Tanzanian actress breaks down as baby daddy marries a different lady

Actress cum business lady Faiza Ally left many feeling sorry for her after uploading a few photos explaining how hurt she felt after watching her baby daddy marry another woman in a colorful wedding held in Tanzania.

The lady says that having watched a man she spent her youth with and even started a family with marry another lady left her feeling broken; and judging from the videos and photos shared on her Instagram confirms indeed Faiza went through a lot.

Faiza Ally’s post

In several photos the lady is seen with swollen eyes which Faiza says she got after crying almost the whole night to help heal the pain she had been experiencing.

Faiza Ally

Ready to move on

In another post, Faiza says she is now ready to let her past go and move on with her life and that of her daughter and son.

https://www.instagram.com/tv/B128Qt3ngw6/?igshid=h8dh8h58f7ua

 

Faiza Asifiwa Kapendeza Baada Ya Kuacha Kuvaa Nusu Utupu

Msanii wa Bongo movie na mzazi mwenzake na Mbunge wa Mbeya Mjini Sugu, Faiza Ally amesifiwa kupendeza na mavazi ya heshima baada ya kuachana na mavazi ya nusu uchi.

Mashabiki waliomuona kwenye moja ya Shughuli Hivi karibuni wamesema kwamba amebadilika katika suala zima la mavazi tofauti na zamani ambapo alikuwa akijiachia nusu utupu akiwa kwenye matamasha.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Faiza amefunguka na kusema kuwa aliamua kuvaa vazi la heshima kwani hakutaka kuongelewa sana kwani amekuwa mtu wa kuongelewa kwenye kila red carpet event.

Faiza ameshawahi kuzua gumzo siku za nyuma Baada ya kuvaa nguo iliyokuwa inaacha makalio yake wazi kutokana na kuchanwa chanwa Lakini pia Faiza ameshawahi kuvaa shati la kiume tu na tai.

Nilipoachana na Sugu Niliogopa Kudhalilika :-Faiza Ally

Mwanadada Faiza Ally anafunmguka na kuongelea ugumu alioupata hasa baada ya kuchana na mwanaume aliwahi kuwa nae katika mahusiano na kuweza kupata nae mtoto wake kwa kwanza wa kike.

Faiza anasema kuwa mara alipoanza kugombana na sugu ambae ni mbunge wa mbeya mjini anasema kuwa ilimfanya kuwa katika wakati mgumu kwa sababu aliona kuwa akiachana nae basi atarudi katika maisha magumu tena watu watamcheka sana.

Faiza ambae anakiri kuumizwa na kuachana kwao kulimuumiza sana hasa ukiangalia kuwa alikuwa ayari ameshazoea maisha fulani ya pesa , ilikuwa inampa wakati mgumu sana kuamua kufanya maamuzi hayo.

Faiza anasema kuwa alikuwa anapata wakati mgumu kurudi yale maisha ya uswahili.

Faiza- Nikipata Ukimwi Nitajitangaza Hadharani

Muigizaji wa Bongo movie na mzazi mwenzake na Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, Faiza Ally amefunguka na kuweka wazi kusababisha endapo siku akijigundua kuwa ni muathirika basi hatajificha bali atajitangaza hadharani.

Faiza amefunguka kuwa endapo itatokea bahati mbaya akakwaa ugonjwa wa Ukimwi a.k.a ngoma, kamwe hatajificha au kujiona tofauti, bali atajitangaza hadharani na kuwapa watu moyo kuwa wanaweza kuishi miaka mingi zaidi.

Katika mahojiano yake na Gazeti la Ijumaa, Faiza ambaye ni mama wa watoto wawili alisema anawashangaa wenye tatizo hilo ambao hujificha na hata wengine kuambukiza wengine, lakini kwa upande wake ataweka hadharani ili kuwapa elimu wengine na kuzuia maambukizi mapya.

Kama mimi ningekuwa na Ukimwi, ningejitangaza hadharani bila woga wowote wala aibu na tena nitasaidia watu wengine wajiepushe na maambuzi mapya“.

Wiki iliyopita Faiza alizua gumzo kwenye Mitandao ya kijamii Baada ya kuposti video iliyomuonyesha akiwa anapima ugonjwa wa Ukimwi na kuanika majibu yake yaliyoonyesha hana maambukizi ya gonjwa hilo.

Faiza Ally Akiri Kuwahi Kuwa Mdangaji

Mzazi mwenzake na Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi maarufu kama Sugu, Faiza Ameibuka na kuweka wazi kuwa ameshawahi kudanga.

Faiza Ally ameeleza kuwa kudanga kwake siyo ishu kwani kama mtu anafanya hivyo kwa kufanya kitu cha maana siyo tatizo Kama atatumia kama njia ya kufanya mambo ya maana.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa, Faiza alisema kama ni kudanga amedanga, lakini alifanya hivyo kwa malengo fulani kwa sababu hakuna anayependa kudanga, alipotatua shida yake kwa sasa amekuwa shujaa na anayejitokeza na kumcheka hajitambui.

Nilidanga kwa sababu zangu nilizokuwa nazo na mwisho wa siku naendelea na maisha yangu”.

Faiza amefungukia biashara zake anazomiliki kwa Hivi sasa ikiwemo tenda ya kuagizia wateja bidhaa kutoka nchini China kuja Tanzania.

Faiza Ally- Ipo Siku Watu Wataelewa Ndoto Zangu

Muigizaji wa Bongo movie na mzazi mwenzake na Mbunge wa Mbeya mjini na msanii Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, Faiza Ally ameibuka na kudai ipo siku watu wataelewa tu ndoto zake.

Faiza Ally amefunguka kuwa watu wengi wanaweza wasimuelewe kwa jinsi anavyopigana na maisha ili tu kutimiza ndoto yake ila ipo siku wataelewa.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers Faiza alisema anakesha China, kubeba mizigo ya watu waliyomuagiza vitu kwa sababu anatafuta pesa na nia yake kubwa ni kuwa tajiri tena kwa kutafuta kwa jasho.

Naona watu hawanielewi mimi ni kukesha na kubeba mizigo ya watu walioaniagiza ni kwa sababu nausaka utajiri tena siyo hela ya haramu ni ya jasho langu na ninataka kuonyesha watu inawezekana na ipo siku watanisimulia tu”.

Mpaka hivi sasa Faiza amekuwa nchini China kwa muda wa wiki kadhaa na amekuwa akionekana akiwa ananunua bidhaa  mbali mbali kwa ajili ya kufanyia biashara anazoagizwa na wateja Wake.

Faiza Ally- Bado Nampenda Sugu

Muigizaji wa Bongo movie na mjasiriamali Faiza Ally amefunguka na kudai bado anampenda Baba wa Mtoto wake ambaye ni Mbunge wa Mbeya Joseph Mbilinyi ‘Sugu’.

Sugu na Faiza walikuwa kwenye mahusiano miaka kadhaa iliyopita lakini pamoja na kuachana wamendelea kukamata headlines kwa maugomvi yao ya mitandaoni.

Faiza pamoja na kumdhalilisha Sugu Mara kwa Mara kwenye mitandao ya kijamii huku akimtuhumu kwa kumtelekeza Mtoto wao bila huduma yoyote.

Pamoja na kukosa maelewano Faiza ameibuka na kudai kuwa bado anampenda sana Sugu na amejaribu kuwa na wanaume wengine lakini ameshindwa ikiwemo kuzaa na mwanaume mwingine.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Faiza ameandika maneno haya:

Baada ya kuandika maneno hayo mashabiki wengi walimjia juu wakidai kwa kuandika hivyo anakuwa anamkosea heshima mke wa Sugu ambaye hivi sasa ni mjamzito wanatarajia kupata Mtoto wao wa kwanza.

Faiza Ally Awatolea Povu Zito Wanaotaka Kuongeza Makalio Kwa Madawa

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara maarufu kwenye mitandao ya kijamii Faiza Ally amejikutwa akiwatolea Povu Zito wanawake ambao wamekuwa wakimsumbua kuhusu madawa ya kuongeza makalio.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Faiza aliweka wazi kuwa kuna wanawake wamekuwa wakimsumbua kwa kutaka kumtuma madawa ya kichina ya kuongeza makalio.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Ijumaa Wikienda, Faiza ambaye pia ni mfanyabiashara alisema hakuna jambo ambalo halipendi kama mtu kumuagiza dawa za kufanya mabadiliko kwenye mwili hivyo anawasihi wanawake wajikubali kama walivyoumbwa.

