Singer Shilole reveals main reason she dumped her young husband, Uchebe

Tanzanian singer Shilole recently had a heart to heart interview with Clouds Digital where she opened up about a few things that led to her failed marriage.

Speaking for the first time, Shilole went on to describe her ex husband as a violent young man. According to her the fella apparently has too much pride and can never accept when he is wrong. So what happened?

Well apparently Shilole found out about her husband mistress and the new born they had recently welcomed. Just like any other woman would, she went on to ask about the rumors which seem to have angered Uchebe. Shishi says things got out of hand after she confronted him about the affair – which had now led to a child being born.

Shilole beaten black and blue

Also read; Shilole’s young husband introduces new found love barely a month after his divorce (Photo)

Violence

However throughout the whole time Shilole says her young bae kept ignoring her as he played his PS; seeing he wasn’t interested in having a mature conversation, Shishi says she then headed to the bedroom where he later followed her.

Apparently the whole time he was quit; the fella had been had plotting on how to punish Shilole for getting involved in his affairs; and this how she ended up with the bruises on her face as seen on the viral photos shared online.

Also read;Shilole left looking unrecognizable after receiving serious beating from young husband (Photos)

Battered Tanzanian actress, Shilole

The lady opens up barely 2 months after they called it quits; however her interview seems to have attracted criticism from fellow women. As seen on the comment section, most went on to advise Shilole to keep her private affairs off social media next time – because at the end of the day her marriage remains sacred!

 

Shilole’s young husband introduces new found love barely a month after his divorce (Photo)

Just wow! Yes, if you remember well a few weeks ago Bongo singer Shilole went on to expose her young husband for physically abusing her. As seen on the photos shared by the singer, it was evident to see the bruises left on her face by the guy she had married and invested in!

Having lived a lie for years, Shilole decided to part ways with the young handsome man as she feared losing her life while trying to keep a man.

She then publicly disowned him and promised to get a divorce (Talaka) which is easily issued; compared to the normal divorce procedures that take forever!

Also read:A happy Shilole and hubby before their love turned sour (Photos)

Shilole battered by husband, Uchebe

New found love

Well, now that he is a single man with little money from his spare parts business; rumor has it that Uchebe bagged himself a younger version of Shilole’s look alike.

Also read: Tanzanian celebrities react to Shilole’s horrifying photos after receiving serious beating from husband

The photo shared on the guys Instagram page however seems to have attracted harsh comments from fans who called out the young man for being a cheat!

Others could not help but compare the new lady to Shilole since the two happen to share a striking resemblance that you cannot overlook.

Shilole and ex husband before their love turned sour

Although the caption used on the photo did not say much; fans in the comment section did not seem impressed with how ungrateful Uchebe was now acting towards the woman helped from the ground up! He went on to caption the photo saying;

Comment with your fav emoji

Uchebe and new found love

Fans on the other hand had this to say:

fans tell off Uchebe
Uchebe trolled

A happy Shilole and hubby before their love turned sour (Photos)

Singer Shilole and husband of 2 years Uchebe left many talking after the lass shared photos showing how badly her husband has been beating her.

This however came as a shocker since the two never showed any signs of abuse; or even embarrassed each other on social media.

But after unveiling the photos through her instagram page; fans now feel that these two have been living a fake life that would have probably cost Shilole her life.

Shilole beaten black and blue

Paul Makonda speaks

However during a press conference held by Paul Makonda who is the Regional Commissioner of Dar es Salaam; he got to reveal that Shilole and Uchebe had been having issues for a while now.

He went on to mention that so far he has intervened thrice after the couple was involved in bad physical fights. According to him, this time around the law will have to deal with the two; and however is found on the wrong will have to face the consequences.

Makonda went on to urge men to avoid turning their wives into punching bags; as he referred to the photos shared by Shilole.

https://www.instagram.com/tv/CCa9qdJBu-T/?utm_source=ig_web_copy_link

Marriage life

Although no union has ever been easy, the likes of Akothee and Zari have strongly asked young women to avoid abusive relationships as it never ends well.

Through her Instagram page Akothee condemned this type of relationships saying she was better off lonely; than damaged from the mental and physical abuse from a carefree man.

SAY NO TO DOMESTIC VIOLENCE ????‍❤️‍????

No woman should go through this kind of humiliation, it’s not that we are weak and can’t fight back , it’s the respect and love that we have for you that brings submission, every woman in love will do everything to keep her marriage going even when you date an imbecile ????, No one wants to live alone ,it’s very lonely up there ,it’s even worse as a celebrity.

Anyway, we also can’t overlook the fact that Shilole and Uchebe shared some memorable moments before their love turned sour. Check out the photos below;

Shilole and Uchebe before love become sour
Uchebe and Shilole on their wedding day
Love birds Shilole with hubby
Shishi with ex hubby
Couple goals

Uchebe Apongezwa Kwa Kumuachisha Pombe Shilole

Mume wa Msanii wa Bongo fleva Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole, Ashraf Uchebe amepewa pongezi nyingi na wasanii mbali mbai Baada ya kuweza kumbadilisha mke wake.

Wasanii wa Bongo movie kama vile Jacob Steven ‘JB’, Steven Mengele ‘Nyerere’ na Single Mtambalike ‘Richie’ wamejikuta wakimpa ­pongeza shemeji yao, Uchebe kwa kumbadili na kumuweka kwenye maadili ya kidini tofauti na alivy­okuwa zamani.

Global Publishers wanaripoti kuwa tukio hilo la kumpongeza Uchebe lilichukua nafasi kwenye msiba wa msanii mwenzao Salome Nonge ‘Mama Abdul’ baada ya Shilole kuonekana kubadilika sana kwani hata mmoja wa wasanii alipommwagia pombe kwa bahati mbaya, alionesha kumaindi kuliko maelezo.

