Ray vanny, Vannesa Watusua Na Dili la Essence Marekani

Wasanii wawili  kutoka katika muziki wa Bongo Fleva waliotajwa  kutumbuiza kwenye tamasha kubwa la EssenceFestival nchini Marekani, wasanii hao ni Vanessa Mdee na Rayvanny.Tamasha hilo ambalo kila mwaka hufanyika huko New Orleans, Louisiana mwaka huu limepangwa
kufanyika kuanzia July 4 hadi 7 mwaka huu.

Wasanii wengine wa Afrika waliotajwa kutumbuiza ni pamoja na Sauti Sol kutokea Kenya, Davido
kutokea Nigeria pamoja na Nasty C wa Afrika Kusini.Wasanii wengine nje ya Afrika ni pamoja na Miss Elliot, Mary J.Blidge, Nas, H.E.R, Teyana
Taylor, Pharrell Williams na wengine.

Tamasha ya Essence fest lilianzishwa na jarida la Essence mwaka 1995 likiwa na lengo la kuwapa
nguvu wanawake wenye asili ya rangi nyeusi na kusherekea tamaduni na muziki wa watu wenye
asili ya Afrika nchini Marekani.

Shaddy Boo Amkubali Zaidi Zari Kuliko Hamisa

Mwanadada maarufu katika mitandao ya kijamii Shaddy boo amfunguka na kujibu swali aliloulizwa na moja ya mashabiki zake kuhusu ni nani anaweza kumchagua zaidi kati ya hamisa na zari kama ikitokea akaambiwa achague mmpj wapo.

Mwanadada huyo ambae aliwahi kum-attack Zari alipokuwa na mahusiano na Diamond na hata baadhi ya picha zake kusambaa katika mitandao akiwa na msanii huyo hivyo kuhisiwa kuwa mwanadada huyo anaweza kuwa na mahusiano na Diamond Platinumz.

Alipokuwa akijibu maswali hayo katika uwanja wa snapchat, Shaddy boo anasema zari ni mwanamke bora na mama bora zaidi kuliko Hamisa hivyo siku zote chaguo lake litakuwa kwa zari na sio Hamisa.

Mashabiki Wamtolea Povu Aliemshauri Diamond Kuhama Nchi.

Moja ya mashabiki wa Diamond alimshauri Diamond platinumz kuhama nchi mara baada ya taarifa kusambaa kuwa msanii huyo amefungiwa kwa muda usiojulikana kisa kuimba wimbo   ambao  ulisgakatazwa kutokana na sababu za kimaadili.

hata hivyo ,shabiki huyo alisema kuwa diamond amekuwa  moja ya wasanii wanaojitolea sana katika kufanya kila kitu kwa jamii lakini serikali haioni mchango wake hivyo, ni bora kuhama nchini na kuhamia kenya au uganda mabako atakuwa huru kufanya kila kitu anachoweza kufanya.

Alichoandika shabiki kumshauri diamond platinumz.

Baada ya maoni hayo , watu wengine walikuja juu na kusema haiwezekanai kwa sababu yeye amekuwa akisaidia jamii basi avunje sheria za nchi na huku watu wakimuangalia hivyo wamuogope kama mungu mtu.

 

Watanzania Kuwania Tuzo za Soundy City Nigeria, Diamond aongoza.

Tuzo za Soundy city awards nchini nigria imetoa majina lukuki ya wasanii watakao wania tuzo hioz kwa mwaka 2019, wakati huo wakitoa idad iyo ya wasanii jambo la kufurahisha ni kwamba kwa Tanzania muziki unazidi kukua na wasanii wanazidi kujulikana nje ya nchi.

Diamond Platnumz atawala nominations nchini Nigeria katika tuzo za Sound City Awards 2019 kwa jina lake kuonekana Mara 11 kwenye vipengele tofauti akiwa single na vya kushirikishwa. Diamond ametajwa kuwania tuzo ya msanii bora wa kiume wa mwaka, digital artist wa mwaka, msanii bora wa pop, msanii bora wa mwaka, etc. Maua Sama anawania msanii bora wa kike wa mwaka Africa akichuana na kina Tiwa Savage na Yemi Alade, .

Vanessa Mdee anawania digital artist of the year pamoja na kina Davido, Diamond, Wizikid, Yemi Alade, Kwangaru ya Harmonize na African Beauty wa Diamond wanawania wimbo bora wa mwaka. Harmonize na boss wake Diamond wote wanachuana kutwaa msanii bora wa kiume Africa. Mboso anawania msanii bora mpya Africa

Kenya imepata nominations kupitia Sauti Sol, Kalgraph Jones , ambapo kwa upande wa mwaka 2018, khaligraphs jones amekuwa moja ya wasanii waliongoza sana Kenya kushinda tuzo mbalimbali ndani na nje ya kenya.

Tuzo hizo zinatarajiwa kutolewa mwakani huku tegemea kkubwa la wasanii hawa ni kura kutoka kwa mashabiki wenyewe.

Wasanii Waguswa na Kijana Aliyeibuliwa na Ugonjwa wa Kutisha

kuna baadhi ya picha na video zimekuwa zikisambaa katika mitandao ya kijamii zikimuonyesha mtoto wa kiume aliyekonda sana na kudhohofika kiasi kwamba anahitaji msaada wa kila kitu,

Mtoto huyo aliibuliwa na mwanadada floraj lauwo kutoka mwanza, huku akiomba watanzania wamsaidie ili aweze kupata pesa kwa ajili a matibabu yake nje ya nchi  na kuisaidia familia yake kwa ajili ya kupata  chakula bora na malezi mazuri kwa kipindi hiki anachoumwa.

Watu wengi wameguswa lakini  jamii inazidi kuwashukuru wasanii ambao wanamajina katika jamii kwa kuliona hili na kulitolea msaada kwa sababu hii imefanya watu wengine pia waguswe kupita wao.

Wasanii kama Wema Sepetu, Zari the Bossy, Riyama Ally, mwanadada Zamaradi Mketema, kaka Millard Ayo,Dogo janja na wengine wengi ambao waliweza hata kuhamasisha kupitia kurasa zao .

Naibu Waziri Awaonya Wanaopiga Picha za Uchi.

Naibu  Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Japhet Hasunga  amewashauri wasanii wanaopiga picha za utupu waache kupiga picha hizo badala yake watembelee Hifadhi za Taifa ili wakapige picha na simba, twiga chui pamoja na sokwe kwa ili  waweze kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini.

Pia amewataka wasanii wenye nia ya kutaka kutengeneza filamu  katika Hifadhi ya Taifa wawasaliane na Uongozi wa Hifadhi za Taifa au wawasiliane na  yeye mwenyewe moja kwa moja.

Ametoa rai hiyo wakati  akifunga tamasha  la utamaduni wa mtanzania inayowakilishwa na jamii za mkoa wa Lindi lililofanyika kwa muda wa siku nne katika  kijiji cha Makumbusho jijini Dar es salaam

Aidha, Ameiasa jamii iitumie mitandao ya kijamii kujipatia elimu badala ya kusambaza picha ambazo ni kinyume cha maadili ya Mtanzania.

Ameongeza kuwa Jamii iwakemee wasanii wenye tabia hiyo badala ya kusubilia Serikali ndo ichukue hatua.

Polepole Akutana na Wasanii Kuzungumzia Changamoto Zao.

katibu mwenezi wa chama  tawala nchini, Mh Humphrey Polepole amekutana na wasanii wa mzuki na miguzo nchini ikiwa ni kama mwakilishi wa serikali na kuongea nao mawili matatu yanayosumbua sanii nchini.

Wasanii wengi walijitokeza ikiwa ni kama wito wa serikali wa kutaka kukutana nao ili waweze kuzungumzia maswla yanayowahusu na kuona ni namna gani wanaweza kuayatatua ili kufanya sanaa ya tanzania iweze kuendelea mbele zaidi.

Ikumbukwe kuwa miezi michache nyuma  katibu mkuu wa chama icho alitangaza kuwa CCM haitawatumia wasanii tena katika shughuli za kichama hasa kampeni kwa uchaguzi utakao kuja kama ilivyokuwa kwa ule uliopita, jambo ambalo liliwafanya wasanii wengi kulalamika na hata kutuma salamu kwa Mh Rais kuangalia swala ilo.

Hata hivyo baada ya kikao icho kuisha hakuna kilichosemwa kuwa kimejadiliwa cha zaidi ya changamoto zinazokabili sanaa ya Tanzania , hivyo bado hakuna mrejesho wa swala hilo mpaka sasa.

Watanzania Walioshinda Tuzo za Africa Entertainment Awards USA 2018

Rayvanny amefanikiwa kuchykuwa tuzo katika kipengele cha Best vocalist of the year 2018

Diamond amefanikiwa kuchukua tuzo mbili ambazo ni  Best collaboration of the year katika wimbo wa  African beauty aliofanya na Omarion na nyingine ni msanii bora wa mwaka wa kiume.

Nandy pia amepata tuzo katika kipengele cha Best female artist of the year 2018

Dj wa msanii maarufu Diamond, anaejulkana kama Rommy Jones amepata Tuzo ya best Dj of the year

 

Miss Ubungo Awakumbuka Wanafunzi wa Umoja.

