JB- Siwezi Kuwa Mrithi Wa Mzee Majuto

Muigizaji wa Bongo movie Jacob Stephen maarufu kama JB amesema hata siku moja hawezi kuwa mrithi wa Marehemu Mzee Majuto.

Mzee Majuto alifariki mwezi uliopita baada ya kuugua kwa muda mrefu, Ingawa alikuwa na umri mkubwa Mzee Majuto alikuwa mmoja wa komedian mkubwa sana Tanzania.

Katika mahojiano aliyofanya na Global Publishers, JB amesema mashabiki wengi wamekuwa wakimwambia kwamba yeye ndiye mrithi wa Mzee Majuto, lakini haiwezekani kushika nafasi yangu maana alikuwa na ladha yake na yeye ana ladha yake katika uigizaji.

Haiwezekani mimi kuwa mrithi wa Mzee Majuto maana alikuwa na kitu cha tofauti sana na alipendwa na watu wengi hivyo ni vigumu kuwa mrithi wake ila ninawaahidi Watanzania kuwafurahisha kwa kadiri ya uwezo wangu katika kuigiza”.

 

Mke wa Mzee Majuto Adaiwa Kufukuzwa Nyumbani kwa Mumewe.

Mke wa marehemu Mzee Majuto anaripotiwa kuondoka nyumbani kwa mume wake jijini Tanga na watoto wake huku ikidaiwa kuwa sababu kubwa ya yeye kurudi nyumbani kwao jijin Dar ni kutokana na maneno aliyoambiwa na watoto wake wakubwa kuwa hawana uwezo wa kumlea mpaka arobaini.

Mwanamke huyo ambae alikuwa bega kwa bega na mzee majuto kwa kipindi chote cha uhai wake na ugonjwa wake mpaka anafariki, alikuwa mke wa pili wa mzee majuto na alibahatika kuwa na watoto nae huku mzee majuto akiwa na watoto wengine wakubwa aliozaa kabla ya kumuona mke huyo aliyepo sasa.

Hata hivyo inadaiwa kuwa mama huyo pamoja na kwamba alikuwa na watoto walikuwa wakisoma jijini Tanga, imemlazimu kuondoka na watoto hao na kuwaacha shule.

Baada ya kumtafuta moja ya watoto wa marehemu Mzee majuto alikiri na kusema kuwa ni kweli mama yao hayupo amerudi Dar lakini aliwaaga kuwa anakwenda nyumbani kwao.

 

 

 

Muigizaji Mtoto wa Miaka Minne Amlilia Mzee Majuto

Mtoto wa miaka minne ambaye anakuja kwa kasik katika tasnia ya uigizaji na Uchekeshaji Maisara Mohamed maarufu kama Maizumo amefunguka kusikitishwa na Kifo cha Mzee Majuto.

Mtoto huyo ameweka wazi kuwa ndoto yake kub a ilikuwa ni kuigiza na Marehemu Mzee Majuto aliyeaga dunia siku chache zilizopita baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, mtoto huyo amefunguka kuwa alikuwa anampenda sana King Majuto na alimuomba baba yake amkutanishe naye lakini hakufanya hivyo.

Nilikuwa nampenda sana King Majuto, nilikuwa napenda kuangalia muvi zake pamoja na matangazo yake, baba aliniambia atanipeleka nikamuone lakini hatukwenda mpaka amekufa”.

Baba Mzazi wa Maizumo Mohammed Omary ambapo kwa upande wake alisema kuwa siku ya msiba unatokea hakuwa nyumbani lakini aliporudi alimuita Mai nakumwambia kuwa Majuto amefariki lakini chakushangaza alilia sana kama mtu mzima na hata shuleni alikuwa anakataa kwenda, hivyo wakafanya kumlazimisha.

Nisha: Sitoweza Msahau Mzee Majuto Maishani

Msanio wa filamu za kibongo na msanii wa Bongo fleva Salma Jabu maarufu kama Nisha amefungukia Kifo Cha Msanii mwenzake mkongwe wa Bongo movie na comedy Mzee Majuto aliyeaga dunia wiki iliyopita.

Nisha amefunguka na kudai yupo katika majonzi mazito katika kipindi hiki ambacho Msanii huyo Nzee Majuto amefariki dunia kwani pengo alilomuachia haliwezi kuzibika katu.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Nisha alieleza kuwa, kifo cha Mzee Majuto kimemuumiza kupitia kiasi na pengo alilomwachia moyoni mwake ni kubwa kwani mashabiki wa filamu hasa za vichekesho wasingemjua.

Mzee Majuto nilikuwa namwita baba kwa sababu amenitoa kisanaa, yaani alikuwa ni kiungo muhimu sana maishani mwangu, machozi na maumivu yangu havitafutika, nashindwa kuamini na pengo lake halifutiki maishani mwangu”.

