Nandy Kupanda Steji Moja na Hamisa Mobetto

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Faustina Charles maarufu kama Nandy ametangaza habari njema kwa mashabiki Wake wanaokaa nje ya nchi kwani anatarajiwa kupanda steji moja na Hamisa Mobetto.

Nandy ambaye anafanya vizuri na ngoma yake ya ‘Aibu’ ameweka wazi kuwa mwezi huu baadae anatarajia kuungana na Hamisa Mobetto kwa ajili ya your yake ya nchini Marekani.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa Wikienda, Nandy ameweka wazi kuwa yeye na msanii mwenzake Aslay wanatarajia kuungana na Hamisa Mobetto nchini Marekani.

Natarajia kusafiri siku ya tarehe 25 mwezi huu kuelekea Marekani kwa ajili yakufanya ziara nikiwa na msanii mwenzangu Aslay na Hamisa kisha nitarudi Bongo tarehe 10, Desemba tukiwa wote watatu, pia hii kwangu itakuwa ni mara ya kwanza kufika huko kwa sababu sijawahi kwenda kabisa”.

Hamisa Mobetto amekuwepo nchini Marekani kwa zaidi ya mwezi sasa ambapo ameonekana akiwa anafanya matamasha katika majimbo mbali mbali katik nchi hiyo.

Nandy Atupwa Kando Kwenye Listi Ya Wasanii 29 Watakaoperfom Fiesta

Clouds Media Group limetangaza Listi ya majina 29 ya wasanii ambao wanatarajiwa kuperfom katika tamasha la Fiesta 2018 litakalofanyika siku ya Jumamosi katika Viwanja vya Leaders Club.

Kwenye orodha hiyo ndefu, wapo wasanii Kama Rostam, Weusi, Maua Sama, Wakazi, Ben Pol, Chege, Fid Q na wengineo, huku wasanii chipukizi nao wakipewa kipaumbele.

1. Weusi  2. Rostam 3. Fid Q 4. Wakazi 5. Rich Mavoco  6. The Mafik 7. Ben pol 8. Rosa Ree 9. Marioo 10. Barnaba  11. Billnass 12. Chege Chigunda 13. Dogo Janja 14. Msami 15. WhoZu  16. Mimi Mars  17. Lulu Diva  18. Zaiid  19.Mesen Selekta 20. Maua Sama 21. Tid 22. Qchief 23. Juma Nature 24.Jolie 25.Benson 26.Jay Melody 27.Mabantu
28.Brian Simba 29.Amber Lulu”.

Suala la kukosekana kwa Msanii Nandy ambaye yupo ndani ya THT limeshangaza watu wengi huku tetesi za chini ya kapeti zikidai kuwa huenda kitendo cha Nandy kuonekana akila bata na Diamond Platnumz Dubai kinaweza kuwa chanzo.

Baada ya tetesi nyingi kusambaa Baada ya jina la Nandy kukosekana Clouds wametoa kauli na kusema kuwa List nyingine ya kambi ya upinzani itatangazwa baadae

N.B kuna Listi ya kambi ya Upinzani bado.  Kama vipi Jumamosii hii tukutane Leaders Club. Kiingilio 10,000/- Ukinunua kwa Tigopesa master-pass QR, na shs 15,000 Kawaida!“.

Willy Paul sets the record straight about dating Nandy

Willy Paul has always flirted with female musicians he collaborated with. He made everyone believe he was dating Alaine before they dropped ‘I Do’ hit song.

The controversial gospel singer did the same thing with Nandy when worked together. The duo dropped ‘Njiwa’ which is the most successful collabo Pozzee has ever done. The song has garnered 6.6 million views on YouTube in just five months.

Brother and sister

Willy Paul opened up about his relationship with Nandy during an interview on Citizen TV’s 10 Over 10 last Friday November 16th.

Willy Paul performing on Citizen TV's 10 Over 10
Willy Paul performing on Citizen TV’s 10 Over 10

He dismissed claims that he was dating the Bongo songstress, Pozzee described his relationship with Nandy as a brother/sister kinda of relationship.

“Kuna a group of people that walikuwa wananizuia kuingia Tanzania but then God akaleta Nandy through na tukafanya song. Sahii inaelekea 10 million views so tunashukuru mungu sana kwa Njiwa. Other than that, hakuna kitu inaendelea kati yangu na yeye. Mimi na yeye ni kama ndugu na dada,” said Willy Paul.

 

Nandy Adaiwa Kumnyakua Bwana Wa Wema

Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri na kibao chake cha ‘Aibu’ Faustina Charles maarufu Kama Nandy amedaiwa kumchukua Mwanaume aliyekuwa kwenye mahusiano na muigizaji Wema Sepetu.

Gazeti la Risasi linaripoti kuwa Mwanaume mmoja anayejulikna Kama Rajabu ambaye ni mfanyabiashara wa Mwanza alikuwa ndio anamuweka Wema mjini lakini Baada ya skendo ya Wema na PCK kutokea inadaiwa bwana huyo alimtosa Wema na kuhamisha majeshi kwa Nandy.

Gazeti hilo linaendelea kuripoti kuwa mara tu baada ya mwanaume huyo kutua kwa Nandy alimpangishia nyumba Masaki jijini Dar na kumnunulia gari la kifahari aina ya BMW X 1 na pia siku ya birthday yake mwanaume alimwagia pesa chafu ukumbini.

https://www.instagram.com/p/Bp9dZByBMxh/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=pqpdgwd4nx78

Baada ya tetesi hizo Gazeti hilo lilimsaka Nandy ili kupata ukweli wake juu ya ishu ambapo alikana kabisa taarifa hizo na kukana kumjua jamaa huyo.

Mh! Waja wana mambo sana, kwanza niseme nashtuka wewe kuniambia mambo ya bwana wa Wema, mimi yule bwana alinipa kama milioni tano hivi nilipozihesabu na nilishangaa kwani sikuwa nikijua kuwa nitapewa pesa hizo lakini si mpenzi wangu, wala sijawahi kujua kama anatoka na Wema.

Ukweli ni kwamba nilimualika kwenye pati yangu akanipa pesa kama mlivyoona lakini sina uhusiano naye wa kimapenzi na wala gari hili hajaninunulia yeye, mimi nimejinunulia mwenyewe kwa kazi zangu tu. Kuhusu nyumba nimepangishiwa na mpenzi wangu ambaye siwezi kumtaja kwa sasa ila ni mtu maarufu tu.

Lakini Nandy alipobanwa zaidi kuhusu jamaa huyo alisema:

Alinipigia simu na kuniambia kuwa anataka kufanya biashara na mimi, akaniambia atakuja Dar, huwezi kuamini alikuja Dar na ikawa ndio imefika siku ya sherehe yangu ya kuzaliwa, nikamualika kwa bahati nzuri akaja”.

 

 

Nandy Amtaja Aslay Kama Msanii Alimtungia Nyimbo Kwa Ajili Ya Albamu Yake

Msanii wa muziki wa Bongo fleva nchini kutoka katika Nyumba ya vipaji Tanzania (THT) Faustina Charles maarufu kama Nandy amefungukia Albamu yake mpya.