Sipendi wanawake kutojikubali. Mimi siwezi kumletea mtu dawa ya kuongeza makalio maana naona kama si za kweli, lakini pia ni vyema kujikubali, hicho ndicho kitu muhimu“.

Faiza ambaye hivi sasa yupo nchini China kwa ajili ya kufunga mizigo ya wateja alianika meseji za wanawake ambao wanaomba kuletewa madawa ya kuomgeza hipsi na makalio.

Biashara Zangu Ndio Zinanikondesha Sio Kingine-FaIza Ally

Muigizaji wa Bongo movie na mzazi mwenza kwa Mbunge wa Mbeya Mjini Sugu, Faiza Ally amefunguka na kuweka wazi kuwa kinachomkondesha kwa hivi sasa ni biashara zake.

Faiza ambaye amesuka gumzo baada ya kuonekana anapukutika mwili wake amedai kuwa anakonda kutokana na mizigo ya watu kuchelewa kufika kwa wakati.

Kwenye mahojiano yake na gazeti la  Ijumaa Wikienda, Faiza amesema kuwa watu wengi wanamzungumzia na kumshangaa jinsi alivyopungua, lakini hawajui ni jinsi gani hali wala halali usiku kwa sababu ya mizigo ya watu kuchelewa kufika bandarini.

Watu wengi wananiuliza ninakondeshwa na nini, lakini hawajui ni jinsi gani ninakosa amani mizigo ya watu walioniagiza isipofika kwa wakati ninachanganyikiwa kabisa”.

Faiza ni mmoja kati ya wajasiriamali wa Kwenye Instagram ambaye anafanya biashara ya Kukutwa watu vitu kutoka China kuja Tanzania.

 

Faiza Achukizwa na Ukaribu wa Mwanae na Mama wa Kambo.

Mwanadada Faiza Ally ameonekana kukwaza na ukaribu alionao mtoto wake wa kwanza wa kike na mke wa  baba wa mtoto huyo.

Faiza Ambae hapo awali aliwahi kutuma ujumb kwa baba wa mtoto kupitia ukurasa wake wa instagram akitaka mtoto huyo aawahi kurid kutokana na kufungua shule aliwafanya baadhi ya watu kumtolea mapovu kutokana na matatizo ya misba aliyokuwa nayo baba wa mtoto wake baada ya kufiwa na mama yake mzazi.

Hata hivyo kuna picha zimekuwa zikisambaa za mtoto wake na mama huyo ambae ni mke wa sugu , picha ambazo zimemkera sana faiza na kumtolea povu mwanamke huyo huku akimuonya kuacha ukaribu na mtoto wake na kumwambia kama anataka mtoto basi atafute wake.

koma kupiga picha na mwanangu zaa wako….baba sasha naomba mkataze mtu mwenye sura mbaya kutafuta kiki kupitia mtoto wangu…unachotaka ni kumtengansha sasg=ha na baba yake na sasa umefanikiwa, sasa mataishia kuona picha tu zake tu insta..

 

 

Faiza- Sijaenda Kwenye Msiba Wa Mama Sugu Sababu Alikuwa Hanipendi

Muigizaji wa Bongo movie na mzazi mwenza wa Msanii wa Bongo fleva na Mbunge wa Mjini Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, Faiza Ally amefunguka na kuweka wazi sababu zilizompelekea mpaka kushindwa kuhudhuria msiba wa Mama Mkwe wake.

Siku chache zilizopita Mama mzazi wa Sugu Bi. Desderia Mbilinyi aliaga dunia baada ya kugua kwa muda mrefu ambapo siku ya jana ilifanyika ibada ya kuaga mwili wa marehemu katika kanisa la Muhimbili hospitali.

Lakini siku ya jana hapo kanisani Faiza hakuonekana kabisa na badala yake alionekana mtoto wake aliyezaa na Sugu hali iliyoibua maswali ya kwanini hakuhudhuria msiba.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Faiza amefunguka kuhusu kutohudhuria Kwenye msiba:

Sijaenda wala sijashiriki Kwenye msiba lakini Sasha ameniwakilisha yupo pale kwa ajili yangu kila mtu akimuona Sasha pale atajua amemuwakilisha Faiza.

Sikujisikia kwenda pale kwa mtu ambaye hajawahi kunipenda na mimi naamini ukienda Kwenye msiba wa mtu ambaye hajawahi kukupenda naamini unaenda kupata dhambi unatakiwa ukifika pale uwe na majonzi na mapenzi kwaiyo sikuhitaji kuwepo sehemu ambayo sijutakiwa kuwepo”.

Faiza amekuwa Kwenye mgogoro wa muda mrefu na Sugu pamoja na Familia yake yote kutokana na malezi ya mtoto wao Sasha.

 

Faiza Ally Azua Mjadala Baada ya Kuweka Picha Akiwa Ananyonyesha.

Mwanadada Faiza ally  siku ya jana aliacha  watu hoi baada ya kuweka picha akiwa anamnyonyesha mtoto wake wa kiume mdogo huku akiwa ameweka picha ya sehemu yake ya maziwa wazi huku mtoto huyo akiwa ananyonya.

Hii sio mara ya kwanza kwa msanii faiza kufanya hivyo kwa sababu alishawahi kuweka picha kiwa leba anajifungua na kusababisha watu wengi kulalamikia picha hiyo huku ikionekana kama ni udhalilishaji kwa wakina mama kama yeye.

Watu wengi wali-react kupitia picha hiyo huku wakimtukana sana kwa kujikosea heshima yeye mwenyewe na wanawake wenzie kwa sababu maswala kama hayo yalipaswa kuwa si ya kuonyesha mpaka katika mitandao ya kijamii kama anavyotaka kufanya yeye.

 

 

Shamsa, Faiza Ally Wamshambulia Zari the Bossy.

Wasanii wa bongo movies nchini wamefunguka na kumshambulia mwanamama Zari The Bossy kwa kile kinachosemekana kuwa mwanadada huyo amekuwa na dharau sana kwa watanzania na kwamba amekuwa akimtesa sana ndugu yao diamond kuhusu watoto wake,

kwa upande wa Faiza Ally ambae yee amewatolea povu mpaka watanzania wenzake na kusema kuwa wamekuwa wakimuona zari kama mtu muhimu sana wakati hakuna chochote cha maana alichonacho mwanadada huyo.

katika ukurasa wake wa instagram ambapo aliweka picha hiyo na kisha baadae kuifuta , faiza laisema ” wanawake bhana mna ujinga mwingi sana , mnataka watu wote tumuone zari kama mnavyomuona ninyi, mimi ninamuona tu ni mshamba wa kiganda kama washamba wote….msinitagi up*** wenu, kwanza mi mzuri sema maisha tu ndo magumu.

katika posti hiyo hiyo, Shamsa nae akaja na kupigilia msumari na kusema “mtu asiyetabasama muda mwingi yeye kafumba mdomo na hana tabasamu mara nyingi anakuwaga sio mtu mzuri kabisa,wanakuwaga na roho mbaya sana zilizokomaa kiasi kwamba hata kujifanyisha hawezi…

Hata hivyo haya yote yanakuja baaada ya mwanamke huyo kuonekana kukataa kuwaona ndugu na watu wa karibu wa msanii Diamond katika birthday party ya mtoto wake huko Afrika ya Kusini.

 

Faiza Ally Adai Sugu Atakuwa Amelogwa

Muigizaji wa Bongo movie na mjasiriamali maarufu Faiza Ally amerudi tena kwenye headlines na sakata la mzazi mwenzake ambaye ni Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi maarufu kama Sugu.

Faiza amemtolea povu zito Sugu na kudai atakuwa amelogwa maana matendo anayefanya sio ya kawaida hata kidogo na anaamini hakuwa hivyo zamani wakati wako wote.

Faiza amefunguka hayo baada ya sakata lao la juzi ambapo Faiza alimtolea povu Sugu Kwenye mitandao ya kijamii na kumtaka amuheshimu baada ya Sugu kumtuma Mke wake kufanya shopping ya Faiza badala ya kumpa pesa.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi cha Refresh cha Wasafi Tv, Faiza ameongea haya:

Kwa jinsi ninavyomjua Baba Sasha ni mtu ambaye ana akili zake lakini sijui labda kalogwa kwa sababu nilijua naye mpaka mtoto akakua kuwa na alikuwa responsible father kwa wakati huo kwa nini sasa hivi amekuwa na mwanamke mwingine amebadilika”.

