitandaokuwa lulu amekuwa hamuheshimu wala kumsaidia lakinni alichukizwa sana na hukumu aliyopewa mwanadada huyo ikiwa kama adhabu ya kifo cha msanii huyo ambae alikuwa katika mahusiano  na Kanumba.

Mama Kanumba Afungukia Ndoa Ya Lulu na Majizzo

Mama mzazi wa aliyekuwa Msanii wa Bongo movie Steven Kanumba, Florah Mtegoa maarufu kama Mama Kanumba amefunguka na kusema yuko tayari kuhudhuria harusi Lulu endapo ataalikwa.

Mama Kanumba ambaye aliweka wazi chuki yake dhidi ya Lulu baada ya kukutwa na hatia ya kumuua bila kukusudia Marehemu Steven Kanumba ambapo alihukumiwa miaka miwili jela.

Mama Kanumba alifurahi baada ya kifungo cha Lulu lakini hivi sasa baada ya Lulu kuachiwa huru Mama Kanumba anafunguka na kusema wazi wazi kuwa hana chuki na Lulu na endapo ataalikwa Kwenye Harusi basi hatasita Kuhudhuria kwani hana kinyongo na Mrembo huyo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kituo cha televisheni cha East Africa, Mama Kanumba alifunguka haya:

Hapa duniani sina chuki kabisa na Lulu na mimi akili yangu kwa hivi sasa akili yangu imeegemea upande mmoja tu nao ni kumuomba Mungu tu maana yeye ndio anatoa haki sawa kwa tajiri na hata masikini pia”.

Lulu alivalishwa pete na mpenzi wake ambaye ni CEO wa EFM Majizzo ambapo ndoa yake inatarajiwa kufanyika Miezi ya mbeleni.

Mama Kanumba Kuifufua Kampuni Ya Kanumba Iliyokufa Baada Ya Kifo Chake

Mama mzazi wa aliyekuwa staa wa Bongo movie Marehemu Steven Kanumba, Florah Mtegoa ameweka wazi nia yake ya kuirudisha sanaa katika ramani miaka baada ya kifo cha mwanaye kwa kuifufua kampuni yake iliyokufa baada ya kifo chake.

Mama Kanumba amefunguka na kusema baada ya kifo cha mwanaye huyo alidhani huenda mtoto wake mwingine, Seth Bosco angeweza kuvaa viatu vya kaka yake na kuiendeleza sanaa lakini amevishindwa.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers,Akipiga stori na Star Showbiz, mama Kanumba alisema kuwa

Baada ya kifo cha mwanangu Kanumba ukweli kila kitu kilivurugika si unajua muanzilishi ni muanzilishi tu nikajua mimi na mwanangu Seth tungeweza kuindeleza lakini baadaye tulishindwa maana Seth alishindwa kuvaa viatu vya marehemu kaka yake kama nilivyotegemea.

Lakini naomba niwaambie kwamba tuko kwenye michakato ya kuifufua kampuni hiyo baada ya kuzisoma chalenji nyingi za tasnia hii ambapo awali sikuwa na uzoefu kama nilionao sasa”.

Baada ya kifo cha Kanumba, Mama Kanumba na yeye alijiingiza kwenye fani hiyo ya kuigiza ingawa amewahi kukiri kuwa mwanaye hakutaka kabisa kumuona akiwa anaigiza lakini anafanya hivyo kwa hivi sasa ili kuingiza kipato.

Mama Kanumba Amuomba Msamaha Muna Baada Ya Kuchekelea Kifo Cha Mwanaye

Mama mzazi wa aliyekuwa staa wa Bongo movie Steven Kanumba, Florah Mtegoa maarufu kama Mama Kanumba amefunguka na kumuangukia Muna kwa magoti baada ya Kauli yake ya kuchekelea Kifo Cha Mtoto wake Patrick.

Jambo hilo lilitokea siku chache baada ya Muna Love kufiwa  na mtoto wake Patrick wiki chache zilizopita ambapo Mama Kanumba aliibuka na kuongea Kauli hii “Muna alinitukana sana, na mungu ametenda”.

Kwenye mahojiano  na Times Fm wiki hii, Mama Kanumba alisema kwamba watu hawakumuelewa alichokimaanisha na watu walikata video fupu tu ya yale yaliyosambazwa.

Muna mwanangu pole sana, ni donda hilo ambalo haliponi ni donda ndugu ila naomba unisamehe.

Sikuwa na  nia mbaya na sikuomba kitokee kilichotokea, watu walininukuu vibaya. Na wewe maneno uliyonisema mwanzoni hukujua kesho mwanangu, wote ni mapenzi ya mungu mimi sina nia mbaya”.

Mama Kanumba ameomba msamaha baada ya watu kumjia juu baada ya kutoa Kauli hiyo.

Steve Nyerere na Mama Kanumba Wafikia Pabaya.