Albamu mpya ya Nandy ambayo hivi sasa iko sokoni inaitwa ‘The African Princess” Kiowa ni albamu yake ya kwanza kuingiza sokoni tangu aanze Sanaa yake ya kimuziki.

Nandy ameweka wazi kuwa Albamu hiyo imemchukua Kama mwaka mzima kuiandaaa tu huku nyimbo zake akiandikiwa na msanii Kama Jay Melody na staa mkubwa wa Bongo fleva Aslay.

Kusema ukweli Albamu yangu imechukua muda mrefu kukamilika kwa sababu nimekuwa nikitungiwa nyimbo na wasanii Kama Aslay na Jay Melody”. 

Kwneye mahojino na kituo kimoja cha habari Nandy amefunguka haya kuhusu muziki wake na albamu yake hiyo:

Imenichukua mwaka mzima kutengeneza albamu yangu ili kupata Kitu kizuri hii imekuwa kwa sababu ya kusafiri kwa ajili ya kufanya shoo mbali mbali ambazo zimechukua muda wangu mwingi”.

 

Nandy Afunguka Baada Ya Kuonekana Tena na Billnas

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Faustina Charles ‘Nandy’ na msanii mwenzake anayefanya muziki wa hip hop William Lyimo ‘Billnas’ walirudi kwenye headlines tena na kuzua gumzo Baada ya kuonekana pamoja.

Gumzo hilo lilizuka wiki iliyopita Baada ya Nandy kiposti picha kwenye ukurasa wake wa Instagram ilimuonyesha akiwa pamoja na Billnas na msanii mwenzao Dogo Janja.

Baada ya kuposti picha hiyo maneno mengi yalisemwa ikiwemo tetesi as kwamba huenda wawili hao wamerudiana ama vipi huku baadhi ya mashabiki kuonekana kufurahia wawili hao Kuwa pamoja.

Kwenye mahojiano yake na Global Publishers Nandy alisema hana kinyongo kabisa Billnas kwani walishamaliza tofauti zao tangu zamani hivyo kwa sasa wao ni washkaji tu na hakuna kingine kinachoendelea kati yao.

Mimi na Bill sasa hivi ni washkaji tu, hakuna chembechembe yoyote ya mapenzi kati yetu, tulishaachana muda mrefu na kila mtu ana maisha yake, sioni tatizo kuwa naye karibu”.

Wawili hao walishawahi kuwa kwenye mahusiano siku za nyuma lakini walikuja kuachana na hata video yao ya faragha kusambaaa kwenye mitandao ya kijamii.

Nandy Azima Tetesi Za Kuwa Mjamzito

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva Faustina Charles maarufu kama Nandy amefunguka na kukataa kata kata tetesi zilizombaa Kwenye mitandao ya kijamii kuwa hivi sasa ni mjamzito.

Nandy ambaye hivi sasa anafanya vyema kabisa na ngoma yake ya ‘Aibu’ amekataa tetesi za kuwa hivi sasa amejazwa kibendi na Kigogo mmoja na kudai ni uzushi tu.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Nandy alisema watu huwa wanaamua tu kuzusha mambo yasiyokuwa na ukweli wowote ule ndani yake, ili mradi tu wafurahishe mioyo yao kitu ambacho kinaumiza.

Hizo tetesi zinazosambaa mitandaoni kwamba nina mimba siyo za kweli, ila naona watu wameamua tu kuzizusha ili wafurahishe mioyo yao, sina mimba jamani naomba waniache“.

 

Rapa Wakazi Kupita Njia za Nandy

Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayefanya miondoko ya kuchana (Rap) Wakazi ameweka wazi nia yake ya kufanya remix ya ngoma ya Msanii wa Bongo fleva Nandy.

Wakazi ameweka wazi kuwa yupo mbioni kutoa remix ya wimbo wa Nandy unaokwenda kwa jina la Aibu ambao unafanya vizuri kwa sasa kwenye chati mbalimbali za redio.

Siku za nyuma Utakumbuka Wakazi alifanya hivyo pia kwenye wimbo, Sijutii wa muimbaji Ruby ambaye anatajwa kuwa hasimu mkubwa na Nandy kimuziki kwa sasa. Pia Wakazi aliwahi kufanya refix ya wimbo wa msanii kutokea nchini Nigeria, Wizkid unaokwenda kwa jina laOjuelegba na kuipa jina la Natokea Dar .

Sina Urafiki Wowote na Billnas- Nandy

Msanii  wa muziki wa Bongo fleva anayefanya vyema na ngoma yake. Mpya ya ‘Aibu’ amefunguka na kuweka wazi kuwa hivi sasa hana Mahusiano yoyote na aliyekuwa mpenzi wake Msanii mwenzake Bill Nas.

Nandy na Billnas waliwahi kuwa wapenzi miaka ya nyuma wakaja kuachana lakini walipata fedheha mapema mwaka huu baada ya video yao chafu ya Kitandani kuvuja Kwenye mitandao ya kijamii.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Nandy aliulizwa kuhusu urafiki wake na Billnas na kama waliacha kuongea baada ya video yao kuvuja Nandy alifunguka:

Hatuna ushikaji kiukweli tangu kipindi kile tatizo lilipotokea, hatujawahi kuwasiliana hata kwenye simu, ila nakumbuka mara ya mwisho tulionana central kituo cha Polisi, kwa hiyo sidhani kama kuna kitu chochote cha kuongea, japo najua tukikutana lazima tutapiga stori, tutacheka na kufurahi pia“.

Lakini pia Nandy amesema kwa sasa hivi amepata mpenzi mwingine na kama Mungu akijalia, hivi karibuni atafunga ndoa.

Nandy Atangaza Ndoa na Mpenzi Wake Mpya

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Faustina Charles ‘Nandy’ amefunguka na kusema hivi sasa amepata mpenzi mpya na endapo Mungu atajaalia basi ndoa itafungwa hivi karibuni.

Kwenye mahojiano na Risasi Vibes, Nandy amesema kwamba kwa sasa hana ukaribu wa aina yoyote ile na msanii mwenzake, William Lyimo ‘Billnas’ ambaye pia amewahi kuwa mpenzi wake, baada ya matatizo yaliyowahi kutokea ya kuvuja kwa video yao chafu.

Nandy amesema kwa sasa hivi amepata mpenzi mwingine na kama Mungu akijalia, hivi karibuni atafunga ndoa.

Shemeji yenu yupo, tusubiri ndoa tu kama Mungu akijalia lakini siwezi  kutaja ni lini kwa sababu naweza nikataja halafu isifanyike, kwa hiyo sasa hivi namuomba tu Mungu iweze kutimia”.

Nandy amefunguka pia kuwa kwa sasa hana urafiki wowote na Billnas tangu sakata lao la video chafu lakini wakikutana wanapiga stori kawaida tu.

Nafurahi Kuona Wasanii wa Kike Tukiwa na Ushindani.

Msanii wa kike kwenye anga za bongo fleva Nandy amefunguka na kusema kuwa amekuwa akifurahishwa sana na kasi ya wasanii wenzake wa kike kwa sasa kutokana na kuwa na ushindani sana sio kama hapo mwanzo walivyokuwa wakisemwa kuwa wasanii wa kike wamekuwa wakibweteka.