Mzee Majuto alifariki dunia siku chache zilizopita katika hospitali ya Muhimbili baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Picha Za Kuagwa Kwa Mwili Wa Mzee Majuto

Mamia ya waombolezaji wamejitokeza katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam kuaga mwili wa aliyekuwa muigizaji nguli wa vichekesho nchini, Amri Athumani ‘Mzee Majuto’ jana Agost 9, 2018.

Mzee King Majuto alifariki dunia jana Agosti 8, 2018 majira ya saa 2:00 usiku katika Hospitali ya Taifa, Muhimbili alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu kwa siku kadhaa.

Baada ya kuaga,  mwili ulisafirishwa kwenda nyumbani kwake jijini Tanga kwa maziko ambayo yatafanyika kesho Ijumaa.

Hizi ni baadhi ya picha za matunzo ya kuuaga mwili wa MZee Majuto:

 

.

 

Rais Magufuli Akiri Kuguswa na Kifo Cha Mzee Majuto

Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Joh Pombe Magufuli amefunguka kuguswa na Kifo Cha mchekeshaji maarufu Mzee Majuto kilichotokea siku ya jana.

Rais Magufuli Martina barua ya Rambi Rambi kwa Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo DKT. Harrison Mwakyembe na kumtaka afikishe salamu hizo kwa Familia ya Mzee Majuto.

Katika salamu hizo Mhe. Rais Magufuli amemtaka Dkt. Mwakyembe kufikisha salamu zake za pole kwa familia ya Marehemu, Wasanii wote nchini, wadau wa sanaa, ndugu, jamaa, marafiki na wote walioguswa na kifo cha King Majuto.

King Majuto alikuwa kielelezo cha safari ndefu ya sanaa kwa nchi yetu, kwa muda wote amedhihirisha kipaji, ujuzi na uwezo wa hali ya juu katika uigizaji na uchekeshaji na hivyo kuwa kipenzi cha Watanzania na wasanii wenzake, hatutasahau ucheshi wake, upendo na uzalendo kwa nchi yake wakati wote wa uhai wake”.

Tanzia- Mzee Majuto Afariki Dunia

Msanii mkongwe wa Bongo movie aliyejizolea umaarufu kwa vichekesho vyake amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Mzee Majuto amefariki usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Muhimbil baada ya kulazwa kwa siku kadhaa tangu wiki chache zilizopita baada ya kuugua.

Taarifa za msiba kwa mara ya kwanza zilitolewa na mchekeshaji Joti Kupitia ukurasa wake wa Instagram:

“R.I.P @Kingmajuto Umetuachia Maumivu Makubwa sana ktk Tasnia ya Comedy Tanzania Sisi wanao,Tutakukumbuka kwa kazi zako,Upendo wako,Tabasamu lako Daima milele,Tulikupenda sana ila Mungu amekupenda zaidi,Pumzika kwa Amani Mzee wetu”.

Mzee Majuto alianza kuugua mwaka jana na mwaka huu serikali kwa kushirikana na wananchi walichanga pesa na kumpelekeka kwenye matibabu nchini India.

Wema Sepetu, Diamond Platnumz mourn Mzee Maji Moto with emotional posts 

Singer Diamond Platnumz and actress Wema Sepetu have mourned popular Tanzanian actor Amri Athuman aka Mzee Majuto who died on August 8 while undergoing treatment at Muhimbili National Hospital in Dar es Salaam.

Maji Moto, who started acting in 1958 while he was still nine-years old, was a respected actor in the country who has played a huge role in shaping up the Tanzanian movie industry.

Sad

On Instagram, Diamond mourned the actor by posting black photo while Wema wished she got a chance to act with him.

“Alipangalo Allah… I wished to work with you baba angu… Ila Allah hakupanga… Kapumzike baba angu… Mungu Mkali jamani….???… Ila kama kuteseka tu umeteseka jamani…. RIP King…” posted Wema Sepetu.

“May your Humble Soul Rest in Paradise KING?…Will always Miss and Love you??,” Diamond captioned the black image.

The veteran actor was suffering from a hernia and had been admitted to the Intensive Care Unit due to his deteriorating condition.

 

RIP! Popular Tanzanian actor Mzee Majuto passes on 

Amri Athuman AKA Mzee Maji Moto, the popular actor from Tanzania, is dead. The actor, who has appeared in numerous Bongo films, passed away while undergoing treatment at Tanzania’s Muhimbili National Hospital in Dar es Salaam.

Maji Moto was suffering from a hernia and had been admitted to the Intensive Care Unit due to his deteriorating condition until August 8 when he passed on.

Long Career

Several celebs including Diamond Platnumz took to social media to mourn the legend, who has been a key pillar in Tanzanian movie industry.

Majuto was born in 1948 and is known for his roles in movies such as Kondakta, Mama Nitilie Movie and King Majuto Returns Home among many others. He started acting while only nine years old.