Baada ya mama wa marehemu Steve kanumba kufunguka na kusema kuwa  mtoto wake alikuwa haongei kabisa na steve nyerere na hata yeye mwenyewe hana mahusiano mazuri na Steve nyerere tangu mtoto wake alipofariki mpaka sasa hawaongei na Steve labda kwa kukutana kwa baahati mbaya.

Baada ya Mama Kanumba kusema hayo , Steve Nyerere aliamua kutupa jiwe gizani huku akigoma kuonyesha alikuwa akimenga nani lakini kwa contenbt yake inaonyesha kuwa alikuwa ni kama anamjibu mama kanumba kwa kile alichokiongea .

Katika ukurasa wake wa instagra, steve nyerere aliandika “ukiona mtu mzima anaongea upumbavu tena mbele ya wajukuu , watoto wake na jamii kwa ujumla  bila kuthamini ukubwa wa jina lake  basi ujue huyo anawashwa washwa sana.”

 

Gabo Amefanikiwa Kuziba Pengo La Kanumba- Mama Kanumba

Mama mzazi wa aliyekuwa staa wa Bongo movie Steven Kanumba, Flora Mtegoa maarufu kama Mama Kanumba amemtaja msanii ambaye anaamini ameziba pengo la Kanumba Kwenye tasnia ya Bongo movie.

Mama Kanumba ambaye naye aliingia Kwenye Bongo Movie mara baada ya mwanaye kufa amemtaja Gabo Zigamba kama Msanii ambaye ameziba pengo la Kanumba.

Kwenye mahojiano  na Wasafi TV, Mama Kanumba amemtaja Muigizaji wa Kiume Gabo Zigamba kama ndiye msanii pekee mwenye uwezo sawa na Kanumba kwa sasa.

Gabo anajitahidi kwa kweli, nilichogundua kwanza anajua kuuvaa uhusika kwenye filamu zake, akiwa kama mlinzi anakuwa mlinzi kweli, akiwa kichaa anakuwa kichaa kweli. Namwambia asikate tamaa kuna watu watamkatisha tamaa kila atapokaribia kuyafikia mafanikio zaidi.”

Lakini pia Mama Kanumba amelinganisha uwezo wa Kanumba na Gabo:

Ni kweli Gabo ‘anashika kijiti cha Kanumba’ anajitahidi, anauthubutu, anajaribu, anajituma na anaweza”.

Mama Kanumba- Siwezi Kuhudhuria Harusi Ya Lulu na Majizzo

Mama mzazi wa aliyekuwa msanii wa Bongo Movie Steven Kanumba, Florah Mtegoa ‘Mama Kanumba’ ametoa povu zito hivi karibuni baada ya kuulizwa Kuhusu Ndoa ya Lulu na Majizzo.

Kwa wiki kadhaa sasa kumekuwa na tetesi kuwa muigizaji wa Bongo movie Elizabeth Michael maarufu kama Lulu na mpenzi wake Majizzo wanatarajia kufunga ndoa hivi karibuni.

Mama Kanumba amefunguka kuwa, endapo atapelekewa kadi ya mwualiko wa harusi hiyo hawezi kwenda kwa sababu tangu atoke gerezani hawajawahi kuonana na Lulu wala kusalimiana naye.

Kwenye mahojiano na Ijumaa Wikienda, Mama Kanumba amedai kuwa, hata hiyo habari yenyewe ya Lulu kuolewa na Majizo anaisikia kwenye vyombo vya habari na kwamba hajui lolote.

Kwanza hiyo habari yenyewe nimeisikia kwenye vyombo vya habari, lakini mimi sijui kabisa kama wanaweza kuniletea hiyo kadi ya mwaliko na hata wakiniletea siendi.

Najua itakuwa ngumu tu katika mazingira tuliyopitia sisi, kwanza mimi sasa hivi muda mwingi ninajikalia nyumbani tu kutoka na maradhi yangu haya presha”.

Mama Kanumba aliweka wazi kutofurahishwa na kitendo cha Lulu kutoka jela mapema baada ya kupata msamaha wa Raisi na kupewa kifungo cha nje mapema mwezi uliopita.

Mama Kanumba Asononeshwa na Kitendo Cha Lulu Kutolewa Jela Mapema

Mama mzazi wa aliyekuwa muigizaji wa Bongo movie Steven Kanumba, Florah Mtegoa maarufu kama Mama Kanumba ameeleza machungu yake baada ya Lulu kuachiwa gerezani jana.

Siku ya jana Jeshi la Magereza lilitangaza rasmi kuwa Elizabeth Michael ‘Lulu’ ameachiwa rasmi kutoka gerezani baada ya kukaa ndani kwa miezi mitano ambapo alitajwa kwenda kuendelea na kifungo chake nje.

Tangu Lulu afungwe Mama Kanumba aliweka wazi kuwa alifurahia kifungo cha Lulu na hata kudai kuwa kifungocha miaka miwili kilikuwa kidogo kwa mauaji ya mtoto wake.