Jamani Uchebe hongera sana maana kazi uliyofanya sio ndogo, nakuambia ni kazi kubwa. Yaani dada yetu Shilole leo hii anaona pombe anaruka hivi? Shemeji yetu hongera, umetukosha“.

Shilole alifunga ndoa na Uchebe mwaka juzi na tangu afunge ndoa ameonekana akiwa kama mwanamke tofauti kama alivyokuwa awali na hata kuonekana akiwa ameanika dini zaidi.

Shilole Awatolea Uvivu Wanaommendea Uchebe

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole amewajia juu na kuwatolea uvivu wanawake wanaomuwinda Mume Wake wa ndoa Uchebe.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Shilole amevunja ukimya, awatolea uvivu wanawake wanaomuwinda mume wake akisisitiza ametumia nguvu kubwa kumpa mwonekano alionao sasa.

Niliridhika na hali yako tangu mwanzo Mpaka sasa unashaini ila wadangaji msivyo na haya mnaanza kumwambia mume Wangu Uchebe amekuwa handsome. Mkome namtunza zamani mlikuwa wapi?”.

Shilole alifunga ndoa na Uchebe Desemba ya mwaka 2017 kabla ya hapo Uchebe alikuwa Fundi gereji na asiyejulikana Lakini tangu ameanza mapenzi na Shilole ameonekana kunawiri na Hivi sasa anaishi maisha ya kifahari na msanii huyo.

Shilole Afungukia Mipango Ya Kuzaa na Uchebe

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole amefunguka na kuwajibu watu ambao wamekuwa wakimteta kwa kuchelewa kwake kumzalia mtoto mumewe Uchebe waliyefunga ndoa mwaka jana.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Dimba, Shilole amefunguka kuwa kushika ujauzito na kujifungua salama ni mipango ya Mwenyezi Mungu, hivyo hana haraka na hilo, kwani anaamini ni muda tu haujafika. ya Mwenyezi Mungu, hivyo hana haraka na hilo, kwani anaamini ni muda tu haujafika.

Nadhani kila kitu ni mipango ya Mungu, wakati ukifika kila kitu kitakuwa hadharani, kwani mimba ni pembe la ng’ombe halifichiki, alisema, Shilole“.

Shilole ameweka wazi kuwa kwa Hivi sasa yuko bize na shughuli zake za ujasiriamali, lakini wakati huo huo akiwa anaihudumia familia yake kama ilivyo kwa wanawake wengine.

Shilole Afungukia Sababu Za Kutomzalia Uchebe

Msanii wa muziki wa Bongo fleva nchini Zuwena Mohamed maarufu Kama Shilole amefunguka na kuanika sababu zinazomfabya mpaka leo hii asimzalie mume Wake Ashraf Uchebe.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi cha Enews cha EATV, Shilole ameweka wazi kuwa sababu pekee iliyomfanya Mpaka sasa hajamzalia Mumewe Uchebe ni sababu anaamini Mungu bado hajambariki Mtoto kwa sasa kwani Mtoto ni zawadi kutoka kwa Mungu.

Lakini pia Shilole ameweka wazi kuwa wao Kama wana ndoa wamekuwa wakijaribu kwa kipindi kirefu sasa kutafuta Mtoto lakini majaaliwa ya Mwenyezi Mungu hayajatimia bado.

Sisi tulikuwa tunatafuta Tupate Mtoto lakini bado hatujajaliwa, unajua mtoto sio kwamba mtu unapachikwa tu, mtoto anatafutwa na hatafutwi siku moja watu wanakaa miaka hata 10 na hwapati Mtoto na wako kwenye ndoa, Mimi tayari Nina watoto wawili na hata hao wengine hawakupatikana hivi hivi”.

Shilole tayari ni mama wa watoto wawili wa kike aliozaa na aliyekuwa mume Wake ambaye pia alifariki Wiki chache zilizopita.

Shilole Afungukia Mkosi Wa Nyumba Yake Mpya

Msanii wa muziki wa Bongo fleva nchini Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole amefunguka na kuweka wazi kuwa baada ya kuhamia kwenye mjengo wake mpya lakini amekiri kukaribishwa na mkosi.

Global Publishers wanaripoti kuwa Shilole alitokelezea kwenye uzinduzi wa Albamu ya Nandy lakini Ghafla aliibua minong’ono Baada ya kuonekana na nundu usoni hali iiyopelekea watu kudhani huenda Mumewe Uchebe amemtembezea kichapo.

Katika mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa Wikienda Shilole alifunguka na kusema:

Aaa…Unajua juzijuzi ndiyo nimehamia nyumbani kwangu Majohe, sasa nyumba yenyewe bado sijaizoea na bado sijaweka umeme, sasa niliporudi usiku nikiwa nimechoka ndiyo nikajikuta napiga mwereka na kuumia hivi.

Si unajua nyumba usiyoizoea? Hayo ndiyo yaliyonikuta na hii pati kwa kuwa nilishaalikwa na kumhakikishia Nandy kuwa nitakuwepo, nimeona nijikongoje nifike haina jinsi”.

Miezi michache iliyopita Shilole alianika mjengo Wake mpya alioujenga kwa kutumia pesa aliyopata kupitia Sanaa na biashara zake.

 

Shilole- Wivu Ndio Umempelekea Uchebe Kuwa Video King

Msanii wa muziki wa Bongo fleva nchini Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole amefunguka na kuweka wazi kuwa sababu za mume wake Asharaf Uchebe kuwa video king kwenye video yake.