Faiza aliendelea kuelekeza tuhuma za kulogwa kwa Sugu:

Mimi nadhani atakuwa amelogwa tena atakuwa amelogwa milogo mibaya ambayo yeye mwenyewe hajui kwa sababu katika hali ya kawaida huwezi kuleta matatizo Kwenye kumlea mtoto mwenyewe mmoja halafu uwezo unao kama hajalogwa atakuwa na matatizo ya akili”.

 

Sugu Bado Ananipenda:-Faiza Ally Afunguka.

Mwanadada Faiza Ally amefunguka alipokuwa akiongea na waandishi kuhusu mahusiano yake na baba watoto wake Mh Sugu , mbunge wa mbeya ambae amepata nae mtoto mmoja wa kike.

Faiza ambae mara nyingi amekuwa akiongea sana katika mitandao ya kamii akilalamika kuhshu mwanaume huyo kutotimiza mahitaji ya mtoto wake na kwamba amekuwa akimtumia mke mwenzake kutuma mahitaji ya mtoto wake anasema kuwa mwanaume huyo inaonekena anapenda anavyokuwa anamtukana katika mitandao ya kijamii na ndio maana hataki kujirekebisha.

Faiza anasema kuwa kamwe hatoacha kumsema Sugu mpaka pale atakapojirekebisha na kutimiza majukumu yake kama baba.

nadhani sugu bado ananipenda na ndio maana hatimizi vizuri majukumu yake ya malezi na matumizi kwa mwanae shasha.nadhani atakuwa anafurahi vile ninavyomsema na mimi sitakaa niache kumsema mpaka atakapoweza kutimiza mahitahi yake ya malezi.

kama huitaji kuwa na ishu na mtu basi unachopaswa ni kusihi na huyo mtu in a right way,lakini ukiona mt anakutafutia vitu vya kukuumiza ujue bado upo kwenye moyo wake. aweke matumizi ya mtoto kwenye akaunti kila mwezi aone kama mimi nitamsumbua tena.

Faiza Ally Awapa Somo Mabinti Kuhusu Wanaume

Msanii wa Filamu za Bongo Movie na mzazi mwenza wa mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi, Faiza Ally amefunguka na kuwapa somo watoto wa kike kuhusu wanaume.

Faiza amewasihi mabinti kutowaendekeza wanaume kiasi cha kukubali mapenzi yawarudishe nyuma kimaendeleo.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Faiza amewapa ushauri wasichana na kujitoa mfano na kuweka wazi kuwa amerudishwa nyuma kimaendeleo na mapenzi na sasa anakuwa kama anaanza upya:

Kama kuna binti anasoma haya naomba nikwambie tu tafuta maisha usikubali kuyumbishwa akili Wanaume wanaume wanarudisha wanawake nyuma mara nyingi sana.

Mimi ni mmoja ya Wanawake waliorudishwa nyuma na mapenzi na kwa sasa ni kama naanza upya kuna wakati mwingine nawish ningeona ya mbele ili nijiokoe lakini siri ya maisha anaijua Mungu pekee lakini pamoja na hayo yote kama bado unaishi unayo nafasi nyingine usikate tamaa”.

Faiza hakumtaja mwanaume aliyemrudisha nyuma kimaendeleo lakini siku za nyuma ameshawahi kumlaumu Baba mtoto wake Sugu kwa kumpumbaza kimapenzi.

Faiza Ally Athibitisha Kumaliza Bifu Lake na Sugu

Muigizaji wa Bongo movie Faiza Ally na mzazi mwenzake ambaye ni  Mbunge wa Mbeya Mjini Mheshimiwa Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ wameonekana kumaliza bifu lao.

Faiza na Sugu wameshawahi kurushiana maneno Kwenye mitandao ya kijamii mara kwa mara na hata kufikia hatua ya Faiza kumtukana matusi ya nguoni mzazi mwenzake.

Hali ilikuwa mbaya baina yao hadi kufikia hatua ya Sugu kutopewa nafasi ya kumuona binti yao anayeitwa Sasha.

Lakini hivi sasa inaelekea hali ni shwari kwani Faiza ameweka picha Mtandaoni zinazomuonyesha Sugu akiwa na binti yake ambaye ameenda kumtembelea mkoani Mbeya.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Faiza aliweka picha ya Baba na mtoto na kusindika na ujumbe mfupi ili kudhihirisha kuwa hivi sasa hana tatizo na mzazi mwenzake huyo.

Faiza ameandika:

Najisikia vizuri kuwaona Baba na mtoto pamoja tena…. Nawapenda sana”

.

 

Faiza Ally Amwita Mtoto wa Mobeto Fake.

Mwanadada hasiye isha drama katika mitandao ya kijamii Faiza Ally amefunguka na kumjibu shabiki alitoa maoni ya kumshauri Faiza Ally hakumremba mtoto wake kama wanavyofanya wasanii wengine, lakini kitu cha ajabu wakati wa kumjibu shabiki Faiza Ally aliongea wazi kuwa hawezi kufanya hivyo kama anavyofanya Hamisa kwa watoto wake.

Katika maoni aliyoamua kujibu shabiki, faiza alisema kuwa hawezi kum-edit mtoto wake kama anavyofanya hamisa kwa mtoto wake na kumvalisha mawigi kwa sababu mtoto wake hivyo ndivyo alivyo.

siwezi kum-edit mtoto wangu mpaka apoteze uhalisia kama huyo wa mobeto , we are comfortable for who we are , na hizo nywele ndio asili yake ya uafrika , siwezi kumuweka dawa wala kumpachika viwigi …she born to be a star , she doesnt have to fake it , tunaishi maisha yetu kabisa.

Haijulikani kama kuna chochoko yoyote kati ya Hamisa na Faiza Ally mpaka afikie hatua ya kumuandikia hivi kuhusu mtoto wake.

 

 

Faiza Adai Gabo ni King’asti Kwani Alimtafutia Jimama La Kumlea

Muigizaji wa Bongo movie Faiza Ally amefunguka mazito na kudai kuwa msanii mwenzake Gabo ni king’asti na hata kudai alimtafutia mwanamke mwenye hela ili amlee.

Bifu la Faiza na Gabo lilianza siku za nyuma baada ya kuigiza movie moja ambayo haijatoka mpaka leo ambapo Faiza ameonyesha kumlaumu Gabo na kudai amemtapeli.

Kwenye mahojiano na Kiss Fm Radio Faiza amefunguka na kukataa tetesi za yeye kuwahi kuwa Kwenye Mahusiano na Gabo na kuweka wazi kuwa Gabo alikuwa King’asti wa rafiki yake:

Ukweli ni kwamba Gabo alikuwa king’asti nilimpa  rafiki yangu anaitwa Karima yaani mtu ambaye nilimpa kazi na nikampa na demu ambaye ana hela”.

Faiza amedai mwanamke huyo ambaye alimpa Gabo ni mwanamama wa kizungu ambaye alivutiwa naye baada ya kumuona Gabo na mara moja wakaanzisha mahusiano na kudai kuwa Gabo amehongwa sana.

Ninaweza Kuzaa na Sugu Ana Mbegu Nzuri:-Faiza Ally

Mwanadada mjasiriamali amabe pia ni bongo movies faiza ally amefunguka na kusema kuwa hana mpango wa kuolewa na mwanaume aliyewahi kuzaa nae mtoto wake wa kwanza ambae ni mbunge wa Mbeya  mjini Mr Sugu lakini anaweza kuzaanae mtoto mwingine kwa sababu baba huyo ana mbegu nzuri.

Sugu ninaweza kuzaa nae mtoto mwingine kwa sababu ana mbegu nzuri sana kanipatia mtoto wa kike mzuri sana, ila sio kuolewa nae kwa sababu tulishashindwana hapo awali  sidhani hata kama tutawezana tena.

Faiza na Sugu walikuwa na watu wa kugombana katika mitandao kila siku kuhusu malezi ya mtoto huku mama huyo akisema kuwa baba hayupo makini katika kumhudumia mtoto wake, hata hivyo faiza amekuwa mtu wa kufunguka mambo mengi sana kuhusu sugu lakini sugu siku zote amekuwa kimya na hataki kuongea chochote kuhusu anayoyasema mzazi mwenzie.