Kwenye mahojiano aliyofanya na MCL digital, Mama Kanumba amefunguka kuwa tangu amepata taarifa kuwa Lulu ameachiwa amekuwa akikosa usingizi na hata presha kupanda kwani ameumizwa sana na taarifa hizo.

Tangu nilipopata taarifa hizi nimejikuta nakosa usingizi na kuumwa presha hivyo leo imenibidi niende kwenye maombi kwa ajili ya afya yangu.

Lakini siku zote naamini Kuwa maskini hana haki”.

Lakini Mama Kanumba amewashukuru wote walioshiriki katika kumtoa na kuongeza kuwa anaamini hiyo yote ni kwa sababu yeye hana hela.

Mama Kanumba Apata Mualiko Nchini Burundi

Mama mzazi wa aliyekuwa staa wa Bongo movie Steven Kanumba, Bi. Flora Mtegoa maarufu kama Mama Kanumba Amelamba shavu zito baada ya kupata mualiko wa kuenda nchini Burundi.

Mama Kanumba Amepata mualiko maalumu kutoka kwa wasanii wa filamu wa nchini Burundi kwa ajili ya kuenda kujifunza kazi za sanaa hasa filamu wanazofanya.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Amani, Mama Kanumba alisema kuwa baada ya kupata mualiko huo kutokana na wasanii hao kuthamini mchango wa marehemu mwanaye, ameona ni vyema kwenda na kitu nchini humo ambapo ataizindua filamu yake inayoitwa Capten Habona.

Yani najisikia ni mtu ambaye ninaheshimika ingawa mtoto wangu hayupo hivyo filamu yangu hiyo nitazindulia huko kwa vile na wao wamenipa heshima kubwa sana kwa kuwa filamu yenyewe ina historia nzuri sana“.

Mama Kanumba aliingia Kwenye sanaa miaka michache iliyopita mara baada ya Steven Kanumba kufariki dunia ambapo alikiri sababu za kimaslahi ndizo zilizomuingiza Kwenye uigizaji japokuwa mwanaye hakupenda aigize.

Mama Kanumba Ateta na Mh Mwakyembe

Mama  mzazi wa marehemu steven kanumba amempongeza mh mwakyembe kwa hatua yake anayotaka kuichukua kuhusu kupitia mikataba ya wasanii ambao walikuwa wakisaini mikataba ambayo inaonekana haiwanufaishi walengwa au ndugu wa  baadhi ya mastaa ambao ni marehemu.

Amesema kuwa hatua hiyo ni nzuri na muhimu kwake kwani amekuwa akiona kazi za mwanae kila siku mitaani lakini yeye hakuna anachonufaika nacho.

Kwangu mimi ni faraja, namshukuru Waziri Mwakyembe kwa kuliona hilo. Kwa mfano mwanangu Steven Kanumba, movie zake naziona lakini mama yake ni masikini wanaofaidi ni wengine, sasa kupitia hilo tamko la serikali nasema asante Mungu,” amesema.

“Mimi ni staa nisiye na hela, kazi za mwanangu naziona tu mtaani lakini mimi ni maskini,” Mama Kanumba ameiambia Clouds TV.

Wiki iyopitia Bungeni wakati wa mjadala wa bajeti ya wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa mwaka wa fedha 2018/19, Waziri Dkt. Harrison Mwakyembe alisema ameunda kamati ya wanasheria ya kuchunguza mikataba ya kibiashara waliyoingia marehemu Steven Kanumba na Mzee Majuto

 

 

Mama Kanumba Amwagia Povu Zito Wema Baada Ya Kugoma Kuigiza Naye

Muigizaji wa Bongo movie Wema Sepetu alifunguka hivi karibuni na kuweka wazi kuwa miaka ya nyuma wakati yupo Kwenye Mahusiano na Marehemu Steven Kanumba alimwambia hataki mama yake aigize.

Tangu Kanumba aage dunia miaka michache iliyopita mama yake mzazi na yeye ameingia Kwenye sanaa ya Bongo movie na hivi sasa ameshaigiza Movie kadhaa.

Siku chache zilizopita Wema Sepetu alifanya mahojiano na Global Publishers ambapo aliulizwa kama atakuwa tayari kushirikiana Kwenye filamu na Mama Kanumba ndipo Wema alitoboa kuwa hawezi kwa sababu  Kanumba alikataa mama yake kuigiza.

Baada ya taarifa hizo kusambaa Mama Kanumba ameibuka na kumtolea povu zito Wema na kudai kuwa sababu pekee ambayo ilimfanya mwanaye amkataze kucheza filamu ni kwa sababu alikuwa anamuangalia yeye na kumtunza lakini hivi sasa hana msaada hivyo inatakiwa aigize.

Kanumba alisema hayo kwa kuwa alikuwa ananitunza yaani ananinunulia vyakula na kunilipa mshahara kila mwezi kama mfanyakazi lakini sasa hayupo, je Wema alitaka nishike bakuli nikaombe barabarani au? Maana kulima siwezi hivyo naona tu bora niigize ili niweze kujikimu kimaisha”.