Nandy anasema kuwa tofauti na ilivyokuwa hapo awali kuwa katika muziki kulikuwa kumetawaliwa na wanaume tu, sasa hivi kuna ongezeko kuba la wasanii wa kike na kumekuwa na ushindani sana kitu kinachotoa matumaini kuwa wanawake wameamka na kutambua kuwa hata wao wanaweza.

Nafurahi sana kuona wasanii wa kike wakishindana vipaji na wanaume  katika muziki ,kwangu nifaraja kubwa na kama tutaendelea hivi basi tutafika mbali.

 

Nafurahi Kuona Wasanii Wa Kike Tukiwa na Ushindani-Nandy

Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayefanya vyema na ngoma yake mpya ya ‘Aibu’ Faustina Charles maarufu kama Nandy amefunguka na kusema anapenda ushindani wa wasanii wa kike.

Nandy ameweka wazi kati ya vitu vinavyo mfurahisha Kwenye muziki huu wa Bongo fleva ni pale ambapo wasanii wa kike wa sasa wanavyoongeza kasi ya ushindani kwenye gemu.

Kutokana na kuwa na ongezeko kubwa la wasanii wa kike tofauti na miaka ya nyuma ambapo sanaa ilikuwa imetawaliwa na wasanii wa kiume na wasanii wa kike walikuwa wa kuhesabika.

Kwenye Interview aliyofanya na Gazeti la Dimba, Nandy amefunguka na kukiri kumekuwapo na ongezeko kubwa la ushindani kati ya wasanii wa kiume na wa kike, hali inayoongeza ladha ya muziki wao.

Nafurahi sana nikiona mwanamke mwenzangu anashindana kipaji na mwanamume, kwangu ni faraja kubwa, kwani tukiendelea hivi tutafika mbali”.

 

Nandy Atangaza Kuukacha Mziki Ukifika Mwaka 2020

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Faustine  Charles maarufu kama Nandy amefunguka na kuweka wazi kuwa ukifika mwaka 2020 ataachana kabisa na muziki.

Nandy ambaye aliingia kwenye muziki rasmi kuanzia mwaka 2016 Kupitia Nyumba ya vipaji THT na kutoa ngoma kali ambazo zimemuweka Kwenye ramani kama Msanii bora wa kike Tanzania ametangaza kuachana na muziki hapo baadae.

Kwenye mahojiano aliyofanya gazeti la Risasi Jumamosi, Nandy alisema ndoto yake ni kuwa mfanyabiashara mkubwa Bongo kwani ndiyo yalikuwa malengo yake pindi tu alipoanza kufanya muziki.

Wakati naanza kufanya muziki nilijiwekea malengo kwamba baada ya miaka mitano niache muziki ili niendeleze biashara zangu, hivyo namshukuru Mungu kwa sababu mpaka sasa nimeshatumia miaka miwili ambayo ni mwaka 2016 na 2017. Kwa hiyo utakapofika mwaka 2020 nitaacha muziki, ila siyo kama nitakuwa sitoi nyimbo hapana nitakuwa natoa lakini kwa mwaka mara moja ili niwe napata muda mzuri wa kusimamia biashara zangu”.

Hivi sasa Nandy anafanya vyema na wimbo wake wa ‘Aibu ambao pamoja na kwamba ni audio tu hauna video umeendelea kumuweka Kwenye ramani kama Msanii bora wa kike Kwenye Bongo fleva.

nady akiri video yake ya utupu ilimpa aibu.

mwanadada NaNdy anasema kuwa moja ya vitu vilivyowahi kumnyima amani na kumtia aibu ni ile video yake iliyosambaa ikimuonyesha yeye na Billnass wakiwa faragha na kusambaa sana katika mitandao ya kijamii .

Nandy ambae alikuwa katika mahusiano na msanii mwenzake Billnass  waliingia matatani siku za nyuma baada ya video hiyo kusambaa katika mitandao ya kijaimii kipindi ambacho Nandy alishakaaa sana kuhusu ukaribu wao na hata kusema kuwa hawakuwa na mahusiano yoyote.

hata hivyo  baada ya kusambaa kwa video hiyo wawili ho walitakiwa kuomba msamaha mbele ya umma kwa kosa hilo huku wakionywa na BASATA.

Nandy afunguka swala la kuacha muziki.

Moja ya wanamuziki wanafanya vizuri katika anga za bongo fleva Nandy amefunguka na kusema kuwa pamoja na kwamba amekuwa akifanya vizuri lakini alishawahi kujiwekea malengo katika hilo kuwa ndani ya miaka mitano basi tayari awe amekwisha fanikisha kila alichokuwa anataka kifanikiwe katika muziki.

Nandy anasema kuwa ndoto yake kubwa akiyonayo maishani ni kiwa mfanya biashara mkubwa sana lakini  haweiz kuacha sasa muziki kwa sababu alishasema atafanya muziki kwa mika ami5 na baada ya hapo ndipo ataendelea na biashara zake.

Mimi ndoto zangu ni kuwa mfanyabiashara mkubwa sana na hata wakati naanza kufanya muziki nilijiwekea malengo baada ya miaka mitano niache muziki na niendeleze biashara zangu na mpaka sasa nimeitumia miaka miwili (2016 na 2017) na mwaka 2020 ndiyo nitaacha muziki, Na sio kwamba nitakuwa sitoi ngoma hapana nitakuwa natoa sema kwa mwaka hata mara moja ha show naweza kuwa nafanya mara moja kwa mwaka ili nipate muda mzuri wa kusimamia biashara zangu” Ameyasema Hayo Nandy kuhusu kuachana na Muziki

Nandy Awahasa Wazazi Kupenda Kuhimiza Watoto Kuvaa Vitu vya Asili

Mwanadada Nandy ambae amekuwa moja ya wasanii wanaovaa sana nguo za sili na urembo wa sili kama vitenge na mabangili amefunguka na kusema kuwa kwa upande wake amekuwa aktika mazingira hayo na ndio maana inampa moyo kuendelea kufanya.

Nandy anasema kuwa wazazi wana nafasi kubwa sana ya kuwahimiza watoto wao kupenda vitu vya asili kama watakuwa wakiwakuza katika misingi ya kuvipenda kuliko kuwanunulia vitu tofauti na vile vya asili,

Akitolea mfano wake anasema kuwa tangu akiwa mtoto mama yake amekuwa akivaa mabatiki na vitenge na hata wao wamekuwa wakishonewa nguo hizo na ndio maana amekuwa akiona na kupenda kufanya hivyo.

Mneno hayo ya nandy yanakuja ikiwa ni kuelekea kilele cha tamasha la Urithi Festival linalotegemewa kufanyika mkoani Dodoma mwezi huu.

Mimi napenda sana kuvaa vitu vya asili na ndio maana mmekuwa mkiniona nashona shona,nimekuwa nikiona tangu nikiwa mdogo mamangu amekuwa akitushonea nguo kwaio nimekuwa nakiona na nikakipenda sana.

Nandy Awatolea Povu Wanaomsema Anabebwa Kimuziki.

Mwanadada Nandy amefnguka na kusema kuwa kuna baadhi ya watu wamekuwa wakimtuhumu na kumwambia kuwa amekuwa akibebwa katika muziki na baadhi ya watu na wala sio kipaji chake, Nandy ameonekana kuchukizwa na maneno hayo.