 

Simuonyeshi Mwanaume Wangu Katika Media kwa Sababu Hatuna Malengo;-Faiza

Mwanadada Faiza Ally amefunguka ya moyoni na kuelezea kiundani sababu gani iliyomfanya hashindwe kuwa  namuweka wazi mpenzi wake ambae ni baba wa mtoto wake wa pili , Faiza ambae amekuwa akiweka picha isiyo taka kumuweka suara mwana ume huyo amesema kuwa sababu kubwa ni kutokana na kuwa hawana malengo yankusihi pamoja na mwanaume huyo lakini sio kwa sababu ni mume wa mtu kama watu wengi wanavyosema.

sipendi kumuonyesha kwa sababu hatuna malengo , hatutegemei kuishi pamoja wala kuoana kwaio i take my time ,when times come kuonyesha kwenye media  nitafanya hivyo.

Faiza anasema kuwa lengo kubwa ilikuwa nikuzaaa watoto wawili kabla hajafikisha miaka 35 na ndio maana amefanikiwa kwa hilo lakini swala la ndoa bado analifanyia kazi.

Faiza- Nampenda Sugu Ila Sio Kimapenzi

Muigizaji wa Bongo movie na Mfanyabiashara Maarufu Faiza Ally ambaye pia ni mzazi mwenza wa msanii na Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ amefunguka kuhusu uhusiano wao kwa sasa.

Siku chache zilizopita Sugu alitoka jela kwa msamaha wa Raisi alipokuwepo kwa miezi kadhaa baada yakukutwa na hatia ya kutoa kauli za uchi Hizi na kumchafua Raisi.

Faiza na Sugu wamekuwa na ugomvi au bifu la siku nyingi huku kwa upande wa Faiza Ikiwa ni kinyongo cha muda mrefu kwani alishawahi kuweka wazi kuwa bado anampenda mzazi mwenzake Lakini pia amekuwa haoni hatari kumwagia mvua ya matusi na hata kumdhalilisha mitandaoni.

Lakini hivi sasa tangu Sugu atoke jela Faiza ameonekana kuwa sawa na Sugu kwani amekiri kuwa anampenda Sugu ingawa hana hisia naye za kimapenzi.

Kwenye Interview aliyofanya na Bongo 5, siku ya Jumapili Kwenye uzinduzi wa filamu ya Mama ya Aunty Ezekiel, amefunguka haya:

Hisia na mapenzi ni tofauti, kwa sababu nampenda mapenzi ya kweli hayajawahi kufutika, i will always love him na kumpenda haina maana kuwa nina hisia naye. Nampenda ni ndugu yangu, baba watoto wangu”.

 

Faiza Amwaga Machozi Baada ya Kubeba Mimba Nyingine.

Mwanadada Faiza Ally amejikuta akiingia katika wakati mgumu baada ya kunasa mimba nyingine ya tatu huku mtoto wake wa kiume wa pili akiwa bado na umri wa miezi nane tu huku yeye mwnyewe akiwa anajipa moyo kuwa hawezi kupata mimba kwa sababu alikuwa akitumia vidonge vya kuzuia mimba.

Alikuwa akitoa taarifa juu ya swala hilo anasema kuwa Faiza  hakujua kama angeweza kubeba mimba kwa sababu alikuwa anatumia njia ya kuzuia mimba lakini kwa bahati mbaya laipata mimba huku akiendelea kunywwa dawa hizo ambazo zilikwedna na kuharibu mimba hivyo kuanza kuumwa bila kujua anaumwa nini.

Msemaji huyo anasema kuwa baada ya hapo alikwenda hospitali ambapo alikwenda na kugundua tatizo kuwa alikuwa na mimba iliyoharibka  kutokana na kutumia vidonge hivyo,alipofika hospitali waligundua tatizo hilo huku wakiona kuwa mimba ilikuwa imeharibika hivyo kuamua kumsafisha ili kumuweka sawa.

Baada ya kuongea na msemaji huyo  gazeti Moja   waliamua kumtafuta faiza ally mwenywe ilikuthibitisha habari hizo na ndipo aliposema haya”ni kweli nilikuwa mjamzito, unajua mimi na baba yake mtoto tunakaa mbalimbali kwahiyo inabidi tutumie dawa za kuzuia mimba, kumbe dawa tulizokuwa tukitumia hazikuwa za kuzia zilikuwa ni za kuharibu kabia kwaio hata ilipoingia kwa bahatimbaya iliharibiwa na dawa hizo, lakini haukutoka vizuri ndio nikawa najisikia vibaya  na kuumwa mpaka nilipokwenda hospitali.

Hata hivyo Faiza Ally alipoulizwa kama angekuwa tayari kuzaa kama mimba hiyo isingeharibika huku wakikariri amneno yake ya mwanzo kuwa watoto wawili wanatosha alijibu kuwa kwa sababu mimba iliingia kwa bahati mbaya hasingeweza kuitoa hata kidogo kwa sababu hawezi kufanya hivyo.

 

Faiza Ally Amchekelea Wema Sepetu

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara maarufu Faiza Ally ameshindwa kuzuia hisia zake na kuchekelea baada ya Wema kupata ubalozi wa Star Times siku ya jana.

Siku ambayo Zari alikuja Tanzania baada ya kupata ubalozi wa bidhaa mbili tofauti Faiza alitoa povu zito na kulalamika makampuni hayo kwa nini yametoa nafasi hiyo kwa mtu ambaye sio Mtanzania.

Faiza Ally alilalamika kwa nini wanatoa ubalozi kwa mtu ambaye ni Mganda halafu wanaacha mastaa kibao ambao ni Watanzania ambao wanaweza kabisa kufanya jukumu hilo.

Siku ya jana Wema Sepetu na wasanii wenzake kadhaa wamelamba dili nono kutoka Kwenye kampuni ya Star Times na kwa kuwa mabalozi wao wote waliowachagua ni Watanzania Faiza amechekelea uchaguzi wa Wema Sepetu.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Faiza amemuandikia ujumbe huu Wema wa kumpongeza:

 

Faiza Ally Akiri Kumlilia Sugu Gerezani, Asema Penzi la Kweli Halifi

Mwanadada Faiza Ally amefunguka na kuonyesha hisia zake baada ya mtoto wake wa kike aliyezaa nae kipind akiwa katika mahusiano ya kimapenzi na mbunge na msanii wa hip-hop Mr Sugu  kutuma ujumbe na zawadi ya chocolate kwa baba yake huku yeye mwenyewe akiwa hajui kama mtoto wake alikuwa anadhamilia kutuma zawadi hiyo kwa baba yake.

Akielezea kwa uchungu, faiza ali anasema kuwa mtoto wae huyo amemliza sana na ameamini kuwa penzi la kweli kwa Sugu kutoka kwake na familia yake halkiwezi kuisha hata kama walishgaachana kitambo.

Nimeumia na kujikuta nikilia baada ya baba sasha kupokea zawadi ya chocolate kutoka kwa mwanae  akiwa gerezani, nimeumia sana na nimeimagine hali hiyo aliyokuwa nayo  na kama ningekuwa mimi maana nimeona ni kama movie.hata sikujua kama chocolate alizokuwa akizifungasha zilikuwa zikienda kwa baba yake, nalia na wala sikuwahi kujua kwamba kuna siku nitakuja kulia kwa sababu ya baba sashatena kwa uchungu.uwiii jamani kweli mapenzi ya kweli hayajawahi kuisha  dah!dunia ina uchungu wa kila rangi,@sashadesderia pole mamy labda unakuwa humaanishi kile ninachomaanisha mimi, au haujui uzito lakini kama mzazi imenigusa sana kutoka moyoni.

Faiza Ally Alilia Umoja na Ushirikiano Kwenye Bongo Movie

Muigizaji wa Bongo movie Faiza Ally amefunguka na kuendelea kulia na Bongo movie huku akiwa sihi wasanii wenzake wazidishe umoja na ushirikiano baina yao.

Faiza Ally ameongea hayo huku akilihusisha tukio la kusikitisha lililotokea siku chache zilizopita baada ya kifo cha Agnes Masogange na ushirikiano wasanii wote walionyeshana.

Faiza amewataka wasanii wa bongo movie kuwa na umoja na ushirikiano kwenye sanaa na kufanya filamu kama walivyokuwa kwenye msiba ambapo amesisitiza kama Ikiwa hivyo basi ni wazi kuwa sanaa hiyo itafika mbali.

Faiza alifunguka hayo kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo aliandika ujumbe huu:

Tunaishi kwa kujifunza na mara nyingi mitazamo ya nje sio halisi, naomba nimpongeze IreneUwoya kwa kuwa rafiki mwema a special kipindi hiki, nimemuona akishiriki na kwenye utulivu sana yaani kasimama kama rafiki na hivi ndio inavyo takiwa, yaani jambo linapo kufika la mtu wa karibu sio kulia sana au kupoteza fahamu lazima usimame ujue hatma ya mwenzio kwanza.