 

Kanumba Alikataa Mama Yake Kuigiza, Siwezi Kuigiza Naye

Msanii wa Bongo movie Wema Sepetu amefunguka na kuweka wazi kuwa kamwe hawezi kuigiza filamu moja na Mama mzazi wa Marehemu Steven Kanumba kwani Mwenyewe hakutaka mama yake ajiingize Kwenye sanaa.

Wema ameanika hayo huku akisisitiza kuwa kipindi wakati Kanumba yuko hai alimweleza Wema ambaye alikuwa mpenzi wake kuwa kamwe hataki mama yake ajiingize kwenye Bongo movie.

Wema alifunguka hayo Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers ambao walimuuliza endapo yupo tayari kucheza filamu na Mama Kanumba ambaye hivi sasa amegeukia sanaa hiyo:

Hapana, siwezi kwa sababu Kanumba alikuwa hataki mama yake aigize na hata mimi alishaniambia, sasa nitavunja makubaliano yetu mimi na Kanumba”.

Lakini pia Kwenye mahojiano hayo Wema alikataa tuhuma alizorushiwa na Mama Kanumba kuwa alipownda nyumbani kwa Wema hakufunguliwa geti badala yake aliishia kuchomeshwa mahindi:

Jamani…kwanza siku hiyo mimi sikuwepo kabisa, niliambiwa tu alikuja na kwa nini nifanye hivyo sasa“.

 

Mama Kanumba Awalalamikia Wasanii Kutofika Katika Kumbukumbu ya Mwanae

Mama wa marehemu Steven Kanumba amewalalamiki wasanii wngi ambao hawakufika katika kumbukumbu ya msanii huyo aliyewahi kuwa nguli na mkombozi wa wasanii wengine katika tasnia ya bongo movie.

Kanumba ambae alikuwa akitimiza miaka 6 tangu kifo chake tarehe 7 April  alifariki baada ya kuwa na ugomvi na mpezni wake lulu michael na kusababisha kifo chake tarehe kama hiyo miaka sita iliyopita.

mama wa marehemu anasema kuwa hashangai sana kuona  wasaini wengi hawajahudhuria katika siku hiyo kwa sababu wasanii hao wameshamaliza msiba lakini yeye bado kwake kidonda ni kibichi na ataendelea kulia tu.

hata hivyo Mama Kanumba anasema kuwa wasanii walipaswa kuwa wengi kutokana na vile kanumba alivyokuwa akiishi na wasanii wenzake wengi walipaswa kumkumbuka.

Idadi ya wasanii waliokuja hapa ni wachache ukilingakisha na namna Kanumba alivyokuwa akiishi nao vizuri,lakini ndio hivyo uwezi kulazimisha watokee,isitoshe labda wao wanaona wamemaliza msiba lakini kwangu  bado upo ila ninachowaombea yasije yakawakuta kama hayandio watajua nin i ninamaanisha.

Mama Kanumba :Kanumba angekuwepo Angemuoa Wema.

Mama wa moja ya wasanii  waliokuwa waigizaji nguli Tanzania , mama Steven Kanumba amefunguka na kukanusha tetesi za kuwa yeye pamoja na Wema amabe aliwahi kuwa katika mahusiano na marehemu mtoto wake kuwa wana ugomvi sio kweli kwa sababu kama yeye Wema ni binti aliyetokea kumpenda sana.

kwakweli wema mimi sina bifu nae na hakuna binti ninaye mpenda kama wema,na ninaomba anielewe hivyo, tukionana tusalimiane na tupendane na hizo habari za kutokunifungulia mlango ni uongo, aache kunifungulia kwani mimi namdai au yeye ananidai.

Mama kanumba pia akanusha tetesi za kwenye mitandao kuwa amekuwa akiombamsaada kwa wema na kwamba amekuwa akienda mpaka nyumbani kwake.

Na wala sijawahi kuomba ela ingawa kuna wengine wanasema kuwa nilitaka kuomba ila sijui na nini, wamuulize hata yeye mwenyewe.sijawahi kwenda kwake eti kulia shida na namshukuru sana kwa sababu ni mtoto mwenye heshima.

Hivi karibuni kulizuka kwa maneno kuwa mama huyo amekwenda kwa wema na akatakaa kumfungulia mlango ,  mama huyo anasema kuwa wema hajawahi kumvunjia heshima hata siku moja na kila siku alikuwa anatamani kanumba angekuwepo basi angemuomba amuoe wema.

Siku zote nimekuwa nikisema kama Mungu angekuwa amemuweka Steven, yule mimi nilikuwa nimempenda na ningempendekeza awe mkwe wangu.

“Lulu Akijishusha Kwangu Akaniomba Msamaha Nitamsamehe”- Mama Kanumba

Mama mzazi wa Marehemu Kanumba ameibuka na kuweka wazi kuwa hana kinyongo na Lulu endapo atakuwa tayari kujishusha na kumuomba msamaha basi atamsamehe.