Aliyewahi kuwa Miss Ubungo mwaka 2014-2016 Diana Kato amewakumbuka wanafunzi wa shule ya umoja na kusherekea siku ya kunawa mikono Duniani pamoja shuleni hapo ikiwa kama moja ya njia ya kukumbuka na kuhamasisha mambo muhimu katika jamii kama ilivyo kwa walimbwende wa tanzania wanavyottumwa kufanya mambo yanayonufaisha jamii.

Diana Kato alifika shuleni hapo kwa lengo la kukutana na wanafaunzi wa shule hiyo na kuwaelismisha juu ya umuhimu wa siku hiyo duniani na kwao pia huko akishirikiana nao katika kufanya jambo hilo.

Diana Kato ambae tangu hapo nyuma amekuwa moja ya mabalozi wanaoshughulikia sana swala la upatikanaji wa maji mashuleni  ilikuwasaidia kujikinga na magonjwa yatokanayo na uchafu.

Hata hivo Diana amesikiliza changamoto mbalimbali zinazopatikana katka shule hiyo na kuahidi kushughulikia anayoweza kwa nafasi yake na kufikisha mengine sehemu zinazohusika.

Wanafunzi wa umoja wakiwa wameshika mabongo ya kuhasisha siku ya kunawa mikono Duniani.

Mikono ya wanafunziwa shue hiyo wakiwa wanafanya zoezi la kunawa mikono na sabuni.

Jinsi Watu Mbalimbali Walivyoguswa na Kupotea kwa Mo Dewji

Tangu kumesambaa na kuthibitika kwa taaarifa kuwa moja ya matajiri wakubwa duniani kutekwa nyara na watu wasiojulikana wasanii mbalimbali wameonekana kuguswa na habari hizo hivyo  kuamua kuonyesha hisia zako katika kurasa zao za instagram.

baadhi ya wasanii hao ni pamoja na

Flaviana Matata.

Mboni.

 Diamond platinumz.

Mwana Fa

Madam Ritha Paulsen

Wasanii Tanzania Watoka Kapa Tuzo za AFRIMMA.

Usiku wa kuamkia october 8 ilikuwa moja ya siku muhimu kutokana na ugawji wa tuzo za AFRIMMA nchi Marekani ambapo kwa upande wa waliokuwa wakiwania tuzo pia wasanii kutoka Tanzania walikuwepo baadhi yao.

Hata hivyo mwaka huu umekuwa tofauti kwa wasanii wa Tanzania kutokana na kwamba wale wote waliowekwa katika kategoria mbalimbali hawakuweza kufanikiwa kuchukua tuzo hizo huku wasanii kutoka Uganda na Kenya wakiinuka kidedea katika tuzo hizo.

Wasanii kama Nandy, Alikiba, Ommy Dimpoz, Vannesa, Diamond Platnumz na pia Navy Kenzo walikuwa aktika kategorai mbalimbali,hata hivyo wasanii kutoka nchi za jirani kama Khaligarph Jones,  na Eddy Kenzo waliweza kuibuka kidedea.

Wafahamu wasanii Wanaotembea na alama za maumivu ya Wapenzi Wao.

Wasanii wengi wamekuwa wakijisahau kuwa kukutana na mtu kwa mara moja na kujiingiza nae kwenye mapezi kuna weza kuwa na mwisho mbaya ndani yake, hii inawafanya wanajikuta wanaingia katika mapenzi mazito na kufikia kuchora tatoo ambazo mwisho wa siku zinakuwa kama kovu katika miili yao juu ya watu ambao inawezekana wakati wa kuachana waliachana kwa chuki na maumivu sana.

wasanii wengi wamekuwa wakichora tatoo  na wanaendelea kuzichora wengi bla kujifunza kutoka kwa wenzao. hawa ni baadhi ambao mpaka sasa wanatembea na maumivi ya makovu hayo.

CASTO NA TUNDA.

Hawa walipoanza casto alikuwa akijiamini sana mpaka kufikia hatua ya kuchora tatoo , pamoja na kelel za watu kumshauri casto lakini hakutaka kumsikiliza mtu, mapenzi yao yanaonekana kufika mwisho inagwa wamekuwa wagumu kuthibitisha hilo.

BROWN  NA WOLPER.

Brown aliamua kuchora tattoo ya wolper kifuani kwa kuamini kuwa hiyo ni alama tosha ya mapenzi yao lakini kwa sasa imebaki kama alama na kovu kwa mwanaume huyo.

NUH MZIWANDA NA SHILOLEH.

hii ni moja ya couple iliyovuma sana kiasi kwamba kila mmoja aliamua kuchora tatoo katika mwili wake yenye jina la mwenzake, lakini baada ya kuachana , shiloleh alifuta na kuchora ua ambalo halikuwa na msingi sana zaidi ya kuficha makovu ana maumivu ya mapenzi ya nyuma.

lakini pia wapo wasanii waliaomaua kuchora tatoo kamaishara ya kuwaonyesha wale watu wa muhimu katika maisha yao na nini wanamaanisha katika maisha yao kwa mfano.

AUNTY EZEKIEL NA TATOO YA MTOTO WAKE.

Aunty aliamua kuweka historia ya mtoto wake wa kike katika bega lake kwa kuliandika jina la mtoto wake kama ishara ya mapenzi yak kwake, ni mtoto wake na siku zote hatakuwa katika maisha yake.

IRENE UWOYA NA TATTOO YA AGNESS.

Baada ya kifo cha rafiki yake mpenzi aliamua kuandika tatoo hii kuonyesha  kuendelea kumkumbuka na kumpenda siku zote katika maisha yake.

 

 

 

 

Mashabiki Waombwa Kumsaidia Hawa wa Nitarejea

Kama mwaka sasa umepita tangu mwanadada hawa alipowahi kutolewa katika vyombo vya habari kuwa alikuwa amekuwa kama teja kutokana na matumizi ya pombe za kienyeji zilizompelekea pia kuacha muziki na kujikuta akibaki nyumbani tu,

Baada ya hapo walimsaidia dada huyo na kwenda sober ambapo alipatiwa matibabu na kuanza kurudi katika hali yake ya kawaida lakini bado alikuwa akihitaji msaada wa hapa na pale ili kurudi kimuziki.

Sasa mapya ayameibuka kuhusu hali ya mwanadada huyu huku akionekana kuendelea kudhoofka kabisa  na hii yote ni kutokana na ukweli kuwa mwanadada huyo kwa sasa ni mgonjwa sana na amekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa ini unaoendelea kutafuna sana afya yake.

Soudy Brown wa kipindi cha shilawadu kutoa Clouds Media amethibitisha ilo baada ya kwenda  kumtembea mwanadada huyo huku akionekana kudhoofika sana na hali yake aliyonayo kwa sasa.

Mwanadada huyo anaomba msaada kwa watu mbalimbali kwa chochcote kwa sababu ya matibabu na pia hata familia yao pia haina uwezo kwa kutoa huduma ya kila kitu.

Davista Afurahishwa na Ukaribu wa Jux na Diamond.

Msanii mpya katika game la muziki ambae ameachia ngoma inayokwenda kwa jina la super woman amefunguka na kusema kuwa amekuwa akifurahishwa sana na ukaribu wa Diamond na Jux kwa sasa na ana imani wanaweza kufanya kazi pamoja.

Davista anasema kuwa mara nyingi katika mitandao ya kijamii wamekuwa wakiwashindanisha wasanii hawa katika mavazi na kuimba nyingi zenye kuibua hisia kitu ambacho kiliwafanya wasanii hawa kuonekana kama wana bifu lakini kumbe sio.

Akiongea na meda, msanii huyo anaefananshwa sana na tkno kutoka Nigeria anasema pia anapongeza sana swala la WCB kuleta jibebe challenge ambayo anaona kuwa itasaidia kuwafichua vijana wenye vipaji waliopo mtaani lakini pia anaomba kusapotiwa katika kazi zake za muziki.

Wasanii wa Bongo Waaswa Kuacha Unafiki na Uoga.

Moja ya wanasiasa nchini, Peter msigwa amewaomba wasanii wa Tanzania kuacha kuwa wanafiki na waoga katika kutetea mambo ambayo yanakuwa na mnufaa kwa jamii hasa pale wanapoamua kufanya kwa ajili ya jamii.

Akiandika katika ukurasa wake, Peter msigwa anasema kuwa  ameona katika mitandao ya kijamii wasanii baadhi yao wakiungana na wasanii wa Uganda katika kampeni yao ya kuishinikiza serikali kumuachia mwanasiasa aliwahi kuwa msanii nchini humu Bob wine.

nimeona baadhi ya wasanii Tanzania wanaandika FREE BOBI WINE , jambo ambalo ni zuri lakini alipoonewa Sugu,Lissu ,Mawazzo ,Saanane,Azori  hapa Tanzania wamekaa kimya , Injustice  to one is injustice to all” Tuache unafiki  na UWOGA , Museveni Free BOBI wine, Magufuli FREE DEMEOCRACY.

 

Ray C, Koletha Mstari wa Mbele Kumshabiki Zari.