Nandy akiongea na bongo 5 anasema kuwa anashangazwa  sana na  watu wanaongea hivyo  kwa sababu kwa upande wake anajua kabisa kuwa amekuwa akifanya kazi na akitoa ngoma kila mara na nzuri zaidi ni kwamba zimekuwa zikipigwa katika station mbalimbali.

Hayo maneno yao hayanipi tabu yoyote kwa sababu kila siku nasikia kuhusu kubebwa kubebwa lakini nyimbo zangu zimekuwa zikipigwa radioni na zimekuwa zikihit kila kona kwa mfano sasa hivi ninogeshe ina viewers zaidi ya milion 5 kwaio siona kama nabebwa.

Hata hivyo Nandy anasema kuwa haogopi kuongelewa kwa sababu hiyo ni kawaida kwake kama star.

Nandy Awashukia Wanaosema Anabebwa Kwenye Muziki

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva Faustina Charles maarufu kama Nandy amewatolea povu zito watu ambao wamekuwa wakimtuhumu Nandy kwa kubebwa Kwenye Muziki.

Nandy amefunguka kuzungumzia kelele ambazo zipo kwenye mitandao ya kijamii kwamba anabebwa kwenye muziki wake na sio kipaji chake ambacho kimemfikisha sehemu aliyofikia.

Kwenye Interview aliyofanya na Bongo 5, Nandy amedai anashangazwa na tuhuma za kubebwa kimuziki Wakati anaimba nyimbo na zinapigwa kila kona  na zinashika chati kama kawaida:

Hayo maneno ya watu hayanipi tabu yoyote kwa sababu each and everyday nasikia kuhusu kubebwa kubebwa lakini nyimbo zangu zinahit redioni na zinapigwa mpaka mikoani na zinatrend Kwenye chati kwa mfano kama sasahivi ‘ninogeshe’ ina viewers milioni 5 kwaiyo suala la kubebwa halipo”.

Lakini pia Nandy amedai yeye kama staa kuongelewa ni jambo la kawaida kwani ukiwa msanii halafu ukaona hakuna hata mtu mmoja anakuongelea basi wewe sio staa.

Tuhuma Za Nandy kubebwa zilianza kutokana na Nandy kuimba nyimbo nyingi za wasanii wa zamani Lakini pia Nandy amewahi kukiri kuandikiwa nyimbo zake nyingi anazoimba.

Nandy Kumuanika Aliyevujisha Video Yake na Billnass.

Kwa muda sasa tangu kulipotokea sakata la video liyokuwa ikimuonyesha Nandy na mpezi wake Billnass wakiwa faragha ambapo baada ya kuvuja na kusambaa sana, mwanadada huyo alionekana kuathirika sana lakini mambo yalikuja kuwa sawa kutokana na kuwaomba msamaha mashabiki na kupewa onyo na TCRA NA BASATA pia,

Sasa mwanadada huyo baada ya ukimya mrefu ameibuka na kusema kuwa muda wote huo alikuwa kimya kutafuata ni anni aliyafeanya kazi ya kusambaa video hiyo aktika mitandao na amefanikiwa kufanya hivuo.

Nandy anasema kuwa sasa hivi atakuwa na amani kwa sababu anataka kurudisha pia heshima yake kwa mashabiki aliokuwa nao kwa sababu kitendo kile kilimuahribia sifa yake kwa mashabiki wake.

Nandy Alamba Dili Nono na Kampuni Ya Mtandao Wa Simu

Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayefanya vyema na kibao chake cha ‘Ninogeshe’ Faustina Mfinanga maarufu kama Nandy amelamba Dili nono na kampuni ya Halotel.

Nandy amechaguliwa na mtandao wa simu wa Halotel kuwa balozi wao mpya kupiti promotion yao mpya ulioizindua uitwayo, Ninogesha.

Akizungumza katika hafla fupi ya kusaini mkataba na msanii huyo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Halotel, Mhina Semwenda amesema kampuni imemchagua Nandy kwa sababu ana uwezo wa kuwa na mchango chanya utakaosaidia kukuza mauzo ya bidhaa na huduma, pamoja na kuimarisha jina la kampuni.

Nandy ni msanii anayekonga nyoyo za mashabiki wake kupitia wimbo wake unaovuma kwa jina la ‘Ninogeshe’ na kumpa umaarufu unamfanya afahamike kwa watu wa rika zote. Unampa umaarufu ambao utasaidia kuiwakilisha vema kampuni ya Halotel“.

Nandy amesema hiyo ni fursa kubwa na ya kipekee kwake kuwa miongoni mwa familia ya kampuni hiyo na kupewa jukumu la kuiwakilisha ipasavyo kwa wateja wake na watanzania kwa ujumla kutokana na huduma bora za mawasiliano inazotoa.

Nandy Aelezea Mfumo wa Familia Anayoitamani.

Mwanadada Nandy amefunguka na kusema kuwa anatamani sana kuwa na familia kubwa na nzuri huku akitaja vigezo vyake vya kuwa na familia hiyo kuwa anataka familia inayomcha Mungu sana na yenye watoto watatu na yenye kujituma kutafuta pesa.

Nandy anasema kuwa anatamani sana kuwa na familia ya kumcha Mungu sana, wenye kutafuta pesa na kupata watoto wasiopungua watoto “kila mmoja anatamani kuwa na familia anayoipanga  mwenyewe kwa uapnde wangu natamani sana kuwa na familia nitakavyopenda na yenye hofu ya mungu, lakini pia ikipendeza nipate watoto wengi. “

Pamoja na kwamba hajasema ni lini ataingia katika ndoa lakini Nandy anaamini kuwa muda wake utafiki na kuingia katika familia na atatiiza malengo yake.

 

Nandy Ashinda Tuzo Nyingine Nchini Kenya.

Mwanadada kutoka Tanzania Nandy ameshida tuzo nchini kenya kutoka Maranatha Awards nchini humo.Tuzo hizo ni tuzo maalum zinazotolewa nchini humo kwa ajili ya wasanii wa injili.

katika tuzo hizo, Nandy ameshinda tuzo hiyo katika kipengele cha Best  Worship Song Cover kupitia wimbo wa Angel benard wa nikumbushe.

Kupitia wimbo huohuo , Angel Benard nae ameshinda tuzo nchini marekani , hivyo hii inaonyesha ni jinsi gani wimbo huo umekuwa na nguvu kubwa.

Nandy Avua Nguo Jukwaani kwa Mzuka wa Mashabiki.

Mwanadada Nandy amejikuta akivua nguoa na kubaki na nguo za ndani baada ya kupanda jukwaani na kuimba nyimbo zilizowapandisha mzuka mashabiki wake na kuanza kumshangilia kwa nguvvu na kujikita akianza kurusha kiatu na kufikia kuvua nguo.

Mambo hayo yametokea alipokuwa akifanya show huko mkoani Tarime maeneo ya Nyamongo ambapo alipoanza kuimba na mashabiki zake kumshangilia kwa mzuka sana ndipo alipojikuta akianza kuvua kitu kimoja na kukirusha na hata baada kuvua nguo ya juu na kubaki na nguo ya ndani.