Siku chache zilizopita Shilole ameachia wimbo wake mpya unaoenda kwa jina la ‘Champion’ na ndani ya video hiyo mumen wake Uchebe amesimama kama video king hali iliyopelekea mashabiki kuhisi huenda msanii huyo amejiingiza kwenye sanaa rasmi.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers , Shilole alisema kuwa, mumewe huyo huwa hapendi sana kumuona akishuti video na wanaume huku ‘akibambiwabambiwa’ hivyo ili kumfanya awe na amani ndipo akamtumia yeye kwenye video hiyo.

Ule wimbo kwanza nilimuimbia yeye, lakini Uchebe ana wivu sana, huwa hapendi kuona nashikwashikwa na wanaume kwenye video au hata kwenye steji, ndiyo maana nikaona kwa wimbo huu ambao nimemuimbia, siyo vibaya nikamtumia na kakinogesha kichupa ile mbaya”.

 

Uchebe Atangaza Vita Kwa Wanaume Wanaommendea Shilole

Mume wa staa wa Bongo fleva na mjasiriamali Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole, Asharaf Uchebe amewachimba mkwara wanaume wowote ambao wanataka kuingilia ndoa yake na Shilole.

Uchebe amefunguka na kudai kuwa atakuwa tayari kwenda hata jela endapo atagundua kuwa kuna mwanaume anamtaka mke wake au hata atagundua kuwa anasalitiwa.

Kwenye mahojiano na Ijumaa Wikienda , Uchebe alisema kuwa anajua anapata tabu gani kuhakikisha anailinda ndoa yake hivyo ataumia sana atakapomkuta mwanaume mwingine anamrubuni mkewe na anaweza kufanya kitu ambacho hakikutarajiwa na watu wengi.

Mimi nampenda sana mke wangu najua wazi ni kiasi gani naumia kuilinda ndoa yangu isiingiliwe na kidudu mtu ila watu hawezi kuelewa hata kidogo hivyo kama nitamkuta mwanaume yeyote au nikimfumania mke wangu huyo mwanaume ama zake ama zangu”.

Shilole na Uchebe walifunga ndoa mwaka jana mwishoni.

 

Shilole Awataka Wasanii Wenzake Waolewe Ili Waache Kuzini Mwezi Huu Mtukufu

Msanii wa Bongo fleva Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole amewataka wasanii wenzake wa kike Kuolewa katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani ili waache kufanya zinaa.

Shilole ambaye alifunga ndoa na mume wake Ashraf Uchebe mwaka jana mwishoni ameonekana kifurahia ndoa hasa kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Kwenye mahojiano na Ijumaa Wikienda, Shilole amekiri kuwa katika mfungo wa mwaka huu, anaona raha mno kwani ndiyo kwa mara ya kwanza umemkuta ndani ya ndoa na amekuwa akifunga na kufanya dua na mumewe tofauti na miaka mingine ambayo alikuwa hajaolewa, alikuwa akilegalega kufanya sala na kufunga.

Huu ni mfungo wa kipekee kwangu kwani ndiyo kwanza umenikuta ndani ya ndoa, kiukweli ninajisikia raha mno ambayo sikuwahi kuipata awali”.

Lakini pia Shilole aliwataka mastaa wa kike ambao hawajaolewa wajitahidi waolewe na waachane na kuzini kwa sababu dua zao ndipo zitakapopokelewa pia anawaombea ili wapate waume wema kama yeye alivyopata mume mwema anayemuongoza katika njia nzuri ya kumjua zaidi Mwenyezi Mungu.

“Sina Ujauzito Bali Nimenenepa Kwa Raha Za Mume Wangu”- Shilole

Mwanamuziki wa Bongo fleva Zuwena Mohamed maarufu kwa jina la usanii kama Shilole amekana Tetesi za kuwa yeye ni mjamzito na kudai amenenepeana kwa sababu ya raha za ndoa.

Tetesi za Shilole kuwa mjamzito zimekuwa zikishika kasi tangu Afunge ndoa ya ghafla na mume wake Uchebe mwaka jana mwishoni.

Na taarifa hizo zinatokana na kiukweli Shilole amenenepa sana na kujiachia mwili wake kiasi ya kwamba kuwa na mwili mkubwa tofauti na alivyokuwa siku za nyuma.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Ijumaa Wikienda, Shilole alisema kuwa, amenenepa kwa ajili ya raha anazopewa na mumewe Uchebe na kuridhika na maisha yake, lakini siyo kwamba ana ujauzito.

Watu wengi wanasema hivyo, lakini mimi sina ujauzito, bali nimenenepa tu kwa raha anazonipa mume wangu,” alisema Shilole na kudai kwamba, wanaosema hivyo siyo watu wabaya kwani wanamtakia heri na mambo mazuri“.

 

Mume Wangu Hakasiriki Akiniona Nakata Viuno Hadharani- Shilole

Mwanamuziki wa Bongo fleva Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amefunguka na kukiri haoni ubaya wa yeye kukata mauno stejini maana yupo kazini.

Suala limekuwa ishu baada ya video yake akiwa anatumbuiza stejini huku anakata kata mauno kihasara hasara stejini kusambaa Kwenye mitandao ya kijamii.

Ndipo watu kuanza kuhoji inakuwaje mke wa mtu anafanya mambo yake hadharani lakini Shilole amewazima watu hao na kusisitiza kuwa Mume wake anajua anachofanya hivyo haoni kama kuna tatizo.

Shilole amefunguka alipohojiwa na Global Publishers kuhusu hilo na kuweka wazi kuwa anawashangaa watu wanaozungumza kuhusu hilo wakati wanajua wazi kuwa ile ndio kazi yake na mume wake Uchebe analitambua hilo hivyo hana neno juu ya hilo.

Mume wangu Uchebe (Ashraf) anajua nikiwa kazini, chochote naweza kufanya jukwaani, haoni shida maana ananipenda na kazi yangu hivyo wanaosema ninawasihi waache kwani pale nilikuwa kazini kwa hiyo lazima niwapagawishe mashabiki wangu”.

