Oga Obinna brings Micone on board in new jam ‘Tonight’ and it’s totally awesome (Video)

Talented comedian and singer Obinna Ike Igwee, better known as Oga Obinna, has teamed up with Micone – a group which is made up of Young Dee, Wanjo and Jey Li – on his latest jam and we really love it.

The song titled Tonight, which is all about having a good time, has been getting a lot of airplay on both TV and radio stations since it came out a few days ago.

The reason I really love this track is because it epitomizes Oga Obinna’s growth as a musician. I think naysayers have started taking him seriously because he has proven time and time again that he has it in him.

Micone
Micone

Tonight is really infectious, perhaps you’ll agree with me after listening to it. I also love the fact that it is a break from all the risque songs that have been topping charts in the last two years or so.

Notably, Micone also did a great job on this jam. Their voices and style blends so well with that of Obinna and I think they need to release more songs together.

To be honest, this is my first time listening to a track by the trio but it’s definitely not my last. I do not know his name but the guy on the last verse really sounds like Nyashinski or is it just me?

The beat and instrumentation on this jam was also impeccable. If you know Starbizz then you must be aware that he never disappoints. The video was also dope, it’s simplicity notwithstanding.

Watch Tonight below and tell us what you think.

https://www.youtube.com/watch?v=xhvAdXQD0e0

Young Dee Aibukia Kwenye Gospel.

Mwanamuziki David Genzi maarufu kama Young Dee amefunguka na kuelezea ujio wake mpya wa nyibo yenye maadhi ya injili, wimbo ambao ameimba kwa ajili ya kumshukuru mungu kwa mambo aliyomtendea mpaka hapo alipofikia.

Young Dee anasema kuwa wimbo huo ambao atamuweka msanii mwenzake Ben pol utakuwa moja ya nyimbo za kusisimua kwa sababu uatkuwa na hadithi ya maisha yake halisi na mafanikio na mapito yake kwa ujumla.

Katika ukurasa wake wa instagram, Young dee aliandika stori ya mtu aliyeumwa kwa masaa manenane tu  lakini kutumia gharama ya zaidi ya milion 14 kwa ajili ya matibabu, hata hivyo anasema kuwa pamoja na yote mtu huyo alijua kuwa kama sio mungu basi wala pesa zake zisingekuwa kitu , hivyo kwa historia hiyo fupi aliyoiweka young dee katka ukurasa wake, mwishoni alimalizia kwa kusema

hapa mimi nawaza kuandika wimbo wa kumsifu mungu muweza wa yote,,aisee #amgrateful  ,,,oii @benpol niandalie chorus baller

Wasanii wengi sasa wameanza kutumia style hii ya kuingia katika muziki wa injili ya kufaya vitu tofauti ambavyo pamoja na kwamba wanamshukuru Mungu lakini pia inaleta radha mpya kwa mashabiki.

Young Dee Yuko Tayari Kwenda Mahakamani Kisa Meneja Wake

Msanii wa hip- hop nchi Young Dee amefunguka na kusema kuwa tangu ametoa wimbo wake wa naoa anafaya kazi yeye mwenyewe  bila kuwa na uongozi wowote kwa sababu alishaachana na uongozi uliokuwa ukimuongoza hapo awali.

Young dee ambae alitangaza kuwa kwa sasa anafungua kampuni yake mwenyewe hivyo kila kitu anachofanya atakuwa akisimamia yeye mwenyewe,.

Hata hivyo alikuwa akiongea na eNEws ta EATV ,YoungDee aliulizwa kuhusu swala la meneja wake huyo anaejulikana kwa jina la Sudi kutaka kwenda kumgungulia mashtaka kwa kile kinachodaiwa kuwa amevunja mkataba bila kufuata makubaliano yao.

Baada ya kuulizwa Young Dee alisema kuwa hata yeye yuko tayari kwenda mahakamni kwa sababu ya swala hilo kwa sababu anachojua ni kwamba walishamalizana siku nyingi.

Mimi nilishafuta kila kitu kisheria na  kuhusu mkataba kama anataka  kufanya chochote afate sheria maana mimi niko tayari hata kwenda mahakamani.

Young dee anasema kuwa alikuwa na malengo aliyokuwa amejiwekea lakini ilifika muda akaona kuwa itakuwa ngumu kuyafanikisha na kwa sababu yeye ni mwanaume na ana majukumu hakuona sababu ya kukaa hapo zaidi ya kupambana.

Young Dee Anyanganywa Gari na Uongozi Wake wa Zamani

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Young Dee amefuguka na kutoa siri kuwa ile gari ya gharama aliyowahi kununuliwa na uongozi wake aliokuwa akifanyanao kazi hana tena kutokana na kwamba kwa sasa yeye na uongozi huo hawafanyi kazi pamoja hivyo  wamechukua gari lao.

Young Dee ambae kwa sasa ametangaza kuwa na uongozi wa kwake mwenyewe na kwamba kwa sasa hana uongozi amekuwa akijiongoza mwenyewe anasema kwa sasa gari hilo hana tena .

Hata hivyo , young dee anasema kuwa anaamini kuwa mambo yake yatamuendea vizuri  ana mpango wa  kununua Lambogini.