Sio kila mmoja anawez akukuchukia vile anaweza kukuchukilia mwingine  vile kundi kubwa la watu wanvayoweza kukuchukulia wewe.pamoja na kwamba mwanadada Zari the bossy amekuwa akipata upinzani mkali sana instagram ahasa katika page mbalimbali za udaku lakini kuna watu bado wanampenda na wanamsifia kila kukicha.

Mwanadada Ray c amekuwa moja ya watu hao wanaomsifia na kumpongeza kila kukicha na kila anapofanya jambo zuri, wikiendi iliyopita mwanadada zari aliweka picha nyingi zinazomuonyesha akiwa katika mashindano ya u-miss huko nchini kwao, wapo waliomponda sana kuwa hajapendeza na gauni alilovaa lakini iemkuwa tofauti kwa mwanadada Ray c na Koletha akutoka bongo movies.

Wasanii hawa wawili wameonekana kutokuwa na team  zamitandao na kumpongeza zri kwa kupendeza huko, wa upande wa Rayc pia amekuwa moja ya watu wanaopenda sana kukosoa kila anapoona mtu mmoja anaingiliwa na kushambuliwa sana katika mitandao ya kijamii , kwa mfano aliwahi kumttetea na hata kumkosoa hamisa kutokana na mambo tofauti tofauti.

Maua Sama ,Diamond Ndani ya Afrima 2018, Vannesa na Alikiba Wakatwa.

Tuzo za afrima nchini nigeria imetoa list ya wasani watakaoshindanishwa katika vipengele mbalimbali katika mashindano hayo.

Huku wasanii kutoka katika lebel  ya WCB wakiongoza katika vipengele mbalimbali huku wasanii wengine wakishindwa kuonekana katika vipengele vyovyote .

kwa upande wa wasanii wa kike, ni msanii Maua Sama pekee aliyeweza kuingia katika mashindano hayo katika kipengele cha  Best Female of Eastern Africa.

Wasanii Wakongwe Wakataa Kuitwa “Legends’

Kumekuwa na ile heshima wanayoitoa baadhi ya wasanii wachanga kwa wasanii waliotangulia kwa kuwaia ma-legends  ikiwa kama njia ya kuonyesha kuwa wanamchnago mkubwa sana katika tasnia ya muziki ukizingatia muziki ulivyo sasa sio kama ulivyokuwa miaka ya nyuma.

Lakini hii inapokelewa tofauti nan wasanii wenyewe kwa sababu sio wote wanaotaka kuitwa hivyo lakini pia sababu yao kubwa ikiwa kuna sifa bza msanii kuitwa legends na sio wanaitwa tu kwa sababu yeye amekaa katika game kwa muda mrefu kuliko wengine.

Nikki Mbishi alishawahi kusema “wasanii weng wa tanzania wanaoitwa legends hawana hata miaka 40 katika game,ila wanaitwa hivyo ili kuzeeshwa na kujiona kuwa hawana kasi yakuendana na watoto wa 98′, sasa kama Dully sykes mkongwe na R.kelly je:

Siku kadhaa kupita , msanii wakazi pia alisema kuwa wasanii wakongwe wanakuwa na tabia ya kwenda katika media kuomba msaada li kusimamaisha muziki wao huku akisema “kama nyie mkilia je wale wasanii wachanga (who look up to you) na hawajawahi kutoka wafanyaje, ebu jaribuni kuwa greatful  for glorious past nad cherish it”

Hata hivyo Tid nae alifunguka na kusema kuwa wasanii wa zamani kidogo wamekuwa wakiitwa wakongwe ili tu ku-step down kutaka kudai maslahi yao huku wakipewa jina la kuwa wakongwe ili kuachana na hai zaoza msingi , Tid anasema”

“legends ni mtu mwenye miaka kuanzia 50 katika game,mimi unaniita legends gani wakati nimeanza muziki miaka 19 tu iliyopita, hata miaka 40 sijafikisha unaniita hivyo, sisi ndio tunatakiwa tule matunda ya muziki,huko ni kutoka kwenye line tu na kuwaweka watu wao kwa sababu sisis tunawadai na wanatuzulumu sana.so diamond was me lakini wakasema wanamleta diamond ili tukushushe.

lakini pia hata Jay Dee aliwahi kuwpasha watu katika mtandao wa Twitter kwa kuandika”mnikome , mkongwe ni Bi Chuka na Khadija Kopa tea mnikome kabisa mimi bado mbichi.”

 

Diamond na Vannesa Kuwania Tuzo Uingereza Tena

Wasanii wanaofanya vizuri sana tanzania katika kutangaza muzikiwa bongo ndani na nje ya nchi mabo kwa sasa wamekuwa kama kaka na dada wa bongo fleva Vannesa Mdee na Diamond Platinumz wameingia katika  headlines tena baada ya kuwekwa tena katika tuzo za huko uingereza wakiwa na wasanii wengi wakubwa.

Tuzo hizo za African Pride 2018 zitakazo fanyika June 3 mwaka huu kutakuwa na wasanii wengine wangi kutoka afrika ambao watachuana vikali na wasanii wetu kutoka Tanzania.

Wasanii kama Tiwa Sawage, Yamei Alade, Kiss Daniel , Patoranking, Davido, Wizkid na wengine wengiwatakuwepo kutafuta msanii vora wa muziki afrika kwa upande wa kike na upande wa kiume.

Vannesa na Diamond sio mara yao ya kwanza kuwania tuzo mbalimbali za nje ya nchi na kutoka na ushindi wa kuwapa tanzania hshima juu ya muziki, hivyo kila la kheri kwa wasanii hawa lakini pia pale wanapohitaji sapoti mashabiki wawe mstari wa mbele kufanya hivyo.

Steve Nyerere Kuwaombea Viongozi Waliofariki.

Kiongozi  wa bongo movies Steve Nyerere  pamoja na team yake ya uzalendo ameanda siku maarumu ya jumamosi hii kwa ajili ya kuwaombea wasanii na viongozi walitangulia mbele ya haki na kuwaenzi watu hao., maombezi ambayo yatafanyika jijini Dar katika viwanja vya Leaders club.

Steve Nyerere amesema kuwa tukio ilo la maombezi litafanyika sambamba na kuwafutulisha watu wote watakaokuwepo ambao watakuwa katika kuendeleza mfungo wa Ramadhan.

tunataka kuwakumbuka ndugu zetu waliotangulia mbele ya haki,sisi tuliobaki tunatakiwa kuwakumbuka na kuwaombea ndugu zetu.sis tupo nyuma yao kwaio kama wazalendo kwanza tumeona tuanda e tukio la aina hiyo kila staa na kiongozi aliyetangulkia mbele ya haki tutamuombea.

Steve Nyerere pia ansema kuwa maombezi haya yatawagusa watu  wote katika tasnia ya sanaa bula kubagua kuwa ni muziki au filamu hivyo itakuwa ni waimbaji, waandaaji wa muziki, waandaaji wa filamu, watayarishaji, waigizaji , nahata waandishi wa habari ambao wamekuwa wakiandika habari za wasanii lakini ndio hivyo wametangulia mbele za haki.

 

Celebrities turn out in huge numbers to bid the late popular video vixen Agnes Masogange goodbye (Photos)

Popular video vixen, Agnes Gerald Masogange died on 20th April following a short illness.

According to reports her death was a result of insufficient air that was caused by an asthma attack.

Her death shook the whole of Bongo entertainment industry as most celebrities could not believe she was gone.

Most celebrities shared their condolences messages through their Instagram page  as they mourned her death.

Celebs gather at leaders Club

For the final send of in Dar Es Salaam; top celebrities accompanied by friends and family gathered at Leaders club for the body viewing.

Among those present were Alikiba, Idris Sultan, Diamond Platnumz, Harmonize, Hamisa Mobetto, Tunda among others who were close to the late vixen. Below are just a few photos from the final send off.

Ray C Awapa Moyo Wasanii Wakongwe

Mwanadada aliwahi kuvuma sana katika tasnia ya bongo fleva mwenye kiuno chake bila mfupa amefunguka na kusema kuwa kuna jini limekuwa likiwasumbua sana wasanii wa muziki hasa wakongwe  na kushindwa kuendelea na muziki wao.Ray C aliyasema hayo baada ya shoo wa Lady Jay Dee kubadlishiwa ukumbi  siku anazindua project yake ya anaweza ambayo ilifanyika wikiendi iliyopiata jijin Dar Es Salaam.

Kupitia ukurasa wake wa instagram, Ray c aliongea hayo baada ya kubadilika kwa ukumbi alitakiwa kufanyia shoo lady jay dee na kisha kuhoji yuko wapi mtu kama Marlow, Mandojo na Domo Kaya, juma nature , anasema kuwa anahisi kuna jini anawavuruga wasanii wakongwe.

Kuna nini bongo fleva, wasanii wapya ni wengi, ooh yes nalijua hilo lakini ukweli ni kwamba nchi yote hapa afrika mashariki nikienda nasikia tu nyimbo za zamani,mimi mwenyewe pamoja na mahanjumat ya pepo la ahera lakini bado sauti ipo nje.nasikia kuna jini mmoja ambae amekuwa akiwafanya wasanii wajione kuwa ndio basi tena.point yake ni moja kuwa anauwezo wa kukujenga na kukumaliza mara moja , jini huyo ni promota.