 

Harmorapa Amtolea Povu Uchebe na Kudai Ameolewa na Shilole

Rapa wa muziki wa Bongo fleva Harmorapa aliyejipatia umaarufu Kwenye mitandao ya kijamii kwa vituko vyake amerudi tena Kwenye headlines na safari hii yuko na Shilole pamoja na mumewe Uchebe.

Harmorapa ameibuka na kudai kuwa Mwanamuziki wa Bongo fleva Shilole amemuoa mumewe Uchebe. Huku akidai kuwa kitendo cha Uchebe kuacha kazi yake ya ufundi gereji na kumtegemea mke wake ni sawa na kuoelewa.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Harmorapa amerusha dongo hili lililowaelekea Uchebe na Shilole:

Uchebe mtoto wa kiume umeachana Kupiga na spana umekimbilia Kuolewa Kwa nini badgirlshishi akuosheshe vyombo? Uchebe mtoto wa kiume rudi gereji ukapige spana la sivyo utapigwa sana vibao na shishi na kufulishwa mpaka chup*, sura yenyewe imekukunjika kama yangu utafikiri tumetoroka kwenye zui la manyani/ hiyo ndio faida ya wanaume marioo vibenteni demu wanahudumia masponsa mzigo tunakula sisi kimya kimya na chup* tunachafua sisi wahudumiaji alafu  vibenteni kama Uchebe kazi yao kutakatisha chup*”.

Shilole na Uchebe walifunga ndoa mwaka jana mwishoni, kabla hawajaoana Uchebe alikuwa fundi magari gereji lakini baada ya kufunga ndoa amekuwa akionekana kila mahali na Shilole akimsindikiza kwenye shoo zake zote hali iliyozua maneno maneno.

Shilole na Uchebe Wamefungukia Tetesi za Kuachana

Mume wa Mwanamuziki wa Bongo fleva Shilole, Uchebe amefunguka kuhusiana tetesi zilizoiandama ndoa yao mwanzoni mwa wiki hii ambapo ilisemekana kuwa wameachana.

Tetesi hizo ziliwashwa pale ambapo Uchebe aliweka UA jeusi kwenye ukurasa wake wa Instagram kuashiria penzi limeingia shubiri na baadae Shilole alilalamika kwenye redio kuwa Uchebe amempa kipigo cha mbwa mwizi.

Alipohojiwa mwandishi kutoka East Africa Tv, Shilole alikana tuhuma zote hizo na kusisitiza kuwa hajaachana na mume wake na wala hana mpango wa kufanya hivyo kwa muda wowote kuanzia sasa.

Lakini na Uchebe nae amesisitiza kuwa hajaachana na mke wake bali kuna watu ambao wanafiki hawataki kuwaona wakiwa wote na nia yao kubwa na kuwagombanisha ili waachane.

Uchebe alipoulizwa kuhusiana na lile Ua alilo liposti ambalo lilizua mambo yote hayo Uchebe alidai kuwa kuna mtu alimhack kwenye akaunti yake na kuuweka upuuzi ule.

Sio kweli sijaachana na mke wangu na wala hatufikirii kuachana, kuna watu wanafiki wanapenda kusikia tumeachana, kuhusu ile post kuna mtu alifanikiwa kuhack acount yangu na kupost vile lakini sijamuacha mke wangu, na wala hatuna ugomvi, na niwaambie tu kuwa hatuachani leo hata kiama”.

Wawili hao walifunga ndoa ya siri mwaka jana mwishoni lakini walikuja kuhalalisha kwa sherehe mapema mwaka huu.

“Nimepigwa Kama Mtoto na Uchebe Kisa Soudy Brown”- Shilole

Msanii wa Bongo fleva Shilole amefunguka na kuelezea kichapo kizito alichotembezewa na mumewe Uchebe ambapo amedai kisa na mkasa ni yeye kucheza mziki na Soudy Brown kwenye sherehe.

Siku ya jana kwenye kipindi cha XXL, Soudy Brown alifunguka kuwa alipokea taarifa kuwa Shilole alipokea kichapo kizito kutoka kwa mumewe Uchebe baada ya kurudi nyumbani usiku wa manane akitokea kwenye party Tabata.

Kupitia kwenye ‘You Heard’ Alitafutwa na kuulizwa kuhusu tetesi za kupokea kichapo hicho usiku usiku Shilole alikiri na kufunguka haya:

Tena Soudy niache kabisa wewe ndio umefanya mpaka mimi nagombana na Mume wangu eti Uchebe ana sema wewe bwana angu kweli? Umeshawahi kunitongoza wewe? Eti kisa siku ile kule Tabata tulivyokuwa tumekaa meza moja eti kakasirika, tulivyokuwa tunacheza mziki kwaiyo ina maana mimi nisicheze na mashabiki eti! MImi sitaki kuhusu kuongea mambo mengi nikaonekana mkorofi wa ajabu”.

 Lakini pia Shilole alikiri kupigwa kama mtoto na Uchebe kiasi kuwa walifunga mtaa hadi kupelekea Shilole kwenda kulala kwa marafiki zake:

Yaani Uchebe amenipiga kama mtoto mdogo lakini haina noma mimi mwanamke na dunia nzima inajua mimi mwanamke kuna mambo mimi nitakuja kusema mazito alafu ndo nitakapodai Talaka yangu”.

Baada ya sakata hilo Shilole alienda kwenye ukurasa wake wa Instagram na kuweka ujumbe huu:

 

 

“Sitakubali Uchebe Aoe Mke Wa Pili”- Shilole

Msanii machachari kabisa wa Bongo fleva mwanadada Shilole amefunguka na kusema katu hatokaa akubali mume wake Uchebe aje aoe mke wa pili kwani yeye hana kasoro yoyote.