Young Dee Akana Kuwahi Kuwa Kwenye Mahusiano na Amber Lulu

Msanii wa Bongo fleva Young Dee ameibuka na kumtolea maneno shombo aliyekuwa mpenzi wake Amber Lulu na kudai hajawahi kuwa na mahusiano naye ya kimapenzi.

Wawili hao waliingia Kwenye bifu zito siku za hivi karibuni na kurushiana maneno mazito na matusi Kwenye mitandao ya kijamii.

Young Dee ameibuka na kuweka wazi kuwa hajawahi kuwa Kwenye Mahusiano na Amber Lulu yaani hajawahi kuwa girlfriend wake bali alikuwa ni mtu aliyekuwa yupo kwa ajili ya kukutana naye kimwili kila muda anaotaka.

Kwenye mahojiano na Sam Misago Tv, Young Dee amefunguka haya:

Amber hajawahi kuwa girlfriend wangu alikuwa ni bootycall wale watu unawapigia sana kumi usiku tu sasa unamuitaje Ex girlfriend wangu wakati sijawahi hata kukutana naye mchana”.

NIlikuwa nakutana na Amber kipindi kile nakunywa makonyagi tu siku hizi nimeacha pombe sina sehemu za kuktana naye maaana sio level zangu”.

Amber Lulu aliweka wazi kuwa bifu lake na Young Dee lilianza mara baada ya Amber kukataa kuwa kwenye Mahusiano naye.

Young Dee Akana Kutoka Kimapenzi na Rosa Ree.

Msanii Young Dee amefunguka na kukanusha habari zinazosambaa kuhusu mahusiano yake na mwnadada Rosa Ree,Young dee anasema kua wamekuwa na uhusiano ya kufanya kazi kwa muda sasa kutokana na nyimbo yao mpya inayokuja hivi karibuni.

Young Dee anasema kuwa wamekuwa karib sana na Rosa kutokana na kazi na wala sio kitu kingine chochote kama wao wanavyosema.

Hatujawahi kuwa na mahusiano na rosa ree, kinachotukutanisha ni muziki tu na waa sio kingine, yeye ni rapa na mimi ni rapa, kwaio tunakutana kwa sababu ya kazi za muziki tu, ni kama mimi na wewe kinachotukutanisha ni kazi na wala hatuuiz vitumbua.- Aliongea young dee akiwa katika The playlist ya Times Fm.

 

 

Ndoa ya Young Dee Yayeyuka , Kumbe Ilikuwa Kiki.

Kulikuwa na picha zilizokuwa zikisambaa katika mitandao ya kijamii zikiomyesha kuwa msanii wa bongo flev, Young Dee amefunga ndoa na mwanamke mmoja inaeemekana kuwa sio wa nchini,maswali mengi yalitanda kutokana na ukimya na usiri wa ndoa hiyo.

Hata hivyo wengi walikuja kuamini kutokana na pongezi nyingi walizokuwa wakipewa  kutoka kwa watu mbalimbali kuhusu hatua aliyoichukua ya kufunga ndoa na mwanamke huyo.

Ndoa hiyo imeota mbawa baada ya kuonekana kwa video  mpya ya Young Dee ya wimbo ulikwenda kwa jina la naoa ambapo picha hizo ni photoshots za wimbo huo.

Imekuwa ni jambo la kawaidia kwa wasanii kufanya kitu kikubwa kitakachowafanya mashabiki kukaa attention kumbe inakuwa ni kiki ya kutaka kutoa wimbo mpya, hiki alichofanya Young Dee pia walishafanya watu wengi katika game.

Young Dee Aukacha na Uongozi Wake.

msanii wa muziki wa rap  nchini young dee amefunguka na kusema kwa sasa amecahana na ule uongozi wake alikuwa chini yake hapo awali ana anategemea kuanza kufanya kazi pekee yake.Young dee anasema kuwa kwa sasa amefungua kampuni yake mwenyewe ambayo itakuwa ikisimamamia kazi zake za sanaa na kampuni hiyo itakuwa chini ya uongozi wake yeye mwenyewe.

Young dee anasema kuwa wiki ijayo atatoa wimbo wake mwenyewe , wimbo ambao ndip utakuwa wimbo wake wa kwanza kutoka katika kampuni yake ambayo ataanza kufanya nayo kazi kupitia wimbo huo unaokuja.

Wikiendi  hii pia kumekuwa na picha zilizosambaa katika mitandao ya kijamii zikimuonyesha msanii huyo akiwa na mwanamke pembeni yake huku wakiwa katika mazingira ya kufunga ndoa.

 

Picha za Young Dee akiwa na Vazi la Harusi Yaleta Utata.

Msanii wa bongo fleva nchini, David Kenzi , ameonekana katika mitandao ya kijamii akiwa na mwanamke pembeni yake huku wakiwa katika vaz la hshima , vazi la harusi huku ikisemekana wawili hao kuwa wamefunga ndoa.