Nahisi Bongo Movie tuna vitu vikubwa sana wote kwa pamoja lakini sijui tunakosea wapi, maana kwa ushirikiano huo huo wa msibani, urudi kwenye kwenye kazi naamini kuna hatua kubwa sana tutapiga, nisema tu mpo vizuri sana, nyinyi ni wa maana sana“.

Agnes Masogange alifariki dunia Ijumaa iliyopita katika kituo cha Huduma za Afya cha Mama Ngoma kilichopo Mwenge jijini Dar ambapo jana aliagwa katika Viwanja vya Leaders na kusafirishwa kwenda kwao Mbeya ambako alizikwa jana Aprili 24, 2018 kijijini kwao Utengule, Mbalizi

Wastara Ametaja Sababu Zilizomfanya Kuolewa na Kuachika Ndoa Tatu

Muigizaji wa Bongo movie Wastara Juma au maarufu kama Wastara Sajuki amefunguka na kuweka wazi sababu zilizomfanya mpaka hivi sasa awe ameolewa na kuachika katika ndoa tatu tofauti.

Wastara alifunguka hayo alipokuwa mgeni maaalumu katika Tamasha la Single mothers ambalo ni tamasha lililowakutanisha wamama wote wanaolea watoto wao wenyewe bila msaada wa Baba wa watoto kwa lugha nyingine ni Single mothers.

Wastara  alisema kuwa, siri kubwa ya ndoa zake kuvunjika ni kutokana na kukosekana kwa maelewano ndani ya nyumba na siyo kwamba huwa anapenda kuachika.

Unajua kuna vitu ambavyo ningevikubali kuvifanya nilipokuwa ndani ya ndoa, ungekuta sasa hivi nimeshakufa hivyo kuolewa na kuachika siyo kupenda, bali nilishindwa kukubaliana na mambo ambayo nilikuwa ninalazimishwa kuyafanya”.

Tamasha hilo la Single mothers lilifanyika katika hoteli ya De Mag Mwananyamala na liliandaliwa na msanii wa Bongo movie Faiza Ally kwa ajili ya kuwakutanisha wamama wote ambao ni Single mothers ili kuzungumzia mambo mbali mbali na kupeana ushauri.

Faiza Aja na Kampeni ya Single Mothers ,Ni Kwa Wamama Wenye Majukumu ya Kulea Watoto Peke Yao

                                                         

Mwanadada Faiza Ally ambae pia ni mfanya baishara maarufu bongo amekuja na kampeni ya single mothers itakayowakutanisha wanamama wanaolea watoto wakiwa peke yao bila kuwa na baba zao.faiz ameamua kufnaya hivyo ili kukutana na wanawake wanaobeba majukumu ya familia wakiwa kama mama na pia wakishika nafasi ya baba ambao wanapatikana wengi sana katika jamii zetu.

Akiwa kama mmoja wa wanawake hao kutokana na kulea mtoto wake wa kike peke yake kwa muda mrefu huku ikisemekana kuwa baba wa mtoto wake muda mwingi alikuwa akikataa kutoa matunzo kwa mtoto wake anaalika wanawake wengine kuja katika siku hiyo ya kukutana kwao ambapo itafanyika april 7 mwaka huu na kuongea matatizo yanayowakabili.

 

 

Faiza Ally Amtolea Povu Zito Gabo Adai Amechelewesha Mafanikio Yake

Msanii wa Bongo movie Faiza Ally amemtolea povu zito staa wa Bongo movie Gabo na kudai amemfelisha na kumkosesha kupata mafanikio aliyoyategemea.

Siku ya Jumapili kwenye Tuzo za Sinema Zetu International Film Festival (SZIFF) Gabo aliibuka kidedea na tuzo tatu ikiwemo msanii bora wa kiume  na kupelekea watu kadhaa kumpongeza huku wengi wakisema amestahili ushindi Ule.

Lakini Faiza amejitokeza na kumpongeza Gabo Lakini pia amemtolea povu zito huku akimtuhumu kwa kumfanyia dhuluma ambayo imemfanya apoteze hela na jitihada zake kurudi nyuma na kushindwa kupata mafanikio.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Faiza amemtolea povu zito sana Gabo:

 

 

 

Faiza: Ina Maana Watanzania Wote Hamkuwaona Mpaka Mkampe Dili Zari

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara maarufu Faiza Ally amerudi tena Kwenye headlines baada ya kutoa povu zito Baada ya Zari kutangaza kama balozi mkuu wa bidhaa za Softcare.

Siku ya jana Zari pamoja na kampuni ya Softcare walifanya mkutano na waandishi wa Habari ambapo walimtangaza Zari kama Balozi wa kuuza Bidhaa hizo ambazo ni pampas za watoto.

Lakini dili hilo lilizua minong’ono kutoka kwa watu hasa kwa sababu kampuni ni ya Tanzania lakini Zari ni Mganda anayeishi nchini South Africa kwaiyo inakuwaje waache mastaa wote wa hapa Tanzania waende Uganda.

Faiza alitoa povu zito juu ya hilo na kuihoji kampuni hiyo kwa nini imewaacha wanawake wengine wengi ambao ni mastaa hapa Tanzania ambao nao wengeweza kufanya kazi hiyo na kumchukua mtu ambaye hata sio Mtanzania.

Kupitia ukurasa wake wa instagram Faiza alitoa povu hili:

Hii sio mara ya kwanza kwa Watanzania kulalamika baada ya Zari kupewa Dili la kutangaza bidhaa za Tanzania alishawahi kuwa balozi wa Danube na Vodacom.

Sikuwahi Kuwaza Kuwa Single Mother:-Faiza Ally

Msanii wa Maigizo nchini faiza ally amefunguka na kusema kuwa katika maisha yake ya ukuaji hakuwahi kuwaza kuwa single mother hata siku moja .Faiza anasema kuwa hata baada ya kupata mtoto alikuwa akijiuliza sana ni kwa sababu ya mwanaume ndio maana anaishi maisha ya kuteseka.

Katika Ukurasa wake wa Instagram Faiza Ally aliandika kuwa amekuwa katika wakati mgumu sana kuwa single mom lakini bado anajifariji kuwa ni bora kuliko mke.

Wakati nakua sikuwahi kuwaza kuwa single mom, lkn kutokana na misimimo yangu wanaume wajinga hawakunielewa nikajikita ktk kujitegemea, baada kuwa mama nikawa najiuliza ni kwa sababu tu ya mwanaume au baba mtoto ndio niishi maisha nisiyo yataka , nikaondoka nikiwa nauchungu mwingi mno lkn nikasema maisha yangu ni bora kuliko kuwa mke! Nikapitia mengi sana haikua rahisi lkn Leo nimesimama imara kwa sababu niliamua kuchagua maisha ninayo ishi kwa hiari ! Nilipita wapi na nikavuka vikwazo vyote ????? Njoo nita share stori yangu na wewe kuwa single mom sio mwisho wako ! Kuna maisha zaidi ya kukaa usipo stahili ! JUA THAMANI YA UANAMKE WAKO BILA KUJALI WANAO BWEKA NJIANI“.

 

“Natamani Ningekuwa na Mabwana Sita Ili Mmoja Aninunulie Simu Maisha Yangu Yaendelee”- Faiza Ally

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara maarufu kwenye mitandao ya kijamii Faiza Ally amefunguka kuhusu kipindi kigumu anachopitia baada ya simu ya yenye thamani ya milioni tatu kushikiliwa na polisi kwa zaidi ya miezi mitatu.

Miezi michache iliyopita Faiza aliacha umma wa Watanzania midomo wazi baada ya kuamua kuanika picha yake mtandaoni akiwa uchi wa mnyama Leba wakati anajifungua mtoto wake wa kiume.

Baada ya kusambaa kwa picha hiyo Faiza alitakiwa kuwasili kituo cha polisi mara moja kwani iliangaliwa kama ni picha ya uchi na ni kinyume na maadili ya Kitanzania na alipofika kituoni hapo simu yake ilichukuliwa kama ushahidi.