Siku chache zilizopita Mkuu wa wilaya ya Pangani, Tanga Bi. Zainab aliushangaza uma wa Watanzania na hata baadhi ya nchi za jirani kwa uamuzi wake wa kumruhusu mume wake aoe mke wa pili ili wasaidiane majukumu ya kumlea.

Baada ya sakata hilo kutrend vibaya mno kwenye mitandao ya kijamii Millard Ayo Tv ilimsaka msanii Shilole ili kumuuliza nini mtazamo wake juu ya jambo hilo kwani na yeye ni mwanamke wa kiislamu aliyeolewa na mwanaume wa kiislamu je kama ataweza kukubali Uchebe alete mke wa pili.

Kwenye Interview hiyo Shilole alifunguka haya yafuatayo:

Kwanza nikuweke wazi kabisa kuwa mimi mume wangu hawezi kuoa mke wa pili hata siku moja yaani hata kama dini inaruhusu unaoa mke wa pili ili iwaje yaani , kwanini? Yaani mimi nina  mapungufu gani mpaka ukaoe mke mwingine mtu mwingine ana mapungufu huwezi kujua lakini mimi sina mapungufu yoyote na mume wangu hawezi kuniacha na kuoa mke wa pili”.

Shilole amesisitiza wanaume wanaotaka kuoa wake wengi kibao hawaijui dini na wanaoa wake wengi kwa ulafi na tamaa lakini pia amesema endapo mume wake atataka mke mwingine basi atamuacha aoe kwa amani.

Shilole: Siwezi Kumpiga Uchebe Hayo ni Mapenzi ya Kitoto

Mwanamuziki wa Bongo fleva Shilole amefunguka na kusema kwenye ndoa yake na Uchebe hawana drama zozote hasa mambo ya kumpiga makofi hawezi kwa sababu Uchebe ni gentleman.

Shilole aliwashtua watu wengi ikiwemo familia yake baada ya kufunga ndoa ya siri iliyohudhuriwa na watu wasiopungua kumi tu nyumbani kwa Babu Tale usiku usiku huku baadhi ya ndugu zake kuonyesha wazi kutofurahishwa na jambo hilo.

Lakini tangu afunge ndoa Shilole amewashangaza wengi kwa ukimya kutawala kwani Kumekuwa na drama nyingi katika mahusiano mengi ya nyuma ya Shilole kwaiyo hali ya ukimya miezi yote hii ni hali ya kushangaza kidogo.

Lakini pia habari za Shilole kuwa mbabe na kuwachapa makofi wapenzi wake sio suala geni kwa mashabiki zake na baada ya kufunga ndoa na Uchebe wengi walikuwa wanasubiria siku Uchebe apigwe makofi ya nguvu na Shilole.

Lakini kwenye Interview aliyofanya na Enews ya East Africa Tv, Shilole amekiri kuwa tabia hiyo ameiacha na ilikuwa ni utoto tu fununu kuwa Uchebe ni kiburi na mkorofi zaidi yake Shilole amelieleza hapa:

Mume wangu ni like gentleman ni mwanaume ambaye ana msimamo mtu akiwa na msimamo kama hujamjua unaweza kusema ana kiburi alafu mimi nilishamjulia mume wangu anapenda nini na yeye alishajua ninapenda nini kwaiyo mambo yanaenda vizuri. Halafu suala la kumpiga makofi kwa Uchebe siwezi pale inakuwa ngumu mwenyewe unamuona yule alikuwa anapigana ana mkanda yule lakini nikimpiga nampiga makofi ya chumbani tu ya kimahaba kaniruhusu mwenyewe lakini kupigana ngumi na mume wangu haitotokea”.

Lakini pia Shilole amesisitiza kuwa tabia yake ya kupiga wanaume ilikuwa zamani ambayo ni tabia ya kitoto aliyokuwa anafanya lakini hivi sasa amekuwa hivyo hawezi kunyanyua mkono wake na kumpiga mumewe na mumewe hawezi kumpiga.

“Natamani Shilole Awe Swala Tano Kama Uchebe”- Rey Jones

Mrembo aliyewahi kuwa Meneja wa wasanii mbali mbali wa Bongo fleva kama vile Maua Sama, Msami baby pamoja na Dito huku akifanya kazi kwa karibu pamoja na wasanii wengine kama Shilole na wasanii wengine.

Rey Jones ambaye ni maarufu kama chui jike amesema anatamani sana rafiki yake Shilole awe mtu wa swala tano kama mume wake Uchebe.

Rey Jones amesema ingawa Shilole ni muislamu mzuri tu tayari lakini anatamani awe kama uchebe ambaye hakosi swala tano kwa siku.

Msanii maarufu Bongo Shilole aliuaga ukapera mwaka jana mwishoni baada ya kufunga ndoa ya siri na mume wake wa hivi sasa Uchebe ambaye ni swala tano na ameshika sana dini.

Rey Jones alimpa ushauri huo Shilole kwenye interview aliyofanya na kituo cha Dizzim Online ambpo alifunguka yafuatayo:

Uchebe ni mtu wa dini dini sana natamani na Shilole nimuone kwenye upande huo ingawa ndio yupo huko tayari lakini ana utofauti na mumewe maana Uchebe ni wale wanaitwa swala tano ile yaani kwa siku hakosi hata moja ila shishi Kama anapiga basi itakuwa moja anagusa gusa yaani mimi nataka aanze kuzipiga zote”.

 

“Mwambieni Uchebe Mwanamke Hachungwi” Dogo Janja

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri kunako tasnia hiyo Dogo Janja amempa ushauri mwanaume mwenzie Uchebe ambaye ameingia kwenye ndoa hivi karibuni ambapo amemfungukia na kumuasa kutomchunga mkewe Shishi.