Ray c anaendelea kuwapa moyo wasanii kwa kuwaambia kuwa hata ingekuwaje lakini wanapaswa kujua kuwa kipaji ndio kila kitu na wala hawana haja ya kuhofia kuhusu watu wengien kama mapromota.

wasanii mna kazi kubwa ya kujiamini kwanza kabla ya kumuamini mtu mwingine,mkishajua aliyewapa viapaji basi mtasimama tena.maana mashabiki wenu bado wapo,kinachohitajika ni kipaji na wala sio promota.

 

 

Wasanii Wahaswa Kuwa Makini Katika Kusaini Mikataba ya Kazi

Wakili wa kampuni ya Selta Tanzania Noeli  Chikwindo amfanya mazungumzo na wasanii mbalimbali nchini na kuwashauri kuwa makini sana wanapokuwa wanasaini mikataba ya kufanya kazi na kampuni au menejiment mbalimbali kwa sababu wanapozingatia sheria ndipo wanapoweza kujitetea na kulinda haki zao.

Wakili huyo anasema kuwa katika mikataba ya kazi za wasanii kuna sheria kama saba ambazo wanatakiwa kuzifuata kabla ya kusaini mkabata wowote ule na wanapaswa kuzijua na kuzifatilia kila mara.

ni vema kbala ya kuweka sahihi katika mkataba ni bora kujua ni kitu gani kwanza unakuwa unasaini,lakini pia uangalia lugha inayotumika katika mikataba iyo na kama unaielewa  kuepuka matatizo yanayweza kujitokeza.

Wakili huyo anasema kuwa wasanii ni kazima watambue haki zao kwanza na ndipo watambue kuwa wanaweza kufanya  kazi na watu wengine hii itasaidia sana kuepuka wasanii kuwa wanalalamika kuwa wanaonewa au kuutapeliwa.

Ma-Miss Kuajiriwa Kufanya Kazi Shirika la Ndege La Taifa

Waziri wa habari m sanaa na michezo mh harrison mwakyembe amependekeza kuwa wanaoshiriki mashindano ya urembo wa ma-miss waajiriwe katika shirika la ndege la taifa kwa sababu wana vigezo vya kutosha.Mh Harrison Mwakyembe aliyasema hyo katika uzinduzi wa mashindano hayo kwa mwaka 2018 yatakayofanyika chini ya kampuni ya The Look baada ya ile ya Lino kuachia ngazi hiyo.

Mh Waziri amesema kuwa wshiriki wengi wa mashindano hayo wanakuwa na uwezo na sifa nyingi za kuwa katka cabin crew ila tu kabla ya kuajiriwa wanapaswakupelekwa kozi fupi ya miezi mitatu katika chuo cha anga kabla ya kuanza kazi na hii itapunguza tatioz la ajira kwa warembo hao.

Hii pia inaweza kusaidia baadhi ya wasichana kwa sababu kuna warembo wamekuwa wakishiriki mashindano hayo na baadae dirazao za maisha kupotea na kujikuta wakiishi maisha magumu sana.

 

Tiko Awasahauri Wasanii wa Bongo Kuwa Watiifu kwa Serikali.

Msanii wa bongo movies nchini Tiko Hasssan amefunguka na kuwataka wasanii wa bongo kuwa watiifu pale wanapoambiwa kutekeleza jambo na serikali ili wasiweze kupatwa na madhara maengine yanayoweza kutokea baada ya kukiuka sheria hizo.

Tiko amesema kuwa kuna baadhi ya wasanii unakuta wanahitajika kufika mahali flani na mamalaka inayohusiana na sanaa lakini wanakiuka maagizo hayo alafu ukifika muda wa kuipoea adhabu anakuwa mkali na wa kuanza kulalamika wakati picdi wanapokuwa wanaitwa inakuwa ni kwa manufaa ya kazi zao wenyewe za sanaa .

Akitolea mfano kutoka kwa wasanii wa muziki, Tiko anasema kuwa serikali kupitia Baraza la habari, sanaa , tamaduni na michezo wamekuwa wakiwaita wasanii ili kukaaa nao chini kuzungumza nao kuhusu marekebisho ya kazi zao hasa wasanii wa muziki lakini wanakuwa wanapuuzia na kushinwa kufika kwa kudharau.

Jamani mastaa tunatakiwa kuheshimu serikali , aple unapoitwa  wito unatakiwa kutii wito huo. kwa sababu hiyo ndo inayosaidia katika kazi za sanaa.- Alifunguka Tiko Hassan alipokuwa akiongea na  za moto moto news.

Haya yote yanakuja baada ya wki moja iliyopita wasanii wengine kukumbwa na sakata la kufungiwa kwa kazi zao na serikali kwa madai ya kwenda kinyume na maadili ya Tanzania katika utoaji wa kazi zao na mavazi yao kitu ambacho kimewaumiza wasanii wengi huku baraza la sanaa likisema kuwa wasanii hao wamekuwa wakipuuzia wito na barua za mazungumzo wanazotumiwa.

 

Baraza Kutoa list Nyingine ya Wasanii na Nyimbo Zisizokuwa na Maadili

Ikiwa bado wasanii mbalimbali wakiendelea kulalamika na kusema kuwa baraza la sanaa limekuwa likiwafungia bila kutoa sababu za kufungiwa kwa nyimbo nyingi za wasanii, baraza la sanaa linajiandaa kutoa nyimbo nyingine ambazo zitachunguzwa na  zikaonekana kuwa na tatizo la kuwa zimeenda  kinyume na maadili ya Tanzania.

Wiki iliyopita baraza la sanaa lilitoa list ya nyimbozaidi ya 10  ambazo zilitakiwa kufungiwa kuchezwa katika vituo mbalimbali vya habari kwa madai kuwa zimekiuka vigezo na masharti na maadili ya tanzania huku msaii wa hip-hop roma mkatoliki akifungiwa miezi sita kutokujihusisha na kazi za sanaa zozote kwa muda wote huo kutokana na kuwepo kwa  baadhi ya maneno yenye matusi katika wimbo wake wa kiba100 aliomshirikisha Stamina na Maua Sama.

Hata hivyo baraza la sanaa linaendelea kuchunguza nyimbo nyingine zilizopo katika muziki na hata zinazoendelea kutoka ili kujiridhisha na maadili yanayopatikana katika nyimbo hizo  na kama kutakuwa na ukiukwaji wa taratibu pia baraza haliwezi kusita kufungia nyimbo hizo au wasanii.

Baraza linawataka wasanii wote kupeleka nyimbo zao katika mamlaka husika kablya ya nyimbo hizo kutolewa na kusambazwa kwa mashabiki ili kuondoa usumbufu unaojitokeza sasa hivi wa kufungiwa.

Huu ni muendelezo na utekelezaji alioanzishwa Mh Naibu Waziri wa habari, tamaduni sanaa na michezo alipoanza kwa kuwafungia wasanii wa kike ambao wamekuwa wakiweka picha za uchi katika mitandao hivyo zoezi ili litakuwa ni kwa ajili ya wae tu wanaokiuka taratibu na kuvunja maadili ya watu katika jamii.

TCRA Yazifungia Nyimbo 13, Diamond na Nay wa Mitego Walizwa Zaidi

Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) imefungia kuchezwa kwa nyimbo kumi na tatu za wasanii mbali mbali huku Nay wa Mitego na Diamond wakiwa na zaidi ya nyimbo moja kwenye orodha hiyo.

Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) imesitisha kuchezwa kwa nyimbo 13 zisizokuwa na maadili zikiwemo mbili za Msanii Diamond Platnumz.

TCRA waliandika maelezo haya na kuorodhesha nyimbo hizo:

Mamlaka ya mawasiliano Tanzania imepokea nyimbo zisizokuwa na maadili kutoka Baraza la Sanaa Taifa (BASATA). Nyimbo hizo zilitolewa na wasanii na kusambazwa katika vyombo mbalimbali vya utangazaji na mitandao ya kijamii. Nyimbo hizo zina maudhui ambayo ni kinyume na maadili na kanuni za huduma za utangazaji (maudhui) 2005”.

Hii ndio listi kamili ya nyimbo zilizotolewa na Mamlaka ya mawasiliano;

 

Mamlaka ya mawasiliano imetuma kopi hiyo ya barua kwa vyombo vyote vya habari na kuvitaka kusitisha kucheza nyimbo hizo mara moja na pia vyombo hivyo vimehaidi kuchukua hatua kali za kisheria kwa chombo chochote kitaendelea kucheza nyimbo hizo.

Wasanii Walioguswa na Hukumu ya Mh. Sugu

Kutokana na hukumu aliyoipokea jana mh joseph mbilinyi ambae jina lake la usanii ni Mr. Sugu siku ya jana February 26  baada ya kukutwa na hatia ya kutoa maneno makali ya kumkashifu Rais wa tanzania, wasanii wemeonekana kuumizwa na hukumu hiyo ambayo imemkabili msanii mwenzeo.

Wasanii hao walijitahidi kutoa maneno ya faraja kwa msanii huyo na familia yake pia kwa sababu hata msanii huyo alipokuwa mbungeni mara nyingi amekuwa akitetea sana swala la muziki na sanaa.