Hata hivyo watu weng wamekuwa wakishangaa kutokana na kitendo hicho kufanyika kimya kimya na hakuna hata wasanii wengi waliokuwa wakijua swala hilo.Hata hivyo msanii huyo mwenyewe pia hakuweka wazi swala hilo , kitu amacho kimewaacha masgabiki katika mshangao wa kutaka kujua kama ni kiki ya muziki mpya unaokuja au ni kweli wamefunga ndoa na mrembo huyo.

Hata hivyo kumekuwa na pongezi kutoak kwa watumbalimbali ambao kwa namna moja au nyingine ni vigumu kujua kama ni kiki kutokana na nyadhifa zao katika jamii, moja ya watu hao ni maulid kitenge ambae alimpongeza sana young dee na kulalamika kwanini hakumualika katika harusi yake.

Lakini pia Jackline Wolper alimtumia Young Dee salamu za pongezi na kumtakia maisha mema katika  ndoa yake hiyo mpya.

Amber Lulu Apewa Kichapo Cha Mbwa Koko na Young Dee

Video Vixen na msanii wa Bongo fleva anayefanya vizuri na Single yake ya ‘Jini kisirani’ Lulu Euggen maarufu kama Amber Lulu amekiri kupokea kipigo cha mbwa koko kutoka kwa msanii mwenzake Young Dee.

Wiki iliyopita kipindi cha XXL cha Clouds Fm waliripoti kuwa Kwenye studio fulani hapa Mjini Amber Lulu alionekana akiwa anapigwa vibao, ngumi na hadi mateke na Young Dee.

Baada ya kipigo hiko Amber aliweka wazi kuwa sababu iliyomfanya mpaka Young Dee ampige ni baada ya kukataa kuwa naye Kimapenzi na kisha kutinga ndani ya studio hizo na mwanaume mwingine.

Kwenye mahojiano na Sam Misago Amber alikiri kupigwa na Young Dee lakini amesisitiza kuwa ulikuwa ni wivu wa kimapenzi:

Kweli Young Dee amenipiga kwa ajili ya wivu mimi ni mzuri lazima unitamani we mwenyewe umeona hili tak* usilitake Tena ? Mimi ni mzuri alafu ananitaka halafu mimi simtaki siwezi kuwa na bwana mariooo alivyoniona akaanza kuniletea Sholo nyingi alafu mimi sitaki shobo”.

Amber Lulu ameshawahi kuwa na Mahusiano na Young Dee katika siku za nyuma lakini wawili hao walishaachana ingawa Amber amekiri mara kwa mara kuwa anampenda sana.

Young Dee- Nataka Kumsaini Young Killer

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya vyema katika ulimwengu wa kuchana Young Dee aka Paka Rapa amefungukia mipango yake kumsaini msanii mwenzake Young killer Msodoki.

Kwa mara ya kwanza Young Dee aliweka wazi mipango yake ya kumsaini Young Killer kwenye label ya King cash ambayo anafanya nayo kazi kwa sasa na  kupitia ukurasa wake wa Instagram aliandika:

Hahaha siku ya kwanza ofisini wakati nataka kumsign mdogo wangu #youngkillermsodokii?? ni kweli anachana sana kijana ana kipaji!”.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, Young Dee alifunguka na kumwagia sifa kibao msanii huyo ambapo aliandika:

Young Killer ni rapa mzuri sana, namkubali sana lakini ishu za kumsaini ni mapema sana pale niliandika kama masihara lakini mimi nadhani ni jambo ambalo linawezekana kama nikiamua kwa sasabu ana kila kitu”.

Hivi sasa Young Killer Msodoki anafanya  kazi chini ya label ya Wanene Entertainment.

Agnes Masogange Alikuwa Mtu Wa Watu- Young Dee

Staa wa Bongo fleva David Genzi maarufu kama Young Dee amefunguka na kusema kuwa marehemu Agnes Gerald ‘Masogange’ alikuwa mtu wa watu sana.

Ikiwa imepita wiki moja sasa tangu Masogange aage dunia mastaa wenzake bado wanaendelea kumkumbuka na kumlilia huku ikionekana wazi kabisa kuwa itakuwa ngumu kuziba pengo lake.

Kwenye mahojiano na Championi Jumatano, Young Dee alisema kipindi cha uhai wake, Masogange alikuwa ni mtu wa watu ambaye alikuwa hapendi ugomvi na hajawahi kusikia akigombana na mtu japo yeye hajawahi kufanya naye kazi.

Japo sijawahi kufanya naye kazi, lakini alikuwa mtu wa watu kwani sijawahi kusikia akigombana na mtu yeyote, kwa sasa wasanii tuendelee kumuomba Mungu na tuachane na maovu pia tuwe wamoja kwani hujui lini utakufa“.

Masogange alifariki dunia Ijumaa iliyopita kwenye Hospitali ya Mama Ngoma iliyopo Mwenge jijini Dar es Salaam baada ya kuugua Ugonjwa wa Nimonia na upungufu wa damu mwilini na kisha kuzikwa wiki hii siku ya Jumatatu kijijini kwao Mbeya.

Nisha Akana Skendo Ya Kumtongoza Young Dee

Muigizaji wa Bongo movie anayefanya vizuri hivi sasa na ngoma yake ya Bachela amejibu tuhuma alizotupiwa kuwa ana Mahusiano ya kimapenzi na msanii wa Bongo fleva Young Dee.