Ikiwa miezi michache tu imepita tangu ndoa iliyofunga mwaka ifungwe kati ya Irene Uwoya na Dogo Janja ndoa iliyoongelewa sana na ndoa iliyofungwa kwa usiri Mkubwa sana.

Pamoja na ndoa ilikuwa ya siri na maisha yao yamekuwa ya siri sana mbali na mitandao ya kijamii lakini juzi kwenye harusi ya Shilole na Uchebe wawili hawa wameonekana hadharani kwa mara ya kwanza.

Kwenye sherehe hiyo ya ndoa ya Uchebe na Shilole ilihudhuriwa na mastaa kibao lakini Uwoya na Dogo Janja wanaweza wakawa wana mfanano mkubwa Sana na maharusi kwani wote walipitia vikwazo mpaka kufunga ndoa lakini pia walifanya ndoa za siri siri Sana.

Kwenye sherehe hiyo Dogo Janja alipiga stori na Dizzim Online na alikuwa na ushauri mmoja tu kwa Uchebe nao ulikuwa Mwanamke hachungwi:

Kiukweli harusi yangu ilikuwa ina privacy sana ila nahisi na sisi soon tutafanya kitu kama hiki tutashiriki na ndugu na marafiki lakini kikubwa nataka niwapongeze Shilole na Uchebe na ushauri wangu endapo yanatokea mambo ya kazi asimbane ampe nafasi kamkuta na kazi zake aendelee kuheshimu kazi za mwenzake na Shilole hivyo hivyo panini ninachomwambia Uchebe mwanamke achungwi sana mwanamke hachungwi kwanza unaanzaje kumchunga mwanamke”.

 

Tazama Mastaa Kama Diamond, Jux, Vanessa na Harmonize Walivyomwaga Mapesa Kwenye Harusi Ya Shilole

Usiku wa Jana ilikuwa sherehe ya harusi (Wedding reception) ya Shilole na Uchebe ambayo ilipambwa kwa kuhudhuriwa na mastaa kibao ambao walimwaga mapesa kwa maharusi.

Ingawa noa rasmi ilifungwa ghafla na kimya kimya mwaka Jana mwishoni kwenye harusi iliyohudhuriwa na watu wasiopungua kumi huku ndufu wa Shilole wakifanya fujo kwa kukataa harusi hiyo isifungwe ingawa mwishowe ikafungwa.

Siku ya Jana kwenye sherehe iliyofanyika rasmi ilihudhuriwa na mastaa wa Bongo movie na bongo fleva kama vile Irene Uwoya na Dogo Janja, Queen Darlene, Diamond, Jacqueline Wolper, Harmonize na Sarah, Babu Tale, Madee, Mbosso, Rachel kizunguzungu na wengine wengi.

Kama kawaida mastaa hao kila mmoja alipata wasaa wa kutoa zawadi kwa maharusi na walifanya kufuru kweli.

1. Harmonize na Sarah

Harmonize na mpenzi wake walianza kwanza kuwamwagua maharusi mahela kibao yaani kuwatunza na walifuatia kwa kuwazawadia gari aina ya Noah lenye thamani ya shilingi milioni Tisa za kitanzania.

2. Vanessa Mdee

Vanessa aliwazadia maharusi Shilole na Uchebe kiasi cha pesa ambacho kitatumika kugharamia honeymoon ambayo watakwenda baada ya ndoa.

3. Juma Jux

Msanii Jux aliwapa maharusi zawadi ya kumsomesha mtoto mmoja wa Shilole shule mpaka atakapomaliza masomo yake.

4. Diamond Platnumz

Kama kawaida ya Diamond alimwambia Shilole achague zawadi yoyote atakayotaka na yeye bilashaka atagharamia kwa pesaa yake mwenyewe.

 

 

Uchebe- Mimi Ndio Nimembadilisha Shilole Hasa Kwenye Suala la Kunywa Pombe

Uchebe ambaye ni mume wa mwanamuziki wa Bongo fleva Shilole, amefunguka na kudai kuwa ndoa yake kwa Shilole imembadilisha sana hasa kwenye suala la kunywa pombe.

Shilole na Uchebe walifunga ndoa ya siri iliyowashtua watu wengi mwezi mmoja uliopita harusi iliyohudhuriwa na watu kumi tu huku ndugu wa karibu wakipinga harusi hiyo kufanyika hadi kufikua hatua ya kupelekana polisi na dada yake kwa kile kilichodaiwa kuwa alifanya fujo ili kuzuia ndoa hiyo.

Lakini Shilole alisisitiza kuwa anampenda Uchebe na kuishia kufunga naye ndoa. Mwezi mmoja baada ya kufunga ndoa na Shilole, Uchebe amefunguka kuhusu maisha ya ndoa na mkewe.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Millard Ago Tv, Uchebe alizidi kufunguka yafuatayo:.

Tarehe ishirini inshallah mwenyezi Mungu akijaalia ndio tutafanya sherehe ya harusi yetu itakayo hudhuriwa na watu wengi zaidi ambao wanatutakia Kheri kea kweli. Lakini pia nashukru tangia tumefunga ndoa mke wangu kabadilika sana hasa suala la pombe kapunguza kabisa yaani hakuwa hivi kwa jinsi nilivyomkuta na sasa tofauti kabisa hata nyie watu mnaomjua mtaona kuna utofauti fulani ila pombe taratibu taratibu ataacha kabisa maana zamani ilikuwa unakuta mtu kaamka asubuhi kashalewa analewa siku nzima Lakini tangu tumefunga ndoa pombe anakunywa kidogo jioni mpaka jioni “.

Lakini pia Uchebe aneongelea suala la akaunti feki kwenye mitandao ya kijamii ambayo inatumia jina lake na kutukana watu ovyo na kuwasihi watu waipuuzie kwani ni wazi kabisa kuwa siyo yeye.