Faiza leo kaamkia Instagram kulalamika juu ya suala hilo na ameandika maneno yafuatayo:

Kama kuna siku nimeamka na maumivu makali ni leo, leo nimetamani ningekuwa mzungu niishi kwenye nchi zenye haki za binadamu maana kuna wakati unaonewa kwenye nchi yako! Huu ni mwezi wa tatu tangu polisi wachukue simu yangu iphone 7+ yenye thamani ya shilingi milioni 3 inaniuma sana naenda kuripoti polisi sahivi nimepewa wiki mbili mbili kisa picha yangu ya leba wanahesabu kama pornography, Nimewaeleza polisi changamoto ninazopitia kwa kukosa simu mimi ni mfanyabiashara shughuli zangu zote zinategemea ile simu kuna emails contacts hata picha za biashara maisha yangu bila hiyo simu ni magumu mimi ni kama wa watoto wawili  mimi ndio nilipe ada ya mwanangu, kodi ya nyumba na maduka, ugali wa watoto ninunue”.

Lakini pia Faiza ametamani angekuwa na mabwana hata sita wamsaidie kununua simu mpya:

Nimewaza mpaka nimetamani ningekuwa na mabwana kama Sita hivi ili mmoja aninunulie simu niendelee na maisha yangu najitahidi nisimame bila mabwana lakini wakati mwingine wanawake tukizidiwa hakuna namna sasa hivi sio sawa mnakuwa kama mnarudisha juhudi zangu nyuma naomba mtoe huku ili maisha yaendelee”.

 

“Nimekuja Mpaka Marekani Kufanya Mapenzi na Baba Watoto Wangu” Faiza Amtolea Povu Mwanaume Aliyemtongoza

Faiza Ally ambaye ni muigizaji wa Bongo movie na mzazi mwenza wa Mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ ameibuka na jipya leo hii baada ya kumwaga povu la aina yake kwenye mtandao wa kijamii.

Faiza amemtolea maneno mazito mwanaume mmoja ambaye ni shabiki anayemfuatilia kwenye mtandao wa Instagram ambapo Faiza amedai mwanaume huyo amekuwa akimtaka kimapenzi na kutaka kumzalisha.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Faiza aliweka picha ya mwanaume huyo na kuandika maneno haya:

Nikiwaonyesha meseji za Whatsapp na Dm za huyu fal* mnaweza mkatambua kuwa muonekano na utu ni vitu tofauti sana. Sasa Malaya wa kiume ni hivi hizo nasty meseji zako ni za kunivunjia heshima yangu pumbavu wewe! Nataka kukwambia wewe hivii na mafala wengine wote kwamba sizalishwi na mtu yoyote hasa mwenye sura ngumu kama yako halafu ninapo posti picha zangu haina maana ninaposti ili nitongozwe kwa taarifa tu hapa nipo na bonge moja Handsome all the way kutoka Marekani kuja kufanya Mapenzi na mimi tu na ni baba watoto wangu sasa sitafuti bwana of course nina bwana na nikitaka mwingine nitapata lakini sio mbaya kama wewe. So kuanzia sasa stop sending your stupid messages on my DM na WhatsApp no yangu ni kwa ajili ya biashara sio kwa ajili ya wapumbavu kama wewe! IDIOT”.

 

Faiza Amshauri Diamond Kuachana Na Zari Ili Apate Muda Wa Kula Ujana.

Baada ya kuenea kwa tetesi kuwa msanii mkubwa wa muziki bongo na mzazi mwenzie Zari The Bossy wanawezekana kuwa katika mgogoro mzito kutokana na tetesi zinazoenea kuwa msanii huyo kwa sasa anatoka kimapenzi na video queen Tunda , Faiza Ally amemshauri Diamond kuachana na stress za kuachana na mzazi mwenzie na kama anataka kumuacha amuache tu kwa sababu yeye bado ni kijana sana bado anahitaji kula ujana.

Faiza anamwambia Diamond kuwa aache kujibebesha mizigo ya kuwa na familia wakati yeye bado ni kijana na anahitaji kutumia ujana wake vizuri kabla umri wake wa kujibebesha majukumu haujafika.

Diamond ni kijana mdogo sana anahitaji kuhave funny na watoto wenzie sio wadada watu wazima, lazima tuangalie watu wa kutembea nao.go baba enjoy the World have funny ndio useto down.jiachie uwe huru ikibidi usiwe na mahusiano kabisa.bado ujaona Dunia hata robo, wewe ni star ela ipo . there is a lot to see nasema with a clean hate no hate  kwa zari na kwa yoyote.

Sio kwa mara ya kwanza Faiza amekuwa akitoa ushauri kwa Diamond kutokana na matatizo yanayomkumba hasa kwa mambo ya mahusiano na jinsi wanawake alionao katika mahusiano wanavyokuwa wanampelekesha.

Itakuwa ni mara ya pili sasa Diamond na Zari wanaingia katika mpasuko wa kimapenzi baada ya kuwa natetesi nyingi zinazokuwa zikisambaa kwamba mwanaume huyo yupo katika mahusiano ya kimapenzi na watu wengine.Mara ya kwanza ilikuwa Hamisa Mobeto na sasa ni mrembo Tunda.

Wizara Ya Afya Waongelea Picha Ya Utupu Ya Faiza Ally

Baada ya kusambaaa kwa picha ya msanii wa bongo movie Faiza Ally ikimuonyesha yupo leba akijifungua na yeye mwenyewe akionekana kusherekea kutimiza kwa miezi minne ya kujifungua mtoto wake huyo wa kiume wizara ya afya waongelea swala hilo.

Faiza Ally ambae baada ya picha hiyo kupostiwa katika ukurasa wake wa Instagram watu wengi walionekana kutokupendezwa na kitu hicho na kujia juu alionekana kutokujali maneno ya watu  na hata kuingia katika ugomvi na baadhi ya wasanii wenzie kutokana na swala hilo,Hata hivyo picha hivyo ilifutwa baada ya muda mfupi kuwekwa na wamiliki wa mtandao wa instagram kutokana na kuripotiwa kuwa ilikuwa haina maadili kwa jamii na kuwa ilikuwa ikiwadharirisha wanawake.

Kampuni ya  GPL iliamua kuwatafuta wahusika wa afya kuzungumzia swla hilo ambalo kwa namna moja ama nyingine linawza kuwahusu ambapo juhudi za kumpata Waziri wa Afya zilishindikana lakini alipatikana msemaji wa wizara hiyo Ndugu  Nsachris  Mwamwaja na kusema kuwa sio vizuri kitendo kama kile kufanyika na wala hairuhusiwi kabisa , lakini pia hata katika maadili ya kitanzania jambo kama hilo haliwezi kuruhisiwa lakini kwa sababu ameposti katika mitandao ya kijamii, wizara inayohusika na mambo ya mitandao wanatakiwa kufatilia swla hilo.

Lakini kwa kuwa aliweka katika mitandoa ya kijamii basi  watu wa sheria za mitandao wanapaswa kufuatilia swala ilo kwa undani zaidi na kwa namna gani wanaweza kuthibiti swala kama hilo lisiweze kutokea tena. maana ni baya na halifai kabisa.

Hata hivyo mwenyewe Faiza Ally alipotafutwa kuulizwa kuhusu hilo alisema kuwa  kwa iyo picha kwake ni jambo la kawaida tu kwa sabau kila mtu anazaa na kuzaliwa tangu enzi za bibi zeu walikuwa wanafanya kitendo hicho kuhusu kujifunza bado sijajua maana bado sijachukuliwa hatua yoyote ila nina jivunia kwa sababu nimeingia leba.

Snura Ajikuta Matatani Baada Ya Kutoa Maoni Kuhusu Faiza Ally.

Baada ya Faiza Ally kuweka picha yake ya utupu ikimuonyesha alivyokuwa leba kipindi anamzaa mtoto wake wa pili wa kiume, baadhi ya watu walishikwa na hasira na wengine waliona kuwa kitendo hicho ni kitendo cha kudharirisha wanawake.Moja ya wasanii wa bongo movies anaefanya vizuri na anaesifika kwa kukata viuno anaejulikana kama Snura Majanga alifunguka na kuongelea swala la Faiza kutuma picha hiyo ni kudharirisha wanawake waliokwend leba tayari.

najua wengi watasema mbona na yeye hana adabu ,ila ukichunguza utagundua sehemu yangu ya kiuno tu ndio inayoniweka matatani, sinaga mambo mengi ya ajabu na sitakuja kuwa nayo kamwe.faiza hii umepitiliza TUSITIRI WANAWAKE WENZIO.. mwanamke anapotaka kuzaa hata kama ni barabarani utafutwa nguo na kuziba …leba ni siri yetu kuna mengi tunayafanya kule ambayo hayapaswi kujulikana nje,ni wengi wanashoot hata video lakini huwa inabaki kumbukumbu yao,na sio kuweka hadharani kila mtu akaona, inakuwaga aibu hasa kwa sisi wanawake, tunadharirika na kupoteza heshima kabisa ya mama, tunadharauliwa sanakwa mtindo huo.hata ndugu zetu wakija hawaruhusiwi kuingia leba zaidi ya manesi na  madaktari  na kama ni private ataruhusiwa kuingia mumeo tu, hizi ndizo tamaduni zetu tusijikatae sana tukaendekeza uzungu, mengine tuwaachie wenyewe sisi tubaki kuwa sisi.#niliemkwazapole -Aliandika Snura katika ukurasa wake wa instagram.