Ikumbukwe kuwa ni kwa mara ya kwanza Sugu alipoingia bungeni aliweza kuomba kulipwa kwa wasanii ili kuweza kunufaika na kazi zao pale wanapokuwa wanafanya kazi zao sehemu mbalimbali.

Baadhi ya wasani ambao waliguswa na tukio hilo ni pamoja na :

Nikki wa Pili;Nguvu ya Mungu ikapate kuwa pamoja na familia yako, gerezani  sio kaburini ,stay strong Jongwe.

Nay wa Mitego;Stay strong brother Sugu.

Rama Dee;Nasikitika sana kama msanii pia na kama rafiki wa karibu wa Sugu, hii picha sio nzuri.

Izzo Bizzness;Stay strong Big Brother Jongwe.

Kala Jeremiah;Stay Strong Jongwe.

Roma Mkatoliki;Hata hili nalo litapita, stay strong  Joseph Zaburi 35:1-28

Hata hivyo wakili mtetezi wa kesi hiyo Bw Peter Kibatala anasema kuwa wanafanya mpango wa kukata rufaa ya kesi hiyo kwa sababu hawajaridhika na mahamuzi ya kesi hiyo.

 

 

 

Wako Wapi Wasanii Walioumizwa na Kifo cha Akwilina Akwilini

Ikiwa jana ndio siku ambayo mwanafunzi wa chuo cha usafirishaji kuagwa mwili wake na kusafirishwa kwenda nyumbani kwao kwa ajili ya mazishi watu wengine wameonekana kusikitishwa na kuhoji wako wapi wale wasanii ambao walipata mshtuko mkubwa siku ya tukio.

Mategemeo makubwa ya mashabiki ilikwa  ni kuona wingi wa wasanii katika kuaga mwili huo siku ya jana ikiwa siku ya kifo chake wengi walionekana kuguswa lakini kitu cha ajabu  wasanii waliojitokeza ni wachache tena wanahesabika.

Acha tuone sababu, je ni kweli wasanii hao waliguswa na msiba lakini kila mtu alikuwa busy na shughuli zake akashindwa kutoa heshima za mwisho kwa mwanafunzi huyo ambae kifo chake kimeumiza watu wengi.

Je ni kweli kuwa wasanii walishindwa kujua kuwa jamii ya wanafunzi wa chuo pia ni  jamii kubwa inayosikiliza muziki wao hivyo kutokea katika msiba kungewafariji wafiwa na wanafunzi lakini pia kungewafanya wanafunzi na wafiwa kuona kuwa hata wao pia  sehemu ya maisha ya wasanii.

Je uwepo wao katika msiba na kuagwa kwa mwili huo sio kuwa ndio fursa ya wasanii kukutana na mashabiki wao hata kama wapo katika hali ya uzuni.

Yako wapi yale majonzi waliyokuwa nayo wasanii hao katika page zao za instagram siku mwanadada huyo anapoteza maisha.

Hapa tunajifunza kuwa wasanii wengi wamekuwa wakitumia mitandao ya kijamii katika kuonyesha hayo yote lakini wanashindwa kutambua kuwa mashabiki wao pia wanawahitaji sana katika kujumuika nao katika matatizo kama hayo.

Hata hivyo, wapo waliojitokeza  kama Bilnass ambae alionekana kwenye misiba na akapata nafasi ya kuongelea masikitiko yake juu ya msiba huo na kusema “kazi ya mungu haina makosa, kikubwa ni kumuombea tu.natoa pole kwa wanafamilia, wanafunzi na wafiwa wote kwa ujumla.

Mwisho wa yote tunatoa pole kwa wafiwa  hasa ndugu wa marehemu na Mungu awatie moyo katika kipindi hiki kigumu.

Mastaa wa Kiume na Muonekano Mpya wa Rangi za Nywele Kichwani

Inaweza kuwa ni fashion mpya iliyoingia mjini kwa sasa wasanii wengi wa bongo wameanza ku-trend nayo sasa, ni upakaji wa rangi nywele.Sio mbaya kubadilisha muonekano wako hasa kwa watu maarufu ili watu wasiweze kukuzoea na muonekano ule ule kila siku lakini pia katika upakaji wa rangi hizo inabidi pia kuzingatia sana rangi yako binafsi ili uweze kutokea.

Hivi karibuni kumezuka wasanii kadhaa wa kiume wameanza ku-trend na stykle hii ya nywele kama:

                                                 

.Huu ni muonekano mpya kwa Alikiba alioamua kutoka nao hivi karibuni.

BEN POL

Wengi walizoea kuona watu wakipaka rangi ya brown. lakini Ben Pol alikuja na muonekano tofauti wa rangi ya kijani kichwani mwake ambayo pia ilimfanya aonekane poa inawa mara ya kwanza wengi walimsema.

Harmonize.

                                  

Harmonize aliamua kutoka na muonekano wa kuweka breach katika nywele zake kica kizima ingawa ilizoeleka kuwa wanaume wamezoea kuweka katikati.

LAVALAVA.

Muonekano huu wa Lavalava unataka kufanana kidogo na ule wa alikiba , ambapo juzi baada ya Alikiba kuachia picha zake watu walianza kuzua gumzo kuwa kuna aliyemuig mwenzie.

OMMY DIMPOZ

                                                 

Ommy Dimpoz ni moja ya wasanii wanaojali sana muonekano wao wa nje hasa katika mavazi na kila kitu kinachomfanya aonekane nadhifu na mwenye kuvutia, yeye pia alitoka na style mpya ya nywele juzi, akiwa ameweka breach.

 

 

Vazi la Suti Kwa Wanawake Lilivyowatoa Mastaa Hawa

Imezoeleka kuwa vazi la suti ni kwa ajili ya wanaume tu na sio vazi lililozoeleka sana kuvaliwa na wanawake lakini sio kwa dunia ya sasa ya usawa.

Vazi la suti linaweza likamtoa vizuri mwanamke endapo tu atalivaa kwa usahihi na kushonwa kwa ufundi zaidi.

Baadhi ya mastaa kama Zari, Jokate, Amber Lulu Irene na Fahyma wamelivaa vazi hili la suti na naomba niseme tu nimevutiwa na uthubutu wao kwani kama tunavyojua fashion is all about taking risks na kuangalia kama utapendeza.

Hawa ni baadhi tu ya mastaa wa kike wakiwa katika mavazi yao ya suti:

1. Jokate Mwegelo

 

2. Amber Lulu

 

 

3. Zari the Bosslady 

 

4. Irene

 

 

5. Fahyma

Kurasa za Wasanii Mbalimbali Zilivyopambwa na ‘Post’ za Valentine.

Ikiwa jana ni siku ya kusherekea sikukuu ya wapendanao, wasanii mbalimbali walikuwa wakiweka posts katika kurasa zao za instagram wakionyesha jinsi walivyokuwa wakishrekea sikukuu hiyo ya wapendanao, inawa wapo walioumia  na pia wao waliokuwa wanapost wapenzi wao na pia wapo walikuwa wakijua uwepo wa siku hiyo lakini wakionyesha kuendelea na kazi kama kawaida.baadhi ya kurasa za wasanii hao ni pamoja na :

RayVany:

Aliweka picha akiwa na mama wa mtoto wake fayhma.

MONI CENTRO ZONE

Aliamua kuweka picha ya mpenzi wake @officilanai ambae ni msanii mwenzake na kumsifia sana.

MOSE IYOBO.

Yeye aliweka picha ya mwanamke aliyeweza kumzalia mtoto wa kike Aunty Ezekiel na kuweka utenzi wa mapenzi wenye hisia kali.

                                         

ZARI THE BOSSY.

Siku yake ilianza kwa kusema kuwa siku ya valentine imekuwa ni ya kawaida sana kwake na anaendelea na kutafuta pesa.

                                        

Lakini ilipofika usiku zari the bossy aliamua kutoa tamko rasmi kuwa hayuko tena katika uhusiano wa kimapenzi na mzazi mwenzie Diamond Platinumz.

                                         

SHILOLEH.

Yeye aliweka picha na mwanaume wake aliefunga nae ndoa hivi karibuni huku wakionyesha wapo Igunga kwa ajili ya kutoa burudani kwa masgabiki zake.

DAYNA NYANGE

Dayna Nyange aliamua kuweka picha ikimuonyesha akiwa ameshika tumbo lake likionekana kama ni mjamzito na kuandika “HAPPY VALNTINES’. Hii iliibua hisia tofauti kwa mashabiki wakitaka kujua na kuhoji ni nani mhusika wa kitumbo hicho.msanii huyo mara ya mwisho alikuwa akisemekana yupo katika mahusino na Dax Cruz.

Vanessa:Muziki wa Afrika Mashariki Haujulikani Sana Nigeria.

Msani wa muziki anaefanya vizuri na album yake ya Money Monday,Vannesa Mdee amefunguka na kusema kuwa wasanii wengi wa afrika mashariki hawajulikana sana Nigeria kama vile ambavyo inadhaniwa au kama ambavyo nyimbo za nigeria zinavyosikika sana Tanzania.