Siku ya jana msanii wa Bongo fleva Amber Lulu alitoboa Siri na kusema kuwa kipindi ana Mahusiano ya kimapenzi na Young Dee, mwanadada Nisha alikuwa anamtongoza Young Dee.

Amber Lulu aliweka wazi kuwa jambo hilo lilikuwa la wazi hadi alikuwa ana ushahidi kwani alikamata meseji za wawili hao huku alikiri kuwa Nisha ni fundi wa mapenzi maana alikuwa anampa maneno matamu Young Dee.

Baada ya kutupiwa tuhuma hizo Enews ya EATV ili mtafuta Nisha kwa ajili ya kujibu tuhuma hizo na moja kwa moja alikataa na kusema kuwa hajawahi kuwa na Mahusiano na Young Dee zaidi ya urafiki:

Mimi sina Mahusiano na Young Dee ila kilichotokea ni kwamba nilikuwa nataka ni kuingia kwenye muziki hivyo  Young Dee kama msanii wa Bongo fleva alikuwa ananisaidia na lazima niwe karibu na wasanii we zangu.

Alafu mimi nimemjua Young Dee kabla hata hajawa na Mahusiano na Amber Lulu kwaiyo ni mtu wangu wa karibu na trust me angekuwa mpenzi wangu nisingeweza kuficha maana mimi nikipenda nataka watu wote wajue”.

 

Amber Lulu: Nisha Alikuwa Anatembea na Young Dee Wakati Niko Naye

Video vixen na msanii wa Bongo fleva Amber Lulu amepasua jipu na kumuanika hadharani msanii mwenzake Nisha na kudai alikuwa anaingilia penzi lake na staa wa Bongo fleva Young Dee kwa kumtongoza.

Amber Lulu aliyewahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Young Dee amekiri kuwa wakati akiwa na Mahusiano na Young Dee alikuwa mtu wa michepuko sana kiasi ya kwamba alishawahi kubamba meseji za  Young Dee na Nisha wakichat kama wapenzi.

Amber Lulu alitoa siri hiyo Kwenye mahojiano aliyofanya na Enews ya EATV ambapo amesema ushahidi kuwa wawili hao walikuwa wakichepuka anao:

Nikiona meseji zao walikuwa wanavhat vizuri tu sema kiroho safi sikumaindi sana kwa sababu hatukuwa official na mimi mwenyewe nilikuwa na mambo yangu pembeni lakini nina ushahidi kuwa Nisha Kapita kwa Young Dee.

Nakusema ukweli Nisha fundi maana ana maneno matamu nini nilisoma mpaka mwenyewe nikakubali”.

Nisha alipoulizwa habari hiyo alikana kusema meseji alizoziona Amber Lulu zilikuwa ni meseji za kikazi tu lakini hajawahi kuwa na Mahusiano ya kimapenzi na Young Dee.

Naibu Waziri Asema,Wimbo wa Bongo Bahati Mbaya Unapoteza Dhana ya Utanzania

Kwa mara ya kwanza siku ya March 14, Baraza la Sanaa nchini pamoja na Naibu Waziri walifanya presss conference na team nzima ya XXL kutoka Clouds Media Group na kufunguka mengi juu ya wasanii na nyimbo zilizofungiwa.

Naibu Waziri na BASATA wameamua kufanya press conference hiyo ili kuzungumza na kuweka wazi mambo mengi ambayo yalikuwa yakizunguka vichwani mwa watu juu ya kufungiwa kwa baadhi ya wasanii na nnyimbo zao huku baadhi ya watu wakisema kuwa BASATA na naibu waziri wamekuwa wakifanya swala hilo kwa miemuko yao wenyewe.

Akitoa ufafanuzi juu ya sababu za kufungiwa kwa wimbo wa bongo bahati mbaya, naibu waziri anasema kuwa wimbo huo umekuwa ukitoa dhana ya utanzania kwa sababu unakuwa kama unasifia nchi za nje na kutoa uhalisia wa msanii huyo ambae anaonekana kama kujuta kuwa Tanzania.

ule wimbo umekiuka misingi ya nchi, unaondoa kabisa dhana ya kujivunia utanzania.ndio maana kuna watu wanakaa wanasema no bora kuzaliwa mbwa ulaya kuliko kuzaliwa tanzania.tumeufungia kwa kufuata sheria na taratibu kabisa.

Katika mjadala huo pia walikuwepo baadhi ya wasanii kama Vannesa Mdee ambao walikuwepo kusikiliza na kujua mambo ambalimbali kuhusu haki za wasanii .

 

Young Dee na Mzazi Mwenzake Wadaiwa Kumtelekeza Mtoto Wao

Mwanamuziki wa Bongo fleva Young Dar es Salaam Young D amekumbwa na skendo mpya ambayo safari hii inamhusisha yeye na mzazi mwenzake kuhusu kumtelekeza mtoto wao anayeitwa Tamar mwenye mwaka mmoja.

Mwaka jana habari zilisambaa mtandaoni kuwa Young Dee alimkataa mtoto wake ambapo mama wa mtoto huyo alijitokeza kwenye vyombo vya habari kudai ametelekezwa yeye na mtoto na baadae Young Dee alijitokeza na kumkubali mtoto wao.