Hata baada ya kumaliza sho, katika ukurasa wake wa instagram nandy alionyesha jinsi gani alifurahia show hiyo na kuandika kuwa ‘Juhudui huzidi kipaji, asanteni sana watu wa nyamongo”

Nandy Adai Yeye Ndio Msanii Mkali Wa Kike Bongo

Staa wa muziki wa Bongo fleva anayeendelea kufanya vizuri na ngoma yake ya ‘Ninogeshe’ Faustina Charles ‘Nandy’ ameibuka na kusema yeye ndio Msanii was kike anayeongoza Bongo.

Nandy amefunguka na kudai anaamini kuwa kwa sasa yeye ndio msanii wa kike ambaye amekuwa consistant na kushika chati za juice kutokana na ngoma anazotoa.

Kwenye Interview aliyofanya na Clouds Tv, Nandy amekiri kuwa yeye ni namba kwa kigezo cha namba ila anawaheshimu wale wote waliomtangulia kimuziki.

“Namba moja kwa Tanzania sasa hivi, au wewe unaonaje?, go with numbers, go YouTube, go Subscriber, go every where, go with numbers. Usiangalie tu nani anafanya nini, angalia numbers.

Kabla sijawa namba moja, namba moja yangu Lady Jaydee lakini bado nitamuheshimu, ni mkubwa amenitangulia. Yeyote yule ambaye amenitangulia lazima nimuheshimu kwamba ni mkubwa”.

Lakini pia Nandy amesema ingawa kuna wasanii wengi wakongwe anaowaheshimu kama Lady Jay Dee lakini haimaanishi wao watakaa Kwenye chati milele lazima wapishane kila mtu kwa nafasi yake atabeba chati.

Nandy Afanya Kufuru Apewa Mtaa Mahali anapokaa.

 

Nandy akiwa na moja ya viongozi wa mtaa huo.

Mwanadada Nandy anaendelea kuonekana mwenye mafanikio hasa baada ya kuonekana sehemu anayokaa kupewa mtaa wenye jina lake na balozi wa mtaa uo.akiwa kama msaani na kioo cha jamii watu wanaokaa katika mtaa huo wamemkubali na kumpenda na kuupa mtaa huo jina lake kama kumbukumbu.

katika video moja iliyoenea mtandaoni nandy alisikika akisema”asante sana balozi wangu kwa kunipa mtaani, ii ni kwa sababu ya kuisi na watu vizuri tangu nimefika hapa mkanikabithi plot na mpka sasa ivi mmeona kuna haja ya mimi kupewa jina la mtaa.”

Video Ya Ngono Yaendelea Kumtesa Nandy

Mwanamuziki wa Bongo fleva Faustina Charles maarufu kama Nandy ameendelea kuandamwa na video yake ya ngono na aliyekuwa mpenzi wake Billnas.

Nandy ambaye kwa hivi sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ya Ninogeshe amekiri kuwa mpaka leo hii bado anapata kipindi kigumu kwa ajili ya ile video yake.

Nandy ambaye amekiri kuwa anatamani sana aweze kupanda usafiri wa umma maarufu kama daladala ili aweze kupata nafasi ya kukutana na mashabiki zake Uso Kwa Uso lakini ameweka iankuwa ngumu kutokana na ile video yake.

Kwenye mahojiano na Showbiz Xtra Nandy alisema kuwa, alipanga karibu mwezi mzima kufanya ziara hiyo ya kila sehemu atakayoenda atumie usafiri wa daladala ili aweze kupata nafasi nzuri ya kujua mambo mbalimbali ndani ya daladala na kuna wakati anazitamani stori za humo.

Nilipanga ndani ya mwezi mzima usafiri wangu uwe huo lakini mambo yakaingiliana na ya kusambaa ile video ya faragha kwenye mitandao ya kijamii, lakini bado dhamira yangu ipo nitafanya hivyo kwa sababu natamani kukutana na watu tofauti”.

Mwezi uliopita Nandy alipata fedheha hiyo baada ya video yake ya faragha na aliyekuwa mpenzi wake Billnas kusambaa Mtandaoni baada ya kukataa sio wapenzi kwa mara nyingi tu.

Nandy Ajiingiza Kwenye Ulimwengu wa Ujasiriamali (+picha)

Mwanamuziki wa Bongo fleva Faustina Charles maarufu kama Nandy ameingia rasmi Kwenye ulimwengu wa ujasiriamali baada ya kutangaza bidhaa yake mpya.

Nandy amesema kuwa ameingia ubia na kampuni ya Grace Products inayojihusisha na utengenezaji wa sabuni za kuogea na vipodozi mbali mbali vya asili na yeye atakuwa ni moja ya wamiliki wa kampuni hiyo.

Nandy aliita waandishi wa habari kwa ajili ya kutangaza kuingia ubia na kampuni hiyo ya Grace Products na atakuwa mmoja wa wamiliki wa kampuni hiyo na jina lake na picha zake zitatumika katika baadhi ya bidhaa hivyo kuwataka mashabiki zake wampe sapoti kwa kununua bidhaa hizo.

Ni wiki chache zilizopita Nandy aliongea na kumpongeza Ali Kiba kwa kinywaji chake cha Mo faya Lakini sasa ameamua kufuata nyendo zake.

Hizi ni baadhi ya Picha katika uzinduzi huo:

.

 

.

Nandy- Nategemea Kuolewa Hivi Karibuni

Mwanamuziki wa Bongo fleva Faustina Charles maarufu kwa Jina la usanii kama Nandy amefunguka na kuweka wazi kuwa anategemea Kuolewa hivi karibuni.

Nandy amefunguka Kwenye mahojiano na gazeti la Risasi Jumamosi kuwa kuna mipango kabambe  ambapo ataolewa hivi karibuni huku akigoma kumwanika mchumba’ke akihofia nyakunyaku wa mjini.

Nimewaambia tu ninyi kwa sababu mmeniwahi kuniuliza, ukweli ni kwamba nitafunga ndoa soon, lakini kuhusu mwanaume wangu, naomba nisimwanike kwa sasa”.

Lakini pia Nandy ameongelea furaha yake aliyonayo kwa hivi sasa baada ya Kupitia kipindi kigumu kwenye maisha yake mwezi uliopita.

Unajua nimepita katika wakati mgumu sana, lakini sikumuacha Mungu kabisa na ndiyo maana hata haya yote yanayonitokea ya kupata mikataba na kufanikiwa hadi kununua gari ni kwa sababu kila kitu changu sasa kiko sawa kabisa”.

Mwezi uliopita Nandy aliposti a kipindi kigumu baada ya video yake ya ngono akiwa na mpenzi wake kwa kipindi hiko Billnas kuvuja Kwenye mitandao ya kijamii na kusababisha kudhalilika kupita kiasi.

Nandy Adaiwa Kuhongwa Gari La Mamilioni

Mwanamuziki wa Bongo fleva kutoka THT, Faustiana Charles maarufu kama Nandy amefungukia tuhuma alizotupiwa na kudaiwa kuwa gari aliliouza nalo sura hivi karibuni Kwenye mitandao ya kijamii amehongwa.

Wiki iliyopita kuna picha na video zilisambaa Kwenye mitandao ya kijamii zikimuonyesha Nandy akionyesha gari lake jipya alilodai amenunua hivi karibuni aina ya Mercedes Benz E-Class E320 CDI.