Vannesa ambae alikuwa Nigeria kwa ajili ya kutangaz album yake ya money monday ameiambia Cloud fm kuwa pamoja na kwamba watu wanahisi nyimbo zetu zinachezawa sana huko, lakini ukweli ni kwamba hata katika club alizokuwa amekwenda wimbo uliokuwa ukipoigwa sana ni wa diamond na Patoranking wa love u die na wa kwake alioimba na Reekado .

hapa Nigeria huo muziki wetu haupo kabisa kwa nguvu zile unavyopaswa kuwepo kwa sababu muziki wetu ni mkali lakini pia hata wasanii wetu ni wakali na wakubwa.

Lakini pia vannesa anasema kuwa nigeria kuna wasanii wengi sana ambao wanajitahidi kukuza muziki wao kwa kuwasapoti sana wasanii wao.

Hii sio mara ya kwanza wasanii kutoka tanzania wamekuwa wakisema kuwa ingawa Tanzania kuna wasanii wakubwa lakini wngi hawajulikana sana nje, Bright alishawahi kuongelea hilo.

Wasanii Wakubwa Bongo Wanaosikilizwa Sana Nchini Kenya.

Wapo wasanii wanaofanya vizuri sana bongo na kazi zao imekuwa zikionekana mpaka nje ya nchi.wapo wanaoendelea kufanya vizuri ili kukuza muziki huona kuufanya upendwe nje ya nchi.Msanii mkongwe kutoka Kenya amewataja wasanii wakubwa tanzania ambao wamekuwa wakisikilizwa sana katika radio na kila mkona nchini kwao Kenya.

Diamond Platinumz.

Diamond ni msanii mkubwa na mwenye kujituma sana.ukiachana drama na skendo nyingi anazokumbana nazo Diamond lakini ni msanii ambae kwa kipindi cha muda mfupi aliweza kupata mafanikio makubwa na kuweza kusaidia wengine kimuziki.kwake yeye mafanikio yake na ya wengine kumuziki ndio kipaumbele kuliko kitu kingine chochote.

Ali kiba.

Amekuja ni mmoja wa wasanii wanaopendwa sana kwa manjonjo na sauti yake anapokuwa jukwani.alikiba ni msanii anaependwa sana na wakina dada kutokana na mvuto alionao.Alikiba amekuwa ni moja ya wasanii wakubwa tanzania kwa miaka mingi tangu aanze muziki.yeye ni moja ya wasanii wakongwe wasiochuja Afrika Mashariki.

Vannesa Mdee

Ukiongelea wasanii wa kike wakubwa waliopata mafanikio kwa  juhudi zao yeye ni namba moja.vannesa amekuwa msichana hasikuwa na aibu katika kusimama na kuitetea kazi yake.siku zote amekuwa ni mtu wa kuthubutu kufanya jambo lolote lifanikiwe.Hajawahi kukata tamaa lakin i pia amekuwa anajituma ili kuendeleza muziki wake.Sasa hivi ameta album yake na amekuwa akizunguka nchi mbalimbali kwa ajili ya kusambaza nyimbo zake.

Wasanii wengine aliowataja ni pamoja na Ben Pol, Chegge na Chin Beez.

 

Wanaonyoa Kiduku Kusakwa na Polisi,Je hii Itahusu Wasanii.

Ilianza kwa kuwafungua wasanii hasa wa kike wanaovaa vibaya ili kulinda maadili ya taifa na wale wote wanaochapisha picha za utupu mitandaoni.zoezi limegeukia upande wa pili na sasa ni watu wote wanaonyoa mtindo unaojulikana kama kiduku ambao mtu hunyoa nywele za pembenina kuacha zilizopo katikati.

katika moja ya magezo yanayotoka kila siku, gazeti la nipashe ya leo imeweka habari kuwa mapolisi jijini dar es salaam wameanza kamata kamata ya vijana wote wanaonyoa style ya nywele inayojulikana kama kiduku na kuweka ndani mara moja.Msako huu utawahusu watu waote wanaonyoa hivyo ikiwa ni moja ya utekelezaji wa kutunza na kulinda maadili ya Taifa.Baada ya kufanya uchunguzi gazeti hilo limebaini kuwa vijana hao wanakamatwa na kushtakiwa kwa kosa la kuvunja maadili ya kitanzania.

swala la kujiuliza ni kwamba je kamata kamata hii inahusu vijana wa mitanai tu au hata wasanii wengi ambao sasa hivi style hii ya nywele imeshakuwa ni kama ya kawaida kwao.Na kama ukamataji huu unamhusu kila kijana mtanzania basi kamata kamata hii itakuwa inawahusu wasanii wengi wakubwa na wadogo wakiwemo Diamond Platinumz.

Ingawa bado haijabainika tamko la kukamtwa kwa vijana wanaonyoa viduku limetoka wapi lakini,lengo kubwa ni kulinda maadili ya TaIfa ingawa pia watu wengi katika mitandao wameonyeshwa kukerwa na ukamataji huo wa vijana.

 

Honeymoon Amuandikia Barua Mh.Juliana Shonza Kuhusu Maadili ya Wasanii

Mtanzania anayeishi Marekani , ambae pia ni  mtengenezaji wa filamu nchini humo, anaejulikana kwa jina la Honeymoon Aljabir ameandika barua ndefu kwa Naibu Waziri wa Habari na Michezo kuhusu kitendo alichokifanya kuhusu kuwafungia wasanii ambao wanavaa utupu na kuchafua maadili.

Honeymoon ambae inasemekana ni dada yake na mwanadada Faiza Ally, ametengeneza filamu kama   Forgotten hero,The king without a crown, na Daddy’s wedding aliigiza monalisa.

Amemshukuru sana Naibu Waziri kwa kuteuliwa na anaamini kuwa ataisaida sana sanaa ya tanzania kukua  na takuwa mstari wa mble katika kusaidia wanawake wenzie katika sanaa.

furaha kwangu ni kwamba mwanamama mwenzangu umechanguliwa utaweza kutusaidia sana wanawake wenzio  katika sanaa ambayo hasa inamilikiwa na wanaume.

Hata hivyo Honeymoon amesema kuwa anashangaa sana kuona kuwa badala  kusaidia wenzake katika  sanaa, ameanza kwa kuwakomoa wasanii wa kike kwa  kuwafungia na kuwakataza bila kujali maslahi yao.hata hivyo mwanadada huyo ameishia kuhoji kuwa kama anataka watu wasivae nguo za kuua maadili , je kabla ya kuja kwa wazungu asili ya mwafika ilikuwa ni nini kama sio kukaa uchi kabisa.

Honeymoon,ameendelea kuhoji kwa nini kuataza kuuliwa kwa maadili kwa wasanii kumejikita zaidi katika kuwakataza wasanii wa kike tu na sio wasanii wa kiume huku akimtolea mfano Idris Sultani ambe hivi karibuni alipiga picha za kutangaza nguo za ndani za Calvin Klein.

By the way malengo yako  ni kwa wasanii wa kike,idrisa amepiga picha za  chupi akini mbona hamjamfungia,na kama kweli una nia nzuri kwanini usichunguze unyanyasaji wa kijinsia ambao wanapitia wasanii wa kike.

Honeymoon anaonyesha hisia zake za huzuni kwa kitendo cha naibu waziri kumfungia gigy money ambae kwa sasa ni mjamzito na anahitaji kufanya kazi ili kupata kipato kitakachomsaidia klea mimba lakini pia kwa mtoto wake anaekuja.

Fikiria huyo mtoto wa kike mjamzito ambae umemfungia , unataka mtoto wake aishi vipi,kama kwlei wewe ni mwanamke unataka kulinda heshima ya wasanii kwanini usitafute wanaojiuza.

Maneno ya mtayarishaji huyo wa filamu yanakuja baada ya msako wa kuwatafuta wasanii ambao wanaharibu maadili ya kitanzania kwa kutupia picha za uchi katika mitandao.

Matukio Makubwa Yaliyotikisa Mwaka 2017, Upande Wa Burudani.

Kila kitu kina historia Duniani, pia kwa upande wa burudani Tanzania kuna matukio makubwa yaliyotokea ambayo utakapo wauliza wahusiaka lazima watakwambia kuwa hawawezi kusahau swala hilo.

Lulu Kufungwa Jela.

Mnamo tarehe 13 November, mwanadada mrembo kutoka bongo movies, alipokea kifungo chake cha kutumikia miaka miwili gerezani baaba ya kukutwa na hatia ya kuuua bila kukusudia.Kesi hiyo ya mauaji ilitokea mwak 2012 baada ya Lulu na aliyekuwa mpenzi wake Kanumba kugombana na kusababisha umauti wa mwanaume huyo.

Tukio ilo lilitikisa Tanzania nzima hasa wapenzi wa sanaa , kwa sababu wengi walikuwa wakimpenda Lulu na kazi zake pia.

 

Kutekwa Kwa Roma  na Wenzake.

usiku wa april 26, wasanii wawili roma mkatoliki na moni centrozone walitekwa na kwenda kusikojulikana huku kukiwa na kigugumizi cha kutokujua wapi walipokuwa.baada ya kupotea kwa wasanii hao wasanii wengi waliungana kwa pamoja na kuanzisha kampeni ya ‘Free Roma’ ili kumsaidia mkewe na familia kujua wapi alipo.

kama baada ya siku 3, roma na wenzake waliachi wa huru na watekaji hao huku wakiwa na majeraha mengi katika miili yao, cha ajabu na kushangaza hakuna anaejua siri ya kutekwa kwao mpaka sasa kwa sababu msanii huyo hakutaka kulizungumzia hilo.