Lulu alifungwa miezi michache iliyopita baada ya kukutwa na hatia ya kumuua bila kukusudia marehemu Steven Kanumba aliyekuwa naye kwenye mahusiano kwa kipindi hiko.

Kipindi chote wakati kesi inasikilizwa ni wazi kabisa Lulu na Mama Kanumba hawakuwa katika nafasi nzuri kwani walionekana wakipishana bila kusalimiana na hata Lulu alipohukumiwa kwenda jela Mama Kanumba alisema amefurahishwa.

Mama Kanumba alijiwa juu na watu hasa mashabiki za Lulu ndipo juzi alipofika kuwa hajawahi kumuombea Lulu mabaya na hana tatizo naye kwani alishamsamehe tangu zamani na hana kinyongo naye.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Millard Ayo Tv, Mama Kanumba amefunguka na kuweka wazi kuwa endapo Lulu Akitoka jela akaenda kumuomba msamaha basi atamsamehe.

Lulu alihukumiwa na Jamhuri ilikuwa nje ya uwezo wangu iwe nilimsamehe au sikumsamehe sikuwa na uwezo wa kufuta kesi. Mimi sina kinyongo na Lulu alikuja mara ya kwanza nikamsamehe na kama akimaliza kifungo akiwa tayari kwa kuwa yeye ni mtoto mimi mtu mzima kwaiyo yeye anapaswa ajishushe kwangu akiwa tayari akinipmba msamaha mimi nitampokea”.

 

Mama Kanumba: Natamani Kwenda Kumuona Lulu Gerezani

Mama mzazi wa aliyekuwa msanii wa Bongo movie Marehemu Steven Kanumba, Mama Kanumba ameibuka na jipya tena huku safari hii anatamani kwenda jela kumuona Lulu.

Mama Kanumba hakuwa na uhusiano mzuri na Lulu kwani mpaka a nafungiwa walikuwa kama wana ugomvi fulani huku Mama Kanumba alidai sababu kubwa ni Lulu kumtupa mama huyo na kutomjali kwa lolote.

Miezi michache iliyopita Muigizaji wa Bongo movie Lulu Michael alifungwa gerezani kwa miaka miwili baada ya kukutwa na hatia ya kumuua bila kukusudia aliyekuwa mpenzi wake Steven Kanumba.

Baada ya Lulu kufungwa Mama Kanumba hakusita kuonyesha furaha yake juu ya Lulu kufungwa na baadae alipoulizwa endapo ana mpango wa kwenda kumtembelea Lulu gerezani alisema hajui mpaka afanye mazungumzo na Mungu wake.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Mwananchi Communications, Mama Kanumba ameibuka na kusema anatamani kwenda kumuona Lulu jela:

Tangu Lulu kahukumiwa nimekuwa nikipokea lawama na watu kunitusi kuwa mimi ndio sababu, na kusahau ya the kwamba mimi nilishamsamehe kama binadamu na siye niliokuwa mlamlamikaji katika kesi hiyo isipokuwa alishitakiwa na serikali”.

Lakini Mama Kanumba amesisitiza kuwa yote yaliyotokea anamuachia Mwenyezi Mungu kwani yeye kufungwa hakuwezi kumrudishia mtoto wake ambaye amekwisha tangulia mbele ya hali.

Mama Kanumba Afunguka Kulizwa na Wema Sepetu

Mama mzazi wa aliyekuwa staa wa Bongo movie Marehemu Steven Kanumba ‘Florah Mtegoa’, Mama Kanumba amefunguka na kudai kuwa Wema Sepetu amemfanyia kitu mbaya hakutegemea.

Mama Kanumba amedai kuwa hivi karibuni aliwasilisana na Wema Sepetu na kukubaliana wakutane na ndipo Wema alipomuita nyumbani kwake Salasala jijini Dar es salaam lakini amedai alipofika getini hakufunguliwa geti.

Inadaiwa kuwa majirani waliokuwa maeneo hayo walimuona mama huyo akiwa amesimama kwa muda mrefu bila kufunguliwa na wamekiri kuwa ni tabia ya Wema kutofungua geti la nyumbani kwake kama huna appointment yoyote kwake.

Kwenye Interview aliyofanya na gazeti la Ijumaa, Mama Kanumba alifunguka na kukiri kuwa jambo hilo lilitokea ambapo aliongea na Wema hivi karibuni kwa simu ambapo walikubaliana aende nyumbani kwake na ndipo alipokodi bajaji mpaka kwake na alipofika alikuwa akigonga geti walinzi walimwambia hawajapewa maagizo yake na alikuwa akimpigia simu hapokei.

Jamani inauma nyie mtu nimekubaliana naye vizuri unakodi bajaji mpaka kwake kulivyo mbali lakini hajali wala hapokei simu nikaamua kuondoka zangu”.