Hali ya Mzee Majuto si Shwari, Arudishwa Tena Muhimbili

Hali ya msanii mchekeshaji  maarufu na mkongwe tanzania mzee majuto imeripotiwa kurudi kuwa mbaya hivyo kufanya kurudishwa tena hospitali ya muhimbili siku ya leo.

Mkurugenzi wa mawasiliano katika hospitali ya muhimbili aminiel aligaesha , ndie aliethibitisha taarifa za kupokelwa kwa mzee majuto aktika hospitali.

Hii inakuwa ni mara ya tatu kwa mzee majuto kwenda hospitali lakini mara ya pili kurudishwa akiwa na hali mbaya kutokana na  operation aliyofanyiwa iliyosababisha kupelekwa india kwa ajilia ya matibabu zaidi.

Hatimaye Mzee Majuto Kulipwa Mamilioni Yake

Muigizaji Mkongwe wa Bongo movie Amri Athumani maarufu kama Mzee Majuto anatarajiwa kuanza kulipwa mamilioni yake ya pesa aliyokuwa anadai katika mikataba mbali mbali.

Habari hiyo njema imekuja Miezi michache tangu Waziri Mwakyembe alipoyataka makampuni mbali mbali yaliyoingia mikataba na Mzee Majuto kisha kumlipa pesa ndogo au kumzulumu Kupitia mikataba hiyo na kumlipa Tena pesa zake.

Kwenye mahojiano na gazeti la Amani Jumatatu iliyopita, nyumbani kwake, maeneo ya Bunju jijini Dar, Majuto alisema aliamua kusamehe ile mikataba midogomidogo ila kwenye ile mikataba mikubwa aliyodhulumiwa.

Niliamua kusamehe ile mikataba yangu midogomidogo ila hiyo mingine aliyosema ataishughulikia muheshimiwa Mwakyembe bado naendelea kuisubiri ila kwa sasa siwezi nikaongea chochote kuhusu hilo, hivyo naomba mumuulize msemaji wa chama cha waigizaji”.

Lakini pia gazeti hilo pia lilifanikiwa kuongea na msemaji wa Chama cha Waigizaji Mkoa wa Kinondoni, Masoud Kaftany ambaye alisema hatua aliyofikia Mwakyembe ya ufuatiliaji wa mikataba ya wasanii akiwemo mzee Majuto inaendelea vizuri na hivi karibuni kila kitu kitakuwa sawa.

Siku ya jana Mzee Majuto alitangaza kuachana na mambo ya sanaa kutokana na maradhi mbali mbali yanayomsumbua.

Mzee Majuto Agoma Kuigiza Tena , Aomba Kuongea Na Waziri na Rais

Msanii wa maigizo ya vichekesho nchini , Mzee Majuto amefunguka na kusem kuwa kwa sasa hana mpango wa kuigiza tena kwa sababu anataka kupumzika na wala hataki kusikia kitu kuhusu sanaa.

Majuto amesema kuwa maamuzi yake hayo kwa sasa ni ya mwisho na hakuna wa kuyabadilisha tena isipokuwa mh mwakyembe au mh raisi magufuli endapo watapata muda wa kuongea nae,lakini si vinginevyo.

Majuto anasema kuw akwa sasa haoni haja ya kuendelea kuigiza lakini kama atapokea ushauri kutoka kwa viongozi hao wawili wakubwa kuhusu sanaa anaweza kuwasilikiza na kubadili mawazo lakini sio mtu mwingine yoyote yule.

Natoa kauli yangu rasmi kuwa sitaku kuigiza tena labda raisi wangu mpendwa Magufuli  au mzee wangu Mwakyembe waniambia hapana endelea ndipo nitawasilikiza,hakuna mtu mwingine wa kunishauri baba yangu alishafariki na mama yangu alishafariki na marafiki zangu wote ni wasanii watupu.

Mara ya kwanza Mzee majuto aliwahi kutangaza kuwa anaachana na kazi ya sanaa na wasanii wengi walimlilia na kumfanya arudishe moyo wake nyuma ili kuendelea na sanaa lakini kwa hapa karibuni Mzee majuto alipatwa na maradhi yaliyomfanya kukaa hospitali kwa muda mrefu hivyo anaona kuwa anahitaji kupumzika kwa sasa.