Hivi karibuni kuna habari zimekuwa zikisambaa zikidai kuwa Young Dee na mzazi mwenzake Mama Tamar wamemtelekeza mtoto wao kwa bibi yake na wote wawili hakuna anayeishi naye kwa sasa.

Mama Tamar amefunguka kupitia Lemut Online na kusema mtoto anaishi kwa bibi yake lakini yeye binafsi hajamtelekeza:

Tamar yuko Tabata ambako ndio nyumbani kwa mama yake na Young Dee analelewa na bibi yake, uamuzi huo ulichukuliwa baada ya kukaa kikao cha familia na tukaamua kuwa achukuliwe na bibi yake na mimi naenda kumuona kila wiki haipiti namuona na pia taarifa kwamba nilimtelekeza wakati mdogo ananyonya sio kweli nilimuacha akiwa na miezi kumi hivi”.

Mama Tamar amesisitiza kuwa yeye na Young Dee Hawako pamoja na pia hawezi kumlazimisha wawe pamoja kama akiamua walee mtoto pamoja basi atakubali wawe kama familia.

“Sijaona Hasara Kufungiwa Bongo Bahati Mbaya”- Young Dee

Mwanamuziki wa Bongo fleva Young Dar es salaam, Young D amefunguka na kudai hajaona kama amepata hasara yoyote kwa ngoma yake ya Bongo bahati mbaya kufungiwa.

Wiki iliyopita TCRA walitangaza rasmi kuwa wamefungia nyimbo 15 zisipigwe kwenye vyombo vya habari kwa kile walichodai kuwa BASATA wamezipitia na kuagiza zifungiwe kwa kukosa maadili ya Kitanzania.

Moja kati ya wasanii waliofungiwa ni Young Dee ambapo wimbo wake uliofungiwa unaitwa Bongo Bahati Mbaya (BBM) kwenye wimbo huo Young Dee anaimba kuwa hajapenda kuzaliwa Tanzania bora angezaliwa mbele pia wimbo huu ulikosolewa na Waziri Mwakyembe.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Millard Ayo Tv, Young Dee amefunguka na kusema Kufungiwa kwa wimbo wake wa Bongo Bahati Mbaya ilikuwa ni Ghafla na hakupewa taarifa yoyote hapo kabla wala kuonywa zaidi ya kuona kwenye mitandao ya kijamii lakini pia amekiri kuwa mpaka hivi sasa hajaona sababu ya wimbo huo kufungiwa Nay haelewi wanataka nini na nini hawataki.

Young Dee amesisitiza kuwa mpaka hivi sasa hajafikiria kwenda BASATA kuulizia kuhusu wimbo wake kufungiwa kwani mpaka hivi sasa hajaona hasara ya nyimbo hiyo kufungiwa labda atakuja kuiona mbeleni lakini hivi sasa.

Young Dee Aliniita Nikampelekee Chakula Nikamkuta Na Mwanamke- Amber lulu

Video vixen na msanii wa Bongo fleva Amber lulu amefunguka na kueleza moja kati ya matukio yaliyomuumiza kwenye uhusiano wake na msanii mwenzake Young Dee ambapo amedai ameshawahi kumfumania na mwanamke mwingine ndani.

Amber lulu amekuwa muwazi sana kila inapokuja kwenye hisia zake na Young Dee kwani ni  mara kwa mara ameweka wazi kuwa ampenda sana hata Kama amemuumiza sana kwa kuchepuka na wanawake wengine.

Amber lulu amekiri kuwa pamoja na kwamba yupo na Prezzo lakini Young dee ni moja Kati ya mwanaume ambaye alimpenda sana lakini pia amekiri kuwa tukio ambalo hatokuja kulisahau kwenye maisha yake ni siku ambayo Kwani alimfumania live.

Kwenye interview aliyofanya na East Africa redio kupitia kipindi cha Planet Bongo, Amber lulu alifunguka mengi:

Yaani hata leo hii Young Dee akimposti demu mwingine Instagram mimi naumia ingawa siwezi kumkataza lakini pia ikitokea nimeachana na Prezzo naweza nikarudiana naye ingawa ameniumiza sana kipindi cha nyuma kama nakumbuka kuna Siku alinipigia Simu akaniambia yuko studio somewhere akaniambia hebu my baby nipikie kile chakula ninachokipendaga ambacho kilikuwa ni ugali na maini basi mwenyewe nikjipikilisha pale unyamwezi pembeni nimemaliza nimebeba kile chakula nimpelekee alikuwa kwenye hoteli Fulani hivii kufika pale namkuta na msichana mwingine kusema kweli niliumia sana”.

 

Amber Lulu’s breakup with Prezzo is now inevitable

Amber Lulu’s break up with Prezzo is no longer a matter of if but when. The Tanzanian video vixen is also anticipating the split with the Kenyan rapper.

Prezzo is a seasoned heartbreaker judging from his past relationships. Any lady who dates him certainly knows she will be dumped at one point or another.

Prezzo hooked up with Amber Lulu sometimes in September 2017. The controversial rapper started his relationship with Lulu while at the same time he was said to be dating Noti Flow.