Mama Kanumba amedai kuwa walikuwa na maongezi ya kawaida tu kwani alikuwa mkwe wake na alikuwa anampenda lakini pia amefunguka na kusema amesikitishwa kwani mpaka hivi sasa hajaombwa radhi na Wema.

Kisa picha ya Mwanae,Mama Kanumba Amwaga Machozi Standi.

Mama mzazi wa marehemu Steven Kanumba ameshangaza wengi baada ya kuanza kumwaga machozi  katika moja ya stand zinazojaza watu jijini dar anzabaada ya kuona bango lenye picha ya mtoto wake katika maeneo hayo.

Mama huyo ambae alishindwa kuzia hasira zake na kulia alisema kuwa mara nyingi amekuwa akiumia sana na kushindwa kujizuia kutoa machozi kila  anapoona picha au kitu chochote ambacho kinamkumbusha mtoto wake.

kila mara nimekuwa nikiziona picha za kanumba katika mabango , lakini sijui kwanini hii imenifanya nipatwe na uchungu na niishiwe na nguvu kabisa.-Alisema Mama Kanumba ambae anasema kuwa alikuwa akielekea maeneo ya segerea kwa ajili ya kyrekodi movie.

Kanumba alifariki miaka zaidi yamitano iliyopita baada ya kuuawa na mpenzi wake (Lulu Michae) waliokuwa na mtafaruku na kusababisha mauaji yake pindi walipokuwa wakizozana.Hata hivyo Lulu alihukumiwa kifungo cha miaka miwili gerezani baaada ya kukuta na hatia ya kuua bila kukusudia.

Mama Kanumba Afunguka Kuhusu Picha za Nabii Tito na Mwanae

Mama wa marehemu Steven Kanumba amefunguka baada ya kusambaa kwa picha za Nabii Tito na mwanae maraehemu steven kanumba  miaka ya nyumba kipindi cha uhai wake.Mama huyo amekiri  kuwa mwanae alishawahi kukutana na nanbii huyo lakini nia yake iligonga mwamba.

Mama Kanumba anasema kuwa nabii tito alikutana na Kanumba na kumuomba ajiunge katika kanisa lake alilokuwa amelianzisha kwa niaba ya kuwavutia watu watakaokuwa wanakuja kwa ajili ya kumshangaa Kanumba   lakini kwa upande wake itakuwa faida kwa sababu atakuwa amejaza watu.

Mama Kanumba anasema kuwa marehmu Steven alikataa kata kata kuhusu ombi hilo kutokana na imani yake haukumtaka kufanya hivyo lakini pia Kanumba hakutaka kuhama kanisa analosali hata siku moja.

Kwa upande wa Seth ambae ni mdogo wake na marehemu Kanumba ambae poia kwenye pia hizo amekuwa akionekana amesema kuwa ni kweli Nabii Tito aliwahi kuja ofisini kwa kaka yake zilizopo Sinza-Mori kipindi hicho kaka yake alikuwa hai na kuwashauri wahamie katika kanisa lake lakini walikataa na ndipo alipowaomba wapige nae nae picha.

Tabii tito ni mkazi wa Dodoma alieibuka kama nabii huku akihubiri neno la Mungu kwa kutumia biblia lakini akisapoti unywaji wa pombe kanisani na kuwa kuoa mwanamke zaidi ya mmoja ni swala halali huku alishauri hata kuona wasaidizi wa ndani pia ni sahihi.

Nabii Tito aliendelea kupata umaarufu baada ya kumuomba msanii Wema Sepetu kusali katika kanisa lake na pia aweze kumuoa ilhali yeye mwenyewe akiwa na wake watano na watoto 12, nabii tito alimuona wema aje katika kanisa lake ili aweze kupata idadi kubwa ya wafuasi kwa kuwa watakuwa wanakuja kumshangaa yeye kanisani.

Mpaka sasa Nabii Tito amekamatwa na kufanyiwa vipimo ambapo alikutwa na magonjwa ya akili na kuanza matibabu lakini pia kesi yake ikiendelea mahakamani, kosa kubwa  la Nabii huyo kufanya mahubii ya dini ya kikristo kwa kutumia msalaba na biblia kinyume na taratibu za kanisa.

Mama Kanumba Akanusha Kuwa Na Kinyongo Na Lulu.

Kuna tetesi zimekuwa zikisambaa mtandaoni kuwa kuna chuki kubwa kati ya mma kanumba na msanii Lulu Michael kutokana na matukio ya nyuma yaliyotokea baada ya kifo cha Kanumba ambapo wengi walitegemea kuwa kungekuwa na uhusiano mzuri kati ya mama huyo na msanii Lulu Michael.