 

 

Mzee Majuto Atangaza Kuwasamehe Wanaomdai

Msanii wa bongo movies mzee majuto  ametangaza kuwasamehe wale wote waliokuwa wakimdai na kusema kuwa hana haja ya juwadai tena hata kama ilikuwa pesa nyingi kiasi gani.

mzee majuto amemuomba mh mwakyembe hasiendelee kuwadai wala kushughulikia swala la madai yake tena kwa sababu alishawasamehe wote anaowadai.

pindi mzee majuto anaumwa na kukosa pesa ya matibabu , waziri mwakyembe akitangaza kufuatilia mikataba yote ya mzee majuto ikiwemo matangazo na kila biashara ya filamu aliyoifanya ili kuangalia sehemu gani wamemdhulumu ili aweze kupata haki yao.

ambapo baada ya kutangaza hivyo aliomba familia ya mzee majuto kutafuta nyaraka zote za mzee majuto ili kufuatilia madai hayo lakini baada ya mzee huyo kupata nafuu amesema kuwa hakuna haja hata kama kuna mtu anamdai shilingi 100.

Mzee Majuto Azungumza Kuhusu Kuzushiwa Kifo

Baada ya kuzushiwa kifo kwa msani wa bongo movies Mzee Majuto, mzee mwenyewe amemzungumza na waandishi wa habari na kukanusha kifo hiko na kusema kuwa yeye bado yuko hai lakini hata kama atakufa anawaomba sana watanzania wamuombee ili aweze kufa kifo  chema.

Akiongea na Global Online tv, mzee majuto anasema kuwa  kuwa anawashukuru watanzania kwa sara zao lakini anawaomba sana waendelee kumuombea huku akiishukuru serikali ya Tanzania kwa matibabu waliompatia.

Ninawaambia watanzania washtute , mimi sijafa mimi mzima jamani,kama mwenyezi mungu atanichukua basi mje mnizike kwa wingi , mniombee ili niende mahali pazuri, mlimpenda sana rafiki yenu kanumba lakini Mungu alimpenda zaidi.

Taarifa hizo ziliazna kusambaa juni 26 mwaka huu lakini mwanae wa kiume aliongea na kukanusha taarifa hizo na kusema kuwa baba yake alikuwa akiendelea vizuri.

TDFAA Wakanusha Taarifa za Kifo cha Mzee Majuto.

Kumekuwa na taarifa ya kifo cha Mzee Majuto katika mitandao ya kijamii  ilhali ni uongo kwa sababu mzee majuto tang ametoka nchini india bado yupo katika hospitali ya Muhimbili na anaendelea vizuri na bado yuko chini ya uangalizi wa madaktari.

Baada ya kuzushwa kwa taarifa hizo za kifo,Chama cha wasanii na waigizaji wametoa taaraifa ya kusikitishwa kwao na taarifa hizo “chama cha uigizaji kinasikitishwa na taaraifa zinazosambaa za uzushi zinazosambaa katika mitandao kuhusu kifo cha mzee majuto na kukanusha taarifa hizo kuwa si za kweli.mzee majuto yupo hai na yupo nyumbani kwake.

Mzee Majuto aliyekwa akisumbuliwa na ugonjwa wa tezi dume alifanyiwa upasuaji nchini lakini kidonda kilishindw kupona kwa haraka hivyo kulazimu kupelekwa nchini India kwa matibabu zaidi na alirejea siku kama mbili zilizopita.

JPM Ahusika Kufanikisha Safari ya Matibabu ya Majuto Nchini India.

Msanii wa filamu za maigizo na vichekeshao Mzee Majuto amefanikiwa safari yake ya matibabu kwenda nchini india kwa ajili ya matibabu  kwa matatizo aliyoyapata alipokuwa nchini kushindwa kufanikiwa hivyo kwenda nchini india .

Akiongea na waandishi wa habari siku ya tarehe 1 May, Steve Nyerere ambae alisaida sana katika zoezi hilo anasema kuwa siku hiyo Mzee Majuto  atatarajiwa kusafiri kwenda india kwa ajili ya matibabu yake huku akiwataja na kuwashukuru sana baadhi ya watu waliokuwepo  katika kfanikisha hilo huku akiwataja Mh Magufuli na Mh Mwakyembe katika kufanikisha hilo.

niseme ahsante sana kwa mh raiis john pombe magufuli , mh mwakyembe pamoja na Ummy Mwalimu kwa kufanikisha hili, lakini pia niwashukuru wasanii kwa kujitoa kwao, Mungu akipenda leo mzee majuto atakuwa njiani kwenda India kwa matibabu.

Hata hivyo Steve Nyerere pia amewatolea povu baadhji ya wasanii wanaokaa kujinadi katika mitandao kuhusu maisha yao lakini mwisho wa siku wanabaki wakiangaika na kuwa wanaomba misaada  wanapopata shida.

Sidhani kama miaka nenda rudi tutakuwa na kazi ya kuwa tunaomba omba tu,tumekuwa watu wa kufanya maparty kila kukicha na kujinadi kuwa ngu zetu za miliona 3, 4 lakini ukimuuliza umejipangaje kwa kesho hamna kitu.

 

 

Mh. Mwakyembe Kupitia Upya Mikataba ya Mzee Majuto.