Amber Lulu and Prezzo

Lulu’s game plan

Amber Lulu is anticipating a breakup with Prezzo and she is already taking steps to cushion herself. The video vixen says she will hook up with her ex boyfriend Young Dee just in case things fail to work with Prezzo.

“Ndiyo siku nikiachana na Prezzo lazima nitarudiana na Young Dee,” wrote Amber Lulu.

Amber Lulu and Young Dee

Amber Lulu used to date Tanzanian rapper Young Dee before Prezzo came into the picture. Lulu and Young Dee broke up in September 2017 before she hooked up with Prezzo.

 

 

Yound Dee:Amber Lulu Hana Hadhi Ya Kutembea Na Mimi

Wasanii Amber Lulu na David Genzi maarufu kama Young Dee wamekuwa katika mgogoro wa muda mrefu huku ikisemekana kuwa wawili hao inawezekana bado wanapendana au wamekuwa wakioneana wivu tena hasa baada ya kuwa wapenzi kwa muda mrefu na kisha kuachana na wote kuendelea na maisha yao ya kawaida. Lakini swala linakuja palepale  ni aidha wawili hao watakuwa bado wanapendana lakini hakuna anaeweza kumuanza mwenzake ndio maana inakuwa ni vita kila siku katika mitandao ya kijamii.

Hivi karibuni Amber Lulu aliwaonya mashabiki katika mitandao kuacha  kumfananisha Young Dee ambae alikuwa mpenzi wake wa zamani na mpenzi wake wa sasa ambae ni Prezzo mwanamuziki kutoka Kenya na kusema kuwa Young Dee hana kiwango chochote cha kulinganishwa na Prezzo katika mambo yote.

Msanii Young Dee ameamua kumjibu na kuwajibu waandishi kuwa amekuwa anachoshwa sana na tabia ya waandishi wa habari kuwa na maswali yanayomuhusu Amber Lulu kwake, na amesema kuwa  Amber Lulu hana hadhi ya kuwa na yeye ana swala la kuwa wanamuuliza maswali ya Amber Lulu mara kwa mara yamekuwa yakisumbua uhusiano wake mpya.

Nimechoka kuulizwa maswali kuhusu mimi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Amber Lulu,hana hadhi ya kuwa na mimi na ninaomba nisiulizwe kwa sababu mnaniharibia sana mahusiano mapya na mpenzi wangu wa sasa.

Amber lulu ambae amejiingiza katika mahusiano na prezzo maekuwa akichukizwa na baadhi ya watu katika mitandao ambao wamekuwa wakimfananisha msanii huyona mpenzi wake huyo mpya .

Amber Lulu: Stop comparing my love Prezzo with Young Dee

Tanzanian socialite has warned people against making comparisons between Prezzo and Young Dee. Amber Lulu says the comparison is a mockery to Prezzo.

For starters, Prezzo is dating Amber Lulu while at the same time he is said to be romantically involved with Kenyan rapper Noti Flow.

Amber Lulu used to date Tanzanian rapper Young Dee before Prezzo came into the picture. Lulu and Young Dee broke up in September this year.

Amber Lulu and Young Dee

It’s an insult to Prezzo

Amber Lulu says comparing her ‘husband’ Prezzo and her ex Young Dee is an insult to her sweetheart. The video vixen says Young Dee and Prezzo should not be compared because they are two different people in different levels.

Amber Lulu and Prezzo

“Usimfananishe mume wangu na watu wengine kwa sababu unakuwa unamkosea adabu, kwa hiyo Young Dee ni Prezzo usiwakee kabisa pamoja kwa sababu ni watu wawili ambao hawezi kuendana hata kidogo,” said Amber Lulu.

 

 

Young Dee- Nimeiga Wimbo Wa Mr. Nice Kwa Heshima

Msanii wa Bongo fleva Young Dee ameibuka na kudai kuwa kitendo cha yeye kuiga wimbo msanii mkongwe wa Bongo fleva Lucas Mkenda maarufu kama Mr.Nice Ilikuwa ni kwa sababu ya heshima aliyonayo kwenye mziki wake na wala sio wizi.

Baada ya Young Dee kutoa wimbo wake mpya unaoenda kwa jina la Kiben10 ambao ndani yake ameweka kionjo cha wimbo wa Mr.Nice bila ruhusa, ndipo pale jasho lilimtoka kwani Mr. Nice alipousikia wimbo huo alimjia juu Young Dee kwenye mitandao ya kijamii na kudiriki kumuita mwizi wa kazi zake na kutishia kumchukulia hatua za kisheria.

Young Dee amemjibu Mr. Nice na amejitetea kuwa yeye kuimba wimbo wake haikuwa kwa nia mbaya bali alifnya vile kwa sababu alikuwa shabiki Mkubwa wa wimbo wa Mr. Nice.