Babu Seya   na Papi Kocha kutoka gerezanai.

Tarehe 9 Desemba mwaka huu Rais Magufuli aliweka tena historia kwa kitendo cha kuwatoa na kuwapa uhuru  wasanii wakongwe Babu Seya na Papi Kocha, hii ilikuwa ndoto ya wasanii na wananchi wengi kutokana na maombi ya wasanii hao kutoka.Tarehe hiyo ilikuwa ni moja ya siku kubwa na yenye furaha sana kwa watanzania wengi sana baada ya wasanii hao wakongwe kutoka.

Hamisa kuzaa na diamond Platinumz

Timbwili lilianza pale ambapoa hamisa alianza kusema kuwa ana mahusiano na msanii mkubwa Tanzania Diamond Platinumz ambapo Diamond alikana taarifa hizo lakini baadae Hamisa alijulikana kuwa ni mjamzito na kufanya watu kaamini kitendo hicho lakini kwa Diamond mwenyewe ilikuwa tofauti kwa sababu alikana katika vyombo vya habari na kusema mimba ya Hamisa sio ya kwake.Hamisa aliamau kuvujisha picha za mahusiano yake na Diamond na kufanya mtandao wa instagram kuzizima na hatimaye Diamond aliamua kuweka wazi na kukubali taarifa hizo katika vyombo vya habari na kuiomba radhi familia yake.

Wasanii na kashfa za madawa ya kulevya

Mh.Makonda  aliibuka na kuanza kupiga vita ya madawa ya kulevya ambapo wasanii wengi walizolewa na kusweka Lumande .Hakuna aliyetegema kuwa wasanii wakubwa na wanaopendwa wanaweza kuwa katika list ya watumiaji wa madawa ya kulevya.Wasanii kama Wema Sepetu, TID, Vannesa Mdee, Mr Blue, Lulu Diva,Tunda na Rommy Jones.Ambapo baada ya kesi na mahojiano, Agness Masogange walikutwa na hatia na mpaka sasa kesi zao ziko mahakamani.

Swala la Wema  Sepetu na vyama vya siasa.

tarehe 24 february wema sepetu aliahama kutoka CCM kwenda CHADEMA, hii ni moja ya headline kubwa katika vyombo vya habari kwa mwaka huu.hii ilitokea siku chache baada ya wema kutajwa kuwa katika list ya wasanii waliokuwa wakitumia madawa ya kulevya.

Lakini tena Deseba 1 , mwaka huu huu tena wema sepetu alitangaza kuhamia kutoka CHADEMA na kurudi tena CCM.

Ndoa ya Irene Uwoya na Dogo Janja

Hii i moja ya mambo yaliyowaacha watu maneno ya kuongea sana katika mitandao ya kijamii, irene uwoya na Dogo janja walifunga ndoa mwishoni mwa mwaka huu.Watu wengi walishangaa kutokana na umri wa Dogo Janja kuwa mdogo zaidi ya mwanamke aliyemuoa.

Penzi la Jux na Vannesa Mdee.

Vannesa Mdee na Jux waliingia katika trending ya mitandaoni mwaka huu baada ya kuwa moja ya couple nzuri na pendwa Tanzania kwa upande wa wasanii, lakini baadae hakuna sababu iliyokuwa wazi ambayo ilisababisha wawili hao kuachana, mashabiki wao walipiga kelele sna na kutaka warudiane.Tamasha kubwa la FIESTA linalozunguka karibia kila mikoa liliwafanya wawili hao kurudiana na kuendelea na mapenzi yao mwishoni mwa mwezi November.

 

 

 

 

Ndoa 5 Za Mastaa Zilizo-kiki Kwa Mwaka 2017

Mwaka 2017 umekuwa mwaka wa kila jambo na matukio mbali mbali kwa mastaa wetu wa Bongo mojawapo kati ya matukio yaliyochukua nafasi ya kutrend sana ni ndoa za mastaa mbali mbali.

Ndoa zilizo fungwa na mastaa mbali mbali zilitawala nakushika headlines na leo tutaangalia Ndoa tano za mastaa zilizotrend sana mitandaoni na hata mitaani ambazo kila mtu alikuwa anaziongelea.

1. Shilole na Uchebe

Ndoa ya Shilole na Uchebe ilikuwa ndoa yenye utata sana ambao ulianzia kwenye familia kwani habari zinadai kuwa familia ya Shiloke haikutaka aolewe na Uchebe hadi kufikia hatua ya kupelekana polisi na hadi siku ya harusi ilifanywa kwa siri na kuhudhuriwa na watu kumi.

2. Rommy Jones na Kay Jord

Ndoa hii ilikiki kwa staili ya kipekee kwani bwana harusi ni kaka Wa mwanamuziki maarufu Diamond Platnumz kilichowavutia watu wengi ni Diamond na Zari kuwa wasimamizi lakini pia familia ya Diamond kutoa zawadi za mamilioni kwa maharusi.

3.Ndoa Ya  Proffesor Jay

Ndoa ya mbunfe wa Mikumi Proffesor Jay iliwavutiwa watu wengi keani ni harusi iliyowakutanisha Wasanii wakongwe wanasiasa na watu mbali mbali lakini pia ndoa hiyo ilisindikizwa na sherehe tatu.

4. Joti na Tumaini

Harusi ya Joti ilizungumziwa sana kwanza kwa sababu hakuna mtu aliyeamini Kama kweli anafunga ndoa watu wengi walijua ni utani tu au litakuwa tangazo lakini ilikuwa ni ndoa kweli na ilikiki sana.

5. Irene Uwoya na Dogo Janja

Hii ndio ndoa ambayo inaweza ikawa imefunika mwaka 2017 kwani ndoa hii ilizungumziwa sana kupita kiasi yote ikisababishwa na tofauti ya umri wa Dogo Janja na mrembo Uwoya.

 

Waliozoea Kuvaa Vichupi Sasa Basi,JPM Kula Nao Sahani Moja

Jana katika kikao cha wazazi CCM kilichofanyika mkoani Dodoma , Mh. Raisi Magufuli aliongea na wazazi kuhusu maadili ya wasanii hasa wa kike ambao wamekuwa wakivaa nguo fupi na kuwaacha miili yao wazi.Raisi Magufuli amesema kuwa amekuwa akishangazwa sana pale anapowasha tv na kuona wanaume wakiwa wamevaa vizuri lakini jinsia ya kike wakiwa uchi kabisa na ni kitu ambacho akimpendezi kabisa.

M. Raisi amesema kuwa anazitaka maamlaka husika hasa TCRA, kuwachukulia hatua wote ambao wamekuwa wakipiga picha za utupu  na kutupia katika mitandao ya kijamii na kama wanataka kukaa uchi basi wakae huku huko katika club lakini sio kuwka katika mitandao.

Mh Raisi alisema kuwa ni aibu kwa wazazi kuangalia katika televisheni watoto hasa wa kike wakiwa uchi na hakuna hatua zozote zinazochukuliwa na mamlaka husika.

Baadhi ya maadili yameanza kupotea na nyinyi wazazi , na mmeshindwa kuyakemea , unapofungulia muziki  ukitaka kuwaona wanaocheza utakuwa ni wanawake tu ndo wako uchi,lakini wanaume hapana baadhi ya wanawake wanaachia viungo vyao.

kwanini uwavulie hata wasiotaka kuoona huo uchi,tena kwa wakati ambao sio muafaka ,nyie kama jumuiya ya wazazi inafika wakati inapaswa  kuyakemea haya , tunaelekea wapi sasa?tunawafundisha nini watoto?kwani akicheza amevaa nguo hatafurahisha?

vyombo vyetu vya habari viko wapi, vyombo vinavyosiamamia hayao wako wapi,je TCRA ambao wana mamlaka ya kufungia hata vyombo vya habari ambavyo vinarusha video za utupu iko wapi?

Ujumbe huu wa mh raisi unaenda moja kwa moja kwa wasanii wengi tanzania hasa wa kike ambao wamekuwa na tabia hii ya kuvaa nguo zinazoonyesha utupu wao, Gigy Money, Sanchoka,Amber Lulu, Pretty kindy , Kidoa na wengine wengi.

Fiesta Kuisha Saa Sita Itaathiri Ndoto Za Wasanii Wengi

Tamasha la Fiesta inasemekana kuwa ni moja ya tamasha kubwa nchini na ikiwezekana hata ikawa ndio tamasha kubwa afrika kufanyika kwa kutembea mikoa karibia nchini nzima.tamasha ilo lililoanza mnamo mwezi september, lilitembea zaidi ya mikoa 15 na fainali ya tamasha ilo limepangwa kufanyika tareh 25 Novemba  mkoa Dar Es  Salaam.