Lakini Kumekuwa na tetesi zinazosema kuwa Nandy amenunuliwa gari hilo kama zawadi na kigogo ambaye anamuweka mjini kwa hivi sasa taarifa ambazo Nandy amezikataa kata kata.

Kwenye Interview na Risasi Jumamosi, Nandy alisema kuwa, gari hilo alilinunua kwa zaidi ya shilingi milioni 70 za Kitanzania kwa jasho lake na hiyo ilitokana na kuingia mikataba na makampuni mbalimbali Tanzania yakiwemo ya michezo ya namba, shirika moja kubwa la ndege na mingineyo.

Watu wengi wanajua kuwa kuna mtu ameninunulia hili gari, lakini siyo kweli kabisa, mimi mwenyewe nina madili mengi ya kufanya na ndiyo yameniwezesha kupata fedha za kununua Benz, yaani kifupi ni jasho langu mwenyewe”.

Nandy Amekuwa akifanya vizuri na ngoma yake mpya ya Ninogeshe ambayo imeshika chati mbali mbali nchini.

Ninogeshe ya Nandy Yamfunika Ommy Dimpoz

Msanii wa kike Nandy ambae anatamba na wimbo wake wa Ninogeshe amkalisha chini msanii mkongwe pia Ommy Dimpoz na wimbo wake wa Yanje ambao pia ulitoka siku chache zilizopita,  nyimbo hizo ambazo zote zinaonekana kuwa zinazopendwa sana  na watu tangu zimetoka zimekuwa zikibadilishana nafasi kwa muda mrefu na sasa nandy amemkalisha ommy kwa nafasi moja.

Siku chache za nyuma msanii ommy dimpoz alisema kuwa hawezi kuangaika kufanya kiki ya kitu chochite ili kuweza kuifanua nyimbo yake ifanye vizuri, zaidi sana anaamini kuwa nyimbo zake za mwanzo zilishamtengenezea jina kubwa la kuweza kutoa wimbo wowote ili kuweza kuhit.

Nandy anakuwa moja y wasanii wa kike wanaofanya vizuri sasa katika muziki na kuwakalisha kina dada wengine wengi kutokana na kipaji chake ambacho amekuwa akikitendea haki.

Nandy Amnyooshea Mikono Ali Kiba Akiri Kumkubali

Mwanamuziki wa Bongo fleva kutoka THT Nandy amekiri kuwa pamoja na mambo mengine yote na maneno yakiwekwa pembeni staa wa Bongo fleva Ali Kiba amemu-insipire sana kwa kinywaji chake.

Nandy amekiri kuwa hatua aliyofikia Ali Kiba ya kuingiza kinywaji chake mtaani ambayo ni Energy drink ni hatua kubwa sana ambayo imempa changamoto hata yeye ya kufanya makubwa zaidi.

Kwenye mahojiano aliyofanya na The Playlist ya Times, Nandy amekiri kuwa kupitia Kiba ni vizuri wasanii wengi wakajifunza kuwa ni vizuri kuwekeza nje ya muziki.

Ameni-inspire kwa kinywaji kwa sababu ukiangalia the package ya kinywaji chake jinsi ilivyo ni project fulani ambayo ipo serious”.

Lakini pia Nandy ameongelea uwekezaji wa wasanii wengine kama Diamond Platnumz ambaye ni mmoja kati ya msanii Lakini pia mfanyabiashara.

Tunaambiwa nje ya kuimba tunatakiwa tuwekeze nje ya muziki wetu na ndicho hiki kaka zetu wanafanya ukimuangalia kama Diamond, Alikiba ni vitu ambavyo wanatuhamasisha”.

Kwa hivi sasa Nandy anafanya vizuri sana ngoma yake ya Ninogeshe inayoshika namba moja kwenye mtandao wa Youtube.

Makampuni ya Nguo za Ndani Yalinitafuta Kufanya Matangazo Lakini Nilikataa_Nandy

Mwanadada Nandy siku ya jana alikuwa na mahojiano na waandishi wa habari wa Clouds Media, na baada ya hapo alipata bahati ya kuongea na Millard Ayo ambapo Nandy alifunguka na kusema kuwa makampuni mengi yalimfuata ili kufanya nae kazi hasa ya kutangaza  kutangaza nguo za ndani.

Hii ilikuja baadaya nandy kuvujisha video akiwa amevaa nguo ya ndani tu akiwa na mpenzi wake Bilnass hivyo hiyo iliwafanya baadhi ya makampuni kuanza kumsumbua kufanya nae matangazo ya chupi.

Akiongea na millard ayo ,Nandy alisema

watu wa nguo za ndaniwalinitafuta sana,watu wengi sana na kuweka madau tofauti tofaut hadi na pedi walinitafuta pia , lakini siwezi kufanya kitu kama hicho kwa sababu hata kipindi kitu hicho kinatokea sikufanya kama makusudi  na nimeniumiza sana na kipo moyoni bado mpaka sasa.siwezi kuchukulia ilo kama fursa na mimi nikakaa na nikaanza kutangaza jamani chupi hii ni kama yangu.

Nandy anasema kuwa hawezi kufanya hivyo kwa ajili ya pesa kwa sababu ana vyanzo vingine vya kumpati apesa labda miaka mitano mbeleni kama mtu ataona kuwa chupi yake itampendeza ndipo atafanya baishara ya matangazo a chupi lakini sio sasa hivi.

Nandy- Nilitaka Kuacha Muziki Kisa Video Chafu

Mwanamuziki wa Bongo fleva Nandy amefunguka na kudai alikuwa tayari kuacha muziki baada ya ile video yake chafu kuvuja Kwenye mitandao ya kijamii.

Wiki chache zilizopita Nandy aliwaacha watu midomo wazi baada ya video yake iliyomuonyesha akiwa kitandani na aliyekuwa mpenzi wake Billnas kivujishwa Kwenye mitandao ya kijamii.

Nandy amekiri kutaka kuacha muziki Kwenye mahojiano na Kipindi cha leo Tena cha Clouds Fm ambapo amezidi kufunguka haya:

Nilihisi kukata tamaa kuachana na muziki kabisa sikuona maana ya maisha. Lakini nilipofika BASATA walinipa ushauri na kunihoji binafsi sikuwa na picha mbaya nyuma katika maisha yangu kama kweli nilivujisha picha zile kwa ajili ya Kiki.

Hali yangu ilikuwa mbaya sana nilipoona ile video sikuamini kabisa macho yangu. Nilizidiwa na Pumu nikakimbizwa hospitali kifupi nilipata Brain Attack niliwaza kuhusu familia yangu nItamtazamaje mama na baba yangu?”.

Nandy jana aliachia wimbo wake mpya ulioandikwa na msanii mwenzake Aslay unaoitwa Ninogeshe.

Nandy Akana Kuvujisha Video Yake Ya Ngono

Mwanamuziki wa Bongo fleva Nandy amekana kabisa taarifa zilizoenea kuwa yeye mwenyewe kwa mkono wake ndiye aliyesambaza video yake ya ngono na Billnas kisa kiki.

Wiki chache zilizopita Nandy na Billnas wali trend vibaya mno baada ya kuonekana kwenye video iliyovuja Mtandaoni wakiwa kitandani wakifanya mambo yao.