Kwenye mahojiano aliyofanya na East Africa Tv kupitua kipindi Chao cha Enews Young Dee alifunguka:

Naomba niseme kuwa sikuwa na nia mbaya bali nia yangu ilikuwa ni kumpa heshima maana hawa ni kaka yangu aliyenitangulia katika gemu alafu ana mchango mkubwa kwenye mziki wetu wa Bongo fleva kwaiyo lengi langi lilikuwq ni kumuonyesha heshima aliyoiweka kwenye mziki wetu wa Bongo fleva kiasi ya kwamba miaka mingi baada ya wimbo huo kuhit lakini bado Una ladha ya kipekee kabisa”.

Mr. Nice Amjia Juu Young Dee Baada ya Kuimuibia Wimbo Wake Wa ‘King’asti’

Msanii mkongwe wa Bongo fleva aliyetamba kwa staili yake ya ‘Takeu style’ ameibuka na kumtolea povu zito msanii mwenzake Young Dee baada ya kusample wimbo wake wa ‘King’asti’.

Mr. Nice amezidi kukaa kwenye headlines kwa wiki hii kuanzia kurudi upya kwa bifu lake na aliyekuwa hasimu wake mkubwa Dudubaya mpaka kuingia kwenye vita ya maneno na Paka rapa Young Dee baada ya Young Dee ku-sample wimbo wake ulio-hit miaka ya nyuma ulioenda kwa jina la ‘king’asti’.

Young Dee ametoa wimbo wake mpya unaoitwa ‘kiben-10’ na amemshirikisha Dayna Nyange ambapo kwenye wimbo huo kuna kionjo na mashairi machache kutoka kwenye wimbo huo wa Mr. Nice ambao amechukua bila ruhusa ya mwenye wimbo huo.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Mr. Nice amemtolea Young Dee povu zito:

Nadhani ni wizi na ni aibu kuchukua kazi ya mtu na kuirudia tena kwa manufaa yako binafsi bila hata kuomba ridhaa yoyote kutoka kwa mwenye kazi yake, ni wizi ambao serikali na jamii nzima imekuwa ikipiga vita every day na ni kosa kubwa kabisa kisheria…..Huyo msanii anayeitwa sijui Young Dee mwelezeni asije kutafuta huruma yangu hapo baadae kwa maana haitakuwepo”.

 

Gigy Money Amshauri Young Dee Kubaki Na Amber Lulu

Msanii wa kike ambae kwa sasa anatamba na kibao chake kipya cha ‘nampa papa’, Gift Stanford maarufu kama Gigy Money, mwisho ni mwa wiki iliyopita alijikuta akitoa povu zito kwa msanii mwenzie wa kiume anaejulikana kama Young dee kutokana na muenendo mbaya alionao katika mahusiano.kwa mujibu wa Gigy Money, Young Dee ni shemeji yake kutoka kwa Amber Lulu ambae pia ni msanii wa Bongo fleva lakini pia aliyekuwa na anaendelea kuwa moja ya ma-video queen wanaofanya   vizuri katika videos za wasanii mbalimbali wakubwa  nchini.

Gigy Money  alisikika akisema kuwa katika wanawake wote aliokuwa nao Young Dee ni msichana mmoja tu Amber Lulu ndie mwenye mapenzi ya kweli kwake sio hao wengine wanamchukulia kama kikatuni .Maneno hayo yalianza baada ya wasnii hao wote watuatu walipokutana nje ya jengo la EATV, wakitoka katika mahojiano ya kipindi cha Friday Nite Live ambapo , Amber Lulu aliona baadhi ya alama za kucha na vidole katika shigo ya Young Dee na kuanza kumshangaa na kumtuhumu kuwa itakuwa alikuwa katika ugomvi na mwanamke mwingine,

Kutokana na tukio ilo Gigy Money alipewa nafasi ya kuongea na kusema kuwa “Young Dee apunguze mitandao ya wanawake, maana inamchanganya wakati ukimwangalia umri wake ni mdogo sana,atulie tu na Amber Lulu maana katika wanawake wake wote mia  Amber Lulu ana mapenzi ya kweli kwake,wengine wote wanafata jina tu ilo la bongo bahati mbaya ,wanamuona kama kinyani wanamtakataka” alifunguka  Gigy Money ambae aliweka wazi pia kuwa kumbe wawili hao walikuwa katika mahusiano ya kimapenzi.

Amber Lulu na Young Dee walikuwa katika mahusiano ya kimapenzi kwa muda kidogo uliopoita huku wakikataa kuwa katika mahusiano hayo, ilifikia hatua mpaka Amber Lulu aliamua kuchora tattooo ya jina la  Young Dee mkononi lakini walipogombana Amber Lulu aliamua kufuta tattoo iyo, hivi karibuni pia kuna picha zilisambaa za amber lulu na Young Dee , picha ambazo ziliwafanya wawili hao kupelekana polisi .

Bifu La Young Dee Na Dogo Janja,Chanzo ni Muna

Kwa muda sasa kumekuwa na chokochoko kati ya wasanii wawili wa muziki wa Bongo Fleva yaani Young Dee na Dogo Janja ambapo katika kufatilia sababu inaonekana ni yale maneno ambayo Young Dee aliyaongea yaliyokuwa yanamuhusu Dogo Janja na Young Killer Msodoki kuwa yeye (Young Dee) ni mkubwa kimuziki hivyo hataki kabisa kusikia watu wakimfanisha na wasanii hao wawili ambao kwake anawaona bado wachanga hawajamfikia kiwango chake. Young Killer alinyamzaza na hajaonekana kuongea chochote kuhusu ili lakini Dogo Janja hakuweza kuvumilia na kuamua kujibu maneno ya Young Dee na kumwambia kuwa hata yeye hawezi kulinganishawa  msanii kama yeye ambae anavuta unga, kabisa hawezi kuongea na ‘mteja’.