Wiki iliyopita mama huyo alifunguka katika vyombo vya habari na kuelezea na kulalamika kuwa Lulu Michael alikuwa akimtukana sana baada ya kutoka jela kwa mara ya kwanza ambapo alikaa kwa takribani mwaka mmoja kipindi upelelezi wa kesi yake ya mauaji ulipokuwa haujakamilika.

mama huyo kwa maelezo yake alionekana  kuwa na chuki na mwanadada huyo na hata kufikia hatua ya kusema kama atataka kwenda jela kumuona Lulu itabidi kwanza aongee na Mungu wake ili aweze kumruhusu kwenda kumuona msanii huyo.

Akiongea katika gazeti la Ijumaa Mama Kanumba anaejulikana kwa jina lake halisi Florah  Mtegoa amesem kuwa tabia ya watu kusambaza maneno na kusema kuwa ana chuki na lulu michael ni uongo kwa sababu yeye hana chuki yoyote na binti huyo na hivi karibuni akipata muda atakwenda kumuona msanii huyo gerezani.

Mama Kanumba anasema kuwa hata kama mahakama isingetaka kumfunga binti huyo bado kwake ingekuwa sawa tu kwa sababu hana lengo lolote la kumuumiza binti huyo na amekuwa akimchukulia kama binti yake.

Sina chuki na Lulu kabisa na tulikuwa karibu nae sana tu,lakini nafikia watu  watu wake wa karibu wanaomzunguka ndio wanaosababisha ukaribu wetu kuparanganyika sana.Lakini moyoni mimi nina mpenda sana Lulu , mimi nina imani ya kikristo kabisa, kwaiyo siwezi kufurahia kuona mwenzangu anapata matatizo , na ipo siku nitamtembelea gerezani.- Aliongea mama huyo.

Lulu alipata hukumu yake ya kuua bila kukusudia mwanzoni mwa mwezi Novemba , ambapo kifungo chake anatakiwa kukitumikia kwa miaka miwili baada kukutwa na hatia ya kumuua Kanumba.

 

Mama Kanumba: Wema Sepetu Ni Mwanamke Wa Kuoa

Mama mzazi wa marehemu Kanumba ambae alikuwa ni msanii mkubwa wa bongo movies  ambae safari yake ilikatika baaada ya kupata umauti baada ya kuuwawa na aliyekuwa mpenzi wake kipindi hicho Elizabeth Lulu Michael mwaka 2012, april 12.

Akizungumza katika Exclusive interview na waandishi wa habari wa kipindi cha Chilawadu kinachorushwa clouds Tv siku ya Ijumaa mama huyo alipata bahati ya kuzungumzia maisha aliyokuwa akiishi mtoto wake huyo kipindi cha uhai wake.

Akijibu swali aliloulizwa kuhusu ni wanawake wangapi Kanumba alishawahi kuwaleta nyumbani na kuwatambulisha mama kanumba alisema kuwa Kanumba alikuwa msiri sana na katika wanawake wote ni Wema Sepetu tu ndie aliewahi kutambulishwa na kuletwa nyumbani kama rafiki ingawa hakusema moja kwa moja kuwa ni mpenzi wake , lakini Wema alikuwa  msichana wa kuoa.

Katika wanawake wote  Kanumba alinitambulisha wema sepetu, na katika wanawake wote  wema alikuwa ni mwanamke anaepaswa kuolewa.Wema ni mwanamke alikuwa akija nyumbani akikuta unapika utaacha atapika yeye kama unaosha vyombo basi ataosha na alikuwa akija kwangu anakuja na madela.

Wema septu akiwa na marehemu Kanumba enzi za uhai wake.

Akiendelea kuongezea Mama Kanumba anasema kuwa hata katika baadhi ya interviews alizowahi kufanya kipindi cha uhai wa marehemu alikuwa akimwambia kila siku ukitaka kuzaa basi unapaswa kuzaa na Wema.Hata hivyo Mama Kanumba anaendelea kusema kuwa katika vitu anavyompendea wema ni kwamba yeye ni msanii wa kwanza siku zote kuongea kila siku  kuwa Kanumba ndio aliyemtoa.

Wema ni mwanamke ambae nilitaka kila siku aweze kuzaa na kanumba, yaani angezaa  na Kanumba ningefurahi sana.Yeye ni binti ambae siwezi kumlinganisha na binti yeyote yule kwa sababu alifundwa na akafundika kabisa achana na haya mambo ya sasa hivi ya kwenye mitandao.

Lakini kitu kingine ninachompendea Wema ni kwamba yuko straight forward sana,ni msanii pekee aliyewahi kukubali kuwa Kanumba ndie aliemuingiza katika sanaa.,

Mama Manumba alisema kuwa pamoja na kuwa wawili hao waligombana lakini hakuwahi kujua kuwa waligombana ingawa alikuwa akiona tu kwenye medias. lakini alitamani sana wema siku zote awe mkwe wake hao wenine yeye alikuwa hawajui kwakuwa kanumba alikuwa msiri sana.