Baada ya kutangazwa katika vyobo vya habari kuwa msanii mkongwe nchini mzee majuto ni mgonjwa sana na aanahitajika kwenda nchini India kwa ajili ya matibabu kuhu akiomba msaada wa kupewa fedha za matatibabu, mh waziri anaeshughulika na maswala hayo ameliambia mbunge kuwa Mzee Majuto ni msanii mkubwa sana na amefanya matangazo na kuingia mkataba na makampuni mengi sana mabyo yamekuwa yakirusha matangazo yake katika televisheni lakini mzee huyo hakufaidia  na kitu chochote.

Akiongea akiwa bungeni mh mwakyembe anasema kuwa “Mzee Majuto mwanasanaa mzuri anaumwa anaomba pesa, mimi leo nachanga kutoka mfukoni lakini leo hii nusu ya mabango ya biashara ni Mzee Majuto, matangazo ya biashara kwenye TV ni Mzee Majuto naomba sasa nitumie nafasi hii kusema nimeunda kamati ya wanasheria tumeanza na kesi ya Mzee Majuto mashirika yote na kampuni zote zilizoingia mkataba na Mzee Majuto tutapitia hiyo mikataba kama ameonewa lazima ilipwe familia yake tumeshachoka, tukimaliza Majuto tuna kuja mikataba ya Kanumba na msanii yoyote ambaye aliingia mkataba wa kipumbavu atuone”  .

Wasanii wengi wamekuwa wakiomba misaada pale wanapopata matatzo ilhali walikuwa na nguvu na jina kubwa ambalo lingeweza kuwaingizia pesa kwa kipindi chote cha ugonjwa au uzee kama Mzee Majuto.

Mzee majuto ameanza kuumwa tangu janauary mwaka huu na kufanyiwa upasuaji , ambapo hivi karibuni alirudishwa hospitali baada ya hai yake kuwa mbaya tena na kusemekana kuwa kidonda alichofanyiwa upasuaji kimeshindwa kufunga, mpaka sasa Mzee Majuto ameamishiwa hosptali ya muhimbili na wizara imepanga kumsaidia ili kupata hali zake za mikataba na matangazo mbalimbali aliyowahi kuyafanya.

 

Mzee Majuto Aomba Msaada wa Matibabu Nchini India

Msani wa maigizo nchini Mzee Majuto anaomba msaada wa kuomba kuchangiwa ela kwa ajili ya matibabu yake anayopaswa kufanyiwa nchini india haraka iwezekanavyo,Mzee Majuto ambae alikuwa akisumbuliwa na tezi duma na kisha kufanyiwa upasuaji January mwaka huu alikimbizwa tena hospitali hivi karibuni baada ya kuonekana kuwa hali yake inaaanza kubaidlika baada ya kidonda alichokwa amefanyiwa upasuaji kushindawa kufunga.

Baada ya kufanyiwa uchunguzi imebainika kuwa njia salama kabisa ya yeye kuendelea kutibiwa ni kwa kupoatawataalamu zaidi nchini india hivyo mzee majuto na familia yake wameomba msaada kwa watanzania ili kupata fedha kwa ajili ya shuguli hiyo.

Akiongea kwa kuthibitisha hilo, mtoto mkubwa wa Mzee Majuto amesma kuwa baba yake anahitaji fedha ili aweze kwenda nje ya nchi kwa ajili ya matibabu.

Hata hivyo, kiongozi ambae amekuwa akiwakilisha wasanii wengine, steve nyerere anasema kuwa huu ndio wakati wa watu kujitokeza na kutoa misaada yao na sio kusubiri mpaka mtu apate matatizo makuwa zaidi  au awe amekufa ndio watu waanze kujitokeza kwa kutoa misaada na kuposti katika mitandao kuonyesha masikitiko yao wakati alipokuwa hai walishindwa kumsaidia.

Mzee Majuto Bado Mgonjwa,Tumuombee:- Mke wa Majuto Awaomba Mashabiki

Mke wa mchekeshaji maarufu nchini Mzee Majuto anaejulikana kama Aisha  Yusuf ameowaomba wasanii, na mashabiki wake kwa ujumla kumuombea sana mzee majuto kutokana na hali yake kuwa mbaya kwa sasa baada ya kufanyiwa upasuaji na kidonda kushindwa kupona.

Hata hivyo aisha ansema kuwa mzee majuto alifikishwa hospitali hapo akiwa na hali mbaya sana wikiendi hii lakini anashukuru mungu kwa sababu kidogo hali yake imebadilika na kuwa nzuri.

Ninachowaomba tu watanzania, wamuombee mume wangu ili aweze kupona na pia tutoke hospitali kwa sababu akilala na mambo yote yanalala.

Mke wa Majuto anasema kuwa mzee majuto amefanyiwa upasuaji wa mara ya pili wa henia baada ya kuwa wanatafuta tiba ya ugonjwa mwinhine na ndipo walipogundua tatizo hili la tezi dume , walipomfanyia mwaka huu januari lakini kidonda bado kinasumbua kupona.