Bifu limeendelea na kuwa kubwa mpaka baadhi ya wasanii waliamua kuingia nakuwashauri kuyamaliza mambo hayo, kati ya wasanii hao ni pamoja na Nikki wa Pili.Lakini jana msanii wa muziki wa singeli Sholo Mwamba nae aliamua kufunguka kuhusu bifu ilo huku akiamua kumwaga ubuyu hadharani kuhusu sababu ya wasanii hao kugombana ni mwanamke.

Akiongea na eNews ,Sholo Mwamba ambae alikuwa chini ya menejiment ya Muna Entertainment alifunguka na kusema kuwa kwa sasa yeye na Muna hawafanyi kazi pamoja na sababu sio kwamba yeye alichokwa na Muna bali yeye alimchoka Muna, alipoulizwa sababau ya yeye kumchoka meneja wake alijibu “Kitu ambacho mimi kiliniuzi na nilikichoka kwa Muda ni kitendo cha sisi wanaume kufanya kazi na kutafuta ela  afu tukienda pale  kwa muna tunakuta madogo wengune wamekaa kwenye makochi wamejiachia, sisi wahuni tunaenda kuimba visingeli vijijini tunaleta mpunga kwa bosi alafu bosi anatumia na wajinga”aliongea Sholo Mwamba

hapo wote vingasti tu, tunawakuta pale kwa bimkubwa wanajiachia achia tu, Dogo Janja, Young Dee, wanagombana wanagombania demu, ila sisi tunakuja kwa bosi tunawakuta hayo mambo ya kugombana ni miyeyusho tu” aliongezea Sholo Mwamba

Hata hivyo Sholo pia anaonekana ana wivu wa mapenzi kwa Muna Love na kufikia hatua ya kusema ” namshangaa bosi si angenipa hata mimi, akinipa sisemi, tunakula kimyakimya”

Dogo Janja Amwita Young Dee Teja

Ikiwa ni siku kadha zimepita na ugomvi kati ya wasanii wa Bongo Fleva Young Dee na Dogo Janja unazidi kuwa mzito huku kila mmoja akitaika kuwa juu zaidi ya mwenzie, ugomvi huu ambao ulianza kwa Young Dee kukataa kabisa kufananisha na wasanii wengine ambao hawapo kabisa katika level zake, kwa mujibu wa Young Dee anasema wasanii kama Dogo Janja  wa Arusha na Young Killer wa Mwanza ni wadodgo sana katika swala la muziki na yeye ndie kaka yao hivyo kwanza wanapaswa kumheshimu lakini pia vyombo vya habari havipaswi kumfananisha wa wasanii hao.

Hata hivyo Dogo Janja ameamua kumjibu rapper huyo  na kusema kuwa yeye hawezi kubishana na Young Dee kwa sababu Young Dee ni teja.Dogo Janja anasema kuwa ni sawa kabisa kwa Young Dee kukataa kufananishwa na yeye kwa sababau hata yeye pia hayuko tayari kabisa kufananishwa na Young Dee kwa sababu rapper huyo anatumia madawa ya kulevya na muda mwingi anaongea akiwa tayari ameshatumia madawa  , na kutokana na matumizi ya madawa hayo ndio maana anaongea mambo ya ajabu ajabu”Young Dee ni mteja,na hawezi kufanana na mim.Mtu mwenye akili timamu hawezi kutukana kwenye Media matusi makubwa kama alivyofanya Young Dee, akiacha unga ndo ninaweza kuzungumza,siwezi jua kama saivi ntakuwa nazungumza  au nabishana  na yeye au na mteja.Mtu mwenye akili timamau unamsamehe  tu maana inawezekana kashavuta mambo yake na yupo kwenye dunia yake nyingine” alifunguka Dogo Janja

Hata hivyo Dogo Janja anasema kuwa yeye hakatai kufananishwa na mtu lakini anaangalia mtu wa kufananishwa nae”mimi pia sipendi kufananishwa  japo pia sikatai kufananishwa, Young Killer nilishawahi kuwa Role model wake kwaiyo kufananishwa nae si kitu kibaya lakini kufananishwa na mla unga ni kukosea.. Young Dee akiacha kula unga tutakaa mezani tuzungumze  lakini kfananishwa nae kwa sasa hivi sitaki”

Baada ya Dogo Janja kuongea hivyo Young Dee  alimjibu tena msanii huyo na kusema kuwa wao kama wasanii wadogo wanatakiwa wamfate yeye kaka yao ili wajue sababu ya yeye  kusema hataki mkufananishwa nao,hata hivo Young Dee anasisitiza kuwa bila yeye wasanii wengine wadogo wasingekuwa hapo kimziki maana wote wamefunguliwa njia na yeye.

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.