 

Shilole Amtolea Povu Mange Baada Ya Kumponda Uchebe

Mwanamuziki wa Bongo fleva Zuwena Ashraf ‘Shilole’ amemjia juu mwanaharakati wa siasa mtandaoni Mange Kimambi baada ya kumponda mume wake Uchebe.

Shilole alifunga ndoa na Uchebe wiki chache zilizopita ambayo ilikuwa ni ndoa ya kimya kimya au ndoa ya siri ilyohudhuriwa na watu wachache lakini iliyozua gumzo kwa sababu ya ugomvi wa familia iliyozua. Lakini tangu ndoa hiyo imefungwa Shilole amekuww na kazi ya kumtetea Uchebe endapo mtu yeyote atamponda.

Siku chache zilizopita Shilole alimtetea tena Uchebe baada ya Mange Kimambi kumponda Uchebe na kudai kuwa ana jina la kienyeji na mbaya. Baada ya kuona hivyo Shilole kupitia ukurasa wake wa Instagram alimwaga povu hili dhidi ya Mange:

Mange my sis nakuheshimu sana pliiiz mume wangu Uchebe mbaya pliiz muache mimi mdogo wako ndio nimeshampenda by the way nina safari ya kuja American soon”.

Lakini baada ya povu hilo Mange alimjibu Shilole kwa kumtaka radhi kumwambia alikuwa anamtania tu aliposema mume wake Uchebe ni mbaya na ana jina la kienyeji ambapo kupitua ukurasa wake wa Instagram aliandika:

I was just joking nakutakia kila la Kheri kwenye ndoa yako ukija kwa Trump basi uje na LA ila use umenisamehe kweli nisije nikaja nikajileta mtegoni alafu nikachezea kipigo cha mwizi maana hiyo sentensi nina safari ya kuja kwa Trump Ina maana nyingi alafu Uchebe shemela nilikuwa nakutania tu mimi mwenyewe jina langu la kienyeji”.

 

 

 

Shilole: Sijaingia Kwenye Ndoa Kwa Ajili Ya Kucheza Mduara

Mwanamuziki wa Bongo fleva Zuwena Ashraf ‘Shilole’ amefunguka na kudai hajaingia kwenye ndoa kucheza mduara yupo kwenye ndoa mazima.

Shilole alizua gumzo wiki iliyopita baada ya kufunga ndoa ya siri na kimya kimya pamoja na mpenzi wake ambaye kwa sasa ni mumewe Uchebe. Ndoa hiyo imezua gumzo Sana kwani ndugu wa Shilole hawakutaka aolewe na Uchebe hadi kufikia hatua ya Shilole kumpeleka Dada yake polisi baada ya kuchukua Simu yake ilimradi tu wazuie harusi hiyo.

Pamoja na misukosuko hiyo Shilole na Uchebe walifunga ndoa ambayo ilihudhuriwa na watu kumi tu. Lakini tangu ndoa hiyo imefungwa Shilole amekuwa mtu wa kulalamika maneno ya kejeli yanayorushwa na watu dhidi ya ndoa yake na Uchebe.

Shilole amefunguka na kusema kuwa watu wasimfikirie ameamua kuingia kwenye ndoa kama maonyesho bali amedhamiria kwenda  kuwa mke mwema anayestahili na kuwa mfano wa kuigwa.

Shilole ameongeza kuwa anajua wazi kuwa kuna watu wanamhesabia siku za ndoa yake kuvunjika kama ilivyo kwa mastaa wengine, lakini kwa jinsi alivyodhamiria kutulia kwenye ndoa yake atawashangaza walimwengu.

Najua wazi watu watakuwa wananihesabia siku ndani ya ndoa yangu lakini ukweli ni kwamba nitawashangaza watu wengi na sina sababu ya kuacha kuwa mke bora na mwenye heshima kwa mume wangu kipenzi Uchebe na uhakika Mwenyezi Mungu atatupa miaka mingi”.

.

 

Shilole Awajia Juu Watu Wanaoiponda Ndoa Yake na Uchebe

Msanii wa Bongo movie Zuwena Ashraf ‘Shilole’ amewajia juu watu wote walio kifua mbele kuisema na kuiponda ndoa yake na Uchebe.

Shilole na Uchebe walifunga ndoa ya siri wiki iliyopita iliyofanyika Nyumbani kwa Meneja wa Diamond Babu Tale na kugudhuriwa na watu wasiopungua kumi.

Tangu ndoa hiyo imefungwa kuna maneno mengi yameibuka mitandaoni hasa kwa sababu kuna ripoti zilizodai kuwa familia ya Shilole haikukubaliana na ndoa hiyo hadi kufikia hatua ya ugomvi mkubwa kutokea kati ya Shilole na Dada yake hadi kufikia hatua ya kupelekana polisi.

Baada ya maneno kuzagaa mtandaoni kuhusu Ndoa hiyo Shilole ameibuka na kudai kusikitishwa na habari za majungu zinazoendelea kusambaa kumhusu mume wake Uchebe:

Kwenye mahojiano na gazeti la Mtanzania Shilole amezidi kufunguka haya:

Mfa maji haishi kutapa tapa , Ndoa yangu imewaumiza wengi wasionipenda, nimeona maneno mengi ya kashfa na majungu wakinichafua sasa mimi nasonga mbele na maisha yangu sina habari na mtu”.

Lakini pia Shilole ameeleza kuwa pamoja na kwamba watu wanamchafua lakini anaamini ndoa yake itadumu na kwa sasa familia yake ipo vizuri na ndoa yake.

Shilole- Dada Yangu Hakutaka Niolewe Sijui Alijua Mimi Bikra?

Mwanamuziki wa Bongo fleva Zuwena Ashraf maarufu kama  ‘Shilole’ amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusiana na ndoa yake iliyofungwa wiki iliyopita.