Wakati tunahangaika kupata matibabu ya nyoga ndipo alipogundulika kuwa anatezi dume ndipo alipofanyiwa upasuaji.

Mzee Majuto Akimbizwa Hospitali Baada ya Kuzidiwa Ghafa.

Mwigizaji wa maigizo ya vichekesho na filamu nchini, Mzee Majuto amekimbizwa hospitali  baada ya hali yake kubadilika ghafa na kuzidiwa .mzee majuto ambae amekimbizwa hospitali ya tumaini jijini dar ambapo alikuwa akipatiwa matibabu tangu mara ya kwanza amepelekwa hospitali hapo kwa ajili ya kuangaliwa tena afya yake.

Ikumbukwe kuwa Mzee Majuto aliwahi kuuumwa mara ya kwanza na kuthibitisha kuwa alikuwa akisumbuliwa na tezi dume hivyo alifanyiwa uapsuaji kwa ajili ya kutibu mardhi hayo lakini hali yake baada ya kubadilika inasemekana kuwa kidonda chake kimekuwa kikimsumbua kwa muda mrefu hivyo kinashindikana kupona na kusababibisha kutoka maji.

Akiongea na waandishi wa habari, mke wa Mzee mMajuto amesema uwa ni kweli mume wake amepeleka hospitali baada ya hali kubadilika na kukimbizwa hospitali huku akisema kuwa tatizo kubwa ni kidonda alichofanyiwa upasuaji kushindwa kupona na kutoa maji.

Mzee Majuto Akiri Sinema Kuwa Ndio Kila Kitu Kwake.

Msanii mkongwe na maigizo na vichekesho nchi Mzee Majuto  ambae amekuwa ni kama mlezi kwa wasanii wengine wa bongo movies amekiri kuwa kazi za sinema na filamu ndio kila kitu katika maisha yake na ndio zinazompa kula na kuishi mjini kwa miaka yote.

Akiongea na wasanii wenzake Jb na Single Mtambalike hivi karibuni walipomtembelea hospitali ambapo amelazwa kwa ajili ya kupatiwa matibabu, Mzee Majuto anasema kuwa anaishukuru na kuheshimu kazi hiyo kwa sababu ndio iliyompa kula na kuishi mjini, huku kisema kuwa pamoja na kwamba amekuwa mgonjwa kitandani lakini ndani anakazi  nane ambazo hazijatoka huku akiitaja ya uganga ndio iliyotoka tu.

Nina miaka 70 sasa na kazi kubwa inayoniweka mjini ni hii ya sinema,nina movis nane nimeziweka ndani kwaio sina presha.nikisikia njaa natoa moja nauza napata kula. na katika hizo nane nimeuza moja tu ya uganga basi.-Alifunguka Mzee Majuto.

Mzee Majuto yuo katika hospitali ya Tumaini jijini Dar, ambapo alilazwa kwa ajili ya kupatiwa matibabu ya upasuaji wa tezi dume iliyokuwa ikimsumbua kwa muda mrefu, hata hivyo hali yake inasemekana kuimarika .

Mzee Majuto Aomba Wasanii na Mashabiki Wamuombee.

Msanii wa maigizo ya  vichekesho na filamu nchini Mzee Majuto amewaomba wasanii na mashabiki zake kuendelea kumuombea kwa sababu hali yake sio nzuri sana pamoja na kwamba ameshatoka hospitali  alipokuwepo kwa ajili ya matibabu yake aliyokuwa  anapatiwa.hata hivyo mzee majuto anasema kuwa alitakiwa kufanyiwa upasuajai lakini ilishindikana kwa sababu ya matatizo aliyokuwa ameyapata daktari wake.

Mzee Majuto aliekuwa akiumwa ugonjwa watezi dume amesema kuwa ugonjwa huo ni hatari kuliko  ambavyo watu wanafikiria kwa sababu unaweza kukutoa Duniani bila hata ya wewe kujua kwaio anaomba watu wamuomee ili aweze kurudi katika hali yake ya kawaida.

Mzee Majuto alilazwa wiki chache zilizopita katika hospitali ya tumaini jijini dar ambapo mh raisi laikwenda hospitalini hapo kwa ajili ya kumjulia hali  msanii huyo na kmpa pole kitu ambacho pia kilimfariji sana msanii huyo.

Hata hivyo Mzee Majuto ambae kwa sasa yuko nyumbani anasema kuwa february 11 anatakiwa kurudi tena hoispitali kwa ajili ya uchunguzi wa maendeleo ya afya yake na kufanyiwa upasuaji kwa sababu daktari aliyekuwa ana mpatia matibabu alikuwa amefiwa hivyo kufanya kusimammishwa kwa matibabu yake.