Hata hivyo tamasha ili linaweza kuwa tofauti na vile ambavyo watu wengi wamekuwa wakizoea linavyokuwa katika miaka yote kwa sababu , kwa kawaida show ya tamasha ilo uisha alfajiri lakini kutokana na tamko la mhshimu  mkuu wa mkoa husika anasema kuwa kwa mkoa wa Dar Es Salam starehe na matamasha katika sehemu za wazi mwisho wake huwa ni saa sita husika , hivyo basi hata tamsha ilo litalazimika kusiha saa sita husika kama sheria inavyosema.

Akiongea na vyombo vya habari, mkurugenzi wa Clouds Medai ambae pia ndie muhandaaji wa tamasha ilo Ruge Mutahaba anasema kuwa wamepokea tarifa hizo na kama sheria inavyosema hivyo hawawezi kupingana na sheria kwaio tamasha kweli litaishia saa siata lakini kama uongozi inawabidi kupunguza  idadi ya wasanii watakao perfom katika tamsaha ilo ili kufukia muda uliopangwa.Akiendelea kuongelea hilo anasema kuwa bado hata hivyo wanaendelea kufanya utaratibu wa kupata kibali cha kuongeza muda li kuweza kupata list ndefu ya wasanii ili waweze kuwaridhisha mashabiki lakini pia hii ni moja ya njia nyingi zinazowaongizia kipato wasanii na kuwaongezea fanbase.

Swala la kufika saa sita kama ndio utaratibu na sheria iliyowekwa basi  tuko tayari, tumeshajiandaa kwa sababu tunajua  na tutabadilisha ratiba, ila kwa bahati mbaya tu ni kwamba  inabidi tupunguze baadhi yawasanii , lakini bado tunafanya utaratibu ili kupata kibali ili tuweze kuongeza muda kwa sabau huwa kuna kibali maarum cha kufanya tamasha kama ilo.-Aliongea Ruge Mutahaba

Hivyo basi kwa wasanii ambao bado walikuwa wakichipukia na wamekuwa na hamu kubwa ya kuonyesha vipaji vyao katika tamsha ilo itakuwa ni moja ya kukatika kwa ndoto zao kwa sababu katika list ya wasanii watakao onyesha umahiri wao itawalazimu kuondoa wasanii wengi zaidi.

 

Kidoa Amtetea Hamisa Mobeto Mitandaoni

Moja ya wauza nyago wanaofanya vizuri kwa sasa katika video za wasanii bongo  Ssha salumu mwenye jina la umaarufu kama Kidoa amefunguka na kumtetea mwanamitindo na video queen Hamisa Mobeto kwa wasanii wengine wa kike ambao wamekuwa wakimsema na kumsimanga kutokaa na nyingi  skendo   anazopitia hasa hili kubwa la kuzaa na msanii mkubwa Diamond Platinumz na mambo yote yanayoendelea kuhusu kesi iliyokuwa imepelekwa mahakamani kuhusu malezi ya mtoto huyo.

Mwanadada huyo anasema kuwa anakuwa anachukizwa na kuumiza na baadhi ya wasanii wenzie wa kike ambao kutwa kukaaa katika mitandao na kuwa wanamsema Hamisa bila kujua ni kitu gani mwenzao anapitia katika kipindi hiki kigumu na badala yake walitakiwa wamsaidia na kumpa sapoti ya ushauri na sio kumsema kila kukicha katika mitandao ya kijamii.

Kidoa ambae alishinda taji la  Ijumaa Sexiest Girl kwa mwaka 2015 anasema kuwa kinachomshangaza ni jinsi wadada wamekuwa wakimsaidia Zari katika kumkandamiza Hamisa bila kujua kuwa maneno yao yanamwathiri mwanadada huyo kisaikolojia ukizingtia ni mbongo mwenzao.

Sio sawa wasanii wenzangu wanavyokaa wakimnyanyapaa hamisa hata kidogo, kutwa kumoiga vijembe wanatakiwa kukaa wakikumbuka kuwa hakuna ajuae kesha yake ,huenda  hata yeye mwenyewe hakuwaza kama yanaweza kumfika hayo yote. -Alisema Kidoa

Hamisa amekuwa ni moja ya wanadada gumzo katika mtandao kwa kipindi cha takribani miezi mitatu sasa tangu mtoto wake wa pili kuzaliwa na hii yote ni kutokana na kujulikana kwa baba wa mtoto kuwa ni wa Diamond Platinumz ambae tayari anafamilia nyingine yenye watoto wawili na Zari The Bossy Lady mwanamama tajiri kutoka Uganda.Hata hivyo Hamisa amekuwa akitajwa karibia kila kona katika mitandao huku wengine wakimkashifu kwa kujitegesha na kufanya makusudi kuzaa na msanii huyo ili aweze kupata pesa

Mastaa Wazidi Kumlilia Lulu Baada Ya Kutupwa Jela Kwa Miaka Miwili

Asubuhi ya leo msanii wa Bongo movie, Elizabeth Lulu Michael amefungwa na mahakama kuu kifungo cha miaka minne jela.

Mastaa mbalimbali wa Bongo movie na Bongo fleva wamejitokeza ili kumfariji Lulu na familia yake katika kipindi hiki kigumu.

Hawa ndio mastaa kwa kupitia mtandao wa YouTube waliojitokeza kumpa moyo na kumfariji Lulu;

1. Diamond Platnumz

2. Wema Sepetu

3. Dr. Cheni

4. Irene Uwoya

5. Dogo Janja

6. shilole

7. Aunty Ezekiel

 

8. Linah Sanga

9. Shilole

.

Hawa Ndio Mastaa Wa Kike Wanaopenda Wanaume Wenye Umri Mdogo (Viben-10)

Moja kati ya vitu vilivyo zoeleka kwenye jamii zetu kwenye masuala ya mahusiano kati ya mwanaume na mwanamke ni umri, tumezoea siku zote kuwa ni lazima mwanamke awe na umri mdogo na kuliko mwanaume yaani mwanaume lazima awe na umri mkubwa kwenye mahusiano.

Kitokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia na ujio wa wazungu basi hilo limebadilika hivi sasa unaambiwa umri  sio kitu bali ni namba tu cha maana mapenzi tu baina ya wawili haijalishi una umri gani.

Hilo pia linatokea pia kwa mastaa wetu ambao wadada wengi sahivi wanapenda kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanaume wadogo kiumri kwa sababu wanazozijua wao wanawake hao wanaitwa masugar mama na vijana wanaolelewa wanaitwa viben-10, serengetiboys au maryoo.

Hawa ni baadhi tu ya mastaa waliowahi kuwa na uhusiano wakimapenzi na wavulana wadogo au mpaka sasa bado wana uhusiano nao.

1. Wema Sepetu na Idris Sultan

Wema Kazaliwa Mwaka 1988 na Idris Kazaliwa Mwaka 1993

2. Zarinah na Diamond

Zari Kazaliwa Mwaka 1980 na Diamond Kazaliwa Mwaka 1989

3. Irene Uwoya na Dogo Janja

Uwoya Kazaliwa Mwaka 1988 na Do go Janja Kazaliwa Mwaka 1994

4. Shilole na Nuh Mziwanda

5. Nisha na Baraka Da Prince

6. Irene Uwoya na Msami Baby

7. Jacqueline Wolper na Brown

 

Je unahisi ni staa gani mwingine anafaa kuingia kwenye orodha hii?

Magari Ya Kifahari Yanayoendeshwa Na Mastaa Tanzania

Hii ni moja ya rekodi iliyotolewa kwa mwaka 2016-2017 kutoka Tanzania.Haya ni baadhi ya magari ya kifahari  yanayomilikiwa au yaliyowahi kumilikiwa na baadhi ya mastaa wa bongo.

1.Masoud Kipanya (Hummer H3)

Amepitia vitu vingi katika jamii, amekuwa akisaidia vijana kwa namna tofauti tofauti kadri vile anavyoweza.ukiachana na utangazaji kama kazi yake , Masoud ni mchoraji wa katuni maarufu Tanzania.

Ndiye mwanzilishi na muhasisi wa mashindano ya Maisha Plus Tanzania.

2.Masanja Mkandamizaji(BMW x6 na Toyota landcruiser)

Ni mchekeshaji maarufu, lakini pia ni mjasiriamali alijikita katika sekta ya kilimo. pia ni mtumishi wa Mungu

 3.Wema Sepetu(Range Rover e Vogue)

Mwanadada anependwa Tanzania, aliwahi kuwa miss tanzania laini kwa sasa ni muingizaji maarufu.Aliamua kijizawadia gari hili siku yake ya kumbukumbu ya kuazaliwa.

4.Quick Rocka(Range Rover Spot)

Amekuwa na mambo ya kimyakimya na hapendi kujionyesha sana, yuko vizuri katika muziki.

5.Gadner G Habash(Discovery 3)

Ni mtangazaji maarufu wa radio Tanzania, alishawahi kuwa mum wa mwanamuzii mkongwe Lady Jay Dee.

6.Alikiba BMW X5)

Anafanya vizuri kwenye game,ingawa ni msanii asiyependa sana kuonyesha nini anamiliki.

7.Diamond Platinumz(BMW X6)

Msanii wa bongo fleva anaefanya vizuri tanzania , pia ni mmoja kati wa wasnii matajiri Tanzania.

 

 

 

 

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.