Shilole na mume wake Uchebe walifunga ndoa ya kushtukiza na ya ghafla mapema wiki iliyopita. Ndoa hiyo ilifungwa kimya kimya huku ikihudhuriwa na watu wasiopungua ishirini.

Habari zilizotapakaa mtandaoni ni kuwa ndoa hiyo ilikuwa ya siri kwa sababu ndugu wa Shilole hawakutaka aolewe na Uchebe kwa sababu zisizojulikana na hivyo kupelekea wao kuisusia ndoa hiyo lakini pia kuna habari zilizodai kuwa Ndoa hiyo ilikuwa ya ghafla kwa sababu Shilole ni mjamzito.

Kwenye mahojiano na Millard Ayo Tv Shilole aliulizwa hasa kwa nini ndoa hiyo ilikuwa ya ghafla na kwa nini ndugu hawakuhudhuria:

Ndoa ilikuwa ya kimya kimya kwa sababu walinifata Maustadhi wakaniambia ndoa haitangazwi inatakiwa kufanywa kwa siri kwa sababu husda nyingi na mambo ni mengi kwaiyo nikafunga Ndola ya kislaamu kwaiyo kilichobaki ni sherehe tu lakini kabla ya Ndoa kuna matatizo ya kifamilia tu yalitokea kuna Dada yangu hakutaka mimi niolewe lakini nilimwambia mimi nimeshafikia umri wa kuolewa sasa sijui ananionaga mimi bado bikra? Nikamwambia dada mimi nataka kuolewa nimeshapata mtu ninampenda usinichagulie mtu wa kuwa naye isitoshe bwana kanipenda nina watoto wawili tayari basi nikawa nishaamua mtu mwingine hawezi kunichagulia mwanaume”.

Shilole amesisitiza kuwa lengo lao la kufanya bonge la sherehe liko pale pale kwani tarehe ishirini na tano watafanya bonge la party watu watakula na kusaza mpaka watabeba takeaway.

Uchebe: Bora Kufa Kuliko Kumkosa Shilole

Uchebe Ashraf ambaye ni mchumba wa Mwanamuziki wa Bongo fleva, Shilole Kiuno amefunguka na kudai ni bora afe kuliko kuishi maisha yake bila kuwa na mpenzi wake Shilole.

Wiki iliyopita kuna habari zilienea na zikisindikizwa na picha iliyomuonyesha Shilole na mpenzi wake wa zamani Nuhu Mziwanda wakiwa kitandani wamelala kimahaba kabisa huku habari zikidai kuwa Shilole kamwaga mchumba ake Uchebe na kumrudia Nuh Mziwanda.

Lakini mara tu habari hizo zilivyoanza kuenea Shilole alitumia mitandao ya kijamii kukana taarifa hizo na kuweka wazi kuwa ile picha iliyokuwa inasambaa mtandaoni ilikuwa ni picha ya zamani enzi yupo na Nuh na aliyesambaza picha hizo ni Nuh katika jitihada zake za kutaka kumgombanisha na Uchebe, tuhuma ambazo Nuh alizikataa kupita kiasi.

Baada ya sakata hilo Mpenzi wa Shilole, Uchebe aliweka wazi kuwa taarifa hizo zilikuwa za kweli lakini pamoja na hayo kuliko kumuacha Shilole basi bora afe tu. Kwenye mahojiano aliyofanya na Over The Weekiend Uchebe amekiri kuwa pamoja na kuwa amegundua kuwa Shilole alirudisha penzi lake kwa bwana ake wa zamani Nuh Mziwanda lakini hayuko tayari kumuacha:

Najua Shilole amenikosea sana  lakini siko radhi kumuacha ninampenda mno na niko radhi kupoteza maisha yangu  kwa ajili yake au niuze chochote nilichonacho ilimradi tu nimridhishe kwa chochote atakacho yeye”.

 

 

Shilole Amtolea Povu Nuh Mziwanda na Kudai Anataka Kumgombanisha na Mpenzi Wake

Mwanamuziki wa Bongo fleva Shilole amemjia juu aliyekuwa mpenzi wake Nuhu Mziwanda na kudai kuwa anataka kumuharibia uhusiano wake na mpenzi wake Uchebe.

Siku ya Jana habari zilienea kuwa Shilole amerudiana na Nuhu Mziwanda na kumuacha mpenzi wake Uchebe. Siku chache zilizopita Uchebe na Shilole walitangaza kuwa wanatarajia kufunga ndoa hivi karibuni na kudai kuwa wanataka kufunga ndoa yao Ulaya. Pia Shilole alimpeleka Uchebe Nyumbani kwao Tabora, Igunga ili kumtambulisha kwa wazazi wao.

Hivyo Jana baada ya habari kusambaa kuwa Shilole kamuacha Uchebe na kurudiana na Nuh Mziwanda watu wengi walishangaa kwani ni juzi tu habari zilisambaa kuwa Nuh Mziwanda amerudiana na make wake Nawal ili wamlee mtoti wao.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Shilole amekataa vikali tetesi hizo za yeye kuachana na Uchebe na kurudiana na Nuh Mziwanda na hata kumnyooshea kidole Nuh na kudai kuwa yeye ndiye aliyesambaza habari hizo za uongo na ile picha ili mradi tu amgombanishe na mpenzi wake Uchebe.

Shilole ametoa tamko lifuatalo kutokana na tetesi hizo:

Ulizani utanikomoa kwa taarifa yako hiyo picha sio ya leo unaunga unga matukio ili kunigombanisha na mchumba wangu? Mashabiki zangu niwaambie tu hiyo staili ya nywele nadhani mnajua kuwa napenda kuitumia. Alipangalo Mwenyezi Mungu binadamu hawezi kulipangua”.

 

 

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.