Niliruhisiwa jumamosi iliyopita lakini kwakweli bado ninaumwa, tezi dume wala sio mchezo kwakweli.ninachoweza kuwaambiwa na kuwaomba ni kwamba ninaomba mniombee  tu , sala zenu pia zinahitajika.

 

 

,

Mzee Majuto Atembelewa na Mh.Rais Hospitalini.

Msanii wa maigizo ya vichekesho nchini , Mzee Majuto amaetembelewa na Mh .Raisi Magufuli hospitalini alipokuwa amelazwa  mpaka sasa ambapo bado anapokea matibabu ya ugonjwa wa tezi dume aligundulika kuwa nao siku kadhaa zilizopita.

Mzee Majuto ameonyeshwa kufurahishwa na ujio wa Raisi na kumpongeza kwa kazi yake nzuri anayoifanya sasa ya kuwafanya wananchi wote kuwa na moyo wa kufanya kazi na kujituma , lakini pia amesifia na kusema kuwa uongozi wa Raisi huyo umekuwa wenye baraka na neema kwa sasa sasa hivi nchi iko vizuri kwa kila mtu,

Akiendelea kuongea baada ya Mh.Raisi kutoka hospitalini hapo, Mzee Majuto anasema kuwa yeye ndie alikuwa mtu wa kwanza kutabiri kuwa Magufuli angeweza kushinda uraisi na angeweza kuiendesha nchi na ndicho anachokifanya sasa.

mii ndie mtu wa kwanza kutabiri kuwa akiwa raisi itakuwa shughuli hapa,nilishukuru kuchaguliwa kwa huyu bwana, hapa tumepata raisi sio masihara hasa, watu wote sasa wana adabu zao.wanajua nini maana ya kazi na akisema tu jambo watu wanatekeleza haraka sana.

wezi wanakamatwa, wala rushwa wanakamatwa, na wenye vyeti feki hata kama ulifanya kazi miaka 20 iliyopita fukuza, hii safi sana.

Sisi wazee tunafarijika sana, hivi viwanda sasa hivi vinatapakaa kila sehemu na leo hamekuja kunitembelea hospitali siujui kama kuna watu hawajajikojolea hapa kwa uoga maana hataki masihara kabisa.hii ndio raha ya kupata kiongozi bora mwenye msimamo.

Pamoja na kumpongeza lakini pia Mzee Majuto anasema kuwa sio kazi rahisi kwa wananchi kupata kiongozi mzuri kama Magufuli hivyo waweze kumtumia vizuri.

Mzee Majuto amelazwa katika hospitali ya Tumaini iliyopo jijini Dar wiki iliyopita baada ya kutolewa nyumbani kwake Tanga na kuletwa huku kwa matibabu zaidi na kukutwa na tezi dume , na mpka sasa bado yuko hospitali kwa kuendelea na matibabu.

Mh.Raisi alipokutana na Mzee Majuto akiwa hospitalini.

Mzee Majuto Kam-miss Lulu

Akiwa kama msanii mkongwe katika tasnia ya filamu Tanzania , ambae kwa sasa amepumzika kufanya kikazi zake za sanaa kutokana na umri kwenda  Mzee Majuto ameonyesha hisia zake za kum-miss msanii Lulu Michael ambae kwa sasa yupo gerezani akitumikia kifungo chake cha miaka miwili.

Lulu ambae alitunukiwa kifungo chake cha miaka miwili tarehe 13 November baada ya kukutwa na hatia ya kuua bila kukusudia msanii mwenzie Steven Kanumba ambae pia alikuwa mpenzi wake ameanza kutumukia kifungo hicho mara baada tu ya kukipokea siku hiyo.

Akiandika katika ukurasa wake wa instagram Mzee Majuto aliweka picha waliopiga siku za nyuma na msanii lulu michael na kuandika  ‘nimekumiss mjukuu wangu

Tangu Lulu kufungwa gerezani watu mbalimbali ikiwepo wasanii ambao wamekuwa wakionesha kusikitishwa na hukumu hiyo.Hata hivyo wapo baadhi ya wasanii waliokuwa wakitoa ushuari kwa lulu walimuomba kutokata rufaa hili kuondokana na mzizi wa fitina katika jamii.

Maisha Ya Mzee Majuto Matatani,Asakwa Na Wasiojulikana

Inadaiwa kuwa ni siku kama kumi zimepita tangu itolewe taarifa  kuwa msanii wa maigizo na vichekesho nchini Mzee Majuto alipotapeliewa fedha zake na kampuni mojawapo hapa nchini  inayohusika na filamu.Akimuelezea Waziri wa habari Mzee Majuto alidai kuwa kwa sasa hali ya maisha yake iko mashakani baada  ya watu hao wasiojulikana kutaka kumuuua kwa sbabau tu amekuwa akidai haki yake.