Kwenye mahojiano aliyofanya leo na kipindi cha Leo Tena cha Clouds Fm, Nandy amekanusha kuwa video yake na Billnas haikuwa mpango wa kiki kama  wengi wanavyodhani na taarifa za kusambaa kwa video hiyo zilimuathiri kiafya kiasi cha kupoteza fahamu mpaka kukimbizwa hospitalini.

Ile video haikuwa kiki na wala sonata tabia ya kufanya kiki, wakati video inasambaa milioni huwa simu na meneja wangu kuniuliza na kiukweli baada ya kuiona ile video nilihisi sio mimi niliishiwa nguvu na uongozi wangu unasema niliishiwa fahamu kwa masaa kadhaa”.

Tangu video hiyo itokee nandy amekiri kuwa katika wakati mgumu kwani ni siku chache zilizopita kuna video iliyo trend ikimuonyesha akiangua kilio stejini hadi kushindwa kupiga shoo na meneja kumtoa stejini.

Nandy: Siyo Sahihi Kujirekodi Ukiwa Mtupu

Mwanamuziki wa Bongo fleva Nandy amefunguka a kuweka wazi kuwa kuvuja kwa video yake ya mahaba chumbani na aliyekuwa mpenzi wake Bilnass imemfunza mambo mengi ikiwemo sio vyema kujirekodi ukiwa uchi.

Sakata hili lilimkuta Nandy wiki iliyopita baada ya video yake akiwa chumbani na mpenzi wake Billnas wakiwa wamevaa nguo za ndani huku wakiwa nikaona ya kimahaba kuvuja mtandaoni na kusababisha tafrani.

Nandy amefungukia majuto yake kwenye mkutano na waandishi wa habari aliofanya alipotoka katika ofisi za mamlaka ya mawasiliano Tanzania na kuweka wazi kuwa amejutia sana kitendo hiko na sasa yupo tayari kushirikiana na serikali kwa ajili ya kutoa elimu kwa watu:

Nipo Tayari kushirikiana na serikali kwa hilo lililotokea na kuelimisha wasanii, wanafunzi na jamii kwa ujumla najua watu wengi wanapitia hatua kama hizi na wengine hata hawajulikani lakini kwa kuwa limetokea kwangu Ilan najua kuna watu wengine wamefanya mambo kama haya na video zimeenda mitandaoni bila idhini yao”.

 

Diamond Akiri Kuwa Yeye ni Bingwa Wa Kiki na Drama

Supastaa wa Bongo fleva Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’ amekiri kuwa yeye ni bingwa wa kutafuta kiki mitandaoni Lakini pia anajulikana kwa kuwa na drama zisizoisha.

Diamond amekiri hayo kwenye mkutano aliofanya na waandishi habari siku ya jana katika ofisi za Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA), kujuzwa mambo kadhaa kuhusu sheria za mitandao.

Diamond ameongea hayo na kuomba radhi kwa mashabiki zake na serikali baada ya kuachia video mbili tofauti zilizomuonyesha akiwa na wanawake wawili huku akifanya matendo yaliyotafsiriwa kinyume na maadili ya Kitanzania.

Na mimi ni miongoni mwa mabingwa wa kiki, najikubali, najua kabisa drama ninazo kila siku lakini tunaziweka vipi zisiende kuwatia dosari viongozi ambao wanapambana kuhakikisha sanaa yetu inafika mbali,

Kwa sababu ikienda kwa mazingira ambayo yalikuwa yamezoeleka huko nyuma unawavunja moyo viongozi ambao wanapigania sanaa ifike mbali”.

Lakini pia kwenye mkutano huo pia Nandy aliomba radhi pia kwa kusambaza video yake ya chumbani na Billnas ambayo ilivuja wiki chache zilizopita.

Mh Mwakyembe Aagiza Nandy Kukamatwa

Mh Waziri wa habari na michezo, Harrison Mwakyembe ameagiza kukamatwa kwa msanii wa muziki wa kizazi kipya mwanadada  Nandy baada ya kusambaa kwa video zake chafu na kufikishwa kituo cha polisi kwa ajili ya mahojiano na uchunguzi zaidi.

Majibu hayo yamekuja baada ya Mh  Goodluck Mlingwa  mbunge kutoka Morogoro alipouliza ni hatua gani za serikali zimekuwa zikichukuliwa ili kupambana na wasanii wanaweka picha za uchi na matuzi katika mitandao.

Hata hivyo, Mwakyembe amethibitisha kuwa mpaka sasa msanii Diamond Platinumz bado yuko polisi alikofikishwa tangu jana kwa ajili ya mahojiano baaada ya kuvujisha video akiwa na wanawake tofauti akiwa faragha.

Tulitunga sheria mwaka 2010 lakini tulikosa shaeria za kubana wasanii  katika maudhui hasa katika upande wa mitandao.tumeshazitunga hizo kanuni na sasa hivi zimeshaanza kufanya kazi.kuna baadhi ya vijana wamekuwa wakifanya uhuni uhni katika mitandao ya kijamii sana na tumeanza kuwafanyia kazi , yupo msanii Diamond Platinumz ambae  amefikishwa polisi tangu jana kutokana na kusambaa kwa picha zake chafu, hata hivyo pia binti nandy pia inabidi akamatwe ahojiwe..

Diamond Afikishwa Polisi Baada Ya Video Yake Kuvuja Mtandaoni

Mwanamuziki wa Bongo fleva Naseeb Abdul maarufu kama Diamond Platnumz amefikishwa polisi jana kwa ajili ya mahojiano baada ya kusambaa kwa video zake zisizo na maadili katika mitandao ya kijamii.

Jamiiforum wnaripoti kuwa hayo yalisemwa na Waziri wa habari, Michezo, Utamaduni na sanaa Dr.  Harrison Mwakyembe akiwa bungeni wakati akijibu swali juu ya kanuni za maudhi ya Mitandaoni aliloulizwa na Mbunge Goodluck Mlinga.

Aidha Dkt. Mwakyembe amesema Msanii Faustina Charles (Nandy) naye atahojiwa na Polisi kufuatia video yake ya faragha akiwa na Msanii mwenzake Billnass kusambaa mitandaoni.

Waziri Mwakyembe amesema kwa sasa wanaangalia  taratibu za kuwafikisha mahakamani.

Popular sassy singer apologizes after an intimate video with ex boyfriend emerges online

Tanzanian singer Nandy has left many talking after a video with her ex boyfriend Billnass emerged online. Well, judging from the videos content it’s obvious to see that this was 18+ rated.

Anyway apparently the video was taken back in 2016 when the two were together. Not many knew about their relationship since they opted to keep it on the low until just recently when the video emerged.

video leaked

According to the two parties, they are not aware of how the video landed on social media. The guy who also happens to be a big Tanzanian artist went on to say that the video was taken by Nandy using her phone which he had no access to.

Nandy on the other hand has been left confused; however she has issued an apology to fans and Tanzanian government for the inappropriate clip. She wrote saying;

 

Nandy Aomba Radhi Mashabiki na Jamii Nzima kwa Ujumla.