 

Mama Kanumba: Nilikuwa Naumia Nikimuona Lulu Anakula Raha, Nimefurahi Alivyofungwa Sahivi Zamu Ya Familia Yake Kulia

Mzazi wa marehemu Kanumba, Mama Kanumba amefunguka kuhusu furaha aliyokuwa nayo baada ya muuaji wa mtoto wake muigizaji Lulu Michael kuwekwa ndani kwa miaka miwili.

Tangu hukumu ya Lulu mengi yamesemwa huku watu wakigawanyika na misimamo kutofautiana kwani kuna watu wanasema kuwa afadhali Lulu amefungwa na kuna wanaosikitika Lulu kufungwa kwa sababu ni binti mdogo.

Baada ya kifo cha Kanumba, Lulu alikuwa karibu sana na Mama Kanumba lakini baadae ghafla ule ukaribu ukaisha na kusababisha tetesi kuenea kuwa wawili hao wamegombana huku sababu ikiwa haijulikani.

Kwenye mahojiano ambayo Mama Kanumba alifanya na Global TV alifunguka yafuatayo:

Kwa kweli tunashukuru haki imetendeka kwaiyo kama familia ya Lulu wamelia mimi ninalia kila siku wao miaka miwili tu atatoka mimi mtoto wangu sitamuona tena yaani harudi tena, Baada ya hukumu kutolewa tulienda makaburini kufanya misa lakini mimi sherehe yangu nitaenda kuifanya kanisani kwa kutoa shukrani ya pekee. Kwa muda mrefu familia yetu imekuwa ikiumia tukimuona Lulu nakula raha anaenjoy anafurahia iiltuumiza sana kwa muda mrefu ni bora mtu usimuone lakini anaposti anavyokula raha kweli tulikuwa tunahuzunika sana, lakini kesi ilivyoanza tulitegemea kesi haki itatendeka na tunashukuru Mungu ametutendea kwa kweli”.

Mara ya kwanza hukumu ilivyotolewa hakimu wa Lulu, Peter Kibatala aliweka wazi nia yao ya kukata rufaa lakini habari zimeenea kuwa kutokea jela Lulu amekataa kukata rufaa badala yake ameamua kutumikia kifungo chake chote cha miaka miwili.

Baada Ya Hukumu ya Lulu Kutolewa , Mama Kanumba Amwaga Chozi

Ikiwa ni dakika chache tu baada ya hukumu kutolewa leo Novemba 13 juu ya kesi iliyokuwa ikimkabili mwanadada Lulu Michael kuhusu kuua bila kukusudia ambapo msanii huyo amehukumiwa miaka miwili jela kwa kukutwa na hatia hiyo.

Mama wa marehemu Steven Kanumba ambae ndie alikuwa mpenzi wa eElizabeth Lulu Michael ameonekana nje ya mahakanma akilia kwa sauti hukua akisema kuwa anaishujkuru sana mahakama na serikali yake wa ujumla juu ya maamuzi waliotoa kuhusu kesi hiyo,mama huyo huku akilia amesema kuwa akitoka mahakamani hapo ataelekea makaburini alipolazwa Kanumba ili kwenda kumpumzisha kwa amani sasa tangu alipokuwa amezikwa .

mimi sina la kusem kwa sasa hivi ila la kwanza namshukuru mwenyezi mungu sana,pili ninaishukuru mahakama kwa kutenda haki na pia naishukuru sana seriakli yangu na hata nikitoka hapa nitaenda makaburini naamini  sasa naenda kumzika  na akapumzike kwa amani.-aliongea Mama Kanumba huku akilia kwa sauti

Kesi ya Lulu ambayo ilisikilizwa ushahidi wote mwezi uliopita ilikuwa imebaki kusikilizwa hukumu tu ambapo leo ndio ilikuwa mwisho wa kesi hiyo , hata hivyo leo tangu kumekucha kume kuwa na tension kubwa ya watu mbalimbali katika mitandao ya kijamii wakimuombea mwandada huyo kheri katika hukumu yake huku wengne wakiomba hasihukumuiwe kwa chochote,

Hata baada ya kutolewa wa hukumu hiyo watu wengi wameonyeshwa kuumizwa na hukumu iyo akiwepo Wema Sepetu ambao kwake ilikuwa ni habari mbaya tena ya kushtukiza sana.lulu atatumikia kifungio hicho cha kuua bila kukusudua kwa muda wa miaka miwili gerezani.

Lulu alikutwa na kesi hiyo mwaka 2012, ambapo alimuua Kanumba aliyekuwa mpenzi wake bila kukusudia kutokana na ugomvi wa mapenzi waliokuwa nao wawili hao ambapo katika purukushani hizo Kanumba alidondoakana kuanguka chini na ndipo mauti yalipomkuta.Hata hivyo baada ya kusikilizwa kwa ushaihidi kutoka kwa watu wa pande zote mbili  mahakama imeamuru lulu kutumikia kifungo hicho baada ya kuona kuwa katika ushahidi wake mwandada huyo alishindwa kuongea vitu vyote vilivyokuwa vimetokea siku ya tukio.

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.