Lakini baada ya posti hiyo ya snura nae faiza aliamua kumjibu na kumjia juu snura kwa kuandika,

Video yako ya Chura na picha ya mimi leba bora nani,na mauno kutwa kucha kuhamasisha ngono kupitia musiki kweli, hebu jiongeze bwana nimezaa hiyo ni natural  mama, wanangu watakuwawasomi hawatakuwa na mawazo ya kipuuzi hivyo, kama za kwako na wengne…so stupid of you kama wewe na mziki wako tu  #postiyamudamfupi @snuramushi. Aliandka Faiza kumjibu Snura.

Hata hivyo posti hiyo iliyokuwa ikimuonyesha faiza yupo leba ilifutwa dakika chache baada ya kuwekwa kutokana na sheria za mitandao  na watu wengi kuiripoti picha hiyo kuwa haina maadili.

 

Faiza Ally: Gabo Sio Aina Ya Mwanaume Naweza Kuwa Naye

Mwanamitindo na muigizaji wa bongo movie asiyeishiwa vituko Faiza Ally ameibuka na kudai kuwa muigizaji wa bongo movie Gabo siyo aina ya mwanaume anayeweza kutembea naye wala kuzaa naye.

Baada ya Faiza kuzaa mtoto wake wa pili anayeitwa Li bila kumtambulisha baba mzazi wa mtoto huyo watu wengi wamekuwa wkijiuliza je ni nani baba mtoto wake? Moja kati ya watu ana ukaribu nao ni mwigizaji Gabo ambaye hata amewahi kuigiza naye filamu inayoitwa ‘baby drama’ na zaidi ya hapo amewahi kusema huko nyuma kuwa amewahi kuwa mpenzi wake hivyo watu wengi hasa mashabiki zake kwenye mtandao wa jamii instagram wamekuwa wakimtaja mwigizaji Gabo kuwa ndiye baba wa mtoto hadi kufikia hatua ya kumfananisha na kudai kuwa wanafanana.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Faiza alifunguka kuwa Gabo sio baba wa mtoto wake na wala hajaona mwanaume wa kutembea naye Tanzania kwa hivi sasa.

Ngoja niwaambieni ukweli kuhusu Gabo naona watu wengi mmeamini kabisa kuhusu Gabo! Ni hivi tulikua na kipindi cha Family love kinachorushwa na Clouds Tv na mimi na Gabo ni wanafamilia na mtoto wangu Li ilitakiwa akizaliwa iwe moja kwa moja familia ya ukweli hata ile posti niliyosema kama Gabo ndiye baba wa mtoto ilikuwa ni kukitafuta kipindi namna ya kujulikana, ukweli ni kwamba mimi na Gabo kwanza ni marafiki, pili ni kaka na dada, tatu ni tumefanya kazi mbili pamoja kwa hiyo katika mapenzi mimi na yeye hatujawahi wala hatutowahi zaidi ni mtu mwenye familia yake ana mke na watoto siwezi especially kwa mtu maarufu! kwa hiyo naombeni mtoe fikra zenu mana naona naitwa mrs Gabo na mtoto wangu juu mnamsema ni wake! hapana si wake. Mimi sina bwana Tanzania niko nalea tu halafu  pia kuwa na mtanzania kwa sasa hapana labda awe na quality ninazo zitaka mimi lakini bado sijaona”.

Alimalizia kufunguka Faiza ingawa mpaka sasa amegoma kumuweka wazi baba wa mtoto wake kwa sababu zake binafsi mwenyewe.

Faiza Ally: Sugu ni Mwanaume Ambaye Hajielewi Sina Muda Wa Kumnyenyekea

Mwanamitindo na muigizaji Faiza Ally amefunguka tena kuhusiana na uhusiano wake na baba wa mtoto wake wa kwanza Mh. Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ Mbunge wa Mbeya Mjini.

Faiza na Sugu wamekuwa katika mabishano ya muda mrefu sana kuhusiana na malezi ya mtoto wao huku Faiza amemshtaki Sugu kwa kukataa kutoa fedha za matunzo ya binti yao.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram amefunguka yafuatayo;

“Kuna wanaume wapumbavu sana mimi nitapigana mwanangu atakua lakini kumbuka sina cha kupoteza mtoto atakapo kuwa wewe ndio utakua umepoteza muda wa kumtunza mwanao kwa sababu ya kuni punish mimi na ujinga wangu! Lakini mimi ntakua nimetimiza majukumu yangu kama mzazi na huenda matusi yangu ndio yananipunguzia stress kwa namna fulani ili maisha yaendelee….sasa weweendelea kunikomesha siku hazigandi”.

Pia Faiza aliendelea kufunguka kwa kulalamika kukerwa na kilichotokea baina yao;

“Ila tu ujue nikiwa najisikia ntakuchamba tu mpaka ntakapo choka na hata nikiacha  ntakua nimeacha kwa sababu nimechoka lakini sio eti ni ache ndo umtunze mwanao, mtunze ndo niache kama humtunzi siachi nikijisikia nakupa za uso mpaka uelekee na usipo elekea basi lakini siwezi kukunyenyekea mpaka nakufa”.

 

Faiza Ally: Diamond Bado Kijana Mdogo Hayupo Tayari Kuoa

Tangu jana kumekuwa na tetesi kwenye mitandao ya kijamii ya kuwa Zari na Diamond wameachana habari hizo zilisababishwa na ujumbe alioweka Zari na kitendo chake cha kufuta picha zote za Diamond kwenye ukurasa wake wa Instagram, hii imetokea siku chache tu baada ya Zari kumsamehe Diamond baada ya kuzaa na Hamisa Mobetto ambapo watu waliamini wamesameheana na yameisha.

Muigizaji na mwanamitindo Faiza Ally amefunguka na kudai kuwa hadhani kuwa Diamond yupo tayari kuoa na kutulia chini na familia kwasababu ya umri wake kuwa bado mdogo.

Kwa kupitia ukurasa wake wa Instagram Faiza ameandika yafuatayo;

“Diamond kijana mdogo sana anahitaji kuhave fun na watoto wenzie na sisi wadada tuangalie watu wakutoka nao…..nenda baba have fun ndo usettle down….jiachie uwe huru ikibidi uwe na mahusiano bado hujaiona dunia hata nusu wewe  ni star, hela ipo there is a lot to see. Naongea kwa roho nyeupe sina chuki na Zari au kwa yoyote nimezurura sana duniani kabla ya kuzaa na kutulia jiachie bwana life is today”.

Aliandika Faiza ambaye ameshawahi kuweka wazi kuwa yeye ni shabiki wa Zari.

Faiza Ally: Alikiba Anafanya Muziki Mzuri Kuliko Diamond

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara Faiza Ally ameibuka tena na kudai kuwa anauelewa zaidi muziki anaofanya Ali Kiba kuliko muziki anaofanya Diamond Platnumz.

Katika mahojiano aliyoyafanya na TBC Faiza alidai kuwa wasanii wote wawili wanajitahidi katika kufanya muziki kwani wana vipaji tofauti kwani mmoja ni muimbaji na mwingine ni mburudishaji.

Faiza aliendelea kusema:

“Kwanza kati ya muziki wa Diamond na Ali Kiba , naupenda zaidi muziki wa Ali Kiba, muziki wake ni mzuri kuliko Diamond, kwani Diamond ni ile full entertainment ukimwangalia tu unatabasamu lakini Ali Kiba ana muziki mzuri. Nikizungumzia mtu aliyeutoa mziki akaupa heshima mpaka akampa changamoto Kiba na yeye akasimama mpaka tukaanza kumuona kwenye hali ya tofauti ni Diamond”.

Faiza ni moja ya watu ambao msimamo wake umekuwa ukibadilika kuhusu nani ni bora kati ya Diamond na Ali Kiba kwani mara kwa mara amekuwa akibadilika kwani leo anaweza akasema Diamond na kesho atasema kuwa ni Ali Kiba.