Akielezea sakata hilo moja ya watu wa karibu kutoka Tanga ambae akutaka jina lake litajwe alidai kuwa ;

Mzee Majuto hana amani kwa sasa , amekuwa akilalamika kuwa kuna watu wanataka kumuua kwa kuwa alikuwa anadai ela zake ambazo mpaka sasa hajapatiwa hata shilingi kumu na yupo tu hajui cha kufanya, mbaya zaidi ni kwamba alipoteza simu yake kwaio hana wa kuwasiliana nae kumsaidia kwa hilo.kwaio kuogopa kwake kunamfanya anyamaze tu sasa hivi.

Akiulizwa na waandishi kutoka kampuni ya Global alipofuatwa nyumbani kwake, Mzee Majuto alikiri kuwa kweli kuna watu wamekuwa wakimtishia kumnyonga na kumpiga risasi lakini hana ufahamu na watu hao.

Licha ya kumweleza waziri lakini mpaka sasa sijapata kitu changu chochote kwa siku,na ninaogopa kuendelea kudai kwa sababu ninatishiwa kuuawa,si unajua siku hizi mtu ukidai haki zako unaweza kunyongwa au ukiwa barazani  unashtukia unapigwa risasi na watu wasiojulikana.

Nilikuwa na namba za waziri na nilimpigia baada ya siku ile kunihaidi atashughulika swala langu,lakini siku ile aliniambia yupo kwenye kikao nimtafute wakati mwingine.Siku chache baadae nikiwa nasafiri kwenye ndege nilipoteza simu kwaio nikawa sina namba tena,imebidi nitulie nimwachie mungu tu  atanilipa hizo fedha ninazodai maana naogopa kunyongwa jamani.

Hata hivyo bado Mzee Majuto anamkumbusha na kumuomba Waziri  mwenye mamlaka hiyo kushughulikia swala lake kwa sababu peke yake anaona ameshindwa kabisa.Mwisho wa mwezi uliopita Waziri wa habari alikutana na wasanii na kuzungumza nao ili kujua changamoto zinazowakabili, na katika mazungumzo yake alihaidi kushughulikiwa watu wote ambao wamekuwa wakiwadhulumu na kuwaonea wasanii katika kuwapatia haki zao.

 

Mzee Majuto aeleza vitu ambazo atajishugulisha nazo baada ya kuamua kustaafu

Alhaji Amri Athumani maarufu kama Mzee Majuto sasa ameamua kuachana na mamba ya sanaa baada ya kufanya kazi ya uigizaji kwa takriban miaka 30.

Mwezi jana muigizaji huyo mkongwe aligonga vichwa vya habari baada ya taarifa potovu kuidai kuwa ameaga dunia ghafla nyumbani kwake Tanga.

Mzee Majuto sasa ameeleza kuwa ameamua kustaafu baada ya kuona umri wake unaenda na uwingi wa changamoto wa kazi yake ya uigizaji.

kwenye mahojiano yake na gazeti la Habari Leo, muigizaji huyo alifunguka na kusema kuwa yeye sasa atajishugulisha na kilimo na kumtumikia Mungu.

“Kwa sasa hivi mimi sanaa basi , nasema kwa kweli sanaa basi labda kutokee mtu anahitaji nimfanyie tangazo lake nikimaliza narudi shambani kwangu nimtumikie mwenyezi Mungu nimuombe toba kwa sababu tuliofanya ni mengi na kuna mazuri na mabaya na mabaya ndiyo yanayotawala kwenye maisha ya ujana kwa hiyo tumuombe toka Mwenyezi Mungu, kwani wakati ndiyo huu ukisema upange siku kila siku utapanga,” Mzee Majuto alisema.

Tazama mahojiano hayo hapo chini:

https://youtu.be/Sf9_vue0ttc

Comedian Mzee Majuto is not dead!

If you are a fan of Swahili comedy then I am sure you know who Mzee Majuto is! As for those who are not familiar with him, then allow me to explain who the comedian is.

Well, Mzee Majuto is among the funniest comedian from Tanzania and has been entertaining many for years now. He has also been featured in a couple of Bongo songs where he always manages to bring out his funny character without trying too hard!

Mzee Majuto

Anyway, a few days ago there were rumors making rounds on social media claiming that the old comedian had passed on. However one of his closest friends has come out to brush off the rumors as the comedian is still alive though his health seems to be deteriorating due to old age.

Through his Instagram page Haji Salum popularly known as Mboto wrote saying;

Mzee Majuto’s health deteriorating

“Baada ya kupata taarifa mbaya kuhusu Mzee Majuto nimelazimika kuja kwake Tanga. Ni kweli anaumwa ila anaendelea vizuri na si kama watu walivyozusha kuwa mzee hatunaye. Kwa sasa mzee ni mzima nipo naye Tanga,”

However it is quite sad to see how old age has turned Mzee Majuto’s life upside down.

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.