Mwanadada nandy kupitia ukurasa wake wa instagram amekubali kosa na kuwaomba msamaha watu wote walioiona na kuguswana hata kuharibu mahusiano yake na mashabiki.

Nandy ameomba msamaha baada ya kuvuja kwa video ilikuwa ukimuonyesha billnass na nandy wakiwa chumbani kitandani huku wakiwa katika hali ya kimahaba na kuvujisha siri waliokuwa wakiificha kwa muda mrefu kuwa wako katika mahusiano ya kimapenzi.

         Napenda kuchukua nafasi hii kuwaomba radhi sana sana  ndugu zangu,familia yangu na rafiki zangu wote kwa kile kilichotokea,bado siki sawa naomba mniombee uzima.

Nandy na Billnass hawatokuwa wasanii wa kwanza Tanzania kuwa na skendo chafu ya ngono kwa kutupia picha hizo katika mitandao ingawa kila mmoja anakataa kukubali kosa la kuwa ndio chanzo cha video hiyo kuenea katika mtrandao.

Nandy Amtupia Lawana Billnass, Ni Baada ya Video Yao Chafu Kuvuja.

Mwanadada Nandy amemtupia lawama mpenzi wake Billnass kwa kuvuja kwa video chafu iliyokuwa ikiwaonyesha wakiwa pamoja faragha, na kuwaomba radhi mashabiki na watu wote waliopatwa na mshtuko kuhusu video hiyo ambayo imesambaa sana ktika mitandao ya kijamii.

Nandy amekubali kuwa ni kweli video hiyo iliuwa ni ya kwake na aliyewahi kuwa mpenzi wake Billnass na waliipiga mwaka 2016 kipindi wapo katika mahusiano lakini anashangaa kuona video hiyo ikiwa imevuja kwa sababu walikubaliana hata mahusiano yao yawe ya siri.

nilikuwa na mahusino na Bilnass 2016, nilikuwa na mahusiano na billnass na tulikubaliana kuwa mahusiano yetu yawe ya siri, sasa silewei kwa sababu gani kaamua kuvujisha ,nimesikitishwa sana , ni video ambayo ilikuwa imeshutiwa kwa snapchat.sasa silewei aliipataje hiyo video kwa sababu mpaka aipate ni mpaka nimrushie kutoka kwangu.Naomba radhi sana familia yangu, kanisani kwangu , mashabiki na serikali yangu kwakweli video imenichefua sana mpaka hapa ninapoongea nimechefuka sana, ila adhabu ya maumivu ninayoyapata  ni kutokana na kumuamini sana mwenzangu.-Aliongea nady alipokuwa akihojiwa na MCL digital.

Sitaki Ugomvi na Mtu: Nandy

Mwanadada mwenye wimbo uliovuma sana kwa hivi karibuni, Nandy amefunguka na kusema kuwa kuna watu wamekuwa wakimuingilia sana katika mabo yake lakini hapendi kuingi katika bifu na msanii mwenzake yoyote.

Mwanadada huyo ameongea hayo alipokuwa akiongea na Clouds  Tv kuwa yeye sio mtu mwenye asili ya ugomvi hivyo mara zote watu wamekuwa wakimuingilia katika mambo yake na amekuwa akikaa kimya

Mimi siku zote huwa sio mgimvi na mara kwa mara nimekuwa nikijiepousha kuingia katika ugomvi na watu.huwa napuuzia na kuwaonyesha watu kuwa wanachokifanya ni cha kijinga, huwa namuonyesha tu kuwa sifatilii kile anachokifanya au kuwa nimeshtuka na matendo yake.

Hivi karibuni kumekuwa na maneno yanayosambaa kuhusu yeye huku wengine wakimhukumu kutoka kimapenzi na bosi wake.

Kivuruge Ya Nandy Ilirudiwa Mara ya Pili.

Wimbo wa kivurge umekuwa ukifanya vizuri kila kona kwa audio na hata baadae baada ya kutolewa kwa video yake.Lakini inasemekana kuwa wimbo huo ulirudia mara ya pili na Nandy na kuufanyia haki zaidi kuliko mara ya kwanza.

Akijibu kuusu swala hilo, alikuwa mlimiki wa wimbo huo ambae pia ni msanii akijulikana kama Jay Melody anaetamba na wimbo wake wa Goroka amesema kuwa ni kweli wimbo huo aliuimba yeye lakini nany aliupenda zaidi hivyo akataka kuuchukua na ndipo waliofanya makubaliano na kuuchukua.

Nandy alinifuata baada ya kusikia nimeutoa na akaomba kuurudia na ndipo nilipokutana na uongozi wake na tukaweka makubaliano mazuri nikampatia, mimi ndie nilieutunga na hakuna hata kipande kilichobadilika-Aliongea Jay Melody.

Alpotafutwa nandy kuthibitisha hilo nae alikubali na kusema kweli aliupenda wimbo huo na kufanya makubaliana na aliyekuwa anaumiliki.

Ni kweli wimbo huo uliimbwa na jay melody lakini kuna makubaliano tuliyafikia ndipo nikaurudia na mimi.

 

Ruby Ajisifu Kuwa Nandy Mamuwezi Katika Muziki

Ruby ni moja ya wasanii waliokuja na kufanya vizuri sana katika tasnia ya muziki lakini ndoto zake zilizimika baada ya kukosana na menejimenti yake na kushindwa kuendelea na muziki kwa kipindi cha muda mrefu kidogo , lakini moja ya wasanii wa kike wenye kipaji cha kuimba na anaweza kufanya vizuri kama atapewa nafasi nyingine ya kufanya muziki.

Hivi karibuni msanii Ruby amekuja na nyimbo yake mpya iliyokwenda kwa jina la ‘are  you ready’, ambayo ni ya kwanza tangu kukaa kwake kimya kwa kipindi kirefu kidogo.

Aliipoulizwa kuhusu kimya chake cha muda mrefu Ruby aliibu kuwa sababu  moja wapo ya kukaa kimya ni kumpa nafasi msanii mwenzie Nandy ili aweze kujulikana katika muziki kwa sababu endapo na yeye angeendelea kufanya kazi basi Nandy asingeweza kufanya vizuri katika muziki kama ilivyo sasa.

Ruby anasema kuwa ujio wa Nandy haukuksumbua sana kwa sababu ana amini kuwa Nandy ni msanii mzuri lakini hakutaka kuanza kujishindanisha nae,lakini pia anasema kuwa watu wengi wamekuwa wakisema kuwa ujio  wa Nandy ulikuwa ni wa kuziba pengo aliloliacha lakini ukweli ni kwamba yeye na Nandy wote wanafanya muziki wa aina moja lakini bado kuna tofauti kubwa kati yao hasa upande wa TONE  na SCALES zao katika muziki wanaoimba.

Hata hivyo Ruby ameomba kutokushindwanishwa na mtu yoote kwa sababu hapendi kushindana na mtu katikamaisha yake zaidi ya yeye mwenyewe tu, na hata kama wanafanya muziki wa aina moja  haimaanishi kuwa wanafanana hata kidogo.

Ruby anatangaza kurudi tena katika muziki na kusema kuwa wakati yupo kimya alikuwa akiumia sana pale alipokuwa akiona mashabiki zake wanalalamika na kumuomba arudi na kwamba walikuwa wakim-miss sana.

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.