Lakini yote kwa yote ushindani huu ndo unafanya muziki wetu kuwa bora zaidi kwani Ali Kiba asingekuwa na changamoto kutoka kwa Diamond asinge kuwa bora alivyo sasa na hivyo hivyo kwa Diamond asingepata changamoto kutoka kwa Ali Kiba basi asingejitahidi kutupa muziki mzuri zaidi tunaopata leo hii.

Sugu Avunja Ukimya Juu ya Swala la Malezi ya Mtoto

Mheshimiwa Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ Mbunge wa Mbeya mjini amevunja ukimya na kufunguka kwa mara ya kwanza juu ya shutuma zinazomkabili  dhidi ya mzazi mwenzie Faiza Ally.

Faiza amekuwa akitumia mitandao ya kijamii kumshutumu Sugu kwa kukataa kumlea binti yao mdogo Sasha. Baada ya juzi kumsema Sugu kuwa hamjali mtoto wake na kukataa kumlipia mtoto huyo ada ya shule hadi kufikia hatua ya Sasha kurudishwa nyumbani.

Kwa mara ya kwanza Sugu kupitia ukurasa wake wa Instagram alifunguka na kusema anamlipia ada binti yake huyo lakini mwenye matatizo ni mama yake kwani humkataza kumuona, aliandika yafuatayo juu ya tuhuma hizo:

“Huwa sipendi kuposti hivi vitu lakini imenibidi,  hizi ni bank slips za ada ya mwisho niliyolipa kwaajili ya Sasha na ilikuwa mwezi huu wa tisa nimuanzishe shule ya Feza Nursery pale Mikocheni, lakini from no where mama yake ghafla akanizuia na kusema hahitaji nilipe ada na kunizuia nimsomeshe tena Sasha! Na kwamba ana uwezo wa kumsomesha mwenyewe shule yoyote anayotaka na ndo kumpeleka huko Hazina international ambako pia hata hivyo nilishaanza kuwasiliana na uongozi ili niendelee tu kulipa ada hata kama nimepigwa marufuku kumuona mwanangu bila sababu. Hivi kama nyie mngefanyaje?

Hata hivyo mara baada ya kusema hayo Faiza alikuja juu na kumuita Sugu muongo na amewahi kulipa ada mara mbili tu tangu mtoto wao aanze kusoma na miaka yote hiyo Faiza ndo alikuwa analipa ada.

Faiza Ampongeza Diamond Kwa Kumkubali Mtoto Wa Hamisa

Mwanamitindo Faiza Ally amefunguka na kumpongeza Diamond kwa hatua aliyochukua ya kwenda kwenye vyombo vya habari na  kuweka wazi kuwa yeye ndiye baba wa mtoto wa Hamisa. Kwa muda mrefu katika mazingira mbalimbali Diamond alikanusha kuwa name uhusiano na Hamisa name pia kuzaa naye. Leo kwa kupitia kipindi cha Leo Tena Diamond amekubali kuwa shetani alimpitia na amewahi kuwa name mahusiano ya kimapenzi na Hamisa.

Baada ya mahojiano hayo kuruka hewani mwanadada Faiza kwa kupitia ukurasa wake wa Instagram alifunguka new kuandika yafuatayo:

“Nasikiliza Clouds FM Naseeb nakupenda wewe ni mwanaume ea maana  saana sema wanawake wa Uswahilini ni kama ile methali ya Hamisi, yaani unaweza ukamtoa Hamisi shamba lakini usilitoe shamba kichwani kwa Hamisi #hope hutarudia Tena ujinga wako”.

Inasemekana Kuwait suala la Diamond kumkubali mtoto huyo na kumuhusumia limemgusa sana Faiza kwa sababu halo aliyonayo saivi ni Kuwa baba wa mtoto wake hamuhudumii mtoto wake ipasavyo ndio maana ameona kitendo alichofanya Diamond ni  cha kishujaa.

Faiza Amtolea Povu Mzazi Mwenzie Sugu

Mwanamitindo na mlimbwende Faiza Ally asiyeishiwa na vituko mtandaoni ameingia katika ugomvi mwingine na mzazi mwenziye Mh. Joseph Mbilinyi “Sugu” mbunge wa Mbeya kuhusiana na malezi ya binti yao Sasha. Kupitia ukurasa wake wa instagram Faiza amefunguka yaliyo moyoni mwake mara baada ya kumpeleka mtoto wake shule na yeye kurudishwa getini kwa sababu ya kushindwa kulipa ada.

Faiza ameandika:

“Na hasira zangu za shule nazirudisha kwake kwa sababu na yeye ni muhusika kama mzazi! Kwanza kabisa nakuita mbunge mpumbavu sana! Inakuaje serikali inakupa madaraka makubwa kiasi hicho? Wakati unashindwa kuendesha maisha ya mtoto wako mmoja tu? Mbunge gani usie jua mwanao analipaje ada? Mbunge gani usiyejua mwanao analala wapi? Mbunge gani usiyejua mwanao ana mahitaji anakula nini? pumbavu wewe unaendekeza mbunge tu na bangi na konyagi? how? Can you call yourself mheshimiwa? Kwa heshma ipi? Hivi wewe ulilazimishwa kunipa mimba? We si ulikuwa unalialia unataka mtoto f*** wewe? Ulinizalisha ili unikomoe? Na kwambia hustahili hata kuwa na rafiki kama Msigwa, Lema sio wenzako u belong kitaa utarudi mtaani there is where u belong unaona wenzako wametupa watoto? Huna hata haya huoni hata mfano kwa Prof. Jay kwa mwanae? how can you punish Sasha for no reason ! Shame on you Joseph! na sasa nakushtaki naona punda haendi  bila mzigo! Eti Jay Z and Obama ndo role models wako how? huoi hao ma role models wako na familia zao wakoje? Sielewi how did i fall in love wewe sijielewi how did i fall in love na inakuaje bado nakupenda mtu kama wewe. Sasa naiomba serikali iingilie kati haya maswala kati ya viongozi wasiojali watoto wao!  I hate you baba jina na nikifa najua ni wewe adui wa maisha yangu!.”

Faiza Ally: Tanzania nzima na East Africa tunatakiwa tumpenda Diamond sana

Faiza Ally amedai kuwa ni sharti Tanzania na Afrika Mashariki nzima kumpenda Diamond. Mrembo huyo aliandika ujumbe wake kwenye mtandao wa Instagram.

Ally alimpigia kifua Diamond kwa kusema kuwa muziki wa Tanzania haukua na ushindani kabla ya Diamond kuingia kwenye game.

“Hivi hamjawaji kujiuliza kwamba toka zamani kabla ya Diamond kulikua na mziki mzuri lkn hakujawahi kuwa na ushindani kama changamoto alio leta Diamond kwenye game. Hivi mnajua kwamba Tanzania nzima na East Africa tunatakiwa tumpenda Diamond sana ???? Hivi hamjawaji kujiuliza kwamba toka zamani kabla ya Diamond kulikua na mziki mzuri lkn hakujawahi kuwa na ushindani kama changamoto alio leta Diamond kwenye game , sasa nasema hivi mziki mzuri peke yake hautoshi na akili kubwa inahusika , unapo kuwa huna akili ktk unalo lifanya ni sawa na mwanamke mzuri hlf hajielewi…. Leo hii kwa u star wenye akili alio uleta Naseeb wazazi wengi wanaona fursa ya mziki kupitia Diamond tofauti na miaka ya zamani, mziki ulikua unaonekana kama sio kazi lkn Leo mziki unaendesha familia nyingi, hata mm ningependa mwanangu awe mwanamziki mwenye mafanikio kama Diamond , sasa nasema hivi ku mpenda Diamond ni amri sio ombi,” aliandika Faiza Ally.

Aliandelea kwa kusema kuwa Diamond ni kama Obama:

” Diamond ni kama Obama marekani kwa watu weusi , yeye alionyesha kuwa mtu mweusi ana uwezo kwenye siasa na Diamond tanzania kaonyesha mziki unalipa na msisahau katoa vijana wengi na bado wengine wamepata ajira kupitia yeye na naona watapata wengi zaidi ! Sasa nakuomba D ufungue music school basi tuwalete watoto wetu na wenyewe wapate mkwanja kama wako maana shule sio maisha pekee mention town na vipaji navyo ni sehemu ya mafanikio ktk maisha a special kwa maisha tunayo elekea , mm nakupendaga sana na zaidi ni jitihada zako kwenye kazi ! Keep it up dogo ? #ZILIPENDWA”

 

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.